Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

18th Portion:

Baada ya kuachana na Mzee Dingi, nilirudi gheto direct. Siku hiyo hiyo mida ya jioni, yule mama mstaafu akanipigia simu;

Mstaafu: "Hujambo mwanangu?"
Analyse: "Mzima mama, shikamoo"
Mstaafu: "Marahaba. Vipi utakuwepo mjini mpaka lini?"
Analyse: "Kuna vitu naweka sawa, vikikamilika nitaondoka. Inaweza ikawa Jumatatu au Jumanne"
Mstaafu: " Tunaweza kuonana kabla hujaondoka?"
Analyse: "Sawa hakuna shida, nadhani Jumatatu jioni nitakuja".


Baada ya kuongea na yule mstaafu, jioni hiyo hiyo, Mzee KY nae akanipigia simu, kuniambia tuonane siku ya Jumatatu jioni bila kukosa, ili tuweke sawa mambo kadhaa. So, ndani ya siku moja nikawa na appointments mbili, na zote jioni.

Wa kwanza kuonana nae ni Mzee KY, tulikutana mida ya saa kumi kumi.

Mzee KY: "Umeshaongea na yule mama au kuonana nae tokea ufike mjini?"
Analyse: "Hapana, kwanini?
Mzee KY: "Ulimwambia chochote labda kuhusu huu mpango?"
Analyse: "Hapana, vipi kwani?"
Mzee KY: "Oky Vizuri, sasa shika hizi hesabu" (akatoa hela na kunipa).

Nikahesabu, zikafika laki 3 na nusu. Nikamuuliza za nini hizi?

Mzee KY: "Huo ndio mgao wako, kwenye ili dili haupo tena"

Nikabaki nimeshangaa, sipo Kivipi?. Maana kama sipo basi dili limekufa, ila yeye mbona anaongea as if dili bado lipo?.

Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu, akaniambia "Wewe ulikuwa plan A, haikuwa plan pekee. Kwahiyo kama nilivyokwambia, naomba ukae pembeni, dili litaenda bila uwepo wako. Na usije kumwambia chochote yule Mama"

Nikabaki na mwangalia tu. Hapa ndio alikuja kunipa maelezo ambayo nilikuja kuhitimisha kuwa, uwepo wangu kwenye lile dili haikuwa coincidence, kila kitu kilikuwa planned. Aliifahamu connection yangu na yule mama, na dhumuni la kunifanya Mimi kuplay role ya mwenyekiti, ili niweze kugain trust ya yule mama Kwa urahisi. Na hata kile kitendo cha Mzee Dingi Kuni unblock na kunitaka nipige nao kazi, yote ilikuwa ni maandalizi ya ili dili. Halikuja ghafla kama nilivyodhani. Baadhi ya maelezo aliyonipa, ndiyo niliyaelezea jana. Japo kuna mengine niliyaelezea jana, ila yeye alikuja kuniambia mbeleni kabisa wakati dili limeshafanyika.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, tukaagana. Sikuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kule kwa mstaafu, ikabidi nielekee kule.

Nikiwa zangu mdogo mdogo nishakaribia kwa yule, Sina ili wala lile. Kumbe Mzee KY alikuwa ameniungia tela. Sikujua kama dhamira yake ilikuwa kupajua ninapoishi au alitaka kujua nitaelekea wapi baada ya sisi kuachana pale kwenye ile Pub. Naingia tu kwenye ile nyumba, na yeye huyu hapa. Kwa haraka haraka, mtu angeweza kuhisi kuwa tulikuwa tumeongozana wakati tunaenda pale.

Nilishtuka kumuona, japo sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia yeye kuwa pale. Yule Mama mstaafu alipotuona wote alifurahi sana;

Mstaafu: "Naona watu muhimu mmeamua kunijia kwa pamoja, karibuni sana"
Analyse: "Asante sana"
Mzee KY: "Kijana alinipigia simu niungane nae kuja kukuona. Vipi za tokea siku ile?
Mstaafu: "Salama tu, Tunamshkuru Mungu uzima upo kama unavyotuona"

Kisha akanigeukia Mimi;

Mstaafu: "Karibu tena nyumbani, ila this time karibu kama mwenyekiti"

Aliniambia hayo maneno huku anacheka, Mzee KY nae akacheka kidogo. Tukaingia na kukaa sebleni kwake. Maongezi yote kayatawala yule mama tu. Kuna muda akaingia chumbani huko, kisha akatoka na hela;

Mstaafu: "Nilikwambia nitakurudishia hela ya Kodi uliyoacha, chukua laki mbili yako. Sitaki dhulma Mimi, najua kijana ndio kwanza unaanza kujijenga".

Mzee KY akamakinika kuona nitafanya nini. Binafsi nikaamua kuzikataa zile hela;

Analyse: "Hapana mama, nilihama kwa hiari yangu hii hela wala sio deni kwako"
Mstaafu: "Chukua mwanangu, hii haiusiani na kule kusainishiana, maana kule najua huwezi kuniangusha. Nakupa kama kijana wangu tu".

Unajua siku zote wakati nakua, kuna methali ilikuwaga maarufu sana.

"Sikio la kufa halisikii dawa"

Ukikanywa, usiposikia lazima uambiwe. Siku zote nilikuwa naichukulia kama methali tu, lakini in a real sense kwa mara ya kwanza nimekutana na ilo "Sikio la kufa". Unajua ili umuokoe mtu anayezama, sharti awe mtulivu vinginevyo mtazama wote. Au la, basi mpe kijiti, akishike umvute. Sasa huyu mama kila nikimpa kijiti, anakikataa. Kimoyo moyo nikajisemea atajijua mwenyewe.

Analyse: "Usijali mama, hiyo hela wewe Kaa nayo. Nimeondoka kwa amani kabisa, nikiichukua nitajisikia vibaya".

Akabaki na hela yake. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Mzee KY akaomba niwapishe waongee kidogo. Sikuwa na namna, nikatoka zangu nje, wakaongea mambo yao kwa takribani nusu saa au dakika arobaini na tano. Baada ya hapo Mzee KY akatoka nje, tukaondoka wote.

Baada ya kutoka pale, akatafuta sehemu. Akaniweka kikao tena;

Mzee KY: "Sikia kijana, hivi unaweza kukadilia gharama kiasi gani imetumika kuandaa Ili dili?".

Ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu akaendelea tena;

"Mlivyokuja kule site, uliwaona wale majirani niliosalimiana nao?. Wale wote nimetoka nao huku. Uliwaona wale watu wanaolima pale?. Sijui hata wanalima nini, ila nao nimewaweka Mimi."

Akaendelea;

"Dili lifanikiwe au lisifanikiwe, hao wote lazima wapate hela yao. Sasa hebu niambie, lisipofanikiwa hela za kuwalipa zinatoka wapi?"

"Kuna watu huwezi kuwasaidia hata ufanye vipi, they are destined to lose. Hata ukisema umuache na hela zake akanunue eneo halali, still zile hela ataenda kuzifukia chini akitegemea zitachipua, ila ataambulia hasara. Najua hukuchukua ile laki mbili yake, sio kwamba huitaki au unamuonea huruma, bali you feel guilty. Nitakupa Mimi ile laki mbili, soon after dili kufanikiwa, ila for now naomba usinizibie njia, maana siwezi elezea nitakachokufanya. Umenisikia..........?'' Akataja jina langu halisi.

Nikashtuka, amelijuaje jina langu?.

Mzee KY: "Wote mliopo kwenye Ili dili hakuna nisiyemjua, kuanzia anapokaa au sehemu zake za kwanza kukimbilia hapa mjini, kwahiyo kabla hujafanya jambo utakalokuja kulijutia, ni heri ujifikirie mara mbili"

Nikabaki nimeduwaa tu Kwa muda, sielewi what next. Akaniambia, "Huna haja ya kuendelea kubaki hapa, wahi ukapange vitu kwenye makazi yako mapya, japo nakushauri hama". Hakusubiria jibu langu, akaondoka.

So, he knows me well?. Why nihame wakati ndio kwanza nimehamia au kuna msala unanisubiria? Wazo likanijia, kwanza yule mstaafu tumejuliana mjini hapa hapa, atajijua mwenyewe, ngoja nijihangaikie Mimi.

Nilivyofika ghetto, Yale maneno ya Mzee KY kuwa nihame pale, yakawa yananijia. Nikajikuta njia panda, nipange vitu au nijiandae kuhama?. Ila nimetoka kulipa Kodi ya miezi 6 siku chache tu zilizopita, nahamaje? Mbona ntakuwa nafaidisha wenye nyumba?. Lakini taswira ya Mzee KY ikawa hainipi picha nzuri ya yajayo. Akili ikaniambia nisipange vile vitu, nihame.

Nikampigia simu mwenye nyumba, kumuomba kesho tuonane kama ataweza. Akakubali.

Asubuhi nilivyoonana nae, nikampanga kuwa nimepata dharura natakiwa kusafiri haraka nje ya mkoa, anirudishie hata nusu kodi. Akanijibu "Mwanangu Cha kukusaidia hapa, labda nikuhifadhie vitu vyako kwahiyo miezi 6 utakayokuwa unapambana na hiyo dharura yako"

Nikaona hapa siwezi ambulia hata mia, cha zaidi nitapoteza muda tu kumbembeleza.

Kipindi Mimi nawaza namna ya kuhama pale. Mzee Dingi akanipigia simu na kuomba tuonane.

Nikafikiria huyu nikutane nae maeneo yapi?. Kipindi kile maeneo ya Tabata kuna mashindano ya mpira wa miguu yalikuwa yanaendelea. Viwanja vilivyokuwa vinatumika ni kile Cha Sigara na cha Tabata shule. Nikaona option ya Tabata shule ndio sahihi, maana ni mbali kiasi na ninapoishi. Lakini sababu nyingine iliyofanya nisione shida kukutana nae Tabata, ni kwavile nilikuwa natarajia kuhama.

Nikamwambia tukutane Tabata shule. Mzee Dingi akagoma, na hii ni kwavile pale ni karibu sana mitaa anayoishi yeye. Nilivyóona bado anakomaa tuchange location, nikamwambia basi sitaki kuonana na wewe. Endelea na mishe zako.

Nilipata ujasili wa kumwambia vile kutokana na sababu Kuu mbili, kwanza kwenye dili lao sipo tena, alafu pili sijui anataka tuongee nini. Alivyoona nimekataa kuonana nae, hakuwa na choice zaidi ya kukubali tukutane maeneo yale.

Mida ya jioni nikasogea pale Tabata shule. Mzee Dingi alikuwa ameshafika kabla yangu. Mara zote ambazo tumekuwa tukikutana, vikao vilikuwa vinafanyikia either bar, pub or kwenye mgahawa. Ila this time hakutaka tukutane maeneo hayo. Akapendekeza tukutane kwenye yale majengo ya shule ya Kijapan (kuna shule ilijengwa na Wajapani maeneo yale). Nikajiuliza mara mbili mbili, why kachagua kule?. Ila kimoyo moyo nikajisemea akileta za kuleta, nitamfumua. Hasira zangu zote ziishie kwake.

Akanielekeza alipokuwa amesimama, nikamfata. Kufika pale, navikuta vizee vyote vitatu vipo. Mzee Dingi, Mzee Kidevu na Mwanasheria feki. Nikajiuliza vinanitakia nini?.

Nilivyowaona, sura zao zote ziliakisi shari, ila sikuwa na namna zaidi ya kuwasogelea. Zikapigwa story za hapa na pale, lakini Unaona kabisa hapa kuna jambo litatokea muda sio mrefu. Na Mimi kwa hasira nilizokuwa nazo, nikawa nasubiria kwa hamu ilo jambo litokee. Kwa jinsi tulivyokuwa tumejipanga, Mzee Kidevu alikuwa nyuma kidogo upande wangu wa kushoto, alafu mwanasheria feki na Mzee Dingi walikuwa mbele, tupo face to face. Tukiwa tunaendelea kuongea upande, kwa ghafla sana yule Mzee Kidevu akanirukia horizontally na kunipiga kichwa cha mbavu. Ni kitu ambacho sikuwa nimekitarajia, nikajikuta nayumba yumba. Kitendo cha kuyumba yumba, wale wazee wote wakanivamia kwa pamoja.

Nikajisemea hapa ndio nilikuwa napataka, ngoja nipunguze hasira zangu. Unajua Kwa jinsi nilivyokuwa nawakadiria, nilihisi dakika 10 nyingi wangesanda kwenye lile valangati. Ila yule Mzee Kidevu sijui hata anakulaga nini aisee, maana kuna muda nilimrushia ngumi, lengo nimpige shingoni, ila at the same time nae akanirushia ngumi. Ngumi kwa ngumi zikakutana, nilipatwa na maumivu kiasi kwamba nikahisi nimepiga mti. Kibaya zaidi yule Mzee hata akuugulia chochote, ndio kwanza anakuja tu.

Kipindi hicho chote, Mzee Dingi na Mwanasheria feki wameshasanda, wameniacha Mimi na Mzee Kidevu. Raia wamejaa wanauliza kuna nini?. Mzee Dingi linawajibu "Mambo ya kifamilia, tuachieni wenyewe". Yule Mzee Kidevu kama angekuwa na pumzi ya kutosha, angeniaibisha pale, kitu pekee kilichofanya akachemka ni pumzi. Nilivyóona kazidiwa, nikaanza kumpelekea punch mfululizo. Kumbe bwana vile vizee vilikuja na back up. Muda wote tokea nimewakuta, kuna jamaa kipande alikuwa amekaa kwa pembeni anachezea simu.

Walivyoona hadi Mzee Kidevu kazidiwa, Mzee Dingi akaita "We Beka fanya kazi yako". Aisee nilivyomuona huyo Beka mwenyewe, sikuwa na namna zaidi ya kukimbia. Nilifungua turbo kuelekea kwenye makazi ya watu, yamekaa kama kota hivi. Nilidhani watanipotezea, nashangaa Beka kaniungia tela, Mzee Kidevu na wale wazee wengine nao wakaanza kuja nyuma yetu. Raia nao hawana dogo, baadhi wameacha kuangalia mpira, wametuungia tela.

Nikipiga hatua zangu mbili, ndio hatua moja ya Beka. Sikwenda mbali sana akanishika. Nikataitishwa. Mwanasheria feki akawa anafanyakazi ya kufukuza watu walau wasogee mbali ba tulipo. Nilivyokuwa chini pale, Mzee Dingi akawa anasema;

Mzee Dingi: "Mvue hivyo vitu alivyovaa ndio vinamtia kiburi"

Beka akanichukulia ile pete yangu yenye kihirizi. Kisha akataka kunivua na kacha niliyokuwa nimevaa mkononi

Mzee Dingi: "Hiyo muachie, haina madhara. Yupo nayo hata kabla hajaoneshwa Dunia ilivyo"

Baada ya kuichukua ile pete, akamkabidhi Mzee Dingi, alafu wakaanza kuondoka. Kwenye wallet nilikuwa na 70k, hawakuigusa kabisa. Yani Wazee shida yao ilikuwa ile pete tu. Nilikuwa bado nimekaa chini nikiwa na hasira, maana yule kipande aliniumiza. Ghafla kuna wazo likanipitia kichwani, sikujiuliza mara mbili, nikanyanyuka na kuanza kuwafata. Nilivyowakaribia nikainama chini na kuchota mchanga, Mzee Kidevu akawa ameniaona;

Mzee Kidevu: "Apostle umenichota unyayo, apostle umenichota unyayo?"

Kiukweli nilifanya vile kama kuwatisha tu, ila Mzee Kidevu akalichukulia serious.

Mzee Kidevu: "Apostle unachotaka kukianzisha unakimudu?. Kumbe mtoto mshenzi sana wewe"

Kabla sijamjibu kitu, yule Beka kipande akawahi kunikamata, akaniminya mkono hadi nikaachia ule mchanga. Nikabaki nimesimama tu. Kila Wakitaka kuondoka, natishia kama nainama kuzoa mchanga, wanarudi.

Mzee Dingi: "Huyu mtoto sio wa kumfanyia mzaha kabisa"

Jamaa kila wakipiga hesabu, walipoacha gari yao ni mbali lazima watembee. Lakini hapo hapo wanahofia huku nyuma naweza fanya jambo baya. Ghafla Mzee Kidevu akanirukia, tukaanguka wote chini. Kisha wakamwambia Beka anibebe mpaka kwenye gari yao.

Muda huo wote raia full kucheka, kelele na kuzomea. Jamaa ikabidi wanipe lift kwa lazima, wakaenda kunishushia Ilala Boma.

Nilichokuja kugundua, kumbe ile Jana nilivyoacha na mzee Kesho Yetu, alimpigia Mzee Dingi na kumwambia Mimi sitoshiriki tena kwenye lile dili, nikiendelea kuwepo kuna uwezekano mkubwa sana wa dili kufeli. Ndio maana kina Mzee Dingi wakaamua kuja kunishikisha adabu na kunipora kile kihirizi, maana waliona sihitajiki tena.

Ambacho Mimi na wale wazee hatukujua ni kwamba, wakati sisi huku tunashikana mashati, upande wa pili Mzee Kesho Yetu alikuwa anakamilisha dili. Jana yake wakati tupo kwa yule mstaafu, walivyo baki peke yao sijui hata alimwambia nini, ila chochote alichomwambia ndicho kilichopelekea wao kwenda kukamilisha dili.

Walau Mimi nilishajua kuwa kwenye lile dili sipo tena, ila kina Mzee Dingi wao walikuwa wanasubiria siku mbili mbele wakakamilishe dili.

Wamechukua pete yangu, na kuondoka kishujaa, kumbe upande wa pili Mzee Kesho Yetu anasepa na mkwanja peke yake.

Kibaya zaidi, anaacha msala ambao ni wetu wote, ilhali sisi wengine hatujajiandaa....
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣chai
 
Aposto Analyse kuna jambo unalitafuta sina haja ya kusema jambo gani ila unalitafuta
210403-devin-carter-stockton-mb-1549.jpg
 
12th Portions:

... Maongezi yakaendelea

Mzee: "Unajua kwanini Baba yako alikuwa anataka uonane na Mimi?
Analyse: "Aliniambia unaweza kunisaidia kwenye maswala ya kazi"
Mzee: "Na mbona hukunitafuta?"
Analyse: (Kimya)
Mzee: "Alichokwambia ni kweli, ila umekuja kwa mtu sahihi, wakati usio sahihi"
Analyse: "Kivipi? "
Mzee: "Tayari nipo nje ya mfumo, wakati ule ingekuwa rahisi sana tofauti na sasa"

"Unajishughurisha na nini sasa hivi?"
Analyse: "Nipo tu Mzee, Sina shughuli maalum"
Mzee: "Una muda gani tokea uanze kutokuwa na shughuli maalum?"
Analyse: "Tokea nimemaliza chuo mambo ndio hivi hivi"
Mzee: "Kama ni hivyo, mbona kipindi chote hicho tumeshindwa kuonana, nilidhani uko busy?"
Analyse: "Kimya...."
Mzee: "Nakumbuka kama nishawahi kukupigia simu sana, ila hukupokea. Mtu ambae huna shughuli maalum, unashindwaje kupokea simu?"
Analyse: (kimya)
Mzee: "Kama kuna kitu kigumu kukielewa, basi ni jinsi vijana wa sasa mnavyofikiria. Mpo busy sana, lakini hakuna cha maana mnachofanya"

Akaendelea "Mifumo yetu hapa nchini jinsi ilivyo, ukitoka tu nje ya mfumo, ni rahisi sana kusahaulika. Wanakuona kama mzigo, hawakupi tena attention sana maana huna msaada kama mwanzo. Hata huu ufugaji na biashara tunazofanya, inakuwa ni kupunguza stress na kujiweka fit financially, maana njia za mkato zote zinapotea". "Ukistaafu, watu uliokuwa nao, wataendelea kuwa karibu na wewe kwa muda, ila kadiri muda unavyosogea ukiwa nje ya mfumo, na wao wanazidi kujiweka mbali na wewe, hatimae ushawishi uliokuwa nao unapotea wote, unabaki kuwa mtu wakawaida mbele yao"

"Baba yako alikuwa anatamani sana usome, na kama ungesoma wakati ule, ilikuwa rahisi kupata sehemu ya kukuweka, ila ukachagua njia tofauti. Haya hebu niambie, ukiachana na makovu kibao uliyokuwa nayo, kipi cha maana unachojivunia katika hizo hustling zako?

Nikabaki kimya. Nae akabaki ananiangalia tu.

Analyse: "Ila Baba hakuwahi niambia yote haya, na sikuwahi kuyajua"
Mzee: "Kwahiyo mpaka ujue faida ya unachoenda kufanya, ndio ukifanye? Haya faida za hiyo njia uliyochagua ni zipi mpaka ukaichagua?"

Nikawa kimya tena. Mzee kila akifungua mdomo, anatoa punch za kwenye mshono.

"Leo hii pakitokea dharura, inahitajika milioni 5 Kwa ajili ya matibabu ya wazazi wenu, familia nzima mkihitajika kuchangia,wewe unaweza kutoa kiasi gani in such short notice?

Nikainama tu, ningesemaje sasa?

"Zamani wazazi walikuwa wanafurahia Sana wakipata watoto wakiume. Ila siku hizi hujui kama ufurahie au la, maana hamtabiriki kabisa. Mapenzi yanawaondolea sana akili, mmekuwa kama mbwa, anayeweza kwenda umbali mrefu sana kufata jike, ila siku akija mwizi nyumbani, atamfukuza mpaka hatua chache kutoka nyumbani, kisha atamuacha. Vya maana hamvipi uzito, ila visivyo na msingi mnavifanya kwa umakini"

Akaendelea:

"Hivi unajua Mimi na Baba yako tumefahamiana vipi?"

Analyse: "Hapana"
Mzee (akasikitika): "Bure kabisa"

Baada ya hapo akatema punch zingine ambazo nilishindwa kuzihimili.

"Kama ilivyokuwa kwa Baba yako, Mimi pia nilikuwa mwanajeshi. Hatukuwa na mazoea wakati tupo kambini. Ukaribu wetu ulianza tulivyochaguliwa kwenda Urusi kwa ajili ya mafunzo maalum yakiweko ya Urubani ambako Baba yako ndio alikuwepo"

"Alikuwa room mate wangu, baada ya kufika kule. Na hata tulipohitimu mafunzo na kurudi nchini, urafiki wetu tayari ulikuwa umekomaa". Akaniuliza "Unajua kwanini yeye alitoka jeshini? "

Japo aliniuliza Mimi lile swali, ila ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu, akaendelea "Kipindi cha vita ya Kagera, wakati wa maandalizi ya mwisho, Mzee wako alipata tatizo la kiafya ambalo lilifanya aonekane unfit kwa wakati ule (Mzee wangu mpaka sasa anachechemea mguu mmoja)".

Akaendelea

"Pamoja na yote, Mzee wako hakutaka kutoka jeshini, akiamini atapona na kurudi nomo, ila kwa shinikizo na Babu yako, ikabidi Baba yako atoke jeshini kwa lazima. Maana walifikia hatua hadi ya kutoelewana kati yao"

"Hata nilivyorudi kutoka vitani, Mzee wako bado alikuwa na hasira na Babu yako. Tulipoteza marubani wengi wazuri, nilijaribu kumwambia pengine hata yeye angeweza kufa kama wengine, ila mpaka leo anaamini yeye angerudi mzima au ni heri kufia kule kuliko kulala kitandani"

Mzee aliongea vitu vingi sana kuhusu Mshua, vingine ndio ilikuwa mara ya kwanza navisikia.

Kiufupi yote aliyokuwa anaongea, ni kama vile alikuwa ananisema. Maana yalifanya nikajisikia vibaya sana. Wakati tunaendelea na maongezi, nikamuuliza

"Kwanini hakuwahi kunigusia chochote juu ya haya mengi? Au kwanini hakuwahi kunisisitizia umuhimu wa hii njia aliyonichagulia yeye?"

Akatoa tabasam fulani hafifu, alaf akaniambia

"Ingekuwa vipi kama angekufosi upite njia aliyoitaka yeye alafu mbeleni mambo yakafeli?"

"Babu yako wakati anamshawishi Baba yako atoke jeshini, aliahidi kumpa kiwanda chake cha upasuaji mbao ili kiwe chanzo chake cha kipato. Ila baada ya Baba yako kuacha kazi jeshini, sehemu ya kile kiwanda ilishika moto, na kwenye harakati ya uokoaji, baadhi ya vitu viliibiwa, vingi viliungua na vingine kupotea, hiyo story nadhani unaijua"

"Kilichofata, Baba yako kazi hana, na kiwanda hakipo. Baada ya hapo Baba yako na Babu yako ukaribu ulipungua sana, maana palitokea ugomvi kati yao.. Baba yako alikuwa akimlaumu sana Babu kwa mambo yake kwenda mlama, maana anaamini yeye kumtoa jeshini, ndio chanzo cha yote. Huu ukaribu kati yao unaouona umekuja hivi karibuni tu."

"Baba yako anakupenda sana, ila hawezi kukupush kwenye njia aliyochagua yeye, anakusupport unapochagua wewe, ili asijekuwa sehemu ya lawama zako, kama ambavyo yeye alishindwa kuacha kumlaumu Baba yake, bila kuangalia nia njema aliyokuwa nayo (Baba yake) kwake"

"Kati ya wanae wote, wewe ndiye anayekukubali sana. Inapotokea umemdisappoint, huwa anaumia sana, ila hawezi kukwambia. Mara nyingi huwa anasema, hivi ulivyo ni copy and paste ya kipindi chake cha ukuaji, ndio maana huwa anashindwa kukulaumu. Hata leo hii Mama yako akimwambia nyie wote sio watoto wake, wale wengine anaweza kukubali ila sio wewe".

Maongezi na Mzee yakawa kama mwiba kwangu. Kila anachoongea kinaniuma. Mzee wangu mara kadhaa amekuwa akimuuliza Bi Mkubwa kama kweli Mimi ni mwanae, au kusema nimerithi tabia ujombani, lakini kumbe uhalisia uko tofauti? Nikiwa nae tunapiga story tunacheka, najua yaliyopita yamepita na kila kitu kipo sawa, ila kumbe anaumia ndani kwa ndani?.

Pale ndio akili ikanifunguka, kumbe sio kila tabasam ni la furaha. Kumbe kicheko nacho kinaweza kikawa njia ya kuficha hudhuni?. Kuna mtu alishawahi kuniambia kuwa tabasamu ni deni, ila sikuwahi kumuelewa alimaanisha nini. Hii siku ndio nikaipata tafsiri ya alichomaanisha. Maana tabasamu ambalo amekuwa akinionesha Mshua wangu, limegeuka kuwa deni kubwa, Deni ambalo nimechelewa sana kulijua. Deni ambalo sijajua ntalilipa vipi. Hakika tabasamu la wakupendao ni deni, maana lina siri nyingi.

Akili yangu ilivurugika, mawazo yakaenda mbali sana, nikawa nakumbuka matukio ambayo nishawahi kumpitisha Mshua. Nikiwaga nyumbani kuna muda tunacheka na kufurahia sana, mbona hajawahi kunionesha kama kuna kitu kinamuumiza ndani ya nafsi yake?. Inawezekana mtu akawa na maumivu ambayo ni ngumu kuyaelezea kwa anayeyasababisha?. Je, na Mimi nitatakiwa kuja kuipitia hii hali dhidi ya wanangu? Kwamba inawezekana nisiweze kuwaelezea kila kitu ? Nitatakiwa kucheka na kufurahi mbele yao, hata kama moyoni nina majeraha?. Heri ya Mimi nimepata mtu wa kunielezea haya mambo, itakuwaje kama wanangu wasipoweza kuyajua maumivu yangu?.

Ni kwamba Mshua alitaka nije kuonana na huyu Mzee, ni Kwa ajili ya kupata connection tu au alihisi ningeweza kuyajua haya mambo?. Inabidi niongee na Mshua, ila nitaanzia wapi? Au natakiwa nikamuombe msamaha kwanza?. Atanielewa? Na mambo yaliyotokea kati yetu ni mengi sana, huo msamaha namuombaje?.

Ilifikia hatua mpaka nikawa sisikii kabisa vitu alivyoendelea kuniambia yule Mzee. Ni kama sikuwa eneo lile kabisa, usikivu ulipotea hadi yule Mzee akaniambia nirudi nyumbani kwanza nikapumzike.

Akanisisitizia kuwa kila wiki end anakuwa pale japo sipo anapoishi, kwahiyo nikiwa na muda niwe naenda kumuona ili tuzidi kuongea.

Tukaagana. Kijana wake akanisogeza tena mpaka Kongowe mwisho.


* ** ******** *****

Njia nzima najilaumu, hadi kichwa kimepata sana moto, kiasi kwamba ukinishtua naweza hata kuzimia. Nikaifikiria ile siku ambayo Mzee ananipigia simu, alaf Mimi nimeiweka silent kisa yule mpenzi wangu wa kipindi kile alikuwa anataka tukiwa pamoja tusitumie simu. Kilichoniuma zaidi sio kwamba yule manzi tumeshaachana, bali ni sababu iliyofanya tuachane. Mimi nilikuwa naamini hapendi tutumie simu tukiwa pamoja, ili akili na mawazo yetu yasiende mbali, kumbe mwenzangu alikuwa na mahusiano na jamaa mwingine, hivyo alikuwa anatengeneza mazingira ya kutokupokea simu.

Nakumbuka kuna siku, wakati ameenda kuoga, nilishika simu yake na kukuta msg toka kwa mtu aliyemsave "Suka". Msg ilimwambia aende tena kulala kwa huyo jamaa, maana ameshamiss alichompa siku iliyopita. Yaani kwangu anakuja mchana mpaka jioni, kwa Suka anaenda kuilaza. Alafu old chatting zikaonesha ni wapenzi wa muda mrefu, japo huyo jamaa amenikuta. Wakati mimi manzi namla kistaarab, Suka yeye anamgeuza atakavyo.

Wakati bado nimeishika, Suka akapiga tena, demu nae anaingia ndani, nikapokea kisha nikaweka loud. Demu hakuongea akaikata. Sikutaka hata tuzozane, nikamwambia avae aende kwa Suka. Imagine mwanamke ninayemvalue high, kumbe akienda kwa Suka, anampa jamaa honi, anaipuliza mpaka inazima.

Maumivu niliyokuwa nayafeel baada ya kutoka kwa Mzee, yaliongezeka maradufu nilipomkumbuka yule manzi, maana nilimuonaga kama wife material. Eti wife material? [emoji28][emoji28][emoji28]wife material my ass**.

Yule manzi alinifanya nikakosa connection ambayo pengine ingeweza kubadili maisha yangu.

Tunasemaga makaburi yamezika ndoto za watu wengi. Ila kwa upande mwingine mapenzi nayo yanaziua sana ndoto, huku yakituacha waotaji tuendelee kuishi kwa msoto.

Kiufupi sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, kama hii siku niliyoongea na huyu Mzee. Vitu alivyoniambia viliniondolea utulivu kabisa.

***** ******* ****** ******** ****** *****

Nilivyokuwa ndani ya daladala, ndio nikashika simu, maana muda wote ilikuwa silent, mfukoni kuepusha usumbufu kwa yule Mzee.

Nakuta missed calls saba, 6 za mpenzi wangu wa wakati huo, moja ya shangazi fulani ambae nilikuwa nae kipindi hicho anaitwa Shani. Sikuwa na mood ya kupiga simu, nikawapotezea.

Kwenda upande wa msg, nakuta msg 4, moja ya shangazi. Tatu za mpenzi wangu. Msg ya mpenzi moja iliuliza niko wapi, nyingine ilitumwa baada ya robo saa ikisema nisipomtafuta ndani ya nusu saa ijayo nisimtafute tena, tunaachana. Ya tatu aliituma hata kabla ya nusu saa aliyonipa kufika, akasema Mimi na yeye basi, nisijisumbue nae. Nikajiuliza huyu alikuwa anataka nini? Nikajaribu kumpigia, nakuta kaniblock. Nikaachana nae. Kusoma ile msg ya shangazi, ananiambia "Pitia nyumbani kwangu, nina zawadi yako", nikajisemea huku ndio pa kwenda.

Nafika kule, nikakuta msosi, nikala, ila akili yangu bado inawaza maneno ya yule Mzee tu. Ikabidi nimchane Shani kuwa mood ya shoo haikuwepo. Akanijibu "Achana na habari za shoo wewe, yani ukishiba tu akili yako inawaza kuparamiana. Hata hivyo bao la kwanza alihitajigi mood, hata uwe hutaki litakuja tu, hebu njoo huku uone."

Kumsogelea nakuta kaniletea zawadi ya PS4 na pad moja. Akaniambia "Leo nataka kukupa vitu unavyopenda tu, leo inabidi ufurahi"

Mood yangu taratibu ikaanza kurudi. Nikamuuliza "Mbona unasema hivyo, kuna zawadi nyingine kwani? Akasema sio zawadi, ni taarifa. Nikamuuliza taarifa gani? Akasema "Nipo tayari sasa, nataka tuzae".

Nilikuwa bado nimeishika ile PS4 mkononi, ikabidi niiweke mezani, kisha nikae ili nimuone vizuri.

Analyse: "Uzae na nani? Kwani nimekwambia nataka mtoto Mimi?"
Shani: "Mbona umeshtuka hivyo, kwani kuna tatizo tukipata mtoto?"
Analyse: : "Nyumbani familia hawawezi kukubali ili jambo"
Shani: "Kwani nazaa na familia au nazaa na wewe, hebu nipishe mie"
Analyse: "Hicho kitu hakipo"
Shani: "Tena usinitibue, hii siku kwangu ni nzuri, mwanaume mzima unaogopa kuwa na mtoto. Na ntawapigia familia yako wote niwachambe, maana wanataka kukuendesha. Wewe mtu mzima, jisimamie"

Nikawahi kuchukua simu yangu ili asije kuiba namba zao mule, maana Kwa akili yake hashindwi kuwapigia kweli.

Akaishia kucheka tu. Alafu akasema;

Shani: "Namba za wakwe ninazo siku nyingi sana, nitaanza na wifi, yeye ndio ataambia na wengine"

Hata hamu na ile zawadi ya PS4 ilikata...

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Hapa ndio title ilipotokea
 
Ni kama kuna mtu karoga kajambia wasimulizi wa jf kwenye vichwa shuzi limeenea sasa whats this?! Nigga alikua very promising saivi baba jeni bai bai aisee watz tuna safar ndef
 
Back
Top Bottom