Siitazami ajali ya ndege kama wengi mnavyoitazama, yawezekana kuna makubwa nyuma yake

Siitazami ajali ya ndege kama wengi mnavyoitazama, yawezekana kuna makubwa nyuma yake

Nimekusoma naona ni kama vile unataka kuaminisha kwa hisia zako washindani wa Precision wanahusika kwenye hii ajali, jambo ambalo siliafiki, ajali mara nyingi huwa haichagui pakutokea.

Masuala mengine kama muda wa uokoaji kuwa mrefu, na kufungia uwanja hapo nakubaliana nawe, naona kama Majaliwa alikurupuka jambo litakalosababishia usumbufu abiria na watumiaji wengine wa uwanja wa Bukoba.

Kuhusu machozi ya mtendaji/bosi wa Precision yanaweza kuwa ni hisia za kibinadamu tu, wala sio sababu za kibiashara kama unavyodhani, uhai wa mwanadamu una thamani zaidi ya ushindani wa kibiashara, usiusemee moyo wa mtu.
Ndio tuvute ndege kama kokoro .... Aseee hii nchi hiiii.... Yule dogo mjsiriamali wa dagaa ameokoa 23 Kwa vifaa duni na elimu duni ya uokoaji .... Lakini utasikia anapongezwa mkuu wa mkoa na mapambio na kusifu jazz band.....
 
britanicca nimekuelewa na kukusikia unachotaka kufikiri nje ya box , yote kwa yote mtoa wazo na mkubali wazo hata mtekeleza wazo Mungu anamuona na uzao wake hautakuwa na amani Duniani.

Mungu anisamehe nimejikuta naomba Maombi mabaya, najikuta nalia japo sijui nalilia nini inamaana hata ile huruma kidogo tu kama punje ya tumbaku haipo😭😭😭😭😭😭😭
 
Ndege kubadili uelekeo, pilot aliabort landing 1st time kutokana na hali ya hewa, inawezekana alivyorudi 2nd time akaona hawezi kutoboa kutokana na hali mbaya ya hewa na akaamua emmergency landing kwenye ziwa.

Kupunguza speed kwa ajili ya emmergency landing na kama kuna upepo mkali ujue analack propelling force hivyo ni rahisi kuelea na kugeuzwa na upepo..

Ni fikra binafsi za kimtaa+idea kubwa kwenye machuma.
 
Na mimi nichangie japo sina uelewa sana na usafiri wa anga kwa kuwa mimi nimezoea kupanda malori ili kupunguza gharama za nauli, kwenye ndege si kuna kitu kinachorekodi mawasiliano kati ya marubani na waongoza ndege kwa nini wasitumie hayo mawasiliano tuweze kujua ukweli kuhusu kutokea kwa ajili. Kwa hali kama hii si tutaendelea kuwa hivi mpaka lini inatakiwa jamani tubadilike viongozi kufumbia mambo yanatupeleka kubaya viongozi kila kitu ni kawaida kwa ajili kulinda ajira zao na matumbo yao ifike muda na sisi watanzania tubadilike kila kitu kinachotokea tunachukulia kawaida kama hakituhusu. Nje ya mada kidogo angalia mitandao wanajipangia tu kuhusu vifurushi(bundle) upandishwaji wa bei ya bidhaa lakini sisi kama raia tunaishia tu kulalamika lakini hatuchukui hatua zozote tutakuaga tunaonewa mpaka lini. Angalia kama hili suala la ajali yaani ndege inavutwa kwa kamba hata kama kweli ajali haina kinga kweli hivyo ndo vifaa vya uokoaji ifike muda tuhoji kwa uwazi na watu wawajibishwe. Haya mambo yanatia hasira sana
 
Kuna taarifa juu ya watu 2 kuzidi ndani ya ndege??

Kuna Bomba unaweza shika ndani ya ndege kama daladala za RANGI tatu mbagala??
Hapana, hao wanaosemekana kuzidi ni kutokana na rekodi ya idadi ya abiria waliosafiri siku hiyo kwenye ndege hiyo lakini uwezo wa ndege ni zaidi ya idadi hiyo ya 45
 
NAULIZA TU HIVI WEWE NDO BRITANICCA WA TWITTER? MBONA WA TWITTER KAMA KALEGEA NA KUJIPENDEKEZA KWA SERIKALI NA WEWE NI TOFAUTI NA CONTENTS ZAKE ? AU?
 
Back
Top Bottom