Zanzibar 2020 Siasa za Zanzibar: Hongera Dr. Mwinyi Kwa Ushindi wa Kishindo, Maalim Makamo wa I, Mteue Balozi Amina Salum Ally Awe Makamo wa II, Utoe Sare Sare Maua

Zanzibar 2020 Siasa za Zanzibar: Hongera Dr. Mwinyi Kwa Ushindi wa Kishindo, Maalim Makamo wa I, Mteue Balozi Amina Salum Ally Awe Makamo wa II, Utoe Sare Sare Maua

Mkuu Proved , kumsingizia mtu kuwa anatamani macho ya wakubwa, ni unajichumia dhambi bure tuu, nilichosema ni mimi huwa napenda macho fulani, na nayapenda tuu hayo macho na sio kuwatamani wenye macho hayo!.
Nitake radhi!.
P
..ooh!...samahani sana kama nimekukwaza.

...Embu niambie...Kuna uwezekano mtu ukapenda kitu chochote bila kutamani?
 
Sasa uchaguzi umeisha, life has to go on back to normal huku tukiendelea kuponya majeraha ya uchaguzi, pole sana kwa washindwa, na hongera kwa washindi.
Ndio tatizo lenyewe lipo hapo, ukishafanya magumagu na kujinyakulia madaraka kwa njia za panya maisha hayaendi mbele. Unaizungumzia 2025 kama ni kesho kutwa. Nashangaa sana kuona watu wakifiria kama hili suala ni la M.Seif binafsi.

Labda nikukumbushe tuu kwenye historia, CCM ni hao hao walikuwa wakienda na ASP. Walishindwa uchaguzi kabla ya uhuru, wakapindua kwa mkono wa Tanganyika. Unfortunately, maisha hayayakusonga mbele kama ulivyoatarajia. Ni miaka +50 sasa, bado tunajadili tunda la mapinduzi yale nalo ni muungano!

Kuna gharama yake kiongozi akipatiwa msaada wa kupata madaraka kwa njia za ghilba. Hatujaijua gharama ya Dr.Mwinyi kusaidiwa na Tanganyika, lakini historia inatuambia lazima kuna gharama yake. Lazima iwepo hakuna kitu kinapatikana bure, hususan Tanganyika inapowacha watu wake walioko karibu na mipaka na kujikita na visiwa vya Zanzibar. Inatuacha wengi bado midomo wazi!
 
Mayala mimi simjui lakini namuelewa anachosema ukimsoma haraka unaweza kudhani alichoandika ndio kieleweke hivyo inabidi kujiongeza kidogo. Sio kwamba yeye mjinga kiasi cha kuamini uchaguzi ni wa haki. kasema hii ndio mara ya kwanza katika history Zanzibar mtu kushinda 76% sote tunajuwa hakushinda na hata kama kashinda bahati kupata 51%. Anyway hili sio suala la uchaguzi kushinda ila naandika kwa herufu kubwa katiba inabadilishwa theluthi 3 kwa hisani imepatikana kitapita kipindi cha mpito miaka 20 mtu kutawala kisingizio hakuna mtu mwingine wa kuweka mambo sawa, wabunge wote wamechaguliwa na CCM sio wananchi, lazima umpigie magoti anayekulisha
 
Hongera sana Mwinyi. Hongera Sana CCM

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Mkuu Bayyo , huwezi kuzuia watu kusema, tena kwenye machungu, watu walioumizwa kwa ndani, wakisema ndio wanapunguza machungu, hivyo ni rukhsa kunitumia mimi kupunguzia machungu.
P
Kwanzaa umsenge.

Lá pili lá pemba halikuhusu.

Lá tatu hayo machungu mumeyasababisha nyinyi sasa pole ni ya nini?

Unafiiki wenu ubakie huko kwenu kwa watanganyika wenzako.


Dhulma mtailipa kwa njia yoyote lililobaki subir teuzi ufanye unyama zaidi kwasababu ndio asili yenu.
 
Wanabodi,

Kwa vile uchaguzi wa Zanzibar pia umesababisha vidonda na bado ni vibichi, damu bado haijakauka, hivyo naomba kuanza bandiko hili kwa a healing massage ya kuponya vidonda kwa kuungana na Watanzania wengine wote wapenda haki, amani na utulivu, kutoa pole kwa wahanga wa kilichotokea Zanzibar kwenye uchaguzi huu, ukiwemo umwakigaji damu, natoa pole kwa wote, na kama ni kweli kuna dhulma zozote zilizofanyika, then JAJI MKUU WA MAJAJI WOTE DUNIANI KWA KUTUMIA SHERIA KUU YA HAKI DUNIANI, THE LAW OF KARMA, will take care of this.

Sasa uchaguzi umeisha, life has to go on back to normal huku tukiendelea kuponya majeraha ya uchaguzi, pole sana kwa washindwa, na hongera kwa washindi.

Siasa za Zanzibar, natoa hongera kwa Dr. Hussein Mwinyi, kwa ushindi wa kishindo, cha kihistoria, haijapata kutokea toka Zanzibar izaliwe, ushindi wa zaidi ya asilimia 50%, siku zote uchaguzi wa Zanzibar matokeo huwa ni close range, lakini safari hii, ushindi wa 76% ni landslide ya funga kazi, na funga kalomo kwa vitimbakwiri vyenye maneno maneno kuhusu uchaguzi wa Zanzibar.

Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar yenye GNU, Maalim Seif Sharrif Hamad atakuwa Makamu wa I, wa rais, namshauri Maalim akubali uteuzi huo, kwa umri wake aliofikia, kipindi hiki kwake ni final finale, kwa uchaguzi wa 2025, kutahitajika damu changa, nashauri Jussa au Hamid apokee mikoba.

Japo kwa maoni yangu baada ya Dr. Mwinyi, mtu wa pili kwa u presidential material ni Prof. Mbarawa,
View attachment 1615747View attachment 1615748View attachment 1615749View attachment 1615750

Na rais Magufuli alimshauri Dr. Mwinyi kuchagua makamu toka Pemba, lakini kwa vile Makamu wa I ni Maalim Seif ni kutoka Pemba, then natoa wito kwa Dr. Mwinyi, amteue, Balozi Amina Salum Ally awe Makamu wa II, ili kutoa sare sare maua na makamu wa huku bara, Mama Samia Suluhu Hassan, tena sare ya Amina Salum Ally na Samia Suluhu Hassan, itakuwa ni sare inayoendana hadi macho!.

Nakuwekea picha 2, moja macho mawili na nyingine macho manne

Pasco
Rejea ya macho
IMG-20201024-WA0026.jpg


IMG-20201030-WA0006.jpg
 
Back
Top Bottom