Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Yaani kuna watu wengi humu hawana uvumilivu hata kidogo na hawana utulivu wa akili. Ni kama hawana kitu kingine cha kufanya zaidi ya kushinda JF. Hebu fikiria mtu analeta bure story kwa hiari yake. Baadae watu wanaanza kumforce kama vile wanamlipa,inakera. kauli yao utasikia kwa nini alikuwa analeta kama hana nafasi ya kuleta mfurulizo? Point ya kijinga sana. Hata kama mtu umeiandaa yote bado huwezi kutuma mfurulizo.
Ni kama hawana kitu kingine cha kufanya..simamia hapa .binafsi hua nashangaa pia inakua kama deni1😌
 
Mie Mbona ndio kiongozi hukoo 🤣😂
Vice atakua aposto na timu yake ikiongozwa na dingi😂!
Wakati unasoma shule nasikia ulikuw unaulizwa unatokea wapi unajibu shinyanga mjini as if shinyanga ni mjini😀😃😄

Nina uhakika Dar hupajui, Dar ina wilaya ngap hivi😀😂
 
kumbe nilisoma vibaya ushangazi huu Walai nazeeka vibaya. nilisoma Antonnia bado una samora hapo? Kweli nazeeka vibaya ☺️
🤣🤣🤣una samora hapo manake ni nini? haha ukaelew kuwa unasosomora hapo nadhani inamanisha kula au kuvua nguo😀
mh kuvua sio unasosomola🤣kweli kiswahili kigumu
 
Hivi Dar ndio mnaita bongo eeh??😂😂😂Nipajulie wapi mshamba mie hata Sijawahi fika huko fanya wepesi shangazi enu nije kutoa huu ushamba aseeh!!😊
Kuna dogo wa kichaga tunapiga story kuhusu daraja la manzese akadakia "pale mansese Pana mamba wengi" (in Chaga lafudhi😀) akilini anadhani tunazungumzia daraja la wami🤣🤣

Uje Dar utapeliw na akina Analyse
 
🤣🤣🤣una samora hapo manake ni nini? haha ukaelew kuwa unasosomora hapo nadhani inamanisha kula au kuvua nguo😀
mh kuvua sio unasosomola🤣kweli kiswahili kigumu
Si ndo hata mie na ukilaza wangu wote nikashindwa kuelewaa mie kiswahili nilifeliiigii mwenzio ☺️
 
Kuna dogo wa kichaga tunapiga story kuhusu daraja la manzese akadakia "pale mansese Pana mamba wengi" (in Chaga lafudhi😀) akilini anadhani tunazungumzia daraja la wami🤣🤣

Uje Dar utapeliw na akina Analyse
Cha kutapeliwa kikwapi sasa labda maparachichi🤣 kwanza hao wanatapeli vyenye pesa ndefuuuu!!
Mi mwenyewe tapeli hahaha wee Jichanganye🙃🤭
 
12th Portions:

... Maongezi yakaendelea

Mzee: "Unajua kwanini Baba yako alikuwa anataka uonane na Mimi?
Analyse: "Aliniambia unaweza kunisaidia kwenye maswala ya kazi"
Mzee: "Na mbona hukunitafuta?"
Analyse: (Kimya)
Mzee: "Alichokwambia ni kweli, ila umekuja kwa mtu sahihi, wakati usio sahihi"
Analyse: "Kivipi? "
Mzee: "Tayari nipo nje ya mfumo, wakati ule ingekuwa rahisi sana tofauti na sasa"

"Unajishughurisha na nini sasa hivi?"
Analyse: "Nipo tu Mzee, Sina shughuli maalum"
Mzee: "Una muda gani tokea uanze kutokuwa na shughuli maalum?"
Analyse: "Tokea nimemaliza chuo mambo ndio hivi hivi"
Mzee: "Kama ni hivyo, mbona kipindi chote hicho tumeshindwa kuonana, nilidhani uko busy?"
Analyse: "Kimya...."
Mzee: "Nakumbuka kama nishawahi kukupigia simu sana, ila hukupokea. Mtu ambae huna shughuli maalum, unashindwaje kupokea simu?"
Analyse: (kimya)
Mzee: "Kama kuna kitu kigumu kukielewa, basi ni jinsi vijana wa sasa mnavyofikiria. Mpo busy sana, lakini hakuna cha maana mnachofanya"

Akaendelea "Mifumo yetu hapa nchini jinsi ilivyo, ukitoka tu nje ya mfumo, ni rahisi sana kusahaulika. Wanakuona kama mzigo, hawakupi tena attention sana maana huna msaada kama mwanzo. Hata huu ufugaji na biashara tunazofanya, inakuwa ni kupunguza stress na kujiweka fit financially, maana njia za mkato zote zinapotea". "Ukistaafu, watu uliokuwa nao, wataendelea kuwa karibu na wewe kwa muda, ila kadiri muda unavyosogea ukiwa nje ya mfumo, na wao wanazidi kujiweka mbali na wewe, hatimae ushawishi uliokuwa nao unapotea wote, unabaki kuwa mtu wakawaida mbele yao"

"Baba yako alikuwa anatamani sana usome, na kama ungesoma wakati ule, ilikuwa rahisi kupata sehemu ya kukuweka, ila ukachagua njia tofauti. Haya hebu niambie, ukiachana na makovu kibao uliyokuwa nayo, kipi cha maana unachojivunia katika hizo hustling zako?

Nikabaki kimya. Nae akabaki ananiangalia tu.

Analyse: "Ila Baba hakuwahi niambia yote haya, na sikuwahi kuyajua"
Mzee: "Kwahiyo mpaka ujue faida ya unachoenda kufanya, ndio ukifanye? Haya faida za hiyo njia uliyochagua ni zipi mpaka ukaichagua?"

Nikawa kimya tena. Mzee kila akifungua mdomo, anatoa punch za kwenye mshono.

"Leo hii pakitokea dharura, inahitajika milioni 5 Kwa ajili ya matibabu ya wazazi wenu, familia nzima mkihitajika kuchangia,wewe unaweza kutoa kiasi gani in such short notice?

Nikainama tu, ningesemaje sasa?

"Zamani wazazi walikuwa wanafurahia Sana wakipata watoto wakiume. Ila siku hizi hujui kama ufurahie au la, maana hamtabiriki kabisa. Mapenzi yanawaondolea sana akili, mmekuwa kama mbwa, anayeweza kwenda umbali mrefu sana kufata jike, ila siku akija mwizi nyumbani, atamfukuza mpaka hatua chache kutoka nyumbani, kisha atamuacha. Vya maana hamvipi uzito, ila visivyo na msingi mnavifanya kwa umakini"

Akaendelea:

"Hivi unajua Mimi na Baba yako tumefahamiana vipi?"

Analyse: "Hapana"
Mzee (akasikitika): "Bure kabisa"

Baada ya hapo akatema punch zingine ambazo nilishindwa kuzihimili.

"Kama ilivyokuwa kwa Baba yako, Mimi pia nilikuwa mwanajeshi. Hatukuwa na mazoea wakati tupo kambini. Ukaribu wetu ulianza tulivyochaguliwa kwenda Urusi kwa ajili ya mafunzo maalum yakiweko ya Urubani ambako Baba yako ndio alikuwepo"

"Alikuwa room mate wangu, baada ya kufika kule. Na hata tulipohitimu mafunzo na kurudi nchini, urafiki wetu tayari ulikuwa umekomaa". Akaniuliza "Unajua kwanini yeye alitoka jeshini? "

Japo aliniuliza Mimi lile swali, ila ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu, akaendelea "Kipindi cha vita ya Kagera, wakati wa maandalizi ya mwisho, Mzee wako alipata tatizo la kiafya ambalo lilifanya aonekane unfit kwa wakati ule (Mzee wangu mpaka sasa anachechemea mguu mmoja)".

Akaendelea

"Pamoja na yote, Mzee wako hakutaka kutoka jeshini, akiamini atapona na kurudi nomo, ila kwa shinikizo na Babu yako, ikabidi Baba yako atoke jeshini kwa lazima. Maana walifikia hatua hadi ya kutoelewana kati yao"

"Hata nilivyorudi kutoka vitani, Mzee wako bado alikuwa na hasira na Babu yako. Tulipoteza marubani wengi wazuri, nilijaribu kumwambia pengine hata yeye angeweza kufa kama wengine, ila mpaka leo anaamini yeye angerudi mzima au ni heri kufia kule kuliko kulala kitandani"

Mzee aliongea vitu vingi sana kuhusu Mshua, vingine ndio ilikuwa mara ya kwanza navisikia.

Kiufupi yote aliyokuwa anaongea, ni kama vile alikuwa ananisema. Maana yalifanya nikajisikia vibaya sana. Wakati tunaendelea na maongezi, nikamuuliza

"Kwanini hakuwahi kunigusia chochote juu ya haya mengi? Au kwanini hakuwahi kunisisitizia umuhimu wa hii njia aliyonichagulia yeye?"

Akatoa tabasam fulani hafifu, alaf akaniambia

"Ingekuwa vipi kama angekufosi upite njia aliyoitaka yeye alafu mbeleni mambo yakafeli?"

"Babu yako wakati anamshawishi Baba yako atoke jeshini, aliahidi kumpa kiwanda chake cha upasuaji mbao ili kiwe chanzo chake cha kipato. Ila baada ya Baba yako kuacha kazi jeshini, sehemu ya kile kiwanda ilishika moto, na kwenye harakati ya uokoaji, baadhi ya vitu viliibiwa, vingi viliungua na vingine kupotea, hiyo story nadhani unaijua"

"Kilichofata, Baba yako kazi hana, na kiwanda hakipo. Baada ya hapo Baba yako na Babu yako ukaribu ulipungua sana, maana palitokea ugomvi kati yao.. Baba yako alikuwa akimlaumu sana Babu kwa mambo yake kwenda mlama, maana anaamini yeye kumtoa jeshini, ndio chanzo cha yote. Huu ukaribu kati yao unaouona umekuja hivi karibuni tu."

"Baba yako anakupenda sana, ila hawezi kukupush kwenye njia aliyochagua yeye, anakusupport unapochagua wewe, ili asijekuwa sehemu ya lawama zako, kama ambavyo yeye alishindwa kuacha kumlaumu Baba yake, bila kuangalia nia njema aliyokuwa nayo (Baba yake) kwake"

"Kati ya wanae wote, wewe ndiye anayekukubali sana. Inapotokea umemdisappoint, huwa anaumia sana, ila hawezi kukwambia. Mara nyingi huwa anasema, hivi ulivyo ni copy and paste ya kipindi chake cha ukuaji, ndio maana huwa anashindwa kukulaumu. Hata leo hii Mama yako akimwambia nyie wote sio watoto wake, wale wengine anaweza kukubali ila sio wewe".

Maongezi na Mzee yakawa kama mwiba kwangu. Kila anachoongea kinaniuma. Mzee wangu mara kadhaa amekuwa akimuuliza Bi Mkubwa kama kweli Mimi ni mwanae, au kusema nimerithi tabia ujombani, lakini kumbe uhalisia uko tofauti? Nikiwa nae tunapiga story tunacheka, najua yaliyopita yamepita na kila kitu kipo sawa, ila kumbe anaumia ndani kwa ndani?.

Pale ndio akili ikanifunguka, kumbe sio kila tabasam ni la furaha. Kumbe kicheko nacho kinaweza kikawa njia ya kuficha hudhuni?. Kuna mtu alishawahi kuniambia kuwa tabasamu ni deni, ila sikuwahi kumuelewa alimaanisha nini. Hii siku ndio nikaipata tafsiri ya alichomaanisha. Maana tabasamu ambalo amekuwa akinionesha Mshua wangu, limegeuka kuwa deni kubwa, Deni ambalo nimechelewa sana kulijua. Deni ambalo sijajua ntalilipa vipi. Hakika tabasamu la wakupendao ni deni, maana lina siri nyingi.

Akili yangu ilivurugika, mawazo yakaenda mbali sana, nikawa nakumbuka matukio ambayo nishawahi kumpitisha Mshua. Nikiwaga nyumbani kuna muda tunacheka na kufurahia sana, mbona hajawahi kunionesha kama kuna kitu kinamuumiza ndani ya nafsi yake?. Inawezekana mtu akawa na maumivu ambayo ni ngumu kuyaelezea kwa anayeyasababisha?. Je, na Mimi nitatakiwa kuja kuipitia hii hali dhidi ya wanangu? Kwamba inawezekana nisiweze kuwaelezea kila kitu ? Nitatakiwa kucheka na kufurahi mbele yao, hata kama moyoni nina majeraha?. Heri ya Mimi nimepata mtu wa kunielezea haya mambo, itakuwaje kama wanangu wasipoweza kuyajua maumivu yangu?.

Ni kwamba Mshua alitaka nije kuonana na huyu Mzee, ni Kwa ajili ya kupata connection tu au alihisi ningeweza kuyajua haya mambo?. Inabidi niongee na Mshua, ila nitaanzia wapi? Au natakiwa nikamuombe msamaha kwanza?. Atanielewa? Na mambo yaliyotokea kati yetu ni mengi sana, huo msamaha namuombaje?.

Ilifikia hatua mpaka nikawa sisikii kabisa vitu alivyoendelea kuniambia yule Mzee. Ni kama sikuwa eneo lile kabisa, usikivu ulipotea hadi yule Mzee akaniambia nirudi nyumbani kwanza nikapumzike.

Akanisisitizia kuwa kila wiki end anakuwa pale japo sipo anapoishi, kwahiyo nikiwa na muda niwe naenda kumuona ili tuzidi kuongea.

Tukaagana. Kijana wake akanisogeza tena mpaka Kongowe mwisho.


* *** ***** ******** *****

Njia nzima najilaumu, hadi kichwa kimepata sana moto, kiasi kwamba ukinishtua naweza hata kuzimia. Nikaifikiria ile siku ambayo Mzee ananipigia simu, alaf Mimi nimeiweka silent kisa yule mpenzi wangu wa kipindi kile alikuwa anataka tukiwa pamoja tusitumie simu. Kilichoniuma zaidi sio kwamba yule manzi tumeshaachana, bali ni sababu iliyofanya tuachane. Mimi nilikuwa naamini hapendi tutumie simu tukiwa pamoja, ili akili na mawazo yetu yasiende mbali, kumbe mwenzangu alikuwa na mahusiano na jamaa mwingine, hivyo alikuwa anatengeneza mazingira ya kutokupokea simu.

Nakumbuka kuna siku, wakati ameenda kuoga, nilishika simu yake na kukuta msg toka kwa mtu aliyemsave "Suka". Msg ilimwambia aende tena kulala kwa huyo jamaa, maana ameshamiss alichompa siku iliyopita. Yaani kwangu anakuja mchana mpaka jioni, kwa Suka anaenda kuilaza. Alafu old chatting zikaonesha ni wapenzi wa muda mrefu, japo huyo jamaa amenikuta. Wakati mimi manzi namla kistaarab, Suka yeye anamgeuza atakavyo.

Wakati bado nimeishika, Suka akapiga tena, demu nae anaingia ndani, nikapokea kisha nikaweka loud. Demu hakuongea akaikata. Sikutaka hata tuzozane, nikamwambia avae aende kwa Suka. Imagine mwanamke ninayemvalue high, kumbe akienda kwa Suka, anampa jamaa honi, anaipuliza mpaka inazima.

Maumivu niliyokuwa nayafeel baada ya kutoka kwa Mzee, yaliongezeka maradufu nilipomkumbuka yule manzi, maana nilimuonaga kama wife material. Eti wife material? 😅😅😅wife material my ass**.

Yule manzi alinifanya nikakosa connection ambayo pengine ingeweza kubadili maisha yangu.

Tunasemaga makaburi yamezika ndoto za watu wengi. Ila kwa upande mwingine mapenzi nayo yanaziua sana ndoto, huku yakituacha waotaji tuendelee kuishi kwa msoto.

Kiufupi sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, kama hii siku niliyoongea na huyu Mzee. Vitu alivyoniambia viliniondolea utulivu kabisa.

***** ******* ****** ******** ****** *****

Nilivyokuwa ndani ya daladala, ndio nikashika simu, maana muda wote ilikuwa silent, mfukoni kuepusha usumbufu kwa yule Mzee.

Nakuta missed calls saba, 6 za mpenzi wangu wa wakati huo, moja ya shangazi fulani ambae nilikuwa nae kipindi hicho anaitwa Shani. Sikuwa na mood ya kupiga simu, nikawapotezea.

Kwenda upande wa msg, nakuta msg 4, moja ya shangazi. Tatu za mpenzi wangu. Msg ya mpenzi moja iliuliza niko wapi, nyingine ilitumwa baada ya robo saa ikisema nisipomtafuta ndani ya nusu saa ijayo nisimtafute tena, tunaachana. Ya tatu aliituma hata kabla ya nusu saa aliyonipa kufika, akasema Mimi na yeye basi, nisijisumbue nae. Nikajiuliza huyu alikuwa anataka nini? Nikajaribu kumpigia, nakuta kaniblock. Nikaachana nae. Kusoma ile msg ya shangazi, ananiambia "Pitia nyumbani kwangu, nina zawadi yako", nikajisemea huku ndio pa kwenda.

Nafika kule, nikakuta msosi, nikala, ila akili yangu bado inawaza maneno ya yule Mzee tu. Ikabidi nimchane Shani kuwa mood ya shoo haikuwepo. Akanijibu "Achana na habari za shoo wewe, yani ukishiba tu akili yako inawaza kuparamiana. Hata hivyo bao la kwanza alihitajigi mood, hata uwe hutaki litakuja tu, hebu njoo huku uone."

Kumsogelea nakuta kaniletea zawadi ya PS4 na pad moja. Akaniambia "Leo nataka kukupa vitu unavyopenda tu, leo inabidi ufurahi"

Mood yangu taratibu ikaanza kurudi. Nikamuuliza "Mbona unasema hivyo, kuna zawadi nyingine kwani? Akasema sio zawadi, ni taarifa. Nikamuuliza taarifa gani? Akasema "Nipo tayari sasa, nataka tuzae".

Nilikuwa bado nimeishika ile PS4 mkononi, ikabidi niiweke mezani, kisha nikae ili nimuone vizuri.

Analyse: "Uzae na nani? Kwani nimekwambia nataka mtoto Mimi?"
Shani: "Mbona umeshtuka hivyo, kwani kuna tatizo tukipata mtoto?"
Analyse: : "Nyumbani familia hawawezi kukubali ili jambo"
Shani: "Kwani nazaa na familia au nazaa na wewe, hebu nipishe mie"
Analyse: "Hicho kitu hakipo"
Shani: "Tena usinitibue, hii siku kwangu ni nzuri, mwanaume mzima unaogopa kuwa na mtoto. Na ntawapigia familia yako wote niwachambe, maana wanataka kukuendesha. Wewe mtu mzima, jisimamie"

Nikawahi kuchukua simu yangu ili asije kuiba namba zao mule, maana Kwa akili yake hashindwi kuwapigia kweli.

Akaishia kucheka tu. Alafu akasema;

Shani: "Namba za wakwe ninazo siku nyingi sana, nitaanza na wifi, yeye ndio ataambia na wengine"

Hata hamu na ile zawadi ya PS4 ilikata...
Women can destroy your dreams bro kama haupo makini

Wanakuharibu wanapoteza dira na kila kitu

Mimi ni Mfano halisi ilinichukua nguvu nyingi mno kurudi kwenye mstari sahihi
 
14th Portion

... Nilivyofika kwake, nilipokelewa vizuri kama vile hatukuwa na ugomvi. Nikala, Kisha nikala tena. Zikafatiwa story za hapa na pale. Kutokana na mishe niliyotakiwa kuifanya kesho yake, sikuweza kulala pale. Muda ulivyosogea, nikamwambia inabidi niondoke. Hakunizuia, maana alijua muda wowote anaweza kunipata. Kabla sijaondoka, nikaomba ile PS niondoke nayo.

Hapo ndio kama nilimtibua nyongo, maana sio kwa maneno aliyonitolea. Kana kwamba dakika chache zilizopita, sio sisi tuliokuwa tunafurahi. "Yani wewe unapenda kupokea, kutoa hutaki, haya nenda kaiombe ruhusa familia yako kuwa nataka kukupa zawadi, wakikubali, njoo uchukue, maana maamuzi yako wanafanya wao". Kiufupi alisema kama sipo tayari kukubali takwa lake, basi nisahau kuhusu ile PS. Nikakubaliana na hali. Nikaondoka.

Wakati nipo gheto nawaza dili la kesho tu. Mfano tukipata million 60, pale mgao wangu sio chini ya 10m. Nikaanza kuipangia matumizi kabisa, hapo ndio nikaona Mzee Dingi alikuwa sahihi, dili likifanikiwa naweza survive mwaka mzima bila stress. Baada ya mawazo ya hapa na pale, nikaamua kulala nitulize kichwa.

***** ***** ******* ** ** ****

Niliamka mapema sana, asubuhi ya siku iliyofuata. Ili niwahi pale maeneo ya kisutu, ile njia inapandisha kuelekea mtaa wa Lumumba. Lengo la kwenda pale ilikuwa ni kununua begi lenye muundo wa briefcase. Wakati nipo njiani naelekea pale, Mzee Dingi akanipigia, na kunitaarifu yule mstaafu amepata dharura, hivyo zoezi halitoweza fanyika siku hiyo, tutaenda kesho yake.

Baada ya kuongea nae, niliendelea na safari yangu, maana kivyovyote vile. Lile begi lazima niwe nalo. Baada ya kulininunua, nikaendelea na mishe zangu kama kawaida, kisha nikarudi ghetto. Kesho yake pia dili likabuma. Safari hii likasogezwa mbele wiki nzima.

Ikabidi tukutane wote kujadili nini kifanyike katika iki kipindi tunasubiria yule mstaafu mambo yake yakae sawa. Katika yale maongezi wakawa wanasema kuna kitu hakipo sawa ndio maana dili linakuwa gumu. Mzee Dingi akashauri kama timu, inabidi twende tena kwa mtaalam wao tukaangalie tatizo liko wapi (wao walishaendaga na huwa wanaenda sana). Kwavile Mimi nilikuwa ndio mgeni, wakashauri niwepo siku ya kwenda. Ila Mzee Kesho Yetu akakataa lile swala, akawaambia kwa mganga sio sehemu unayoenda enda tu kila ukitaka. Na kwavile wao walishaenda wiki chache zilizopita, basi ni apostle (Mimi) ndio natakiwa niende.

Mzee KY: "Huyu bwana mdogo ndio inabidi kwenda nae kuangalia shida nini, maana kila kitu kilikuwa sawa kabla hajahusishwa"
Mzee Dingi: "Ni wazo zuri pia, kwahiyo anaendaje?"
Mzee KY: "Nitaenda nae Mimi"
Mzee Dingi: "Ungepumzika tu mkuu, acha niende nae"
Mzee KY: "Hapana hakuna haja, nitaenda nae. Maana nataka nimpeleke sehemu tofauti na ile niliyowapeleka last time"
Mzee Dingi: "Sawa hakuna kama ni hvyo"

Nia yao ilikuwa zoezi la kwenda kwa mtaalam lifanyike wik end, ila nikawaomba wik end hiyo waniache nifanye mambo yangu, alafu jumatatu ndio twende huko kwa mtaalam. Baada ya kuelewana, tukasambalatika, kila mtu na uelekeo wake.

Jumapili asubuhi nikawasiliana na yule Mzee wa Kongowe, akaniambia nimsubirie pale pale aliponichukua mtoto wake mara ya mwisho. Mida ya saa nne, tayari nilikuwa pale, alivyofika tukaondoka wote.

Tulivyofika pale shambani, tulizunguka zunguka kwenye mifugo yake huku tunapiga Story. Dhumuni la kwenda kuonana nae safari hii ilikuwa ni kutaka kumuomba kama anaweza kunisaidia kuniunganisha sehemu yoyote ya ajira, maana maisha ya kuunga unga hayanaga dhamana.

Mzee: "Hicho ndicho najaribu kufanya mwanangu, ila sio rahisi kama unavyodhani"
Analyse: "Ila ulikuwa kwenye mfumo wao Mzee, japo ni ngumu, ila huwezi kosa namna"
Mzee: "Mambo hayapo hivyo kijana. Mimi pia nilifanya kuchomekwa tu, kama unavyojua sitokei kwenye familia zenye mashina na mizizi ya kisiasa. Watu wa kupenyezwa wanapigwa vita sana na inner circle. Na kibaya zaidi utawala ni mpya, kila mtu anajaribu kujitengenezea yeye njia, nani atanikumbuka?
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje kijana wako"
Mzee: "Nitaendelea kuangalia angalia, ukipatikana upenyo, nitakwambia. Ila Sasa hivi wamebana sana mianya yote. Na walengwa tunaobanwa ni sisi, sio wao"
Analyse: "Sawa Mzee"
Mzee: "Mlango mmoja ukifungwa, kuna mwingine mahali fulani utafunguliwa kwa ajili yako, unachotakiwa ni kuwa tayari muda wote maana hujui ni lini, wapi au kutoka Kwa nani mlango wako utafungukia. Kwa umri wako hutakiwi kukata tamaa kabisa, siku zote tumaini ni sauti ya Mungu ndani yetu, bila hiyo huna cha maana utakachofanya".
Analyse: " Nimekuelewa Mzee"
Mzee: "Sawa, nitaendelea kuangalizia upenyo sehemu, ukipatikana nitakwambia, ila am not promising you anything"
Analyse: "Sawa, nashkuru sana"

Tukaendelea na shughuli zingine za hapa na pale, mpaka muda wake wa kuondoka ulivyofika, tukaondoka wote.

Niliendelea kujilaumu mpaka basi, kwa nafasi niliyopoteza. Niliipiga teke njia rahisi, nikachagua kuhangaika kusikokuwa na faida. Kesho jumatatu ilibidi asubuhi ninyonge tai, moka nzuri, unyunyu kisha nielekee ofisini, ila sababu ya uzembe, ntaenda kukutana na wazee wasio na hekima, ili twende kwa mganga. Maisha haya [emoji28][emoji28][emoji28]

Kesho yake mapema nikakutana na Mzee KY maeneo ya mbezi stand ya gari ndogo, safari ya kuelekea Moro ikaanza. Baada ya kufika Moro, tulitembea kwa dakika kama 30 kisha tukaachana na mji, na kuchukua njia kuingia ndani ndani huko. Safari nzima, mawazo yangu yapo kwenye mazungumzo yangu na yule Mzee kule Kongowe.

Mimi na Mzee KY hatukupiga story nyingi njiani, ni Mzee ambae sio muongeaji, muda mwingi anasikiliza tu. Na hizo story chache tulizopiga, ni kwamba alikuwa ananiuliza kitu, then ananiacha nibwabwaje.

Baada ya mwendo wa kama lisaa na nusu au mawili, tukafika mwisho wa safari yetu, then tukaelekea kwa huyo mtaalam wake.

Inaonekana alishawasiliana na yule mtaalam, kumjulisha ujio wetu. Maana tulivyofika, baada ya salamu hapakuwa tena na mazungumzo mengi, nikaambiwa niingie kwenye chumba kilichokuwa vyumba vya nyuma. Mzee KY akamwambia mtaalam bwana mdogo atoke kaiva, mganga akacheka tu. Nikaingia kupikwa kwa mara ya kwanza.

Niliambiwa vitu vinavyotakiwa kununuliwa mfano nazi, karatasi nyeupe, wembe, unga nk. Hela ilitolewa, vikafatwa. Palifanyika mambo mengi sana na mazito, tena kwa muda mrefu. Nilianza kwa kusuguliwa na mchanganyiko wa unga wa sembe na tui la nazi mwili mzima. Vikafatia visomo, chale kuanzia unyayoni mpaka utosini. Kiufupi zoezi lilikuwa zito. Kimoyo moyo najiuliza "Huyu ni Mimi ndio nafanyiwa hivi au?''. Baada ya hapo nikatakiwa kutoka nje vile vile na boksa yangu, mpaka katikati ya kiwanja alafu nirudi ndani. Nikamuuliza yule mganga, "Natoka hivi, na wale watu waliopo nje je?". Mganga akanikata jicho, kiasi kwamba nikajikuta nanyanyuka.

Aisee ukiona mtu anahela, wewe muheshimu tu, haijalishi kazipata vipi. Watu wanasuffer mazee, kila njia ni tough.

Mida ya jioni ndio tulimaliza. Nikapewa dawa ambazo nilitakiwa kujifukiza kwa siku kadhaa, na zingine ambazo nilitakiwa kuoga, lakini hizi za kuoga, sikutakiwa kuziogea bafuni au chooni. Kuna dawa ilikuwa mchanganyiko wa unga mweusi, na mafuta mafuta, hiyo nilitakiwa kuichanganya kwenye mafuta ya nazi, kisha niwe napaka viganjani na usoni kabla ya kutoka nyumbani na kwenda kwenye mishe mishe zangu. Lakini pia nilipewa kitu mfano wa hirizi, ambayo upana wake unakaribia kucha ya kidole cha shahada. Hiyo niliambiwa niwe nayo muda wote. Hizi dawa mbili (ya kupaka na hirizi) zilifanya mpaka kesho nina bifu na Mzee Dingi.

Kila kitu kilivyokuwa kimekamilika, tukaaga na kuondoka. Njiani Mzee KY ananiambia, "Bwana mdogo ukiwa serious kwenye maisha utafika mbali sana, ila kwa muda mchache ambao nimespend na wewe, tatizo lako kubwa ni moja tu"

Nikamuuliza tatizo gani??. Akanijibu, "You don't smile easily". Nikatatizika kidogo, "Kuto tabasamu nalo ni tatizo?". Akanijibu "Bado una mengi ya kujifunza". Nikabaki namwangalia tu. Katikati ya story zilizoendelea, nikajikuta namwambia "Sikuwahi fikiria kama siku moja ningeangukia huku". Akacheka.

Mzee KY: "Tukiwa wadogo, ni ndoto ya kila mtoto kuwa rubani. Hii Dunia jinsi ilivyo, ukiteleza kidogo tu inakuchagulia njia"

Hapo ndio akaniambia machache kuhusu yeye. Katika hayo maongezi yetu ndio niligundua kuwa ana masters ya uhandisi wa umeme, lakini pia ana CPA, ana uwezo wa kuzungumza lugha 3 za kimataifa kwa ufasaha kabisa. Chuo alisomeaga Uganda. Na ana ofisi mbili town, lakini just for backup, japo zinafanya vizuri.

Nilimshangaa sana kwanini ameamua kuendelea na njia ile wakati ana uwezo wa kutengeneza decent money?

Mzee KY: "Sikia bwana mdogo, hii Dunia inaweza kukuchapa alafu haikupi kabisa muda wa kujutia. Na hata ukiwa kwenye kujutia, inaweza ikakuchapa tena, kiasi kwamba ukiwa kwenye kujutia kwako, ndani yake ukapata majuto mengine".

Wakati najaribu kujiuliza amemaanisha Nini, akaendelea, "Unatakiwa kujutia huku unaenda nayo, maana muda haukusubiri".

"Sema sijui kwanini wewe umeingia huku, ila binafsi kisasi na kinyongo nilichokuwa nacho juu ya mtu fulani ndio kimeniingiza huku. Nilipima kina Cha maji kwa mguu, sasa nimeshazama tayari".

Hakuongea tena mpaka alivyonishusha mbezi mwisho.

. ****** ******** ********** ** ***

Baada ya pale, nikanyoosha mpaka gheto kwangu. Kwavile sikuwa nimejiandaa sehemu ya kuogea, ikabidi nibebe ndoo yangu hadi kwenye kiwanja cha shule ya msingi (nilikuwa jirani na shule), nikaenda kuogea pale chap, then nikarudi ghetto kujifukiza ile dawa nyingine. Baada ya hapo nikalala.

Kabla ya kwenda kwa mganga, kuna vitu vingi sana nilikuwa sivielewagi, na sivipatii majibu. Nilikuwa nikipishana na vijana (wakike kwa wakiume), unakuta mtu smart, lakini macho mekunduu kuliko kawaida, japo sio mlevi wala mvutaji sigara. Au mkipishana unahisi harufu ya moshi tu. Nilikuwa najiuliza, hivi hapa mjini kuna watu wanapikia majiko ya kuni au?. Kumbe hakuna bhana, vijana wanajifukiza sana. Tena wameanza kuoga moshi kabla hata ya Corona.

Hizo siku tatu za kujifukiza, nilikuwa nanuka moshi muda wote. Kibaya zaidi, zile dawa za kuoga hutakiwi kutumia sabuni.

Kipindi naendelea na ile dozi. Mzee Dingi akawa ametupa taarifa kuwa alipigiwa simu na yule mlengwa wetu, wamekubaliana zoezi litafanyika siku 6 tokea hiyo siku. Maana alikuwa anajipanga, akishanunua lile eneo basi mipango yake mingine iende haraka pia.

Nikamaliza masharti, tukabaki tunamsikilizia yule mstaafu, japo tulipiga dili kama mbili, na zote zilitiki vizuri tu.

Kile kihirizi alichonipaga yule mtaalam, aliniambia kwavile natakiwa niwe nacho muda wote mwilini, basi naweza kukihifadhi kwa namna tatu. Mosi, nikifunge kwenye kamba, alaf nikibane mkononi kama wanavyofanya makepteni wa mpira, Pili, nikizungushie big g, alaf nikienda eneo la tukio, nikibane mdomoni, tatu, nikitengenezee bangili, au pete ya kukibana then niivae.

Mimi nilitengeneza pete za kacha zile, alafu nikakishonea pale. Nikaivaa kwenye kidole cha pete, mkono wa kulia.

Zikiwa zimebaki siku tatu twende kwenye lile dili kubwa. Nilikuwa zangu gheto tu nimekaa, wazo likanijia nikajaribishe zile dawa sehemu. Akili ikanituma niende kwa Shani.

Mida ya jioni, nikaoga, nikapaka mafuta yangu ya nazi yenye dawa, mikononi na usoni. Kisha nikatoka.

Aisee Hii Dunia ni zaidi ya tuijuavyo. Kuna vitu vingi sana vipo beyond our explanations.......
[emoji847]
 
14th Portion

... Nilivyofika kwake, nilipokelewa vizuri kama vile hatukuwa na ugomvi. Nikala, Kisha nikala tena. Zikafatiwa story za hapa na pale. Kutokana na mishe niliyotakiwa kuifanya kesho yake, sikuweza kulala pale. Muda ulivyosogea, nikamwambia inabidi niondoke. Hakunizuia, maana alijua muda wowote anaweza kunipata. Kabla sijaondoka, nikaomba ile PS niondoke nayo.

Hapo ndio kama nilimtibua nyongo, maana sio kwa maneno aliyonitolea. Kana kwamba dakika chache zilizopita, sio sisi tuliokuwa tunafurahi. "Yani wewe unapenda kupokea, kutoa hutaki, haya nenda kaiombe ruhusa familia yako kuwa nataka kukupa zawadi, wakikubali, njoo uchukue, maana maamuzi yako wanafanya wao". Kiufupi alisema kama sipo tayari kukubali takwa lake, basi nisahau kuhusu ile PS. Nikakubaliana na hali. Nikaondoka.

Wakati nipo gheto nawaza dili la kesho tu. Mfano tukipata million 60, pale mgao wangu sio chini ya 10m. Nikaanza kuipangia matumizi kabisa, hapo ndio nikaona Mzee Dingi alikuwa sahihi, dili likifanikiwa naweza survive mwaka mzima bila stress. Baada ya mawazo ya hapa na pale, nikaamua kulala nitulize kichwa.

***** ***** ******* ** **

Niliamka mapema sana, asubuhi ya siku iliyofuata. Ili niwahi pale maeneo ya kisutu, ile njia inapandisha kuelekea mtaa wa Lumumba. Lengo la kwenda pale ilikuwa ni kununua begi lenye muundo wa briefcase. Wakati nipo njiani naelekea pale, Mzee Dingi akanipigia, na kunitaarifu yule mstaafu amepata dharura, hivyo zoezi halitoweza fanyika siku hiyo, tutaenda kesho yake.

Baada ya kuongea nae, niliendelea na safari yangu, maana kivyovyote vile. Lile begi lazima niwe nalo. Baada ya kulininunua, nikaendelea na mishe zangu kama kawaida, kisha nikarudi ghetto. Kesho yake pia dili likabuma. Safari hii likasogezwa mbele wiki nzima.

Ikabidi tukutane wote kujadili nini kifanyike katika iki kipindi tunasubiria yule mstaafu mambo yake yakae sawa. Katika yale maongezi wakawa wanasema kuna kitu hakipo sawa ndio maana dili linakuwa gumu. Mzee Dingi akashauri kama timu, inabidi twende tena kwa mtaalam wao tukaangalie tatizo liko wapi (wao walishaendaga na huwa wanaenda sana). Kwavile Mimi nilikuwa ndio mgeni, wakashauri niwepo siku ya kwenda. Ila Mzee Kesho Yetu akakataa lile swala, akawaambia kwa mganga sio sehemu unayoenda enda tu kila ukitaka. Na kwavile wao walishaenda wiki chache zilizopita, basi ni apostle (Mimi) ndio natakiwa niende.

Mzee KY: "Huyu bwana mdogo ndio inabidi kwenda nae kuangalia shida nini, maana kila kitu kilikuwa sawa kabla hajahusishwa"
Mzee Dingi: "Ni wazo zuri pia, kwahiyo anaendaje?"
Mzee KY: "Nitaenda nae Mimi"
Mzee Dingi: "Ungepumzika tu mkuu, acha niende nae"
Mzee KY: "Hapana hakuna haja, nitaenda nae. Maana nataka nimpeleke sehemu tofauti na ile niliyowapeleka last time"
Mzee Dingi: "Sawa hakuna kama ni hvyo"

Nia yao ilikuwa zoezi la kwenda kwa mtaalam lifanyike wik end, ila nikawaomba wik end hiyo waniache nifanye mambo yangu, alafu jumatatu ndio twende huko kwa mtaalam. Baada ya kuelewana, tukasambalatika, kila mtu na uelekeo wake.

Jumapili asubuhi nikawasiliana na yule Mzee wa Kongowe, akaniambia nimsubirie pale pale aliponichukua mtoto wake mara ya mwisho. Mida ya saa nne, tayari nilikuwa pale, alivyofika tukaondoka wote.

Tulivyofika pale shambani, tulizunguka zunguka kwenye mifugo yake huku tunapiga Story. Dhumuni la kwenda kuonana nae safari hii ilikuwa ni kutaka kumuomba kama anaweza kunisaidia kuniunganisha sehemu yoyote ya ajira, maana maisha ya kuunga unga hayanaga dhamana.

Mzee: "Hicho ndicho najaribu kufanya mwanangu, ila sio rahisi kama unavyodhani"
Analyse: "Ila ulikuwa kwenye mfumo wao Mzee, japo ni ngumu, ila huwezi kosa namna"
Mzee: "Mambo hayapo hivyo kijana. Mimi pia nilifanya kuchomekwa tu, kama unavyojua sitokei kwenye familia zenye mashina na mizizi ya kisiasa. Watu wa kupenyezwa wanapigwa vita sana na inner circle. Na kibaya zaidi utawala ni mpya, kila mtu anajaribu kujitengenezea yeye njia, nani atanikumbuka?
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje kijana wako"
Mzee: "Nitaendelea kuangalia angalia, ukipatikana upenyo, nitakwambia. Ila Sasa hivi wamebana sana mianya yote. Na walengwa tunaobanwa ni sisi, sio wao"
Analyse: "Sawa Mzee"
Mzee: "Mlango mmoja ukifungwa, kuna mwingine mahali fulani utafunguliwa kwa ajili yako, unachotakiwa ni kuwa tayari muda wote maana hujui ni lini, wapi au kutoka Kwa nani mlango wako utafungukia. Kwa umri wako hutakiwi kukata tamaa kabisa, siku zote tumaini ni sauti ya Mungu ndani yetu, bila hiyo huna cha maana utakachofanya".
Analyse: " Nimekuelewa Mzee"
Mzee: "Sawa, nitaendelea kuangalizia upenyo sehemu, ukipatikana nitakwambia, ila am not promising you anything"
Analyse: "Sawa, nashkuru sana"

Tukaendelea na shughuli zingine za hapa na pale, mpaka muda wake wa kuondoka ulivyofika, tukaondoka wote.

Niliendelea kujilaumu mpaka basi, kwa nafasi niliyopoteza. Niliipiga teke njia rahisi, nikachagua kuhangaika kusikokuwa na faida. Kesho jumatatu ilibidi asubuhi ninyonge tai, moka nzuri, unyunyu kisha nielekee ofisini, ila sababu ya uzembe, ntaenda kukutana na wazee wasio na hekima, ili twende kwa mganga. Maisha haya [emoji28][emoji28][emoji28]

Kesho yake mapema nikakutana na Mzee KY maeneo ya mbezi stand ya gari ndogo, safari ya kuelekea Moro ikaanza. Baada ya kufika Moro, tulitembea kwa dakika kama 30 kisha tukaachana na mji, na kuchukua njia kuingia ndani ndani huko. Safari nzima, mawazo yangu yapo kwenye mazungumzo yangu na yule Mzee kule Kongowe.

Mimi na Mzee KY hatukupiga story nyingi njiani, ni Mzee ambae sio muongeaji, muda mwingi anasikiliza tu. Na hizo story chache tulizopiga, ni kwamba alikuwa ananiuliza kitu, then ananiacha nibwabwaje.

Baada ya mwendo wa kama lisaa na nusu au mawili, tukafika mwisho wa safari yetu, then tukaelekea kwa huyo mtaalam wake.

Inaonekana alishawasiliana na yule mtaalam, kumjulisha ujio wetu. Maana tulivyofika, baada ya salamu hapakuwa tena na mazungumzo mengi, nikaambiwa niingie kwenye chumba kilichokuwa vyumba vya nyuma. Mzee KY akamwambia mtaalam bwana mdogo atoke kaiva, mganga akacheka tu. Nikaingia kupikwa kwa mara ya kwanza.

Niliambiwa vitu vinavyotakiwa kununuliwa mfano nazi, karatasi nyeupe, wembe, unga nk. Hela ilitolewa, vikafatwa. Palifanyika mambo mengi sana na mazito, tena kwa muda mrefu. Nilianza kwa kusuguliwa na mchanganyiko wa unga wa sembe na tui la nazi mwili mzima. Vikafatia visomo, chale kuanzia unyayoni mpaka utosini. Kiufupi zoezi lilikuwa zito. Kimoyo moyo najiuliza "Huyu ni Mimi ndio nafanyiwa hivi au?''. Baada ya hapo nikatakiwa kutoka nje vile vile na boksa yangu, mpaka katikati ya kiwanja alafu nirudi ndani. Nikamuuliza yule mganga, "Natoka hivi, na wale watu waliopo nje je?". Mganga akanikata jicho, kiasi kwamba nikajikuta nanyanyuka.

Aisee ukiona mtu anahela, wewe muheshimu tu, haijalishi kazipata vipi. Watu wanasuffer mazee, kila njia ni tough.

Mida ya jioni ndio tulimaliza. Nikapewa dawa ambazo nilitakiwa kujifukiza kwa siku kadhaa, na zingine ambazo nilitakiwa kuoga, lakini hizi za kuoga, sikutakiwa kuziogea bafuni au chooni. Kuna dawa ilikuwa mchanganyiko wa unga mweusi, na mafuta mafuta, hiyo nilitakiwa kuichanganya kwenye mafuta ya nazi, kisha niwe napaka viganjani na usoni kabla ya kutoka nyumbani na kwenda kwenye mishe mishe zangu. Lakini pia nilipewa kitu mfano wa hirizi, ambayo upana wake unakaribia kucha ya kidole cha shahada. Hiyo niliambiwa niwe nayo muda wote. Hizi dawa mbili (ya kupaka na hirizi) zilifanya mpaka kesho nina bifu na Mzee Dingi.

Kila kitu kilivyokuwa kimekamilika, tukaaga na kuondoka. Njiani Mzee KY ananiambia, "Bwana mdogo ukiwa serious kwenye maisha utafika mbali sana, ila kwa muda mchache ambao nimespend na wewe, tatizo lako kubwa ni moja tu"

Nikamuuliza tatizo gani??. Akanijibu, "You don't smile easily". Nikatatizika kidogo, "Kuto tabasamu nalo ni tatizo?". Akanijibu "Bado una mengi ya kujifunza". Nikabaki namwangalia tu. Katikati ya story zilizoendelea, nikajikuta namwambia "Sikuwahi fikiria kama siku moja ningeangukia huku". Akacheka.

Mzee KY: "Tukiwa wadogo, ni ndoto ya kila mtoto kuwa rubani. Hii Dunia jinsi ilivyo, ukiteleza kidogo tu inakuchagulia njia"

Hapo ndio akaniambia machache kuhusu yeye. Katika hayo maongezi yetu ndio niligundua kuwa ana masters ya uhandisi wa umeme, lakini pia ana CPA, ana uwezo wa kuzungumza lugha 3 za kimataifa kwa ufasaha kabisa. Chuo alisomeaga Uganda. Na ana ofisi mbili town, lakini just for backup, japo zinafanya vizuri.

Nilimshangaa sana kwanini ameamua kuendelea na njia ile wakati ana uwezo wa kutengeneza decent money?

Mzee KY: "Sikia bwana mdogo, hii Dunia inaweza kukuchapa alafu haikupi kabisa muda wa kujutia. Na hata ukiwa kwenye kujutia, inaweza ikakuchapa tena, kiasi kwamba ukiwa kwenye kujutia kwako, ndani yake ukapata majuto mengine".

Wakati najaribu kujiuliza amemaanisha Nini, akaendelea, "Unatakiwa kujutia huku unaenda nayo, maana muda haukusubiri".

"Sema sijui kwanini wewe umeingia huku, ila binafsi kisasi na kinyongo nilichokuwa nacho juu ya mtu fulani ndio kimeniingiza huku. Nilipima kina Cha maji kwa mguu, sasa nimeshazama tayari".

Hakuongea tena mpaka alivyonishusha mbezi mwisho.

. ****** ******** ********** ** ***

Baada ya pale, nikanyoosha mpaka gheto kwangu. Kwavile sikuwa nimejiandaa sehemu ya kuogea, ikabidi nibebe ndoo yangu hadi kwenye kiwanja cha shule ya msingi (nilikuwa jirani na shule), nikaenda kuogea pale chap, then nikarudi ghetto kujifukiza ile dawa nyingine. Baada ya hapo nikalala.

Kabla ya kwenda kwa mganga, kuna vitu vingi sana nilikuwa sivielewagi, na sivipatii majibu. Nilikuwa nikipishana na vijana (wakike kwa wakiume), unakuta mtu smart, lakini macho mekunduu kuliko kawaida, japo sio mlevi wala mvutaji sigara. Au mkipishana unahisi harufu ya moshi tu. Nilikuwa najiuliza, hivi hapa mjini kuna watu wanapikia majiko ya kuni au?. Kumbe hakuna bhana, vijana wanajifukiza sana. Tena wameanza kuoga moshi kabla hata ya Corona.

Hizo siku tatu za kujifukiza, nilikuwa nanuka moshi muda wote. Kibaya zaidi, zile dawa za kuoga hutakiwi kutumia sabuni.

Kipindi naendelea na ile dozi. Mzee Dingi akawa ametupa taarifa kuwa alipigiwa simu na yule mlengwa wetu, wamekubaliana zoezi litafanyika siku 6 tokea hiyo siku. Maana alikuwa anajipanga, akishanunua lile eneo basi mipango yake mingine iende haraka pia.

Nikamaliza masharti, tukabaki tunamsikilizia yule mstaafu, japo tulipiga dili kama mbili, na zote zilitiki vizuri tu.

Kile kihirizi alichonipaga yule mtaalam, aliniambia kwavile natakiwa niwe nacho muda wote mwilini, basi naweza kukihifadhi kwa namna tatu. Mosi, nikifunge kwenye kamba, alaf nikibane mkononi kama wanavyofanya makepteni wa mpira, Pili, nikizungushie big g, alaf nikienda eneo la tukio, nikibane mdomoni, tatu, nikitengenezee bangili, au pete ya kukibana then niivae.

Mimi nilitengeneza pete za kacha zile, alafu nikakishonea pale. Nikaivaa kwenye kidole cha pete, mkono wa kulia.

Zikiwa zimebaki siku tatu twende kwenye lile dili kubwa. Nilikuwa zangu gheto tu nimekaa, wazo likanijia nikajaribishe zile dawa sehemu. Akili ikanituma niende kwa Shani.

Mida ya jioni, nikaoga, nikapaka mafuta yangu ya nazi yenye dawa, mikononi na usoni. Kisha nikatoka.

Aisee Hii Dunia ni zaidi ya tuijuavyo. Kuna vitu vingi sana vipo beyond our explanations.......
@analyse , uko serious ulipitia haya au unatupiga kamba?
mpaka chale, hirizi, kuoga sehemu ya wazi....[emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji44],

kumbe akina UMUGHAKA mko wengi aiseee...... yeye alipiga miti jini
 
Back
Top Bottom