Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Ila all in all Analyse una akili nyingi sana na ni mwandishi mzuri

Pili, una uwezo mkubwa wa kuhimili hisia maana masimango ya watu humu na bado unajibu kwa utulivu, no panic
Kuna some comments nilikuwa nikisoma mwenyewe nakasirika

Tatu, kupitia story hii walau nimepanua uelewa wangu wa namna ya kumuomba Mungu, kama mtu anafikia extent ya kwenda kwa mganga kupikwa, hizo ishu za kutapeliwa hutoboi bila msaada Mungu
 
21st Portion:

...Nyumbani nilipokelewa vizuri tu, tena kwavile safari walijua nimekuja kuwaangalia sababu ya ugonjwa wa Mama, hivyo Mshua hakuwa mkaksi kwangu. Hali ya Mama ni kweli haikuwa nzuri, alikuwa haishi kulalamika maumivu na vichomi vya mara kwa mara. Mwanzoni walivyompeleka hospitali, alipewa tu dawa ambazo walidhani zingeweza kulitatua tatizo lake. Ila alitumia mpaka zikaisha, ila tatizo likaendela.

Nilivyofika ikabidi nishauri turudi tena hospital kwa uangalizi zaidi. Na kweli tulivyoenda tena, wale madaktari baada ya vipimo vyao, wakasema Mama anasumbuliwa na appendix na kwa stage iliyofikia, inatakiwa afanyiwe upasuaji haraka sana. Binafsi nikishasikia habari za upasuaji, huwa naichukulia kama habari nzito hata kama ni upasuaji mdogo. Ikabidi tushauriane kama familia nini kifatie, maana Kwa mazingira ya hospital ya pale kijijini, haikunipa amani kabisa kuwaruhusu wamfanyie upasuaji Mama. Mshua akabisha bisha sana pale, Mama nae asivyopenda kusafiri, akawa anasisitiza tufanyie pale pale. Kwavile watoto tuko wengi kuliko wazazi wetu, mawazo yetu ndio yakapita, kuwa upasuaji usifanyikie pale kijijini.

Baada mjadala huo kuisha, ukaibuka mjadala wa hospital gani aende. Nikashauri twende Bugando Mwanza, kwanza ni karibu lakini pia pale Mama atakuwa chini ya uangalizi mzuri wa Dada. Mshua akashauri twende Dar, kule huduma ni nzuri na kuhusu sehemu ya kufikia atafikia kwangu.

Analyse: "Kule Mama hawezi kuwa comfortable tofauti na kwa Dada"

Mshua: "Kwanini asiwe comfortable?"

Analyse: "Sasa unadhani Mimi na wewe tutaweza kumpa uangalizi mzuri kuliko Dada?"

Mshua: "Kwani mpaka tumuangalie Mimi na wewe?"

Analyse: "Sasa nani mwingine atamuangalia?"

Mshua: "Mkeo"

Analyse: "Mke yupi Mzee?. Sina mke mjini Mimi"

Mshua: "Huna mke, au huwa anakuja na kuondoka?"

Mama: "Nyie mkishaanza kubishana hapo, mpaka apatikane mshindi Mimi ntakuwa nishajifia hapa"

Ikabidi mazungumzo na Mshua yakome kwa muda. Tukaadhimia Mama aende Bugando. Tulisafiri nae mpaka kule, Mshua yeye alibaki. Kufika Bugando tukawaelezea tuliyoambiwa hospital kule kijijini, tukawapa na makaratasi ya vipimo vyao walivyofanya. Wakayasoma, kisha wakashauri afanyiwe vipimo upya, baada ya hapo ndio taratibu zingine zifatie.

Majibu ya vipimo vyao pale Bugando yaliporudi. Mama akaonekana hana tatizo appendix, isipokuwa kwenye mifupa ya nyonga uloto ndio umepungua (sababu ya umri), hivyo mifupa inasagana na kumletea maumivu. Akapewa dawa na ushauri wa baadhi ya vyakula anavyotakiwa azingatie, Kisha tukaruhusiwa. Hakufanyiwa upasuaji. Tukaendelea kukaa Mwanza, tukishangaa Jiji kidogo. Mshua akawa anataka turudi;

Mshua: "Ameshapewa dawa, fanya mpango arudi sasa"

Analyse: "Ngoja walau tufanye utalii kidogo kwa wiki hii kisha tunarudi"

Mshua: "Umenisikia vizuri nilichokwambia?. Nimesema fanya mpango Mama arudi, wewe hata ukiendelea kukaa mwaka, Sina tatizo"

Sister: "Lakini Baba, ungemuacha hata siku chache, huko anawahi kufanya nini?"

Mshua: "Hivi nyie sijui hata kama mnanielewa. Yani mnanipangia juu ya mtu ambae mmezaliwa mkanikuta nae?. Nimesema namuhitaji mke wangu"

Tulianza tunajadiliana kawaida tu, ila Mshua akaenda anabadilika mdogo mdogo. Kesho yake tukarudi nyumbani. Home Sweet Home.

Mshua: "Kwahiyo hawa madaktari wa hapa kijijini walikuwa wanataka kufanyia mazoezi mwili wako?"

Mama: "Yameshapita hayo, makosa hutokea"

Mshua: "Ni kwavile huo upasuaji haukufanyika tu, ila nadhani wangeomba uhamisho. Lakini hata hivyo lazima niwafate tukaambizane ukweli"

Analyse: "Hata ukiwafata itabadili nini, acha tu yapite"

Mshua: "Ili limepita, lakini maradhi hayaishi kuja, nataka siku nyingine wakiiona hii sura, wakumbuke notsi zote walizosoma hadi wakahitimu"

Nikamkubalia tu, then nikaingia jikoni kutaka kusaidia kupika maana hatukula njiani. Mshua akaniambia nijipikie mwenyewe tu, maana chakula cha Mama ameshakipika. Nilijua asingeniruhusu kula kile chakula, ila nikamjaribu tu;

Analyse: "Lakini wote tumetoka safari"

Mshua akacheka kwanza, "Yani ninunue mahitaji yote humu ndani, pia nikupikie. Huyu ni mke wangu"

Analyse: "Na Mimi ni mwanao"

Mshua: "Nani kakwambia?. Una uhakika gani wewe ni mwanangu?. Ukiachana na sisi kufanana maana hata Mimi na Mama yako tunafanana, una ushahidi gani mwingine?. Huyu ni mke wangu, ukitaka cheti Cha ndoa kipo, wasimamizi wapo. Wewe unachochote cha kuthibitisha wewe ni mwanangu?.

Mama yeye anacheka tu, wala hachangii chochote. Mshua najua alikuwa katika mood ya utani, lakini kwenye mood ile ile ya utani, nilikuwa na uhakika kile chakula siwezi kula, otherwise mood yake ingechange. Maana nakumbuka kipindi niko O level, Mshua alikuwa na kawaida ya kutupikia. Tukitoka shule tunakuta chakula tayari. Ilitokeaga nikasingiziwa mimba, Mshua alimaindigi kwamba anatupikia chakula (Mimi na mdogo wangu), tukishiba tunaenda kusumbua watoto wa watu. Alisema hatokaa atupikie tena maana tushakuwa vidume. Japa lile soo, baada ya mtoto kuzaliwa iligundulika sihusiki, ila Mshua aliendelea kunimaindi, yeye msimamo wake siku zote ilikuwa mwanamke hawezi kukusingizia mimba kama hujalala nae.

Nikaingia zangu jikoni kupika.

***** ****** *****

Siku zilisogea sana, nilikaa takriban mwezi na nusu. Mpaka jioni moja Mshua aliniomba tuongee mida ya usiku shughuli za nyumbani zikiwa zimepoa.

Siku hiyo hiyo, baada ya kula chakula cha usiku, tukaenda kukaa nje kwenye bustani. Tukiwa pale nje akaniuliza "Vipi unashida gani safari hii?"

Nilikaa kimya kwa muda, nilikuwa najaribu kutafakari, nianzie wapi kumuomba msamaha? Au nifunguaje haya mazungumzo?

Alivyoona nipo kimya sana, akabaki ananiangalia tu bila kusema chochote. Kisha akanyanyua simu yake, na kuniuliza:

Mshua: "Najua unatatizo, vipi niende ndani, alaf tuongee kwa njia ya simu?

Nikatabasam tu.

Analyse: "Nilionana na yule Mzee"

Mshua: "Aliniambia kuwa ulienda shambani kwake"

Analyse: "Kwanini hukuwa niambia yeye ni nani, au mipango uliyokuwa nayo juu yangu?"

Mshua: "Unadhani hiyo ingeweza kubadili kitu?"

Analyse: "Sio kubadili kitu tu, bali ingebadili maisha yangu yote"

Mshua: "Kwani sasa hivi huwezi kubadili hayo maisha yako?"

Analyse: "Sio kiwepesi kama ambavyo ingekuwa mwanzo"

Mshua: "Unapenda kufanya mambo kiwepesi au kwa njia ulizochagua wewe?

Analyse: "Hakuna anayependa kupita njia ngumu, ni matokeo tu ya machaguo yetu ndio yanaweza kutupitisha huko"

Akakaa kimya kwa muda. Alaf kabla hajaongea chochote, nikaona niutumie ule ukimya kumuomba msamaha.

Analyse: "Najua nimeku disappoint sana, nimefanya maamuzi mengi ambayo yameuvunja sana moyo wako na wangu. Ila...."

Kabla sijamalizia, akanikatisha.

Mshua: "Mimi ndio mwenye makosa hapa. Kama kuna anayetakiwa kuomba msamaha kwa kuivunja mioyo yetu, basi ni Mimi"

Akaendelea:

"Unajua katika maisha yangu, sikuwahi kabisa kufikiria kujiunga na jeshi. Ndoto na mipango yangu mingi ilikuwa sehemu nyingine kabisa. Mimi kujiunga na jeshi, ilikuwa ni ndoto ya Babu yako, yeye ndiye aliyenipush sana kuingia kule, japo nilikataa kwa nguvu zangu zote.

Kama ilivyokuwa kwako, nilivyomalizaga kidato cha nne, sikutaka kuendelea zaidi, nilitaka kuwa mfanyabiashara, ila Babu yako alitaka niendelee zaidi, ila kwa kupitia jeshini. Palitokea sintofahamu nyingi kati yetu, hadi ikapelekea Mimi kuondoka nyumbani na baadhi ya mifugo yake

Siku niliyorudi nyumbani, japo nilirudi na zaidi ya nilichoondoka nacho, ila Babu yako hakutaka kunipokea. Ilibidi wazee wa Kijiji wahusike katika kutupatanisha. Pamoja na adhabu ya bakora nilizopogwa mbele yao, Babu yako aliweka sharti la Mimi kujiunga na jeshi, hapo ndio ataweza kunisamehe kabisa na kunichukulia tena kama mwanae.

Sikuwa na jinsi, ilibidi nikubali, japo kutoka moyoni nilijenga chuki na yeye, kwa kunilazimisha kitu nisichotaka. Nilivyoingia jeshini, baada ya muda nikachaguliwa kwenda kozi Urusi. Hapo kidogo ndio nikaanza kulipenda jeshi. Kabla sijaondoka nchini, Babu yako akataka niache nimeoa kabisa. Hapo ukatokea ugomvi mwingine, maana sikuwa tayari kwa jambo lile kwa muda ule.

Nikaambiwa kama sipo tayari kuoa, basi inabidi niache nimechumbia. Pia nikakataa. Wakati najiandaa na safari, Babu yako akaniambia atamchumbia mwanamke kwa niaba yangu. Nikamwambia sitomtambua. Nikaondoka tukiwa hakuna maelewano mazuri.

Nilivyohitimu na kurudi Tz, nilikuwa sitaki kwenda kusalimia nyumbani, maana ningekabidhiwa mke ambae sio chaguo langu. Nilikuja kupata matatizo ya kiafya jeshini, kwa mara nyingine tena Babu yako akaingilia kati kinyume na matakwa yangu, nikajikuta rasmi nimetoka jeshini. Nilivyorudi nyumbani, mwanamke niliyechaguliwa na Babu yako, ndio akapewa jukumu la kuniuguza kwa ukaribu. Kitendo cha kuwa nae karibu kwa muda mwingi, kikajenga mazoea kati yetu. Nikajikuta naanza kumkubali."

Kufikia hapo nikaanza kujiuliza maswali, huyu mwanamke anayezungumziwa hapa ndio Mama yetu au? Ikabidi nimuulize,

Analyse: "Huyo mwanamke aliyekutafutia Babu, ndio Mama?"

Mshua: "Ndio. Kwani vipi?"

Analyse: (nikacheka kidogo) "Kumbe ulitafutiwa mke na Babu?"

Mshua: (akanikata jicho) "Acha dharau kijana, kuna baadhi ya mambo yako nje ya upeo ,huwezi kuelewa sawa?"

Nikawa, mpole, Kisha nikawa najizuia kucheka. Mwisho wa siku tukajikuta wote tunacheka 😅😅😅😅.

Akaendelea na story:

"Kabla afya yangu haijatengamaa vizuri, ile biashara aliyopanga kunipa Babu yako, ikapata ajali ya moto. Nikajikuta sina kazi, Sina kiwanda. Hapo ndio hasira juu ya Babu yako zikazidi. Nikaamua kuondoka pale kijijini, na kwenda mbali nao kuanzisha maisha yangu mengine, kivyangu, bila wao. Mwaka 82 nikaamua kumuoa rasmi Mama yenu, kipindi ana ujauzito wa dada yenu.

Majukumu yalipozidi kuongezeka, ikabidi nisogee sehemu za mbali zaidi ili kutafuta kipato. Niliamini umri niliokuwa nao, ndio wakati sahihi wa kupambana. Hakuna sehemu katika hii nchi ambayo sijafika. Nimenusulika kufa mara kadhaa huko migodini, nilishawahi kufukiwa hadi na kifusi. Huu mguu niliomia kipindi nipo jeshini, katika harakati za utafutaji, umeshavunjika tena mara kadhaa. Lakini pamoja na yote hayo, sikufikiria ku-make peace na Babu yako.

Sikuwahi kuwasiliana nae wala kurudi tena pale kwake. Kwa muda mrefu nilikuwa nikimchukia kwa maamuzi aliyoyafanya juu yangu, maana ni kama yaliniharibia maisha. Nilitamani sana angesimama upande wangu, au kusimamia yale niliyojipangia, na sio kunilazimisha kuwa vile anavyoona yeye inafaa.

Ila Mwenyezi Mungu ana njia nyingi sana za kutuonesha mambo ambayo sio rahisi kuelezeka. Hata uwe na moyo mgumu kiasi gani, akiamua kukufikishia ujumbe wake, basi jua atakufikishia tu, hata kwa namna ambayo hukuitarajia

Baada ya miaka mingi kupita, chuki na hasira juu ya Babu yako zikiendelea kuwepo. Alikuwa akinitafuta na kunitumia barua kupitia kwa wafanyabiashara waliokuwa wanatembea vijiji kwa vijiji, ila sikuwahi kumuandikia chochote. Ujumbe wangu nilikuwa naurudisha kwa mdomo tu, japo wahusika waliufikisha.

Mwenyezi Mungu akaamua kunionesha jambo. Mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru wa nchi hii, ila macho yangu yangu yaliendelea kuwa gizani kwa muda mrefu.

Ile siku ambayo wewe uliyozaliwa, ndio siku ambayo macho yangu yalianza kuona. Ujio wako, ulifanya hasira zote nilizokuwa nazo juu ya Babu yako kufutika. Pengine usingezaliwa, ningeendelea kuwa kipofu, japo macho yangu hayakuwa na tatizo. Ningeendelea kuamini nipo sahihi"

Sikuelewa anamaanisha nini, ikabidi niendelee kumsikiliza. Hapo ndio akanifunulia kurasa za kitabu ambacho sikuwahi kukisoma kabla. Kurasa ambazo zilikipa thamani kubwa sana kile kitabu. Kurasa zilizofanya niyatazame baadhi ya mambo, kwa mtazamo tofauti kabisa....
Beautiful story
 
21st Portion:

...Nyumbani nilipokelewa vizuri tu, tena kwavile safari walijua nimekuja kuwaangalia sababu ya ugonjwa wa Mama, hivyo Mshua hakuwa mkaksi kwangu. Hali ya Mama ni kweli haikuwa nzuri, alikuwa haishi kulalamika maumivu na vichomi vya mara kwa mara. Mwanzoni walivyompeleka hospitali, alipewa tu dawa ambazo walidhani zingeweza kulitatua tatizo lake. Ila alitumia mpaka zikaisha, ila tatizo likaendela.

Nilivyofika ikabidi nishauri turudi tena hospital kwa uangalizi zaidi. Na kweli tulivyoenda tena, wale madaktari baada ya vipimo vyao, wakasema Mama anasumbuliwa na appendix na kwa stage iliyofikia, inatakiwa afanyiwe upasuaji haraka sana. Binafsi nikishasikia habari za upasuaji, huwa naichukulia kama habari nzito hata kama ni upasuaji mdogo. Ikabidi tushauriane kama familia nini kifatie, maana Kwa mazingira ya hospital ya pale kijijini, haikunipa amani kabisa kuwaruhusu wamfanyie upasuaji Mama. Mshua akabisha bisha sana pale, Mama nae asivyopenda kusafiri, akawa anasisitiza tufanyie pale pale. Kwavile watoto tuko wengi kuliko wazazi wetu, mawazo yetu ndio yakapita, kuwa upasuaji usifanyikie pale kijijini.

Baada mjadala huo kuisha, ukaibuka mjadala wa hospital gani aende. Nikashauri twende Bugando Mwanza, kwanza ni karibu lakini pia pale Mama atakuwa chini ya uangalizi mzuri wa Dada. Mshua akashauri twende Dar, kule huduma ni nzuri na kuhusu sehemu ya kufikia atafikia kwangu.

Analyse: "Kule Mama hawezi kuwa comfortable tofauti na kwa Dada"

Mshua: "Kwanini asiwe comfortable?"

Analyse: "Sasa unadhani Mimi na wewe tutaweza kumpa uangalizi mzuri kuliko Dada?"

Mshua: "Kwani mpaka tumuangalie Mimi na wewe?"

Analyse: "Sasa nani mwingine atamuangalia?"

Mshua: "Mkeo"

Analyse: "Mke yupi Mzee?. Sina mke mjini Mimi"

Mshua: "Huna mke, au huwa anakuja na kuondoka?"

Mama: "Nyie mkishaanza kubishana hapo, mpaka apatikane mshindi Mimi ntakuwa nishajifia hapa"

Ikabidi mazungumzo na Mshua yakome kwa muda. Tukaadhimia Mama aende Bugando. Tulisafiri nae mpaka kule, Mshua yeye alibaki. Kufika Bugando tukawaelezea tuliyoambiwa hospital kule kijijini, tukawapa na makaratasi ya vipimo vyao walivyofanya. Wakayasoma, kisha wakashauri afanyiwe vipimo upya, baada ya hapo ndio taratibu zingine zifatie.

Majibu ya vipimo vyao pale Bugando yaliporudi. Mama akaonekana hana tatizo appendix, isipokuwa kwenye mifupa ya nyonga uloto ndio umepungua (sababu ya umri), hivyo mifupa inasagana na kumletea maumivu. Akapewa dawa na ushauri wa baadhi ya vyakula anavyotakiwa azingatie, Kisha tukaruhusiwa. Hakufanyiwa upasuaji. Tukaendelea kukaa Mwanza, tukishangaa Jiji kidogo. Mshua akawa anataka turudi;

Mshua: "Ameshapewa dawa, fanya mpango arudi sasa"

Analyse: "Ngoja walau tufanye utalii kidogo kwa wiki hii kisha tunarudi"

Mshua: "Umenisikia vizuri nilichokwambia?. Nimesema fanya mpango Mama arudi, wewe hata ukiendelea kukaa mwaka, Sina tatizo"

Sister: "Lakini Baba, ungemuacha hata siku chache, huko anawahi kufanya nini?"

Mshua: "Hivi nyie sijui hata kama mnanielewa. Yani mnanipangia juu ya mtu ambae mmezaliwa mkanikuta nae?. Nimesema namuhitaji mke wangu"

Tulianza tunajadiliana kawaida tu, ila Mshua akaenda anabadilika mdogo mdogo. Kesho yake tukarudi nyumbani. Home Sweet Home.

Mshua: "Kwahiyo hawa madaktari wa hapa kijijini walikuwa wanataka kufanyia mazoezi mwili wako?"

Mama: "Yameshapita hayo, makosa hutokea"

Mshua: "Ni kwavile huo upasuaji haukufanyika tu, ila nadhani wangeomba uhamisho. Lakini hata hivyo lazima niwafate tukaambizane ukweli"

Analyse: "Hata ukiwafata itabadili nini, acha tu yapite"

Mshua: "Ili limepita, lakini maradhi hayaishi kuja, nataka siku nyingine wakiiona hii sura, wakumbuke notsi zote walizosoma hadi wakahitimu"

Nikamkubalia tu, then nikaingia jikoni kutaka kusaidia kupika maana hatukula njiani. Mshua akaniambia nijipikie mwenyewe tu, maana chakula cha Mama ameshakipika. Nilijua asingeniruhusu kula kile chakula, ila nikamjaribu tu;

Analyse: "Lakini wote tumetoka safari"

Mshua akacheka kwanza, "Yani ninunue mahitaji yote humu ndani, pia nikupikie. Huyu ni mke wangu"

Analyse: "Na Mimi ni mwanao"

Mshua: "Nani kakwambia?. Una uhakika gani wewe ni mwanangu?. Ukiachana na sisi kufanana maana hata Mimi na Mama yako tunafanana, una ushahidi gani mwingine?. Huyu ni mke wangu, ukitaka cheti Cha ndoa kipo, wasimamizi wapo. Wewe unachochote cha kuthibitisha wewe ni mwanangu?.

Mama yeye anacheka tu, wala hachangii chochote. Mshua najua alikuwa katika mood ya utani, lakini kwenye mood ile ile ya utani, nilikuwa na uhakika kile chakula siwezi kula, otherwise mood yake ingechange. Maana nakumbuka kipindi niko O level, Mshua alikuwa na kawaida ya kutupikia. Tukitoka shule tunakuta chakula tayari. Ilitokeaga nikasingiziwa mimba, Mshua alimaindigi kwamba anatupikia chakula (Mimi na mdogo wangu), tukishiba tunaenda kusumbua watoto wa watu. Alisema hatokaa atupikie tena maana tushakuwa vidume. Japa lile soo, baada ya mtoto kuzaliwa iligundulika sihusiki, ila Mshua aliendelea kunimaindi, yeye msimamo wake siku zote ilikuwa mwanamke hawezi kukusingizia mimba kama hujalala nae.

Nikaingia zangu jikoni kupika.

***** ****** *****

Siku zilisogea sana, nilikaa takriban mwezi na nusu. Mpaka jioni moja Mshua aliniomba tuongee mida ya usiku shughuli za nyumbani zikiwa zimepoa.

Siku hiyo hiyo, baada ya kula chakula cha usiku, tukaenda kukaa nje kwenye bustani. Tukiwa pale nje akaniuliza "Vipi unashida gani safari hii?"

Nilikaa kimya kwa muda, nilikuwa najaribu kutafakari, nianzie wapi kumuomba msamaha? Au nifunguaje haya mazungumzo?

Alivyoona nipo kimya sana, akabaki ananiangalia tu bila kusema chochote. Kisha akanyanyua simu yake, na kuniuliza:

Mshua: "Najua unatatizo, vipi niende ndani, alaf tuongee kwa njia ya simu?

Nikatabasam tu.

Analyse: "Nilionana na yule Mzee"

Mshua: "Aliniambia kuwa ulienda shambani kwake"

Analyse: "Kwanini hukuwa niambia yeye ni nani, au mipango uliyokuwa nayo juu yangu?"

Mshua: "Unadhani hiyo ingeweza kubadili kitu?"

Analyse: "Sio kubadili kitu tu, bali ingebadili maisha yangu yote"

Mshua: "Kwani sasa hivi huwezi kubadili hayo maisha yako?"

Analyse: "Sio kiwepesi kama ambavyo ingekuwa mwanzo"

Mshua: "Unapenda kufanya mambo kiwepesi au kwa njia ulizochagua wewe?

Analyse: "Hakuna anayependa kupita njia ngumu, ni matokeo tu ya machaguo yetu ndio yanaweza kutupitisha huko"

Akakaa kimya kwa muda. Alaf kabla hajaongea chochote, nikaona niutumie ule ukimya kumuomba msamaha.

Analyse: "Najua nimeku disappoint sana, nimefanya maamuzi mengi ambayo yameuvunja sana moyo wako na wangu. Ila...."

Kabla sijamalizia, akanikatisha.

Mshua: "Mimi ndio mwenye makosa hapa. Kama kuna anayetakiwa kuomba msamaha kwa kuivunja mioyo yetu, basi ni Mimi"

Akaendelea:

"Unajua katika maisha yangu, sikuwahi kabisa kufikiria kujiunga na jeshi. Ndoto na mipango yangu mingi ilikuwa sehemu nyingine kabisa. Mimi kujiunga na jeshi, ilikuwa ni ndoto ya Babu yako, yeye ndiye aliyenipush sana kuingia kule, japo nilikataa kwa nguvu zangu zote.

Kama ilivyokuwa kwako, nilivyomalizaga kidato cha nne, sikutaka kuendelea zaidi, nilitaka kuwa mfanyabiashara, ila Babu yako alitaka niendelee zaidi, ila kwa kupitia jeshini. Palitokea sintofahamu nyingi kati yetu, hadi ikapelekea Mimi kuondoka nyumbani na baadhi ya mifugo yake

Siku niliyorudi nyumbani, japo nilirudi na zaidi ya nilichoondoka nacho, ila Babu yako hakutaka kunipokea. Ilibidi wazee wa Kijiji wahusike katika kutupatanisha. Pamoja na adhabu ya bakora nilizopogwa mbele yao, Babu yako aliweka sharti la Mimi kujiunga na jeshi, hapo ndio ataweza kunisamehe kabisa na kunichukulia tena kama mwanae.

Sikuwa na jinsi, ilibidi nikubali, japo kutoka moyoni nilijenga chuki na yeye, kwa kunilazimisha kitu nisichotaka. Nilivyoingia jeshini, baada ya muda nikachaguliwa kwenda kozi Urusi. Hapo kidogo ndio nikaanza kulipenda jeshi. Kabla sijaondoka nchini, Babu yako akataka niache nimeoa kabisa. Hapo ukatokea ugomvi mwingine, maana sikuwa tayari kwa jambo lile kwa muda ule.

Nikaambiwa kama sipo tayari kuoa, basi inabidi niache nimechumbia. Pia nikakataa. Wakati najiandaa na safari, Babu yako akaniambia atamchumbia mwanamke kwa niaba yangu. Nikamwambia sitomtambua. Nikaondoka tukiwa hakuna maelewano mazuri.

Nilivyohitimu na kurudi Tz, nilikuwa sitaki kwenda kusalimia nyumbani, maana ningekabidhiwa mke ambae sio chaguo langu. Nilikuja kupata matatizo ya kiafya jeshini, kwa mara nyingine tena Babu yako akaingilia kati kinyume na matakwa yangu, nikajikuta rasmi nimetoka jeshini. Nilivyorudi nyumbani, mwanamke niliyechaguliwa na Babu yako, ndio akapewa jukumu la kuniuguza kwa ukaribu. Kitendo cha kuwa nae karibu kwa muda mwingi, kikajenga mazoea kati yetu. Nikajikuta naanza kumkubali."

Kufikia hapo nikaanza kujiuliza maswali, huyu mwanamke anayezungumziwa hapa ndio Mama yetu au? Ikabidi nimuulize,

Analyse: "Huyo mwanamke aliyekutafutia Babu, ndio Mama?"

Mshua: "Ndio. Kwani vipi?"

Analyse: (nikacheka kidogo) "Kumbe ulitafutiwa mke na Babu?"

Mshua: (akanikata jicho) "Acha dharau kijana, kuna baadhi ya mambo yako nje ya upeo ,huwezi kuelewa sawa?"

Nikawa, mpole, Kisha nikawa najizuia kucheka. Mwisho wa siku tukajikuta wote tunacheka 😅😅😅😅.

Akaendelea na story:

"Kabla afya yangu haijatengamaa vizuri, ile biashara aliyopanga kunipa Babu yako, ikapata ajali ya moto. Nikajikuta sina kazi, Sina kiwanda. Hapo ndio hasira juu ya Babu yako zikazidi. Nikaamua kuondoka pale kijijini, na kwenda mbali nao kuanzisha maisha yangu mengine, kivyangu, bila wao. Mwaka 82 nikaamua kumuoa rasmi Mama yenu, kipindi ana ujauzito wa dada yenu.

Majukumu yalipozidi kuongezeka, ikabidi nisogee sehemu za mbali zaidi ili kutafuta kipato. Niliamini umri niliokuwa nao, ndio wakati sahihi wa kupambana. Hakuna sehemu katika hii nchi ambayo sijafika. Nimenusulika kufa mara kadhaa huko migodini, nilishawahi kufukiwa hadi na kifusi. Huu mguu niliomia kipindi nipo jeshini, katika harakati za utafutaji, umeshavunjika tena mara kadhaa. Lakini pamoja na yote hayo, sikufikiria ku-make peace na Babu yako.

Sikuwahi kuwasiliana nae wala kurudi tena pale kwake. Kwa muda mrefu nilikuwa nikimchukia kwa maamuzi aliyoyafanya juu yangu, maana ni kama yaliniharibia maisha. Nilitamani sana angesimama upande wangu, au kusimamia yale niliyojipangia, na sio kunilazimisha kuwa vile anavyoona yeye inafaa.

Ila Mwenyezi Mungu ana njia nyingi sana za kutuonesha mambo ambayo sio rahisi kuelezeka. Hata uwe na moyo mgumu kiasi gani, akiamua kukufikishia ujumbe wake, basi jua atakufikishia tu, hata kwa namna ambayo hukuitarajia

Baada ya miaka mingi kupita, chuki na hasira juu ya Babu yako zikiendelea kuwepo. Alikuwa akinitafuta na kunitumia barua kupitia kwa wafanyabiashara waliokuwa wanatembea vijiji kwa vijiji, ila sikuwahi kumuandikia chochote. Ujumbe wangu nilikuwa naurudisha kwa mdomo tu, japo wahusika waliufikisha.

Mwenyezi Mungu akaamua kunionesha jambo. Mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru wa nchi hii, ila macho yangu yangu yaliendelea kuwa gizani kwa muda mrefu.

Ile siku ambayo wewe uliyozaliwa, ndio siku ambayo macho yangu yalianza kuona. Ujio wako, ulifanya hasira zote nilizokuwa nazo juu ya Babu yako kufutika. Pengine usingezaliwa, ningeendelea kuwa kipofu, japo macho yangu hayakuwa na tatizo. Ningeendelea kuamini nipo sahihi"

Sikuelewa anamaanisha nini, ikabidi niendelee kumsikiliza. Hapo ndio akanifunulia kurasa za kitabu ambacho sikuwahi kukisoma kabla. Kurasa ambazo zilikipa thamani kubwa sana kile kitabu. Kurasa zilizofanya niyatazame baadhi ya mambo, kwa mtazamo tofauti kabisa....
Waoooohhh ww ni msimuliaji mzuri sana ..
Unamaliza nakutuacha na viulizo..
 
Back
Top Bottom