Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

inatakiwa ufahamu mzee dingi anaishi kwa mchongo, km kwenda kwake anafanya mzunguko kiasi hiko na kubadili dala dala hizo ndio arudi kwake hivi anaweza kuweka hela ac moja kweli??

au unasoma story kutafuta makosa sio kujifunza mkuu,.
shida ujuaji mwingi watu, soma enjoy kula kona...yaani mtu anasoma hadithi utafikiri anaenda jibu pepa ya necta...

Yaani Mtendaji Apostle alitakiwa awapotezee tu.
 
Kwa madawa hayo najua kabisa siwezi ni kakwepa kutapeliwa, kama mzee DINGI kubwa la utapeli alienda kutoa hela ATM na vidawa vyake . Je, kwa mti mkavu itakuwaje?
 
16th Portion:


... Usiku huo nilitafakari mambo mengi sana. Ila jambo kubwa ni kitendo cha wale washirika wangu wote kunipa false direction ya sehemu wanazo ishi. Tokea nilivyoamua kujiunga nao rasmi, Mzee Dingi nilidhani amehamia Mbagala au maeneo ya huko, ila kumbe sivyo. Tafsiri iliyonijia, hata wale wengine nao nikaanza kuwa na mashaka na makazi yao. Kwa ufupi, wote walijua Mimi napatikana Tabata, ila wao sijui wanapokaa. Na kibaya zaidi, Mzee Dingi anapajua ninapokaa. Ule mshtuko alioupata baada ya kuniona mitaa ya kwake, ulinipa tafsiri ya hatari. Hii kwangu haikuwa nzuri, nikaadhimia kuhama. Nikampigia dalali anifanyie mpango kesho nipate chumba.

******* ****** ****** *****

Palivyokucha, nikaanza pilika pilika na dalali wangu. Baada ya kuzunguka nyumba kadhaa, hatimae nikapata chumba maeneo ya Tabata Segerea, kwa Bibi pale (kwa wale waliosoma story ya fumanizi la mama mwenye nyumba, nyumba yenyewe ni hii). Nilidhamiria kukaa pale kwa miezi michache, alaf ndio niende eneo jingine nje ya Tabata nitakalokaa kwa kutulia.

Nilitafuta usafiri wa kunihamisha siku hiyo hiyo. Mama mwenye nyumba hakuwepo, nilifanya kumpigia na kumtaarifu kwa njia ya simu. Alisikitika kuhama ghafla, akataka kujua kama kuna tatizo, ila nikamtoa wasi wasi nimepata kazi sehemu, hivyo nataka nihamie karibu na nitakapofanya kazi, ili kupunguza gharama za usafiri. Huyu mama nilishakaa kwenye nyumba zake mbili. Ile ya kwanza tulikuwa wapangaji tupu, hii ya pili ambayo nahama, yeye ndio alikuwa anaishi hapo.

Akaniuliza vipi kuhusu kodi yangu iliyobaki, maana ilikuwa imebaki miezi mingi. Nikamwambia asiwe na wasi, maana nimehama kwa hiari yangu, basi kodi nasamehe.Tukamalizana hivyo. Nikahamisha vitu vyangu.

Nilivyoingiza vitu vyote ndani ya makazi yangu mapya, sikutaka hata kuvipanga vizuri. Nilifunga Kitanda tu.

Baada ya hapo, nikaona niende bank kuweka ile hela iliyobaki, toka kwenye hela niliyochukua kwa Mzee Dingi, sikutaka kuendelea kukaa nayo ndani.

Nikajiandaa kama kawaida ili nitoke. Unajua ngozi ya uso wangu ni ya mafuta, nikipaka lotion, walau kuna unafuu. Ila Sasa kile kitendo cha kuwa naongezea na mafuta ya nazi juu yake, kikawa kinaleta changamoto, nikipigwa na jua kidogo, uso unang'aa kama kitumbua, Yani nikiwa kwambali unajua kabisa Analyse yule anakuja. Hiyo hali ikawa inaniboa, ikabidi nibadili namna ya kupaka yale mafuta ya nazi. Nakumbuka mtaalam aliniambia natakiwa kuyapaka kidogo tu maeneo ya usoni na viganjani. Nikaanza kuwa nayapaka kidogo chini ya mdomo wa chini, alaf na sehemu ya ndani ya masikio. Yani mtu ningekutana nae, kwa haraka haraka angeweza kuhisi nimekosea tu kwenye kujipaka, au pengine hata asing'amue, maana nilikuwa nayapaka kidogo sana.

Tokea niwe na yale mafuta na kile kihirizi, route za mjini hakuna siku niliyowahi toa hela yangu kumpa konda. Tena wale ndio wepesi kinoma, ukimgusa bega kidogo, mtapiga story hadi mwisho wa safari. Alaf nikishuka wananiaga kama vile tunajuana miaka mingi sana.

Leo hii nikisikia mtu katapeliwa kimazingara, siwezi mlaumu kabisa. Akili inakuwa sio yake muda ule. Baadae sana ndio ufahamu unamrudia.

***** ****** ***** ** **

Nilitoka mpaka bank, NMB tawi la Mandela. Pale pale alipowithdraw hela Mzee Dingi. Nilichagua tawi lile, maana ndio lilikuwa karibu na Mimi.

Baada ya pale, sikutaka kulala kule kwangu siku ile. Niliadhimia kwenda kulala kwa Shani. Hivyo nilirudi gheto kwangu na kuchukua kibegi changu cha kazi, na nguo nitakazo vaa hiyo kesho siku ya dili, pia nikapitia sehemu na kumnunulia vitu kadhaa vya kupika ambavyo najua angehitaji. Kisha nikaelekea kwake.

Nilivyokuwa mazingira ya pale kwake, walau mawazo ya kazi ya kesho yalipungua. Naweza sema, niliyasahau kwa muda, au tuseme alinisaahulisha kila kitu.


** ** ***** *****

Asubuhi niliamshwa na simu toka kwa Mzee Dingi, akaniambia niwahi kusogea meeting point, ili niweze kuondoka na wale wazee wengine.

Nikajiandaa kama kawaida, Kisha nikapaka yale mafuta. Sikutaka hata kusubiria chai, japo Shani alisisitiza sana.

Ilitakiwa nikutane nao pale mataa ya ubungo. Nilichelewa kidogo, nikawakuta tayari wamefika, wananisubiria Mimi tu. Nikajitosa kwenye gari ya yule Mzee KY, safari ikaanza.

Kila nikiwa na wale wazee, nilikuwa napatwa na mawazo ya kujilaumu sana. Nilimpotezea Mzee wa maana ambae angeweza kubadili maisha yangu, ila nimejikuta naangukia kwenye himaya ya wazee wa ajabu. Nilipata funzo kwa njia ngumu sana, kwamba usiharibu maisha yako kwasababu ya watu wengine. Maana utaacha mambo yako, kwa ajili yao, ila ikifika wakati wa wao kufanya yao, hawatojiuliza hata mara mbili, watakupotezea bila kujali ulijitoa vipi kwao au ulikuwa na mchango gani.

Safari nzima ilitawaliwa na ukimya. Na ungetuona tulivyokuwa serious na tumependeza, ungeweza hisi ni wana familia tunaenda ukweni kutoa mahari. Maana kijana nilikuwa peke yangu, nimezungukwa na wazee tu.

Ndani ya ile gari tulikuwa watu wanne. Mimi, Mzee KY, mwanasheria feki na Mzee Kidevu. Mzee Dingi yeye alitakiwa kuja na yule mlengwa wetu.

Tulisogea hadi eneo la tukio. Gari ikaenda kupack mbele zaidi, kwenye nyumba fulani kuu kuu isiyokuwa na uzio. Mzee KY akasalimiana na majirani pale, kisha akatukaribisha ndani, na kutwambia kuwa pale ni kwake.

Yani jamaa alitafuta na nyumba kabisa, na hata majirani wanamjua na wamemzoea. Kiufupi alikuwa kajipanga. Nilistaajabu sana, huyu Mzee ni mtu wa aina gani?

Wote kwa pamoja tukatulia, huku tukisubiria signal ya Mzee Dingi.

Mzee KY akatukumbushia tena umuhimu wa kila mmoja kuplay part yake bila kutetereka.

Katika zile siku kadhaa nilizokuwa nakutana nao kupanga hii plan, niligundua kuwa Mzee wa KY ndiye aliyekuwa kiongozi wa kile kikosi. Na hata dili nyingi kubwa, yeye ndio alikuwa anatengeneza plan nzima, namna gani iwe, na yupi achukue nafasi ipi.

Tukiwa pale kwenye makazi feki ya Mzee KY, Mzee Dingi akatuma msg ; "Get Ready"

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
 
Sorry guys portion ya leo imekuwa fupi, kutokana na mazingira niliyopo. Nimejitahidi tu walau kuandika ili nisipitishe siku bila kupost, kama nilivyoahidi. Next portion nitafidia.

Nipo mazingira tight. πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™
 

Mbona tushafuturu jamani hujashusha
 
Sorry guys portion ya leo imekuwa fupi, kutokana na mazingira niliyopo. Nimejitahidi tu walau kuandika ili nisipitishe siku bila kupost, kama nilivyoahidi. Next portion nitafidia.

Nipo mazingira tight. πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™
Upo kwa shaniπŸ˜‹
 
Apostle kama apostle[emoji28]
 
Sorry guys portion ya leo imekuwa fupi, kutokana na mazingira niliyopo. Nimejitahidi tu walau kuandika ili nisipitishe siku bila kupost, kama nilivyoahidi. Next portion nitafidia.

Nipo mazingira tight. [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
Usjali shukrani sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…