Siasa zimezidi The Law School of Tanzania. Hiki chuo kimulikwe!

Siasa zimezidi The Law School of Tanzania. Hiki chuo kimulikwe!

Disemba 10, 2015 Magufuli wakati akitangaza Baraza lake la Mawaziri alimteua Dk. Harrison Mwakyembe kuwa Waziri wa Katiba na Sheria nafasi aliyoishikilia mpaka 23 Machi 2017 alipobadilishiwa wizara na kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akijaza nafasi ya Bwana Nape Nnauye. Shule ya Sheria Tanzania (LST) ipo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria.

Malalamiko juu ya usahishaji wa mitihani na utoaji matokeo wa LST kuwa mbovu hayajaanza jana, ni ya muda mrefu toka tu shule hiyo ilipoanzishwa mwaka 2008. Pindi alipokuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mwakyembe alikuwa akiisimamia shule hiyo na hata kufanya mazungumzo na watendaji wake hata hivyo hakuwahi kutoa uamuzi wowote juu ya mamalamiko hayo, tafsiri inayoweza kusemwa ni kuwa aliyapuuza. Mfano tarehe 22 Februari 2017 alitembelewa na makamu mkuu wa Chuo, Lukumay na viongozi wengine na kufanya mazungumzo wayajuayo wao ama labda walijitetea juu ya mamalamiko ya wanafunzi na akayaamini na kutochukua hatua, angalia hapa Law schoool wamtembelea dkt Mwakyembe ofisini kwake mjini Dodoma

Kumteua Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati itayochunguza malalamiko ambayo hakuyachukulia hatua ama ambayo aliyapuuza wakati wa uongozi wake wa Wizara sio jambo sawa. Kwanza tayari mtu huyu ana mgongano wa maslahi, maana anachunguza kitu ambacho anakijua tayari kwa kuwa malalamiko juu ya LST sio jambo jipya. Mheshimiwa Waziri Ndumbaro, tafadhali mteue mtu mwingine asiye na mgongano wa kimaslahi awe kiongozi wa kamati hiyo, Mwakyembe hastahili sio tu kuwa Mwenyekiti bali hata kuwa mjumbe wa kawaida wa Kamati hiyo.

Pichani ni Mwakyembe akiwa pamoja na Kina Lukumay ambao kimsingi ndio
Screen Shot 2022-10-14 at 3.08.29 PM.png
wanaotuhumiwa kuonea
 
Disemba 10, 2015 Magufuli wakati akitangaza Baraza lake la Mawaziri alimteua Dk. Harrison Mwakyembe kuwa Waziri wa Katiba na Sheria nafasi aliyoishikilia mpaka 23 Machi 2017 alipobadilishiwa wizara na kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akijaza nafasi ya Bwana Nape Nnauye. Shule ya Sheria Tanzania (LST) ipo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria.

Malalamiko juu ya usahishaji wa mitihani na utoaji matokeo wa LST kuwa mbovu hayajaanza jana, ni ya muda mrefu toka tu shule hiyo ilipoanzishwa mwaka 2008. Pindi alipokuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mwakyembe alikuwa akiisimamia shule hiyo na hata kufanya mazungumzo na watendaji wake hata hivyo hakuwahi kutoa uamuzi wowote juu ya mamalamiko hayo, tafsiri inayoweza kusemwa ni kuwa aliyapuuza. Mfano tarehe 22 Februari 2017 alitembelewa na makamu mkuu wa Chuo, Lukumay na viongozi wengine na kufanya mazungumzo wayajuayo wao ama labda walijitetea juu ya mamalamiko ya wanafunzi na akayaamini na kutochukua hatua, angalia hapa Law schoool wamtembelea dkt Mwakyembe ofisini kwake mjini Dodoma

Kumteua Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati itayochunguza malalamiko ambayo hakuyachukulia hatua ama ambayo aliyapuuza wakati wa uongozi wake wa Wizara sio jambo sawa. Kwanza tayari mtu huyu ana mgongano wa maslahi, maana anachunguza kitu ambacho anakijua tayari kwa kuwa malalamiko juu ya LST sio jambo jipya. Mheshimiwa Waziri Ndumbaro, tafadhali mteue mtu mwingine asiye na mgongano wa kimaslahi awe kiongozi wa kamati hiyo, Mwakyembe hastahili sio tu kuwa Mwenyekiti bali hata kuwa mjumbe wa kawaida wa Kamati hiyo.

Pichani ni Mwakyembe akiwa pamoja na Kina Lukumay ambao kimsingi ndio View attachment 2386996wanaotuhumiwa kuonea

Umedadavua vyema.

Muhimu ni kuendeleza mapambano katika fronts zote.

Kupigania haki hakujawahi kuwa rahisi au bila gharama.
 
Mwananchi
https://www.mwananchi.co.tz › kitaifa
Majaji wakaa kando uchunguzi mitihani ya mawakili

5 hours ago — Timu iliyoundwa na Chama cha Majaji Wastaafu (Tarja) kuchunguza kiini cha kufeli kwa kiwango kikubwa kwa watahiniwa ....

Timu iliyoundwa na Chama cha Majaji Wastaafu (Tarja) kuchunguza kiini cha kufeli kwa kiwango kikubwa kwa watahiniwa katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST) imejitoa kufanya kazi hiyo na kuiachia timu iliyoundwa na Serikali....
Jitihada mbalimbali za kupata ukweli wa kadhia hii zinakuwa zinazimika haieleweki ni kwa sababu gani haswa:

IMG_20221024_074306_021.jpg


Ni coincident au mizengwe?
 
Jitihada mbalimbali za kupata ukweli wa kadhia hii zinakuwa zinazimika haieleweki ni kwa sababu gani haswa:

View attachment 2396062

Ni coincident au mizengwe?
Mizengwe. Serikali inataka ifanye kazi yenyewe, sababu walizotoa majaji hazina mashiko kwa kuwa kukinzana kwa majibu (kama kupo) kutakuwa ndio chachu yenyewe ya kupata ukweli.

Wao majaji waliunda kamati ya uchunguzi, lakini serikali imeunda kamati ya kufanya tathmini, ni mambo mawili tofauti.

Siku 30 za Kamati ya Mwakyembe zinaisha tarehe 12.11.2022 ajabu wao Kamati siku za kupokea maoni kwa njia ya maandishi wameweka 7 tu, wangefanya hata iwe siku 18 na wao watumie siku 12 kuchambua maoni na kuandaa taarifa.
 
Mizengwe. Serikali inataka ifanye kazi yenyewe, sababu walizotoa majaji hazina mashiko kwa kuwa kukinzana kwa majibu (kama kupo) kutakuwa ndio chachu yenyewe ya kupata ukweli.

Wao majaji waliunda kamati ya uchunguzi, lakini serikali imeunda kamati ya kufanya tathmini, ni mambo mawili tofauti.

Siku 30 za Kamati ya Mwakyembe zinaisha tarehe 12.11.2022 ajabu wao Kamati siku za kupokea maoni kwa njia ya maandishi wameweka 7 tu, wangefanya hata iwe siku 18 na wao watumie siku 12 kuchambua maoni na kuandaa taarifa.

Hii nchi ni ngumu sana agenda kuu ni ujanja ujanja na wizi wizi tu.

Maoni kuhusu Law School, Mzengwe au ajali?

Haipo nia njema dawa yake ni kujiandaa kwa option zero.
 
Back
Top Bottom