Sijajutia kabisa safari yangu ya Morogoro kuangalia maeneo (ardhi) ya uwekezaji

Mzee omba Mungu sana kwenye hiyo shughuli, kusingekuwa haya mambo ya kishenzy tungekuwa mbali sana!

Hivi road ya handen tokea Moro imeisha? Muhimu sana hiyo!
Halafu unawasikia wapuuzi fulani, wasomi uchwara wanakwambia 'Uchawi haupo' eti ni mambo ya kusadikika tuu..nami huwa naishia kusema tu ''Inhiiiiiiiiii !!''.
 
Mkuu Gairo ni best sana kwa kilimo cha kumwagilia , lakini pia kilimo cha seasonal kinakubali kuna vijiji huko milimani ukiiacha barabara ya kuu ukaingia ndani ndani huko lubeho , mandege mpaka njungwa maharage na mahindi yanakubali na wana maji mazuri sana !
Karibu Gairo , nimejenga na nimewekeza huko japokua naishi Dar es Salaam .

Ni sehemu ambayo kiukweli ukituliza kichwa unafanya vizuri !!
Kiufupi Morogoro ni mkoa wa fursa kwa wachapakazi.
Wilaya nisiyoipenda kwa mkoa wa Morogoro ni Ifakara maana kuna joto kama kwa shetani
 
Ahsantee sana mkuu. Bado narudi morogoro nilipapenda mvomero na kilosa ni pazuri sana.japo sijaenda sehemu nyingi hapo Gairo Tyr nimechukuapo kaeneo kakuanzia. Siyo kurudi hivihivi. Tu
 
Kweli nchi yetu Mungu ameibariki sana ni sisi tu tunakosa hamasa pia serikali ndio ingewekeza maeneo kama hayo kupitia BBT na project nyingine nyingi sasa hivi tusingekuwa tunaletewa mahindi ya msaada na ngano kutoka Ukraine au Russia.
 
Mimi nimesoma Dakawa high school kipindi hicho ikiwa mchanganyiko na sasa ni girks,vipi kuhusu Doma karibu na mikumi panafaa kwa kilimo?
 
Ahsantee sana mkuu. Bado narudi morogoro nilipapenda mvomero na kilosa ni pazuri sana.japo sijaenda sehemu nyingi hapo Gairo Tyr nimechukuapo kaeneo kakuanzia. Siyo kurudi hivihivi. Tu
Hapo uliposema kuna pumba nyingi na za bei rahisi ndio pa kutia kambi ya kufuga nguruwe na kuku , unayanenepesha kwa wingi unapakia kwenda kuuza Dar ,aisee bonge la fursa mkuu
Chakula cha kuku na nguruwe hasa pumba maeneo mengi ni ghali sana
Nitakucheki pm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…