Siasa za kilaghai za Polepole: Awamu ya Nne aliunga mkono Katiba Mpya; Awamu ya Tano alikataa, Awamu ya Sita anaitaka kwa gia ya Shule ya Uongozi

Siasa za kilaghai za Polepole: Awamu ya Nne aliunga mkono Katiba Mpya; Awamu ya Tano alikataa, Awamu ya Sita anaitaka kwa gia ya Shule ya Uongozi

Haka kajamaa KANAFIKI SANA. Ni KACHUMIATUMBO KAJASIRIASIASA.
Watu ktk kundi hili walifanikiwa kuteka akili za JPM. Hayupo sasa!
Rais SSH asipowachunga wataisumbua sana Serikali yake.
Hilo darasa analodai la uongozi sijui anamfundisha nani. Political economics?! Hayo masomo wanasoma watu wenye IQ ndogo za chini. Ni masomo unayoweza kuhitimu hadi PhD ukiwa kitandani umelala, au, unasoma huku ukiwa unakunywa pombe.
hii ndiyo asili ya watu wa kigoma; kafulila, dr. walid kabouru, felx mkosamali, zito kabwe hawa ni zaidi ya vinyonga, ni zaidi ya wachumia tumbo
 
Ya Mbowe aliekawaaminisha Lowasa fisadi ba badae akawaaminisha Lowasa ni msafi mlisikiliza.
Ukisema Mbowe aliwaaminisha Lowassa fisadi unaweza kujikuta hata hujui unacho Ongea!!..Hebu tutafakari Kwa Pamoja Lowassa yuko wapi na anafanya nini?!!.. Watanzania tuache Dhana!!!...Pole Pole ni tofauti sana,ukimchambua in 10 years hata sijui mnapata ujasiri gani wa kusoma hiyo shule ya uongozi!!!...Unajua mawaziri wakuu nao wamewekewa Kinga akiwemo Lowassa?!!..
 
Haka kajamaa KANAFIKI SANA. Ni KACHUMIATUMBO KAJASIRIASIASA.
Watu ktk kundi hili walifanikiwa kuteka akili za JPM. Hayupo sasa!
Rais SSH asipowachunga wataisumbua sana Serikali yake.
Hilo darasa analodai la uongozi sijui anamfundisha nani. Political economics?! Hayo masomo wanasoma watu wenye IQ ndogo za chini. Ni masomo unayoweza kuhitimu hadi PhD ukiwa kitandani umelala, au, unasoma huku ukiwa unakunywa pombe.
Kweli mkuu tunakosa viongozi wenye akili kubwa
 
Kwa nini mnahangaikia pumba za Polepole si mtoke na mchele wenu muwalishe Watanzania? , Why are you disturbed with his actions/words if they are hypocritical?
 
Bila kujua kupitia andiko lako ...ndio unajifunua na kuonekana Kama una IQ Ndogo,laabda pengine huelewi maaana ya Political Economics....wewe.mzungumzie Polepole ...!
Hivi unajua Dunia inavyo3 deshwa na kutawaliwa.....😊😊
Mitandao ya kijamii imeleta shida Sana ...kila mru no Mtaalam wa kila kitu!
Ujinga,Upumbavu wa Polepole usikufanye na wewe kuwa mjinga!
Usimshambulie mtoa hoja. hizo makitu ni fani ya watu wenye iq ya kawaida tu, ila ikitokea mtu wa iq pana akazisoma anakuwa hatari sana,

kwa waliopita shule mgumu hizo kitu unaweza ukazisoma na kupata phd ndani ya miezi 3
 
Ni kwanini wanasiasa Afrika wakishaingia katika nafasi fulani hawataki kutoka na kwenda kuanzisha ujasiriamali kama wanavyowaambia vijana wajiajiri kwa ujasiriamali? Afrika kuendelea ni ndoto kubwa
Hela ya siasa ni hela ya kuchota na inapatikana kirahisi sana ukiwa kibaraka wa kiongozi wa nchi!

Humphrey PolePole alibahatika kuwa katika channel hio na akaonja utamu wa Uchawa kwa raisi😅! Ujasiriamali gani utafanya ndani ya miaka mitano uweze kumiliki mabilion ya fedha? Wote hao yeye, Makonda na vijana wenzao waliokuwa kwenye channel now ni mabilionea wa kimya kimya!

Utauza nini upate hayo mabilion ndani ya miaka mi 4? Labda uwe drug dealer mkubwa!
 
Kwa nini mnahangaikia pumba za Polepole si mtoke na mchele wenu muwalishe Watanzania? , Why are you disturbed with his actions/words if they are hypocritical?
Akili zake ni za nduli, Julius Nyerere alishatuelekeza, nduli wanatakiwa kupigwa
 
Aende zake huko chato akajenge lichuo lao la uongozi kama anataka mbona wakat baba yao akiwa hai hakumshauri ujenzi wa chuo cha uongozi leo ameliona kwa kuwa yupo nje ya mkate mtamu kakome kbsa kajaamaa haka tena hakafai.
 
Huu ulaghai wa hali ya juu unaofanywa na Polepole, alikuwa anapinga katiba mpya enzi ya mwendazake, alitumia muda mwingi kukata viuno akicheza mabolingo huku akijirekodi katika camera, alishuhudia na akawa sehemu ya tawala ya hovyo kabisa katika historia ya nchi hii,alikuwa sehemu ya tawala katili ya kiuwaji isiyojali demokrasia wala haki. Eti leo anahubiri shule ya uongozi.

Anatembea na jina la Rais wake mfukoni akiwa hana imani na Samia, anatembea huku nakule akishawishi wana CCM wamkubali mtu wake kisa alifanya kazi na JPM, na HPP alikuwa sehemu ya walioshinikiza SSH asichukue mamlaka, Mwenzie wa Kemondo katulia,yeye bado anaipima mamlaka ya nyumba kubwa, mamlaka ijibu mapigo kwa ukali wote

Namshauri huyo anayejazwa upepo na HPP asijiingize mkenge,ataisoma namba
Samia inatakiwa amshughulikie Polepole ipasavyo na haraka, apewe kesi ya Money laundaring akazae jela
 
Aende zake huko chato akajenge lichuo lao la uongozi kama anataka mbona wakat baba yao akiwa hai hakumshauri ujenzi wa chuo cha uongozi leo ameliona kwa kuwa yupo nje ya mkate mtamu kakome kbsa kajaamaa haka tena hakafai.
Kinafiki Sana kile kijamaa, wakati hule wa dikteta alikuwa anamsapoti kila kitu,
 
Mawazo hayapigwi rungu
Polepole ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Acheni chuki binafsi.

Shida ya Polepole ni moja tu, ni opportunist, lakini kwenye ishu ya kutoa maoni yake, hajakosea popote, ni haki yake
 
Mkuu umechokoza Sukuma gang and cdm...subiri matusi
 
Mawazo hayapigwi rungu
Polepole ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Acheni chuki binafsi.

Shida ya Polepole ni moja tu, ni opportunist, lakini kwenye ishu ya kutoa maoni yake, hajakosea popote, ni haki yake
Ni kweli, gharama ya demokrasia ni pamoja na kusikiliza wajinga na wanafiki.
 
Akiwa kwenye tume ya Warioba aliwahi kusikika akisema kuna chama bila msaada wa polisi hakiwezi kushinda uchaguzi. Je ameshafikia hiyo topic kwenye shule yake?
 
Back
Top Bottom