Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Dah ila Apostle unazingua, kwanin haumtonyi mmama wa watu mwenye moyo mwema,

maana hao wapigaji wao wanataka kumpiga izo million 40 wakale bata tu na sio kingine.

ila aisee wazazi wanajua unapambana mjini kumbe unanyang'anyana mchanga na wakina mzee dingi
Hapo kwenyewe kumejaa dhuruma Wajanja wa Mjini wamekutana
 
18th Portion:

Baada ya kuachana na Mzee Dingi, nilirudi gheto direct. Siku hiyo hiyo mida ya jioni, yule mama mstaafu akanipigia simu;

Mstaafu: "Hujambo mwanangu?"
Analyse: "Mzima mama, shikamoo"
Mstaafu: "Marahaba. Vipi utakuwepo mjini mpaka lini?"
Analyse: "Kuna vitu naweka sawa, vikikamilika nitaondoka. Inaweza ikawa Jumatatu au Jumanne"
Mstaafu: " Tunaweza kuonana kabla hujaondoka?"
Analyse: "Sawa hakuna shida, nadhani Jumatatu jioni nitakuja".


Baada ya kuongea na yule mstaafu, jioni hiyo hiyo, Mzee KY nae akanipigia simu, kuniambia tuonane siku ya Jumatatu jioni bila kukosa, ili tuweke sawa mambo kadhaa. So, ndani ya siku moja nikawa na appointments mbili, na zote jioni.

Wa kwanza kuonana nae ni Mzee KY, tulikutana mida ya saa kumi kumi.

Mzee KY: "Umeshaongea na yule mama au kuonana nae tokea ufike mjini?"
Analyse: "Hapana, kwanini?
Mzee KY: "Ulimwambia chochote labda kuhusu huu mpango?"
Analyse: "Hapana, vipi kwani?"
Mzee KY: "Oky Vizuri, sasa shika hizi hesabu" (akatoa hela na kunipa).

Nikahesabu, zikafika laki 3 na nusu. Nikamuuliza za nini hizi?

Mzee KY: "Huo ndio mgao wako, kwenye ili dili haupo tena"

Nikabaki nimeshangaa, sipo Kivipi?. Maana kama sipo basi dili limekufa, ila yeye mbona anaongea as if dili bado lipo?.

Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu, akaniambia "Wewe ulikuwa plan A, haikuwa plan pekee. Kwahiyo kama nilivyokwambia, naomba ukae pembeni, dili litaenda bila uwepo wako. Na usije kumwambia chochote yule Mama"

Nikabaki na mwangalia tu. Hapa ndio alikuja kunipa maelezo ambayo nilikuja kuhitimisha kuwa, uwepo wangu kwenye lile dili haikuwa coincidence, kila kitu kilikuwa planned. Aliifahamu connection yangu na yule mama, na dhumuni la kunifanya Mimi kuplay role ya mwenyekiti, ili niweze kugain trust ya yule mama Kwa urahisi. Na hata kile kitendo cha Mzee Dingi Kuni unblock na kunitaka nipige nao kazi, yote ilikuwa ni maandalizi ya ili dili. Halikuja ghafla kama nilivyodhani. Baadhi ya maelezo aliyonipa, ndiyo niliyaelezea jana. Japo kuna mengine niliyaelezea jana, ila yeye alikuja kuniambia mbeleni kabisa wakati dili limeshafanyika.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, tukaagana. Sikuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kule kwa mstaafu, ikabidi nielekee kule.

Nikiwa zangu mdogo mdogo nishakaribia kwa yule, Sina ili wala lile. Kumbe Mzee KY alikuwa ameniungia tela. Sikujua kama dhamira yake ilikuwa kupajua ninapoishi au alitaka kujua nitaelekea wapi baada ya sisi kuachana pale kwenye ile Pub. Naingia tu kwenye ile nyumba, na yeye huyu hapa. Kwa haraka haraka, mtu angeweza kuhisi kuwa tulikuwa tumeongozana wakati tunaenda pale.

Nilishtuka kumuona, japo sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia yeye kuwa pale. Yule Mama mstaafu alipotuona wote alifurahi sana;

Mstaafu: "Naona watu muhimu mmeamua kunijia kwa pamoja, karibuni sana"
Analyse: "Asante sana"
Mzee KY: "Kijana alinipigia simu niungane nae kuja kukuona. Vipi za tokea siku ile?
Mstaafu: "Salama tu, Tunamshkuru Mungu uzima upo kama unavyotuona"

Kisha akanigeukia Mimi;

Mstaafu: "Karibu tena nyumbani, ila this time karibu kama mwenyekiti"

Aliniambia hayo maneno huku anacheka, Mzee KY nae akacheka kidogo. Tukaingia na kukaa sebleni kwake. Maongezi yote kayatawala yule mama tu. Kuna muda akaingia chumbani huko, kisha akatoka na hela;

Mstaafu: "Nilikwambia nitakurudishia hela ya Kodi uliyoacha, chukua laki mbili yako. Sitaki dhulma Mimi, najua kijana ndio kwanza unaanza kujijenga".

Mzee KY akamakinika kuona nitafanya nini. Binafsi nikaamua kuzikataa zile hela;

Analyse: "Hapana mama, nilihama kwa hiari yangu hii hela wala sio deni kwako"
Mstaafu: "Chukua mwanangu, hii haiusiani na kule kusainishiana, maana kule najua huwezi kuniangusha. Nakupa kama kijana wangu tu".

Unajua siku zote wakati nakua, kuna methali ilikuwaga maarufu sana.

"Sikio la kufa halisikii dawa"

Ukikanywa, usiposikia lazima uambiwe. Siku zote nilikuwa naichukulia kama methali tu, lakini in a real sense kwa mara ya kwanza nimekutana na ilo "Sikio la kufa". Unajua ili umuokoe mtu anayezama, sharti awe mtulivu vinginevyo mtazama wote. Au la, basi mpe kijiti, akishike umvute. Sasa huyu mama kila nikimpa kijiti, anakikataa. Kimoyo moyo nikajisemea atajijua mwenyewe.

Analyse: "Usijali mama, hiyo hela wewe Kaa nayo. Nimeondoka kwa amani kabisa, nikiichukua nitajisikia vibaya".

Akabaki na hela yake. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Mzee KY akaomba niwapishe waongee kidogo. Sikuwa na namna, nikatoka zangu nje, wakaongea mambo yao kwa takribani nusu saa au dakika arobaini na tano. Baada ya hapo Mzee KY akatoka nje, tukaondoka wote.

Baada ya kutoka pale, akatafuta sehemu. Akaniweka kikao tena;

Mzee KY: "Sikia kijana, hivi unaweza kukadilia gharama kiasi gani imetumika kuandaa Ili dili?".

Ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu akaendelea tena;

"Mlivyokuja kule site, uliwaona wale majirani niliosalimiana nao?. Wale wote nimetoka nao huku. Uliwaona wale watu wanaolima pale?. Sijui hata wanalima nini, ila nao nimewaweka Mimi."

Akaendelea;

"Dili lifanikiwe au lisifanikiwe, hao wote lazima wapate hela yao. Sasa hebu niambie, lisipofanikiwa hela za kuwalipa zinatoka wapi?"

"Kuna watu huwezi kuwasaidia hata ufanye vipi, they are destined to lose. Hata ukisema umuache na hela zake akanunue eneo halali, still zile hela ataenda kuzifukia chini akitegemea zitachipua, ila ataambulia hasara. Najua hukuchukua ile laki mbili yake, sio kwamba huitaki au unamuonea huruma, bali you feel guilty. Nitakupa Mimi ile laki mbili, soon after dili kufanikiwa, ila for now naomba usinizibie njia, maana siwezi elezea nitakachokufanya. Umenisikia..........?'' Akataja jina langu halisi.

Nikashtuka, amelijuaje jina langu?.

Mzee KY
: "Wote mliopo kwenye Ili dili hakuna nisiyemjua, kuanzia anapokaa au sehemu zake za kwanza kukimbilia hapa mjini, kwahiyo kabla hujafanya jambo utakalokuja kulijutia, ni heri ujifikirie mara mbili"

Nikabaki nimeduwaa tu Kwa muda, sielewi what next. Akaniambia, "Huna haja ya kuendelea kubaki hapa, wahi ukapange vitu kwenye makazi yako mapya, japo nakushauri hama". Hakusubiria jibu langu, akaondoka.

So, he knows me well?. Why nihame wakati ndio kwanza nimehamia au kuna msala unanisubiria? Wazo likanijia, kwanza yule mstaafu tumejuliana mjini hapa hapa, atajijua mwenyewe, ngoja nijihangaikie Mimi.

Nilivyofika ghetto, Yale maneno ya Mzee KY kuwa nihame pale, yakawa yananijia. Nikajikuta njia panda, nipange vitu au nijiandae kuhama?. Ila nimetoka kulipa Kodi ya miezi 6 siku chache tu zilizopita, nahamaje? Mbona ntakuwa nafaidisha wenye nyumba?. Lakini taswira ya Mzee KY ikawa hainipi picha nzuri ya yajayo. Akili ikaniambia nisipange vile vitu, nihame.

Nikampigia simu mwenye nyumba, kumuomba kesho tuonane kama ataweza. Akakubali.

Asubuhi nilivyoonana nae, nikampanga kuwa nimepata dharura natakiwa kusafiri haraka nje ya mkoa, anirudishie hata nusu kodi. Akanijibu "Mwanangu Cha kukusaidia hapa, labda nikuhifadhie vitu vyako kwahiyo miezi 6 utakayokuwa unapambana na hiyo dharura yako"

Nikaona hapa siwezi ambulia hata mia, cha zaidi nitapoteza muda tu kumbembeleza.

Kipindi Mimi nawaza namna ya kuhama pale. Mzee Dingi akanipigia simu na kuomba tuonane.

Nikafikiria huyu nikutane nae maeneo yapi?. Kipindi kile maeneo ya Tabata kuna mashindano ya mpira wa miguu yalikuwa yanaendelea. Viwanja vilivyokuwa vinatumika ni kile Cha Sigara na cha Tabata shule. Nikaona option ya Tabata shule ndio sahihi, maana ni mbali kiasi na ninapoishi. Lakini sababu nyingine iliyofanya nisione shida kukutana nae Tabata, ni kwavile nilikuwa natarajia kuhama.

Nikamwambia tukutane Tabata shule. Mzee Dingi akagoma, na hii ni kwavile pale ni karibu sana mitaa anayoishi yeye. Nilivyóona bado anakomaa tuchange location, nikamwambia basi sitaki kuonana na wewe. Endelea na mishe zako.

Nilipata ujasili wa kumwambia vile kutokana na sababu Kuu mbili, kwanza kwenye dili lao sipo tena, alafu pili sijui anataka tuongee nini. Alivyoona nimekataa kuonana nae, hakuwa na choice zaidi ya kukubali tukutane maeneo yale.

Mida ya jioni nikasogea pale Tabata shule. Mzee Dingi alikuwa ameshafika kabla yangu. Mara zote ambazo tumekuwa tukikutana, vikao vilikuwa vinafanyikia either bar, pub or kwenye mgahawa. Ila this time hakutaka tukutane maeneo hayo. Akapendekeza tukutane kwenye yale majengo ya shule ya Kijapan (kuna shule ilijengwa na Wajapani maeneo yale). Nikajiuliza mara mbili mbili, why kachagua kule?. Ila kimoyo moyo nikajisemea akileta za kuleta, nitamfumua. Hasira zangu zote ziishie kwake.

Akanielekeza alipokuwa amesimama, nikamfata. Kufika pale, navikuta vizee vyote vitatu vipo. Mzee Dingi, Mzee Kidevu na Mwanasheria feki. Nikajiuliza vinanitakia nini?.

Nilivyowaona, sura zao zote ziliakisi shari, ila sikuwa na namna zaidi ya kuwasogelea. Zikapigwa story za hapa na pale, lakini Unaona kabisa hapa kuna jambo litatokea muda sio mrefu. Na Mimi kwa hasira nilizokuwa nazo, nikawa nasubiria kwa hamu ilo jambo litokee. Kwa jinsi tulivyokuwa tumejipanga, Mzee Kidevu alikuwa nyuma kidogo upande wangu wa kushoto, alafu mwanasheria feki na Mzee Dingi walikuwa mbele, tupo face to face. Tukiwa tunaendelea kuongea upande, kwa ghafla sana yule Mzee Kidevu akanirukia horizontally na kunipiga kichwa cha mbavu. Ni kitu ambacho sikuwa nimekitarajia, nikajikuta nayumba yumba. Kitendo cha kuyumba yumba, wale wazee wote wakanivamia kwa pamoja.

Nikajisemea hapa ndio nilikuwa napataka, ngoja nipunguze hasira zangu. Unajua Kwa jinsi nilivyokuwa nawakadiria, nilihisi dakika 10 nyingi wangesanda kwenye lile valangati. Ila yule Mzee Kidevu sijui hata anakulaga nini aisee, maana kuna muda nilimrushia ngumi, lengo nimpige shingoni, ila at the same time nae akanirushia ngumi. Ngumi kwa ngumi zikakutana, nilipatwa na maumivu kiasi kwamba nikahisi nimepiga mti. Kibaya zaidi yule Mzee hata akuugulia chochote, ndio kwanza anakuja tu.

Kipindi hicho chote, Mzee Dingi na Mwanasheria feki wameshasanda, wameniacha Mimi na Mzee Kidevu. Raia wamejaa wanauliza kuna nini?. Mzee Dingi linawajibu "Mambo ya kifamilia, tuachieni wenyewe". Yule Mzee Kidevu kama angekuwa na pumzi ya kutosha, angeniaibisha pale, kitu pekee kilichofanya akachemka ni pumzi. Nilivyóona kazidiwa, nikaanza kumpelekea punch mfululizo. Kumbe bwana vile vizee vilikuja na back up. Muda wote tokea nimewakuta, kuna jamaa kipande alikuwa amekaa kwa pembeni anachezea simu.

Walivyoona hadi Mzee Kidevu kazidiwa, Mzee Dingi akaita "We Beka fanya kazi yako". Aisee nilivyomuona huyo Beka mwenyewe, sikuwa na namna zaidi ya kukimbia. Nilifungua turbo kuelekea kwenye makazi ya watu, yamekaa kama kota hivi. Nilidhani watanipotezea, nashangaa Beka kaniungia tela, Mzee Kidevu na wale wazee wengine nao wakaanza kuja nyuma yetu. Raia nao hawana dogo, baadhi wameacha kuangalia mpira, wametuungia tela.

Nikipiga hatua zangu mbili, ndio hatua moja ya Beka. Sikwenda mbali sana akanishika. Nikataitishwa. Mwanasheria feki akawa anafanyakazi ya kufukuza watu walau wasogee mbali ba tulipo. Nilivyokuwa chini pale, Mzee Dingi akawa anasema;

Mzee Dingi: "Mvue hivyo vitu alivyovaa ndio vinamtia kiburi"

Beka akanichukulia ile pete yangu yenye kihirizi. Kisha akataka kunivua na kacha niliyokuwa nimevaa mkononi

Mzee Dingi: "Hiyo muachie, haina madhara. Yupo nayo hata kabla hajaoneshwa Dunia ilivyo"

Baada ya kuichukua ile pete, akamkabidhi Mzee Dingi, alafu wakaanza kuondoka. Kwenye wallet nilikuwa na 70k, hawakuigusa kabisa. Yani Wazee shida yao ilikuwa ile pete tu. Nilikuwa bado nimekaa chini nikiwa na hasira, maana yule kipande aliniumiza. Ghafla kuna wazo likanipitia kichwani, sikujiuliza mara mbili, nikanyanyuka na kuanza kuwafata. Nilivyowakaribia nikainama chini na kuchota mchanga, Mzee Kidevu akawa ameniaona;

Mzee Kidevu: "Apostle umenichota unyayo, apostle umenichota unyayo?"

Kiukweli nilifanya vile kama kuwatisha tu, ila Mzee Kidevu akalichukulia serious.

Mzee Kidevu: "Apostle unachotaka kukianzisha unakimudu?. Kumbe mtoto mshenzi sana wewe"

Kabla sijamjibu kitu, yule Beka kipande akawahi kunikamata, akaniminya mkono hadi nikaachia ule mchanga. Nikabaki nimesimama tu. Kila Wakitaka kuondoka, natishia kama nainama kuzoa mchanga, wanarudi.

Mzee Dingi: "Huyu mtoto sio wa kumfanyia mzaha kabisa"

Jamaa kila wakipiga hesabu, walipoacha gari yao ni mbali lazima watembee. Lakini hapo hapo wanahofia huku nyuma naweza fanya jambo baya. Ghafla Mzee Kidevu akanirukia, tukaanguka wote chini. Kisha wakamwambia Beka anibebe mpaka kwenye gari yao.

Muda huo wote raia full kucheka, kelele na kuzomea. Jamaa ikabidi wanipe lift kwa lazima, wakaenda kunishushia Ilala Boma.

Nilichokuja kugundua, kumbe ile Jana nilivyoacha na mzee Kesho Yetu, alimpigia Mzee Dingi na kumwambia Mimi sitoshiriki tena kwenye lile dili, nikiendelea kuwepo kuna uwezekano mkubwa sana wa dili kufeli. Ndio maana kina Mzee Dingi wakaamua kuja kunishikisha adabu na kunipora kile kihirizi, maana waliona sihitajiki tena.

Ambacho Mimi na wale wazee hatukujua ni kwamba, wakati sisi huku tunashikana mashati, upande wa pili Mzee Kesho Yetu alikuwa anakamilisha dili. Jana yake wakati tupo kwa yule mstaafu, walivyo baki peke yao sijui hata alimwambia nini, ila chochote alichomwambia ndicho kilichopelekea wao kwenda kukamilisha dili.

Walau Mimi nilishajua kuwa kwenye lile dili sipo tena, ila kina Mzee Dingi wao walikuwa wanasubiria siku mbili mbele wakakamilishe dili.

Wamechukua pete yangu, na kuondoka kishujaa, kumbe upande wa pili Mzee Kesho Yetu anasepa na mkwanja peke yake.

Kibaya zaidi, anaacha msala ambao ni wetu wote, ilhali sisi wengine hatujajiandaa....
KY sio fala narudia Tena[emoji23]
 
3rd Portion:

... Maelezo ambayo nilikuja kupewa baadae na head prefect, ni kuwa inaonekana mshua alinitafuta sana kwenye simu kabla hajaenda pale shule, ila hakufanikiwa kunipata. Kwavile hatujawasiliana muda mrefu, na akisema arudi kijijini, maana yake utapita muda mrefu mwingine bila kuonana, ndio akaona afunge safari mpaka shule. Kufika pale akajitambulisha kama mzazi wangu, na akaomba kuonana na mimi. Walim wakashangaa, mzazi wake Analyse?, Wewe ni baba yake mkubwa au mlezi? Dingi akawa hajaelewa. Akawaambia yeye ni Mzee wangu kabisa, Mwalim wa nidham akaona mshua anamletea masihara, ili swala la wanafunzi kuleta wazazi feki inabidi likomeshwe, akamwambia Mzee akae kwenye benchi. Baada ya kushauriana na mkuu wa shule, wakataka kumpeleka Mzee Polisi. Mshua akawakazia, walivyoona yupo serious sana, wakamuomba ID yoyote.

Akawapa voters ID, walivyoona mfanano wa majina, walim wakachoka. Ikabidi waanze kuulizana, kama wewe ndio baba yake, yule aliyekuja nae ni nani? Hapo ndio wakampa picha nzima. Mzee akacheka (Mzee wangu akiwa na hasira sana, kuna kicheko fulani kinakujaga automatically). Mwisho wa siku wakaazimia head prefect awe ananipigia simu mara kwa mara, akinipata, anipe zile taarifa za kuhitajika shule kwa ajili ya usajili. Na ahakikishe ananishawishi niende na mzazi niliyempeleka last time.

Walimu walikuwa na shauku ya kuniona Mimi maana nimecheza na akili zao, ila Mshua target zake ilikuwa ni kumuona yule mzazi niliyempeleka badala yake. Mwamba Sina ili wala lile, kesho yake nikapanda Simba Mtoto, safari ya shule ikaanza. Nilivyofika, nikaunga moja kwa moja mpaka nguvu mali, nikapoa kwa mshikaji wangu pale Galanosi, kesho yake asubuhi, tukabebana Mimi na yule Mchaga hao mpaka shule.

Ile shule ilivyo, ukishaingia kupitia main entrance, unakata upande wa kulia, ndio kuna ofisi za walim pamoja na head master. Upande wa kushoto, kulikuwa na korido inayoelekea madarasani, lakini pia mwanzoni kuna njia ya kwenda vyooni, na ngazi za kuelekea madarasa ya juu. Sasa kwenye hizi ngazi ndio alikuwa kakaa Mshua ananisubiria Mimi na baba yangu tufike. Na sisi tulivyofika, direct tukakata kona kulia, hatukuangalia nyuma. Mzee akatuungia tela mdogo mdogo. Machale ni kama yalinicheza hivi, nikapata hisia zinaniambia geuka nyuma, kugeuka nakutana na Mshua kakaza sura kimtindo, mikono yote miwili kaikutanisha nyuma ya makalio, kama wanavyopendaga kutembea wazee. Alipoona nimegeuka, akasimama kwa muda Nikapatwa na mshtuko, maana sikutarajia kumuona pale, nikajikuta nimeita "Baba?". Yule Mchaga alikuwa bado hajausoma mchezo, akaitikia "Naam jembe langu". Ila alivyogeuka, na kukuta nimeelekeza attention kwa mtu mwingine, akili yake ikaload faster, akajikuta anatukana kichini chini "Ku***na walai".

Mshua akawa anamuangalia tu, huku kaweka tabasam la mamba. Mchaga akapiga hesabu za haraka, akaona hapa akiingia ofisini, basi hatoweza kutoka, anaweza akaishia polisi. Akapitisha wazo la kutoweka eneo lile, ila njia peke rahisi ni kupitia upande aliosimama Mshua, pia japo shule haikuwa na fensi, ila kukimbilia upande waliopo wanafunzi inaweza ikawa msala zaidi, maana wanafunzi hawana dogo. Akaamua kurudi na njia tuliyojia, upande aliosimama Mshua. Kosa alilofanya Mchaga, alim-underestimate Mshua, labda alijiona yeye kijana zaidi akijilinganisha nae, so angemzidi nguvu. Mchaga alitoka speed ghafla, mshua akawahi kumrukia, wakavaana mpaka chini. Kitendo cha kuanguka chini tu, Mshua kama kawaida yake, akamuwahi Mchaga na kabali moja matata. Mchaga kila akirusha ngumi, Mshua hana habari, ndio kwanza anazidi kukaza mikono. Wanafunzi wakajaa madirishani, kelele zikazagaa eneo lile, wengine wakaanza kutoka madarasani kuja kushuhudia kwa ukaribu.

Walim ikabidi waanze zoezi la kuwaachanisha, walipofanikiwa, Mchaga macho yalikuwa mekunduu kama katoka kulala au kulia. Walim wakawa wanafukuza wanafunzi warudi madarasani, Kisha wakawaomba Baba na yule Mchaga waende ofisini kwa mazungumzo, maana kwa umri wao haifai kushikana mashati namna ile. Wakiwa wanakaribia mlango wa ofisi ya walim, yule Mchaga aligeuka, akatoka speed, akaelekea upande zilipo hostels za wanafunzi wa advance, akapita kwenye senyenge, alivyotokea upande wa pili, akaongeza speed, akapotelea kwenye makazi ya watu. Hakuna hata mwalim aliyejisumbua kumkimbiza, wakabaki wanamwangalia tu. Ila wanafunzi ndio wakawa wanamzomea. Jamaa akasepa, msala nikabaki nao peke yangu. Kikao kikafanyikia ofisi ya walimu wote, mwanenu nikapigishwa magoti huku nasemwa..

Ubaya wa ofisi ya walimu, hata yule mwalim ambae hakujui, lazima apate cha kukuongelea. Nilitembezewa fimbo za kufa mtu siku ile, japo mshua hakunipiga, ila alichangia pakubwa sana kuikuza adhabu yangu, maana aliongea mengi sana, kiasi kwamba nikaonekana kituko. Mshua alilipa ile hela ya faini, nikaruhusiwa kwenda darasani. Aliamua kuondoka siku hiyo hiyo, hakujisumbua kuongea na Mimi baada ya kutoka mle ofisini, na hakunipa hata shiling 10 Kwa ajili ya matumizi pale shuleni. Kiufupi aliniacha kikauzu sana. Nimeingia class sina mzuka hata kidogo, mda wote nimelala kwenye dawati. Mida ya mchana baada ya msosi, nikaamsha zangu kuelekea hostel. Nikalala mpaka mida ya jioni.

Wakati natoka kula msosi wa usiku shuleni, yule jamaa yangu wa Galanosi akanipigia simu, anauliza nimemfanya nini Mchaga? Maana kakutana nae ana nundu kwenye kona ya uso, alaf kamuahidi kwamba siku akikutana na Mimi, sitokaa nimsahau maishani mwangu kwa atakachonifanya. Ikabidi nimuelezee kwa ufupi yaliyojili. Jamaa alicheka sana, mwishowe akaniambia nikienda shuleni kwao niende kwa tahadhari, maana Mchaga alimaanisha alichokisema. Tukaishiana hapo, then nikaenda chamber kupiga msuli. Tokea siku ile nikaanza kupiga sana msuli, sikuwa na msala mwingine wowote, japo walimu waliendelea kuwa wananizingua hapa na pale, ila niliamua kuwa mpole.

Mshua hakuwahi kunitafuta tena, sio kwa simu wala msg. Ni kama alinizila. Kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa mwisho, nikaanza kumfukuzia demu mmoja wa O level pale pale shuleni, alikuwa mweupe, sauti nyembamba na kishundu fulani cha kuvunjia shingo, maana akikupita lazima ugeuke. Siku moja nimekaa nae maeneo ya garden mida ya jioni, naendelea kuingizia mistari, maana alikuwa bado hajaeleweka. Katika maongezi akaniambia "Wewe hapa Tanga sio kwenu, unasema unanipenda, wakati siku sio nyingi utamaliza shule, utaacha umenitumia alafu utaondoka".

Nikamjibu kuwa mgeni Tanga hainizuii Mimi kumpenda yeye, umbali sio kikwazo kwangu. Akaniuliza "Unamaanisha unachosema? Kuwa utarudi kwa ajili yangu?, Niambie ukweli, sitaki uongo". Nikasita kidogo kutoa jibu, yeye akaendelea "Mimi ninachohitaji kujua ni Nia yako tu, kama kweli utataka kurudi, mimi nitakurudisha". Ile kauli ikanimakinisha kidogo, nikamuuliza "Utanirudisha kivipi? " Akajibu "Wewe ilo niachie Mimi, je ni kweli unanipenda na ungependa kurudi kwa ajili yangu, nikurudishe??

Nikabaki nimeduwaa kwa muda, najiuliza "Huyu anaongelea nini?".....

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Aise dogo[emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
18th Portion:

Baada ya kuachana na Mzee Dingi, nilirudi gheto direct. Siku hiyo hiyo mida ya jioni, yule mama mstaafu akanipigia simu;

Mstaafu: "Hujambo mwanangu?"
Analyse: "Mzima mama, shikamoo"
Mstaafu: "Marahaba. Vipi utakuwepo mjini mpaka lini?"
Analyse: "Kuna vitu naweka sawa, vikikamilika nitaondoka. Inaweza ikawa Jumatatu au Jumanne"
Mstaafu: " Tunaweza kuonana kabla hujaondoka?"
Analyse: "Sawa hakuna shida, nadhani Jumatatu jioni nitakuja".


Baada ya kuongea na yule mstaafu, jioni hiyo hiyo, Mzee KY nae akanipigia simu, kuniambia tuonane siku ya Jumatatu jioni bila kukosa, ili tuweke sawa mambo kadhaa. So, ndani ya siku moja nikawa na appointments mbili, na zote jioni.

Wa kwanza kuonana nae ni Mzee KY, tulikutana mida ya saa kumi kumi.

Mzee KY: "Umeshaongea na yule mama au kuonana nae tokea ufike mjini?"
Analyse: "Hapana, kwanini?
Mzee KY: "Ulimwambia chochote labda kuhusu huu mpango?"
Analyse: "Hapana, vipi kwani?"
Mzee KY: "Oky Vizuri, sasa shika hizi hesabu" (akatoa hela na kunipa).

Nikahesabu, zikafika laki 3 na nusu. Nikamuuliza za nini hizi?

Mzee KY: "Huo ndio mgao wako, kwenye ili dili haupo tena"

Nikabaki nimeshangaa, sipo Kivipi?. Maana kama sipo basi dili limekufa, ila yeye mbona anaongea as if dili bado lipo?.

Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu, akaniambia "Wewe ulikuwa plan A, haikuwa plan pekee. Kwahiyo kama nilivyokwambia, naomba ukae pembeni, dili litaenda bila uwepo wako. Na usije kumwambia chochote yule Mama"

Nikabaki na mwangalia tu. Hapa ndio alikuja kunipa maelezo ambayo nilikuja kuhitimisha kuwa, uwepo wangu kwenye lile dili haikuwa coincidence, kila kitu kilikuwa planned. Aliifahamu connection yangu na yule mama, na dhumuni la kunifanya Mimi kuplay role ya mwenyekiti, ili niweze kugain trust ya yule mama Kwa urahisi. Na hata kile kitendo cha Mzee Dingi Kuni unblock na kunitaka nipige nao kazi, yote ilikuwa ni maandalizi ya ili dili. Halikuja ghafla kama nilivyodhani. Baadhi ya maelezo aliyonipa, ndiyo niliyaelezea jana. Japo kuna mengine niliyaelezea jana, ila yeye alikuja kuniambia mbeleni kabisa wakati dili limeshafanyika.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, tukaagana. Sikuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kule kwa mstaafu, ikabidi nielekee kule.

Nikiwa zangu mdogo mdogo nishakaribia kwa yule, Sina ili wala lile. Kumbe Mzee KY alikuwa ameniungia tela. Sikujua kama dhamira yake ilikuwa kupajua ninapoishi au alitaka kujua nitaelekea wapi baada ya sisi kuachana pale kwenye ile Pub. Naingia tu kwenye ile nyumba, na yeye huyu hapa. Kwa haraka haraka, mtu angeweza kuhisi kuwa tulikuwa tumeongozana wakati tunaenda pale.

Nilishtuka kumuona, japo sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia yeye kuwa pale. Yule Mama mstaafu alipotuona wote alifurahi sana;

Mstaafu: "Naona watu muhimu mmeamua kunijia kwa pamoja, karibuni sana"
Analyse: "Asante sana"
Mzee KY: "Kijana alinipigia simu niungane nae kuja kukuona. Vipi za tokea siku ile?
Mstaafu: "Salama tu, Tunamshkuru Mungu uzima upo kama unavyotuona"

Kisha akanigeukia Mimi;

Mstaafu: "Karibu tena nyumbani, ila this time karibu kama mwenyekiti"

Aliniambia hayo maneno huku anacheka, Mzee KY nae akacheka kidogo. Tukaingia na kukaa sebleni kwake. Maongezi yote kayatawala yule mama tu. Kuna muda akaingia chumbani huko, kisha akatoka na hela;

Mstaafu: "Nilikwambia nitakurudishia hela ya Kodi uliyoacha, chukua laki mbili yako. Sitaki dhulma Mimi, najua kijana ndio kwanza unaanza kujijenga".

Mzee KY akamakinika kuona nitafanya nini. Binafsi nikaamua kuzikataa zile hela;

Analyse: "Hapana mama, nilihama kwa hiari yangu hii hela wala sio deni kwako"
Mstaafu: "Chukua mwanangu, hii haiusiani na kule kusainishiana, maana kule najua huwezi kuniangusha. Nakupa kama kijana wangu tu".

Unajua siku zote wakati nakua, kuna methali ilikuwaga maarufu sana.

"Sikio la kufa halisikii dawa"

Ukikanywa, usiposikia lazima uambiwe. Siku zote nilikuwa naichukulia kama methali tu, lakini in a real sense kwa mara ya kwanza nimekutana na ilo "Sikio la kufa". Unajua ili umuokoe mtu anayezama, sharti awe mtulivu vinginevyo mtazama wote. Au la, basi mpe kijiti, akishike umvute. Sasa huyu mama kila nikimpa kijiti, anakikataa. Kimoyo moyo nikajisemea atajijua mwenyewe.

Analyse: "Usijali mama, hiyo hela wewe Kaa nayo. Nimeondoka kwa amani kabisa, nikiichukua nitajisikia vibaya".

Akabaki na hela yake. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Mzee KY akaomba niwapishe waongee kidogo. Sikuwa na namna, nikatoka zangu nje, wakaongea mambo yao kwa takribani nusu saa au dakika arobaini na tano. Baada ya hapo Mzee KY akatoka nje, tukaondoka wote.

Baada ya kutoka pale, akatafuta sehemu. Akaniweka kikao tena;

Mzee KY: "Sikia kijana, hivi unaweza kukadilia gharama kiasi gani imetumika kuandaa Ili dili?".

Ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu akaendelea tena;

"Mlivyokuja kule site, uliwaona wale majirani niliosalimiana nao?. Wale wote nimetoka nao huku. Uliwaona wale watu wanaolima pale?. Sijui hata wanalima nini, ila nao nimewaweka Mimi."

Akaendelea;

"Dili lifanikiwe au lisifanikiwe, hao wote lazima wapate hela yao. Sasa hebu niambie, lisipofanikiwa hela za kuwalipa zinatoka wapi?"

"Kuna watu huwezi kuwasaidia hata ufanye vipi, they are destined to lose. Hata ukisema umuache na hela zake akanunue eneo halali, still zile hela ataenda kuzifukia chini akitegemea zitachipua, ila ataambulia hasara. Najua hukuchukua ile laki mbili yake, sio kwamba huitaki au unamuonea huruma, bali you feel guilty. Nitakupa Mimi ile laki mbili, soon after dili kufanikiwa, ila for now naomba usinizibie njia, maana siwezi elezea nitakachokufanya. Umenisikia..........?'' Akataja jina langu halisi.

Nikashtuka, amelijuaje jina langu?.

Mzee KY
: "Wote mliopo kwenye Ili dili hakuna nisiyemjua, kuanzia anapokaa au sehemu zake za kwanza kukimbilia hapa mjini, kwahiyo kabla hujafanya jambo utakalokuja kulijutia, ni heri ujifikirie mara mbili"

Nikabaki nimeduwaa tu Kwa muda, sielewi what next. Akaniambia, "Huna haja ya kuendelea kubaki hapa, wahi ukapange vitu kwenye makazi yako mapya, japo nakushauri hama". Hakusubiria jibu langu, akaondoka.

So, he knows me well?. Why nihame wakati ndio kwanza nimehamia au kuna msala unanisubiria? Wazo likanijia, kwanza yule mstaafu tumejuliana mjini hapa hapa, atajijua mwenyewe, ngoja nijihangaikie Mimi.

Nilivyofika ghetto, Yale maneno ya Mzee KY kuwa nihame pale, yakawa yananijia. Nikajikuta njia panda, nipange vitu au nijiandae kuhama?. Ila nimetoka kulipa Kodi ya miezi 6 siku chache tu zilizopita, nahamaje? Mbona ntakuwa nafaidisha wenye nyumba?. Lakini taswira ya Mzee KY ikawa hainipi picha nzuri ya yajayo. Akili ikaniambia nisipange vile vitu, nihame.

Nikampigia simu mwenye nyumba, kumuomba kesho tuonane kama ataweza. Akakubali.

Asubuhi nilivyoonana nae, nikampanga kuwa nimepata dharura natakiwa kusafiri haraka nje ya mkoa, anirudishie hata nusu kodi. Akanijibu "Mwanangu Cha kukusaidia hapa, labda nikuhifadhie vitu vyako kwahiyo miezi 6 utakayokuwa unapambana na hiyo dharura yako"

Nikaona hapa siwezi ambulia hata mia, cha zaidi nitapoteza muda tu kumbembeleza.

Kipindi Mimi nawaza namna ya kuhama pale. Mzee Dingi akanipigia simu na kuomba tuonane.

Nikafikiria huyu nikutane nae maeneo yapi?. Kipindi kile maeneo ya Tabata kuna mashindano ya mpira wa miguu yalikuwa yanaendelea. Viwanja vilivyokuwa vinatumika ni kile Cha Sigara na cha Tabata shule. Nikaona option ya Tabata shule ndio sahihi, maana ni mbali kiasi na ninapoishi. Lakini sababu nyingine iliyofanya nisione shida kukutana nae Tabata, ni kwavile nilikuwa natarajia kuhama.

Nikamwambia tukutane Tabata shule. Mzee Dingi akagoma, na hii ni kwavile pale ni karibu sana mitaa anayoishi yeye. Nilivyóona bado anakomaa tuchange location, nikamwambia basi sitaki kuonana na wewe. Endelea na mishe zako.

Nilipata ujasili wa kumwambia vile kutokana na sababu Kuu mbili, kwanza kwenye dili lao sipo tena, alafu pili sijui anataka tuongee nini. Alivyoona nimekataa kuonana nae, hakuwa na choice zaidi ya kukubali tukutane maeneo yale.

Mida ya jioni nikasogea pale Tabata shule. Mzee Dingi alikuwa ameshafika kabla yangu. Mara zote ambazo tumekuwa tukikutana, vikao vilikuwa vinafanyikia either bar, pub or kwenye mgahawa. Ila this time hakutaka tukutane maeneo hayo. Akapendekeza tukutane kwenye yale majengo ya shule ya Kijapan (kuna shule ilijengwa na Wajapani maeneo yale). Nikajiuliza mara mbili mbili, why kachagua kule?. Ila kimoyo moyo nikajisemea akileta za kuleta, nitamfumua. Hasira zangu zote ziishie kwake.

Akanielekeza alipokuwa amesimama, nikamfata. Kufika pale, navikuta vizee vyote vitatu vipo. Mzee Dingi, Mzee Kidevu na Mwanasheria feki. Nikajiuliza vinanitakia nini?.

Nilivyowaona, sura zao zote ziliakisi shari, ila sikuwa na namna zaidi ya kuwasogelea. Zikapigwa story za hapa na pale, lakini Unaona kabisa hapa kuna jambo litatokea muda sio mrefu. Na Mimi kwa hasira nilizokuwa nazo, nikawa nasubiria kwa hamu ilo jambo litokee. Kwa jinsi tulivyokuwa tumejipanga, Mzee Kidevu alikuwa nyuma kidogo upande wangu wa kushoto, alafu mwanasheria feki na Mzee Dingi walikuwa mbele, tupo face to face. Tukiwa tunaendelea kuongea upande, kwa ghafla sana yule Mzee Kidevu akanirukia horizontally na kunipiga kichwa cha mbavu. Ni kitu ambacho sikuwa nimekitarajia, nikajikuta nayumba yumba. Kitendo cha kuyumba yumba, wale wazee wote wakanivamia kwa pamoja.

Nikajisemea hapa ndio nilikuwa napataka, ngoja nipunguze hasira zangu. Unajua Kwa jinsi nilivyokuwa nawakadiria, nilihisi dakika 10 nyingi wangesanda kwenye lile valangati. Ila yule Mzee Kidevu sijui hata anakulaga nini aisee, maana kuna muda nilimrushia ngumi, lengo nimpige shingoni, ila at the same time nae akanirushia ngumi. Ngumi kwa ngumi zikakutana, nilipatwa na maumivu kiasi kwamba nikahisi nimepiga mti. Kibaya zaidi yule Mzee hata akuugulia chochote, ndio kwanza anakuja tu.

Kipindi hicho chote, Mzee Dingi na Mwanasheria feki wameshasanda, wameniacha Mimi na Mzee Kidevu. Raia wamejaa wanauliza kuna nini?. Mzee Dingi linawajibu "Mambo ya kifamilia, tuachieni wenyewe". Yule Mzee Kidevu kama angekuwa na pumzi ya kutosha, angeniaibisha pale, kitu pekee kilichofanya akachemka ni pumzi. Nilivyóona kazidiwa, nikaanza kumpelekea punch mfululizo. Kumbe bwana vile vizee vilikuja na back up. Muda wote tokea nimewakuta, kuna jamaa kipande alikuwa amekaa kwa pembeni anachezea simu.

Walivyoona hadi Mzee Kidevu kazidiwa, Mzee Dingi akaita "We Beka fanya kazi yako". Aisee nilivyomuona huyo Beka mwenyewe, sikuwa na namna zaidi ya kukimbia. Nilifungua turbo kuelekea kwenye makazi ya watu, yamekaa kama kota hivi. Nilidhani watanipotezea, nashangaa Beka kaniungia tela, Mzee Kidevu na wale wazee wengine nao wakaanza kuja nyuma yetu. Raia nao hawana dogo, baadhi wameacha kuangalia mpira, wametuungia tela.

Nikipiga hatua zangu mbili, ndio hatua moja ya Beka. Sikwenda mbali sana akanishika. Nikataitishwa. Mwanasheria feki akawa anafanyakazi ya kufukuza watu walau wasogee mbali ba tulipo. Nilivyokuwa chini pale, Mzee Dingi akawa anasema;

Mzee Dingi: "Mvue hivyo vitu alivyovaa ndio vinamtia kiburi"

Beka akanichukulia ile pete yangu yenye kihirizi. Kisha akataka kunivua na kacha niliyokuwa nimevaa mkononi

Mzee Dingi: "Hiyo muachie, haina madhara. Yupo nayo hata kabla hajaoneshwa Dunia ilivyo"

Baada ya kuichukua ile pete, akamkabidhi Mzee Dingi, alafu wakaanza kuondoka. Kwenye wallet nilikuwa na 70k, hawakuigusa kabisa. Yani Wazee shida yao ilikuwa ile pete tu. Nilikuwa bado nimekaa chini nikiwa na hasira, maana yule kipande aliniumiza. Ghafla kuna wazo likanipitia kichwani, sikujiuliza mara mbili, nikanyanyuka na kuanza kuwafata. Nilivyowakaribia nikainama chini na kuchota mchanga, Mzee Kidevu akawa ameniaona;

Mzee Kidevu: "Apostle umenichota unyayo, apostle umenichota unyayo?"

Kiukweli nilifanya vile kama kuwatisha tu, ila Mzee Kidevu akalichukulia serious.

Mzee Kidevu: "Apostle unachotaka kukianzisha unakimudu?. Kumbe mtoto mshenzi sana wewe"

Kabla sijamjibu kitu, yule Beka kipande akawahi kunikamata, akaniminya mkono hadi nikaachia ule mchanga. Nikabaki nimesimama tu. Kila Wakitaka kuondoka, natishia kama nainama kuzoa mchanga, wanarudi.

Mzee Dingi: "Huyu mtoto sio wa kumfanyia mzaha kabisa"

Jamaa kila wakipiga hesabu, walipoacha gari yao ni mbali lazima watembee. Lakini hapo hapo wanahofia huku nyuma naweza fanya jambo baya. Ghafla Mzee Kidevu akanirukia, tukaanguka wote chini. Kisha wakamwambia Beka anibebe mpaka kwenye gari yao.

Muda huo wote raia full kucheka, kelele na kuzomea. Jamaa ikabidi wanipe lift kwa lazima, wakaenda kunishushia Ilala Boma.

Nilichokuja kugundua, kumbe ile Jana nilivyoacha na mzee Kesho Yetu, alimpigia Mzee Dingi na kumwambia Mimi sitoshiriki tena kwenye lile dili, nikiendelea kuwepo kuna uwezekano mkubwa sana wa dili kufeli. Ndio maana kina Mzee Dingi wakaamua kuja kunishikisha adabu na kunipora kile kihirizi, maana waliona sihitajiki tena.

Ambacho Mimi na wale wazee hatukujua ni kwamba, wakati sisi huku tunashikana mashati, upande wa pili Mzee Kesho Yetu alikuwa anakamilisha dili. Jana yake wakati tupo kwa yule mstaafu, walivyo baki peke yao sijui hata alimwambia nini, ila chochote alichomwambia ndicho kilichopelekea wao kwenda kukamilisha dili.

Walau Mimi nilishajua kuwa kwenye lile dili sipo tena, ila kina Mzee Dingi wao walikuwa wanasubiria siku mbili mbele wakakamilishe dili.

Wamechukua pete yangu, na kuondoka kishujaa, kumbe upande wa pili Mzee Kesho Yetu anasepa na mkwanja peke yake.

Kibaya zaidi, anaacha msala ambao ni wetu wote, ilhali sisi wengine hatujajiandaa....
Nilichojifunza,
1. Kuna mifumo ndani ya mifumo ya serikali
2. Mjini lazima ungangamae na usimwamini yeyote,watu hawana huruma
 
9th Portion:


.....Bi Mkubwa ikabidi aniulize kwa upole tu "Tuambie mwanangu, huyu jamaa unashida nae ipi?". Nikaendelea kuwa kimya tu kwa muda. Fikra ndio zikaanza kunituma, huenda kuumwa kwangu yule Kisauti akawa anahusika. Nilikuwa nishamsahau kabisa. Nilipatwa na hasira kuona nateseka kwa kosa lisilokuwa langu. Mshua alivyoona bado nipo kimya, sijamjibu Mama chochote, akanyanyuka na kuanza kuondoka. Bi mkubwa akamuuliza

Bi Mkubwa: "Baba nanii unaenda wapi sasa?

Mshua: "Sasa mtu haongei, nitakaa hapo siku nzima?"

Bi Mkubwa: "Unajua ili ni tatizo kubwa sana, usilifanyie mzaha"

Mshua: "Mzaha anaufanya huyo hapo, katibua watu mjini huko, karudi kutupa sisi shida"

Bi Mkubwa: "Kwahiyo tumuache afe"

Mshua: "Na akiendelea kukaa kimya, atakufa kweli"

Nilivyoona mzozo utaenda kuwa mkubwa, ikabidi niwafungukie issue nzima ilivyokuwa. Baada ya hapo wakaanza kujadiliana nini kifanyike. Bi Mkubwa akashauri wampigie simu Kisauti ili kumuomba msamaha, Kisha waangalie namna gani wanalimaliza lile jambo. Ila Mshua akagoma.

Bi Mkubwa: "Mwanao hali yake sio nzuri huyu, tuwasiliane na mdeni wake, tumlipe yaishe"

Mshua: "Hatuwezi lipa hela ambayo hatujachukua. Huo ni unyonge, na siwezi kuufanya. Dawa ya moto ni moto, kwavile kaanza yeye, acha tuendeleze, ngoja niwasiliane na Mzee Taba, ili tumpeleke kwa mtaalam"

Bi Mkubwa: "Mwanangu haendi kwa mtaalam wala kilingeni, kesho asubuhi naenda nae kanisani kwenye maombi"

Mshua: "Kwa hali ilivyo, lazima twende tu, na ilo halina mjadala"

Ukatokea mvutano mwingine pale, wapi nipelekwe hiyo kesho. Ila Mshua kutokana na commanding force yake, ikaamriwa nipelekwe kwa mtaalam. Kesho yake asubuhi na mapema tukaenda hadi kilingeni. Bi Mkubwa nae hakutaka kubaki nyumbani, alitaka awe na Mimi muda wote ili kujua hatma yangu.

Kufika kwa mganga tukapokelewa vizuri. Kutokana na hali niliyokuwa nayo, nikapewa kipaumbele kuonana na mtaalam. Tulivyoingia ndani, akaanza kuweka vitu vyake sawa, ongea ongea mambo yake pale.

Kuna muda nadhani alipandisha mashetani, maana lafudhi ilibadilika. Yeye ni mtu wa Kanda ya ziwa, ila ghafla akaanza kuongea lafudhi ya kimasai. Kuna mtu mwingine ambae ni msaidizi wake, ndio akawa anasaidia mwongozo wa yaliyokuwa yanaongelewa. Zoezi lilidumu kama nusu saa, then akarudi normal. Bila hata sisi kuongea sana, akaniambia, "Kijana unabahati sana kuendelea kuliona jua mpaka muda huu. Wapinzani wako, dhamira yao ni ya dhati". Mshua akauliza, kwahiyo nini kifanyike?. Yule mtaalam akasema kwasasa kuna kitu inabidi nimfanyie ili kudhibiti maumivu, alaf usiku ndio tutafanya zoezi kamili la kumtoa kwenye hii hali". Mshua akasema sawa, hakuna shida.

Mtaalam akaanza kufanya kazi yake pale. Mle ndani kulikuwa na kinu kikubwa kama vile wanavyotwangiaga wanawake, ila chenyewe kimechakaa sana, yawezekana ni cha muda mrefu, na rangi yake ilikuwa nyeusi tii, na mistari mistari myeupe. Sasa baada ya mtaalam kufanya mambo yake, akataka kupanda juu ya kile kinu, sikujua dhumuni lake lilikuwa ni lipi, maana wote mle tulibaki kuwa watazamaji tu. Wakati yupo juu ya kile kinu, alianguka yeye na kinu chake na kutanguliza uso chini. Alivyofika chini, kimya kikatawala. Urefu alioanguka ulikuwa mdogo sana, hata mtoto mdogo angeweza kusurvive, ila cha ajabu mganga alizimia. Yule msaidizi wake ndio akamkimbilia ghafla na kumnyanyua. Akachovya ule usinga kwenye kibakuli fulani kilikuwa pembeni, alaf akaanza kumpiga nao, huku anaongea maneno ambayo sikuyaelewa. Baada ya muda, mtaalam akaamka, anaongea ila sauti inatoka kwa mbali sana kama kakabwa au ametoka kukabwa.

Muda huo wote, sisi tupo kimya tu. Fahamu zilipomrudia vizuri na kuwa na utimamu wake. Akatwambia kwa upande wake, ili zoezi lipo nje ya uwezo wake, yani limemshinda. Akatuelekeza kwa mtaalam mwingine, aliyekuwa kijiji cha pili ambaye anaweza kutusaidia. Mshua na Bi Mkubwa wakawa wanajadiliana, Mshua anauliza kama twende siku hiyo hiyo, au kesho yake, ila Mama anataka turudi nyumbani. Yule mtaalam akawaambia, kadiri mnavyochelewa, ndivyo mnavyojisogeza kwenye kilio. Muwahisheni huyu, vinginevyo mtamkosa.

Bila kupoteza muda, tukafunga safari mpaka kwenye hicho kijiji. Tukaulizia hadi tukafanikiwa kumfikia yule mganga. Kutokana na miundombinu ya kijijini ilivyo, tulijikuta tunafika pale jua likiwa limeshaanza kupungua nguvu.

Tulipokelewa vizuri na msaidizi, tukakaa foleni kusubiria zamu yetu ifike.

Mida ya saa kumi na mbili kasoro, ndio tukafanikiwa kuonana nae. Hapo Bi Mkubwa nafsi haijamtulia kabisa. Muda wote kama ana mashaka na mganga. Ile hali ya Bi Mkubwa ikawa inamkera yule mtaalam. Akatwambia "Kuna hii dawa, ili zoezi lifanikiwe, inabidi wote watatu muilambe". Akaanza kutaka kumpa Bi Mkubwa, Mama akasita kidogo. Yule mganga akamkata jicho. Ikabidi Bi Mkubwa akubali kuilamba. Cha ajabu baada ya Bi Mkubwa kuilamba, sisi wengine hatukupewa. Bi Mkubwa akahoji kulikoni? Yule mganga akatoa usinga na kumpiga nao kichwani, Bi Mkubwa akasombwa na usingizi. Mimi na Mshua tukajikuta tunatazamana tu bila kusema chochote.

Baada ya salamu, akatwambia "Poleni sana na safari, maana huku tulipo ni mbali sana na mlipotoka". Baada ya kumuelezea dhumuni letu la kuwa pale, nae akafanya standard procedures zao (naziita standard procedure maana kote nilipoenda naona wanafanya hivyo). Baada ya muda kidogo akaanza kutwambia. Akaendelea "Tatizo lililowaleta hapa nimeliona vizuri sana, ila kwa bahati mbaya lipo nje ya uwezo wangu"

Mshua akamuuliza "Unamaanisha nini?". Yule mganga akasema "Aliyemfanyia hivi kijana wako, ni mtu aliyedhamiria sana, na hata huko alipoenda, ni Kwa mtu mwenye uwezo wa juu kuliko wangu. Hapa ninaweza kuliona tatizo, lakini uwezo wa kulitatua ndio sina"

Mshua akawa kama mtu aliyekata tamaa, akamuuliza yule mtaalam "Sasa unatusaidiaje au unatushauri kitu gani?. Yule mganga akamjibu "Kitu ninachoweza kuwasaidia kwasasa ni kuwapa sehemu ya kupumzika usiku wa leo, na kesho patakapokucha, nawashauri mtafute mganga mwingine".

Kusikia vile, hata Mimi nikajihisi kukata tamaa, Kisauti amedhamiria kunipoteza.

Mshua akamuuliza, dhumuni la yeye kumfanyia vile Bi Mkubwa ni lipi?. Mtaalam akamwambia "Huyu hakuwa na utulivu wa nafsi, kadiri muda unavyoenda angeweza kunikwaza, ila msiwe na wasi, ataamka ndani ya muda mchache ujao.

Mshua akaomba tuondoke siku ile ile. Wakasaidiana kumuweka Bi Mkubwa ndani ya gari, na kumlaza siti za nyuma. Mimi na Mshua tukawa mbele, safari ikaanza.

Tukiwa njiani, Bi Mkubwa ndio fahamu zikamrudia, akajiinua na kukaa. Mshua akageuka na kumuuliza anajiskiaje? Bi Mkubwa hakujibu kitu, ila likamtoka fyonyo moja refu. Kiasi kwamba kule mbele tukapatwa na hali ya kutaka kucheka. Kuzuga ikabidi nigeukie nje, maana ningecheka yangezuka mengine. Mshua sababu ya kuendesha, plus ubovu wa barabara hakuweza kugeukia nje,alaf kicheko kikataka kumponyoka. Akazuga kupiga chafya na kujikoholesha. Picha nzima Bi Mkubwa akawa kaisoma. Bi Mkubwa ni dizaini ya wale wa wamama ambao Ukifanya kosa anaweza akakukata jicho kali hata kwa dakika 5 nzima, sasa ndicho kilichotokea kwenye gari. Alimkata jicho Mshua, kiasi kwamba kule mbele Mshua akawa anahisi ile hali. Ila hapo hapo anajizuia kucheka tena, maana heri ya Mimi, yeye angecheka tena ile safari ingekuwa chungu kwake.

Wote tukawa kimya, unasikika mziki tu kwenye radio. "Zima mamiziki yako inaniumiza kichwa Mimi" Bi Mkubwa akawaka ghafla, Mshua wala hakuongea kitu, akazima, safari ikaendelea.

Njiani nzima akawa anasikika Bi Mkubwa tu, anatusema weee, alaf anakaa kimya. Baada ya muda kidogo anatusema tena, Kisha anakaa kimya.

Mshua yeye yupo kimya tu, macho yako mbele muda wote. Kadiri gari inavyonesa nesa kwenye ile barabara mbovu, na Mimi ndivyo ninavyozidi kugugumia maumivu, Mama nae anakunja sura kwa uchungu, kama vile na yeye anaumia. Mshua yupo kimya, hana story na mtu. Ila kila Bi Mkubwa akimsema, yeye ananikata jicho Mimi, kujaribu kunionesha kuwa Mimi ndio chanzo.....

Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Hapo kwa bi mkubwa nimecheka mpaka machozi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
Inategemea na wahusika mkuu ukitaka mastaa Bei huwa juu Sana maana malipo yao nayo yapo juu lakin ukichukua wale wa Hali ya Kati na ukataka kila tukio liwe Kama hivi ilivyosimuliwa ni zaidi ya 100m
Lakini lazima hela italipa aisee na movie kuchukua tuzo kadhaa. Kama ile movie ya VIVA RIVA ya Djo Tunda wa Munga, au movie ya TSOTSI. Waigizaji wasio mastaa ila walio serious na kazi
 
Lakini lazima hela italipa aisee na movie kuchukua tuzo kadhaa. Kama ile movie ya VIVA RIVA ya Djo Tunda wa Munga, au movie ya TSOTSI. Waigizaji wasio mastaa ila walio serious na kazi
Ndio itawezekana, yaani inawezekana kabisaaaaaa
 
Back
Top Bottom