Heading isomeke KUSIMAMISHWA na sio KUFUKUZWA, Kama barua unavoeleza
Kama una uelewa mpana juu ya haya mambo utakua unajua kwamba shule zote zinajiepusha na neno kufukuzwa Kwa sababu mwenye mamlaka ya kufukuza ni Bodi ya shule au kamati ya shule! Na kwa maana hiyo shule inauwezo wa kusimamiaha kwa siku kadhaa zosizozidi 90 kusubiri kikao Cha kamati au Bodi.
Hata hivyo yapo makosa ambayo yanatoa room kwa adhabu Kali kama hiyo.
Kwa barua hii ambayo haijataja hata makosa ya wanafunzi Bali imetaja makosa ya wazazi ambayo ni katika mchakato wa kisiasa Ila wkahusishwa walimu hakutoi uhalali wowote kuwasimamisha watoto Kwa sababu hakuna uhusiano wa Moja kwa Moja ukiacha ushahidi.
Soma barua inaelekeza ukawatafutie shule nyingine! Hiyo ni automatic dismissal!
Kiuhalisia agizio Hilo la Mkuu wa WILAYA ambaye namuita mjinga ni ukiukwaji wa Haki za binadamu wazi wazi na inafaa asasi za kiraia na viongozi wa dini pamoja na tume ya Haki za binadamu kuongilia kati, sababu Elimu ni Moja wapo ya Haki za binadamu kwa mujibu wa AZIMIO LA UMOJA WA MATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU! (UDHR)
Kama taifa haya sio mambo ya kufumbia macho sababu yanapotupeleka ni pabaya sana na matokeo yake kwa kizazi kinachokuja hayatahimilika.
Wakati wajinga wakishani wanalazimisha loyalty wenye hekima wanaona kinacholazimishwa ni uasi na chuki.
Chama kiache kujihusisha na uporaji wa Haki za binadamu kuanzia
1. Haki ya kuishi
2. Haki ya kupata huduma za jamii kama elimu.
Hatujui ni Haki ipi itaenda kuporwa soon!
Kukaa kimya ni kuficha moto uvunguni.