Sina hakika kwanini EAC hawajafanya harmonization katika hili, hata hivyo bado kuna mambo ya msingi nawe pia uyabainishe. 1. Je ushuru wa Barabara unakadiriwa kwa kutumia kigezo gani? kwasababu kama usemavyo ndivyo, kuna haja ya kujiuliza ukubwa wa athari kwa Barabara baina ya safari mbili (yaani kutoka Rusumo hadi Dar na kutoka Rusumo hadi Kigali). Nionavyo mimi magari ya Rwanda "yanaathiri" barabara kutoka Rusumo hadi Dar wakati yale ya Tanzania "yataathiri" barabara kutoka Rusumo hadi Kigali ambapo ni distance fupi (if am right). Hivyo ndiyo yaweza kuwa sababu ya kuweka tozo tofauti. Aidha sababu nyingine ni idadi ya magari yanayovuka kila upande (basing on revenue collection); kwa kuwa magari mengi ni kutoka Tanzania, kiwango kidogo cha tozo kinaweza kuleta makusanyo makubwa tofauti na magari yatokayo Rwanda kuingia Tanzania hayana budi kulipa kiwango kikubwa ili kuwa na significant revenue (kama siyo mengi).
Mkuu weka tofauti kando kaka, Hii ni business usifanye mchezo. Mwanzoni walikuwa wakitoza 150 USD per truck sasa wameongeza mpaka 500USD kwa magari ya TZ pekee, Ya nchi zingine wanachaji hiyohiyo 150usd. Sasa inaonekana hujui hali ipoje kaka.
Ikiwa kweli hali ndio iko hivyo, ni vema tuchujue charge kwa upande wa Rwanda/Kenya; Rwanda/Uganda na Rwanda/Burundi (ceteris paribus). Tukijua hivyo tutaweza kuona nini Tanzania inaweza kufanya. Na nmna mojawapo ni kutumia "US style"; kiburi cha Rwanda kinatoka Kenya, Mombasa Port na Trilateral cooperation lakini Kenya inauza Tanzania zaidi ya 50% ya mauzo yake yote EAC; hivyo namna rahisi ni ku-deal na Kenya kwa kumuanzishia mashrti magumu ya kuingiza bidhaa zake Tanzania (based on cost-benefit analysis). Hii itamlazimisha Kenya apeleke hoja EAC kwanini Tanzania imeweka masharti mapya na hapo ndipo Tanzania ita-lobby kupata maamuzi yatakayotengua tozo mpya ya Rwanda (Reverts all new rates imposed by any EAC country on specific dates before negotiating) .
Usiwe mwepesi mkuu, ngoja kwanza atupe info zaidi huyu murutongore kama yuko sahihi. Sioni kwanini Rwanda ilikuwa inataka kuwa na rate moja na Tanzania bilateral badala ya Regional? Na je vigezo gani havina budi kutumika kama tutafikia kuwa na equal rates wakati (huenda) magari kutoka kila upande yanatumia barabara umbali tofauti?
Toa maelezo zaidi acha unazi, Rusumo/Kigali-Rusumo/Dar how? Na je kwanini accomodating ya Kigali iwe bilateral badala ya Regional approach kama hiyo ndiyo hoja?
Mkuu salute nimependa uchambuzi wako. Tatizo sasa ni hao watendaji inakuwaje,
chama@ZeMarcopolo@Ritz hivi TISS haina kitengo cha ECONOMIC INTELIGENCY UNIT ambacho kinadeal na mambo ya business both domestic na international?