Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

11th Portion:

... Kabla sijamfata nje, nikahakikisha kwanza kama milango Iko wazi au kama kaacha kamfungia Bi Mkubwa kwa nje. Nilivyokuta Iko wazi, ndio nikamfata.

Tofauti na matarajio yangu, kule nje Mshua alikuwa mpole sana kuliko kawaida yake. Na alikuwa anaongea kama mtu ambae mawazo yake yapo mbali sana.

Mshua: "Hivi unajua Mimi na yako ndoa yetu inamuda gani?
Analyse: "Nahisi kama thelathin naaa hivi"
Mshua: "Unahisi sio?". Sasa sikiliza, nilianza mahusiano na Mama yako mwaka 75, ila nilikuja kufunga nae ndoa mwaka 82. Katika kipindi icho chote tulikuwa na furaha sana. Na hata baada ya kufunga ndoa furaha na upendo viliongezeka pia. Katika kipindi chote icho, ugomvi serious ambao ulishawahi kutokea kati yetu, ilikuwa ni mara moja, mengine ni ya kawaida tu"

Nikabaki namwangalia tu, bila kumkatisha. Akaendelea "Ila tokea umezaliwa wewe, ugomvi kati yetu imekuwa kitu cha Kawaida sana. Kwanza sasa hivi Mimi sio priority tena kwa mke wangu, hasa wewe ukiwepo hapa nyumbani"

Nikajikuta nataka kucheka, yani Mshua na umri ule bado analia wivu?. Akaniwahi "Cheka uone nini kitafatia". Nikajibana, ila yeye ndio akajikuta anacheka [emoji28][emoji28].

Akaniambia sikia "Nakukumbusha kuwa wewe sio last born, na Safari hii ukiondoka hapa usirudi tena bila mke. Yani wewe yeyote tu njoo nae Mimi kama baba nitampokea". Nikabaki nimeshangaa, Mzee Vipi?

Akaendelea "Ili kulegeza bond ya wewe na Mama yako, inabidi na wewe uoe, swala la utamuoa nani, utajua mwenyewe"

"Pia kitu kingine cha muhimu, unamkumbuka yule Mzee niliyekupaga namba yake?". Nikamjibu ndio, "Ukifika mjini, safari hii fanya juu chini uonane nae". Nikamjibu hakuna shida nitafanya hivyo.

Tukaongea mambo mengine tofauti tofauti ya kiutafutaji. Wakati tunahitimisha, ili turudi ndani maana Bi Mkubwa alituita tukale, Mshua akanisisitiza tena "Ukijiona unataka kurudi huku bila mke, basi uishie center, nitakufata tuongelee huko huko, na hakuna kumwambia Mama yako kuwa unakuja. Ila ukijitoa akili ukaja mpaka huku kijijini bila mke, basi jua lazima nikuozeshe binti yeyote wa hapa kijijini, swala la kumpenda, utampenda mbele ya safari ukishamzoea. Na ni lazima uondoke nae". Kumbe Bi Mkubwa alikuwa kasimama dirishani, haya maongezi ya mwisho mwisho akayasikia, nae akatoka nje "Kumbe ndio maana mmekuja kujificha, hayo ndio maongezi yenyewe?. Kama wewe ulitafutiwa mke, hizo ni enzi zenu, sio zama hizi. Mwanangu hachaguliwi mke, mwanangu oa ukiwa tayari, na ukiwa na mwanamke utakayemtaka, wala hakuna presha."

Hii kauli ya Bi Mkubwa nikawa sijaielewa, anamaanisha Mshua alitafutiwa mke?. Sikutaka inipite, ikabidi niulize. "Kumbe Baba alitafutiwa mke?". Mama akataka kujibu, ila Mshua akamuwahi na kunijibu "Achana nae, hajui anachokiongea huyo.

Mama (akacheka kidogo): "Kwamba sijui ninachokiongea?. Kumbe wanao hawajui story yako? (Akacheka tena)"

Analyse: "Story gani hiyo?. Baba siumetoka kuniambia umejuana na Mama tokea miaka ya 70, ukamuoa miaka ya 80?. Kuna story tofauti na hiyo?". Mama akawa anacheka tu.

Mshua: "Kwani mtu akituma mshenga, hapo anakuwa katafutiwa mke?. Huyu mama ako haelewi mambo yanavyoenda". Akamalizia kwa kicheko.

Ila kila Bi Mkubwa alipokuwa anataka kuongea, Mshua anamcrash as if anazuia asiongee. Nikajaribu kum-probe Bi Mkubwa walau anipe hiyo story ila akaishia kucheka.

Mama: "Atakuambia mwenyewe huyo, ila Cha msingi oa mwanamke utakayemtaka wala asikulazimishe"

Mshua: "Si alikuja na yule rafiki yangu, nusura ufe kwa kihoro hapa ukijua ndio mka mwana [emoji28][emoji28][emoji28]"

Bi Mkubwa akamkata jicho bila kusema kitu, alaf akanigeukia Mimi, "Sema na wewe usije kutuletea kizaa zaa kama cha yule wa kipindi kile"

Nikaishia kutabasam tu, Kisha tukaingia ndani kula.

******** ****** ******* ***** *******

Baada ya siku mbili nikaondoka pale nyumbani. Kufika town, ramani zote hazisomeki. Nikamcheki yule Mzee, baada ya kunitambua tukaongea mawili matatu. Akaulizia kuhusu afya yangu, then tukaweka appointment nikaonanae mwishoni mwa wiki. Akanielekeza maeno ya Kongowe, kuna sehemu unapanda milimani, Mlamleni kwa mbele mbele huko. Sikuwa nimewahi kufika maeneo yale, ila nikasema itabidi niende.

Ilivyofika siku tuliyokubaliana. Wakati nipo njiani, akanipigia simu. Baada ya salamu akaniuliza,

Mzee: "Vipi umeshaanza safari ya kuja huku?"
Analyse: "Ndio Mzee"
Mzee: "Ukifika Kongowe mwisho, subiria hapo, kuna kijana wangu yupo njiani nae anakuja huku. Yupo na gari, mtakuja wote"
Analyse: "Sawa Mzee"

Nikafika mpaka pale, nikasubiria. Muda kidogo napigiwa simu, baada ya kuongea nae ndio nikajua ni huyo kijana ninayetakiwa kwenda nae. Nikasogea hadi alipopaki gari, then safari ikaanza. Njiani no story, hadi tunafika.

Kufika, ni eneo fulani kubwa, pia lina uzio. Ila kwa ndani sehemu kubwa Iko wazi, kuna mabanda mengi ya mifugo na nyumba moja ya kuishi watu, ambayo imejitenga kiasi chake.

Tukapokelewa na mlinzi. Baada ya muda kidogo, yule Mzee ndio akaja. Tokea nimeanza kuwasiliana nae, kwa mara ya kwanza hiyo ndio siku tulikuwa tunaonana. Nilishtuka kumuona, japo hiyo siku ndio ilikuwa tunakutana ana kwa ana, ila sura yake haikuwa ngeni kwangu, ni mtu ambae sura yake iko very popular. Alishawahi kuhudumu nyazfa kadhaa kwenye serikali, awamu za nyuma kabla ya Ngosha.

Ni mtu ambae najua tunatokea nae mkoa mmoja, ila sikuwahi jua kama anafahamiana na Mshua. Na hata Mshua siku zote anavyoniambiaga nikaonane nae, hakuwahi niambia huyo mtu ni nani haswa.

Yule Mzee kaniambia nimsubirie amalizie kuangalia mifugo yake na kuweka mambo sawa, kisha tutaongea. Na kweli baada ya kama dakika 45, akaniambia tuongozane kuelekea kwenye ile nyumba iliyojitenga. Lakini kabla hatujaifikia, akabadili mawazo, akamuagiza mmoja wa vijana waliokuwepo pale atuletee vitu, then tukaenda kukaa chini ya mti.

Wakati tunaweka viti vizuri ili tukae, akaniambia

Mzee: "Mbona kama umeshangaa kuniona Mimi, ulitarajia kukutana na nani?
Analyse: "Hapana sio hivyo Mzee, ni vile sikutarajia kukutana na sura ninayoifahamu"
Mzee: "Haya niambie ushawahi kuiona wapi hii sura unayosema unaifahamu?"

Sikujibu kitu, nikaishia kutabasam tu kama namna ya kuzuga.

Mzee: "Inaonekana uko busy sana"
Analyse: "Hapana Mzee"
Mzee: "Kwanini hukunitafuta kipindi chote icho, mpaka ile juzi ulivyo nipigia?."

Nikakosa utetezi.

Akaendelea

Mzee: "Kipindi kile tunawasiliana kwa mara ya kwanza, ndio nilikuwa kwenye mchakato wa kustaaf. Kwasasa nimstaafu, nakujaga kupoteza muda na mifugo huku"
Analyse: "Ni jambo zuri, ukisema ukae tu, mwili utashambuliwa sana na maradhi"
Mzee: "Ni kweli, maana umri huu hakuna tena kash kash"

Tuliongea vitu kadhaa, ambavyo ni kama tulikuwa tunajenga msingi wa dhumuni lililofanya tuwe pale. Baada ya hizo story za hapa na pale kuisha, tukaenda kwenye dhumuni sasa. Maongezi ambayo mpaka leo natamani nisingeyasikia au kuyajua. Ni maongezi ambayo kila nikiyafikiria, huwa naishia kujifyonya mwenyewe.

Maongezi ambayo yalifanyika kwa masaa machache ila yamekuwa yakiniumiza kwa muda mrefu.

Kiufupi, ni maongezi ambayo yananifanya najilaumu kila iitwayo leo......

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Dingi wako mtambo ee sasa ungerudi bila mke ha ha sipati pic sijui ungeozeshwa nani [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Hahaha dah,kwa hiyo mzee ukatoka nduki baada ya beka kuitiwa kazi yake????
 
18th Portion:

Baada ya kuachana na Mzee Dingi, nilirudi gheto direct. Siku hiyo hiyo mida ya jioni, yule mama mstaafu akanipigia simu;

Mstaafu: "Hujambo mwanangu?"
Analyse: "Mzima mama, shikamoo"
Mstaafu: "Marahaba. Vipi utakuwepo mjini mpaka lini?"
Analyse: "Kuna vitu naweka sawa, vikikamilika nitaondoka. Inaweza ikawa Jumatatu au Jumanne"
Mstaafu: " Tunaweza kuonana kabla hujaondoka?"
Analyse: "Sawa hakuna shida, nadhani Jumatatu jioni nitakuja".


Baada ya kuongea na yule mstaafu, jioni hiyo hiyo, Mzee KY nae akanipigia simu, kuniambia tuonane siku ya Jumatatu jioni bila kukosa, ili tuweke sawa mambo kadhaa. So, ndani ya siku moja nikawa na appointments mbili, na zote jioni.

Wa kwanza kuonana nae ni Mzee KY, tulikutana mida ya saa kumi kumi.

Mzee KY: "Umeshaongea na yule mama au kuonana nae tokea ufike mjini?"
Analyse: "Hapana, kwanini?
Mzee KY: "Ulimwambia chochote labda kuhusu huu mpango?"
Analyse: "Hapana, vipi kwani?"
Mzee KY: "Oky Vizuri, sasa shika hizi hesabu" (akatoa hela na kunipa).

Nikahesabu, zikafika laki 3 na nusu. Nikamuuliza za nini hizi?

Mzee KY: "Huo ndio mgao wako, kwenye ili dili haupo tena"

Nikabaki nimeshangaa, sipo Kivipi?. Maana kama sipo basi dili limekufa, ila yeye mbona anaongea as if dili bado lipo?.

Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu, akaniambia "Wewe ulikuwa plan A, haikuwa plan pekee. Kwahiyo kama nilivyokwambia, naomba ukae pembeni, dili litaenda bila uwepo wako. Na usije kumwambia chochote yule Mama"

Nikabaki na mwangalia tu. Hapa ndio alikuja kunipa maelezo ambayo nilikuja kuhitimisha kuwa, uwepo wangu kwenye lile dili haikuwa coincidence, kila kitu kilikuwa planned. Aliifahamu connection yangu na yule mama, na dhumuni la kunifanya Mimi kuplay role ya mwenyekiti, ili niweze kugain trust ya yule mama Kwa urahisi. Na hata kile kitendo cha Mzee Dingi Kuni unblock na kunitaka nipige nao kazi, yote ilikuwa ni maandalizi ya ili dili. Halikuja ghafla kama nilivyodhani. Baadhi ya maelezo aliyonipa, ndiyo niliyaelezea jana. Japo kuna mengine niliyaelezea jana, ila yeye alikuja kuniambia mbeleni kabisa wakati dili limeshafanyika.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, tukaagana. Sikuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kule kwa mstaafu, ikabidi nielekee kule.

Nikiwa zangu mdogo mdogo nishakaribia kwa yule, Sina ili wala lile. Kumbe Mzee KY alikuwa ameniungia tela. Sikujua kama dhamira yake ilikuwa kupajua ninapoishi au alitaka kujua nitaelekea wapi baada ya sisi kuachana pale kwenye ile Pub. Naingia tu kwenye ile nyumba, na yeye huyu hapa. Kwa haraka haraka, mtu angeweza kuhisi kuwa tulikuwa tumeongozana wakati tunaenda pale.

Nilishtuka kumuona, japo sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia yeye kuwa pale. Yule Mama mstaafu alipotuona wote alifurahi sana;

Mstaafu: "Naona watu muhimu mmeamua kunijia kwa pamoja, karibuni sana"
Analyse: "Asante sana"
Mzee KY: "Kijana alinipigia simu niungane nae kuja kukuona. Vipi za tokea siku ile?
Mstaafu: "Salama tu, Tunamshkuru Mungu uzima upo kama unavyotuona"

Kisha akanigeukia Mimi;

Mstaafu: "Karibu tena nyumbani, ila this time karibu kama mwenyekiti"

Aliniambia hayo maneno huku anacheka, Mzee KY nae akacheka kidogo. Tukaingia na kukaa sebleni kwake. Maongezi yote kayatawala yule mama tu. Kuna muda akaingia chumbani huko, kisha akatoka na hela;

Mstaafu: "Nilikwambia nitakurudishia hela ya Kodi uliyoacha, chukua laki mbili yako. Sitaki dhulma Mimi, najua kijana ndio kwanza unaanza kujijenga".

Mzee KY akamakinika kuona nitafanya nini. Binafsi nikaamua kuzikataa zile hela;

Analyse: "Hapana mama, nilihama kwa hiari yangu hii hela wala sio deni kwako"
Mstaafu: "Chukua mwanangu, hii haiusiani na kule kusainishiana, maana kule najua huwezi kuniangusha. Nakupa kama kijana wangu tu".

Unajua siku zote wakati nakua, kuna methali ilikuwaga maarufu sana.

"Sikio la kufa halisikii dawa"

Ukikanywa, usiposikia lazima uambiwe. Siku zote nilikuwa naichukulia kama methali tu, lakini in a real sense kwa mara ya kwanza nimekutana na ilo "Sikio la kufa". Unajua ili umuokoe mtu anayezama, sharti awe mtulivu vinginevyo mtazama wote. Au la, basi mpe kijiti, akishike umvute. Sasa huyu mama kila nikimpa kijiti, anakikataa. Kimoyo moyo nikajisemea atajijua mwenyewe.

Analyse: "Usijali mama, hiyo hela wewe Kaa nayo. Nimeondoka kwa amani kabisa, nikiichukua nitajisikia vibaya".

Akabaki na hela yake. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Mzee KY akaomba niwapishe waongee kidogo. Sikuwa na namna, nikatoka zangu nje, wakaongea mambo yao kwa takribani nusu saa au dakika arobaini na tano. Baada ya hapo Mzee KY akatoka nje, tukaondoka wote.

Baada ya kutoka pale, akatafuta sehemu. Akaniweka kikao tena;

Mzee KY: "Sikia kijana, hivi unaweza kukadilia gharama kiasi gani imetumika kuandaa Ili dili?".

Ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu akaendelea tena;

"Mlivyokuja kule site, uliwaona wale majirani niliosalimiana nao?. Wale wote nimetoka nao huku. Uliwaona wale watu wanaolima pale?. Sijui hata wanalima nini, ila nao nimewaweka Mimi."

Akaendelea;

"Dili lifanikiwe au lisifanikiwe, hao wote lazima wapate hela yao. Sasa hebu niambie, lisipofanikiwa hela za kuwalipa zinatoka wapi?"

"Kuna watu huwezi kuwasaidia hata ufanye vipi, they are destined to lose. Hata ukisema umuache na hela zake akanunue eneo halali, still zile hela ataenda kuzifukia chini akitegemea zitachipua, ila ataambulia hasara. Najua hukuchukua ile laki mbili yake, sio kwamba huitaki au unamuonea huruma, bali you feel guilty. Nitakupa Mimi ile laki mbili, soon after dili kufanikiwa, ila for now naomba usinizibie njia, maana siwezi elezea nitakachokufanya. Umenisikia..........?'' Akataja jina langu halisi.

Nikashtuka, amelijuaje jina langu?.

Mzee KY
: "Wote mliopo kwenye Ili dili hakuna nisiyemjua, kuanzia anapokaa au sehemu zake za kwanza kukimbilia hapa mjini, kwahiyo kabla hujafanya jambo utakalokuja kulijutia, ni heri ujifikirie mara mbili"

Nikabaki nimeduwaa tu Kwa muda, sielewi what next. Akaniambia, "Huna haja ya kuendelea kubaki hapa, wahi ukapange vitu kwenye makazi yako mapya, japo nakushauri hama". Hakusubiria jibu langu, akaondoka.

So, he knows me well?. Why nihame wakati ndio kwanza nimehamia au kuna msala unanisubiria? Wazo likanijia, kwanza yule mstaafu tumejuliana mjini hapa hapa, atajijua mwenyewe, ngoja nijihangaikie Mimi.

Nilivyofika ghetto, Yale maneno ya Mzee KY kuwa nihame pale, yakawa yananijia. Nikajikuta njia panda, nipange vitu au nijiandae kuhama?. Ila nimetoka kulipa Kodi ya miezi 6 siku chache tu zilizopita, nahamaje? Mbona ntakuwa nafaidisha wenye nyumba?. Lakini taswira ya Mzee KY ikawa hainipi picha nzuri ya yajayo. Akili ikaniambia nisipange vile vitu, nihame.

Nikampigia simu mwenye nyumba, kumuomba kesho tuonane kama ataweza. Akakubali.

Asubuhi nilivyoonana nae, nikampanga kuwa nimepata dharura natakiwa kusafiri haraka nje ya mkoa, anirudishie hata nusu kodi. Akanijibu "Mwanangu Cha kukusaidia hapa, labda nikuhifadhie vitu vyako kwahiyo miezi 6 utakayokuwa unapambana na hiyo dharura yako"

Nikaona hapa siwezi ambulia hata mia, cha zaidi nitapoteza muda tu kumbembeleza.

Kipindi Mimi nawaza namna ya kuhama pale. Mzee Dingi akanipigia simu na kuomba tuonane.

Nikafikiria huyu nikutane nae maeneo yapi?. Kipindi kile maeneo ya Tabata kuna mashindano ya mpira wa miguu yalikuwa yanaendelea. Viwanja vilivyokuwa vinatumika ni kile Cha Sigara na cha Tabata shule. Nikaona option ya Tabata shule ndio sahihi, maana ni mbali kiasi na ninapoishi. Lakini sababu nyingine iliyofanya nisione shida kukutana nae Tabata, ni kwavile nilikuwa natarajia kuhama.

Nikamwambia tukutane Tabata shule. Mzee Dingi akagoma, na hii ni kwavile pale ni karibu sana mitaa anayoishi yeye. Nilivyóona bado anakomaa tuchange location, nikamwambia basi sitaki kuonana na wewe. Endelea na mishe zako.

Nilipata ujasili wa kumwambia vile kutokana na sababu Kuu mbili, kwanza kwenye dili lao sipo tena, alafu pili sijui anataka tuongee nini. Alivyoona nimekataa kuonana nae, hakuwa na choice zaidi ya kukubali tukutane maeneo yale.

Mida ya jioni nikasogea pale Tabata shule. Mzee Dingi alikuwa ameshafika kabla yangu. Mara zote ambazo tumekuwa tukikutana, vikao vilikuwa vinafanyikia either bar, pub or kwenye mgahawa. Ila this time hakutaka tukutane maeneo hayo. Akapendekeza tukutane kwenye yale majengo ya shule ya Kijapan (kuna shule ilijengwa na Wajapani maeneo yale). Nikajiuliza mara mbili mbili, why kachagua kule?. Ila kimoyo moyo nikajisemea akileta za kuleta, nitamfumua. Hasira zangu zote ziishie kwake.

Akanielekeza alipokuwa amesimama, nikamfata. Kufika pale, navikuta vizee vyote vitatu vipo. Mzee Dingi, Mzee Kidevu na Mwanasheria feki. Nikajiuliza vinanitakia nini?.

Nilivyowaona, sura zao zote ziliakisi shari, ila sikuwa na namna zaidi ya kuwasogelea. Zikapigwa story za hapa na pale, lakini Unaona kabisa hapa kuna jambo litatokea muda sio mrefu. Na Mimi kwa hasira nilizokuwa nazo, nikawa nasubiria kwa hamu ilo jambo litokee. Kwa jinsi tulivyokuwa tumejipanga, Mzee Kidevu alikuwa nyuma kidogo upande wangu wa kushoto, alafu mwanasheria feki na Mzee Dingi walikuwa mbele, tupo face to face. Tukiwa tunaendelea kuongea upande, kwa ghafla sana yule Mzee Kidevu akanirukia horizontally na kunipiga kichwa cha mbavu. Ni kitu ambacho sikuwa nimekitarajia, nikajikuta nayumba yumba. Kitendo cha kuyumba yumba, wale wazee wote wakanivamia kwa pamoja.

Nikajisemea hapa ndio nilikuwa napataka, ngoja nipunguze hasira zangu. Unajua Kwa jinsi nilivyokuwa nawakadiria, nilihisi dakika 10 nyingi wangesanda kwenye lile valangati. Ila yule Mzee Kidevu sijui hata anakulaga nini aisee, maana kuna muda nilimrushia ngumi, lengo nimpige shingoni, ila at the same time nae akanirushia ngumi. Ngumi kwa ngumi zikakutana, nilipatwa na maumivu kiasi kwamba nikahisi nimepiga mti. Kibaya zaidi yule Mzee hata akuugulia chochote, ndio kwanza anakuja tu.

Kipindi hicho chote, Mzee Dingi na Mwanasheria feki wameshasanda, wameniacha Mimi na Mzee Kidevu. Raia wamejaa wanauliza kuna nini?. Mzee Dingi linawajibu "Mambo ya kifamilia, tuachieni wenyewe". Yule Mzee Kidevu kama angekuwa na pumzi ya kutosha, angeniaibisha pale, kitu pekee kilichofanya akachemka ni pumzi. Nilivyóona kazidiwa, nikaanza kumpelekea punch mfululizo. Kumbe bwana vile vizee vilikuja na back up. Muda wote tokea nimewakuta, kuna jamaa kipande alikuwa amekaa kwa pembeni anachezea simu.

Walivyoona hadi Mzee Kidevu kazidiwa, Mzee Dingi akaita "We Beka fanya kazi yako". Aisee nilivyomuona huyo Beka mwenyewe, sikuwa na namna zaidi ya kukimbia. Nilifungua turbo kuelekea kwenye makazi ya watu, yamekaa kama kota hivi. Nilidhani watanipotezea, nashangaa Beka kaniungia tela, Mzee Kidevu na wale wazee wengine nao wakaanza kuja nyuma yetu. Raia nao hawana dogo, baadhi wameacha kuangalia mpira, wametuungia tela.

Nikipiga hatua zangu mbili, ndio hatua moja ya Beka. Sikwenda mbali sana akanishika. Nikataitishwa. Mwanasheria feki akawa anafanyakazi ya kufukuza watu walau wasogee mbali ba tulipo. Nilivyokuwa chini pale, Mzee Dingi akawa anasema;

Mzee Dingi: "Mvue hivyo vitu alivyovaa ndio vinamtia kiburi"

Beka akanichukulia ile pete yangu yenye kihirizi. Kisha akataka kunivua na kacha niliyokuwa nimevaa mkononi

Mzee Dingi: "Hiyo muachie, haina madhara. Yupo nayo hata kabla hajaoneshwa Dunia ilivyo"

Baada ya kuichukua ile pete, akamkabidhi Mzee Dingi, alafu wakaanza kuondoka. Kwenye wallet nilikuwa na 70k, hawakuigusa kabisa. Yani Wazee shida yao ilikuwa ile pete tu. Nilikuwa bado nimekaa chini nikiwa na hasira, maana yule kipande aliniumiza. Ghafla kuna wazo likanipitia kichwani, sikujiuliza mara mbili, nikanyanyuka na kuanza kuwafata. Nilivyowakaribia nikainama chini na kuchota mchanga, Mzee Kidevu akawa ameniaona;

Mzee Kidevu: "Apostle umenichota unyayo, apostle umenichota unyayo?"

Kiukweli nilifanya vile kama kuwatisha tu, ila Mzee Kidevu akalichukulia serious.

Mzee Kidevu: "Apostle unachotaka kukianzisha unakimudu?. Kumbe mtoto mshenzi sana wewe"

Kabla sijamjibu kitu, yule Beka kipande akawahi kunikamata, akaniminya mkono hadi nikaachia ule mchanga. Nikabaki nimesimama tu. Kila Wakitaka kuondoka, natishia kama nainama kuzoa mchanga, wanarudi.

Mzee Dingi: "Huyu mtoto sio wa kumfanyia mzaha kabisa"

Jamaa kila wakipiga hesabu, walipoacha gari yao ni mbali lazima watembee. Lakini hapo hapo wanahofia huku nyuma naweza fanya jambo baya. Ghafla Mzee Kidevu akanirukia, tukaanguka wote chini. Kisha wakamwambia Beka anibebe mpaka kwenye gari yao.

Muda huo wote raia full kucheka, kelele na kuzomea. Jamaa ikabidi wanipe lift kwa lazima, wakaenda kunishushia Ilala Boma.

Nilichokuja kugundua, kumbe ile Jana nilivyoacha na mzee Kesho Yetu, alimpigia Mzee Dingi na kumwambia Mimi sitoshiriki tena kwenye lile dili, nikiendelea kuwepo kuna uwezekano mkubwa sana wa dili kufeli. Ndio maana kina Mzee Dingi wakaamua kuja kunishikisha adabu na kunipora kile kihirizi, maana waliona sihitajiki tena.

Ambacho Mimi na wale wazee hatukujua ni kwamba, wakati sisi huku tunashikana mashati, upande wa pili Mzee Kesho Yetu alikuwa anakamilisha dili. Jana yake wakati tupo kwa yule mstaafu, walivyo baki peke yao sijui hata alimwambia nini, ila chochote alichomwambia ndicho kilichopelekea wao kwenda kukamilisha dili.

Walau Mimi nilishajua kuwa kwenye lile dili sipo tena, ila kina Mzee Dingi wao walikuwa wanasubiria siku mbili mbele wakakamilishe dili.

Wamechukua pete yangu, na kuondoka kishujaa, kumbe upande wa pili Mzee Kesho Yetu anasepa na mkwanja peke yake.

Kibaya zaidi, anaacha msala ambao ni wetu wote, ilhali sisi wengine hatujajiandaa....
Mwanangu Apostle nimecheka sana mida hii saa7 usiku nikiwa Bar hadi Barmaids wananishangaa mkuu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom