Kalpana
JF-Expert Member
- Jun 16, 2017
- 32,603
- 62,269
Nimefika kipenzi..huyu mtu mbad anajua kusimulia hatari
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimefika kipenzi..huyu mtu mbad anajua kusimulia hatari
Sawa ccy asante sana.Nimefika kipenzi..huyu mtu mbad anajua kusimulia hatari
Na usijibu upupuHakuna issue ya kusadikika wala makosa madogo madogo. Sometime watu wanasema, ili wapate Cha kukosoa, hali inayopelekea kuwaondolea umakini.
Kwa faidanya huyo jamaa uliyemquote, dada alivyonipigia cm, kuna kitu nilikisema, nilisema hivi
"Tokea nilivyowatafutaga kuwapa habari juu ya Mimi kubadilisha line, sikuwatafuta tena, na hiyo siku dada ananipigia cm ilikuwa ni zaidi ya mwezi nipo kimya"
Sasa anapotokea mtu kuuliza, nilifuta majina na kubadili line, dada alinipata vipi, unahisi huyo mtu uelewa wake upoje?. Ndio maana sometime sijibu maswali, nayaangalia tu 😅😅😅😅
Nipe link pia mkuu. Zingine sijasomaDone mkuu
Lakini hii story ikiwa kwenye kitabu hutaisoma hata kurasa 3Alafu kuna watu unakuta wanasema Watz hawapendi kusoma maandishi mengi wakati uzi huu unaonyesha jinsi watu walivyo nashauku na kusoma
Nipe link pia mkuu. Zingine sijasoma
Kwamba mchagga alisema hatokaa akusahau kamwe2nd Portion:
... Ilivyofika siku aliyosema ataenda pale shule, niliwasiliana nae mapema tu asubuhi, akaniambia nitangulie shule, anikute ofisini.
Nikasubiria wanafunzi wengine wametoka assembly na kuingia madarasani, Kisha mdogo mdogo nikaingia eneo la shule. Kufika ofisini, Mwalim ananiuliza umefata nini bila ya mzazi?. Nikamjibu kuwa baba Yuko njiani, amesema anikute ofisini. Hapo namjibu, ila nina hofu ya kutosha, kwanza sielewi yule mchaga akija atasema Nini, tusije umbuka kama Ochu. Sasa ile hofu niliyokuwa nayo, ikamhadaa Mwalim, akaona kijana nipo serious, nimeshikika. Nikaambiwa nikae kwenye benchi nje ofisi pale.
Kama dakika 45 hivi, mchaga hatokei. Head Master akanimind, walim nao wakaanza kunisema (siunajuaga walim wakiwa wengi ofisini). Ghafla naona yule mchaga kaja, begi lake mgongoni kama vile katoka safari. Kufika karibu, akapokewa na head Master. Wakati wanasalimiana, nikageuza shingo ili nimsalimie, maana alinipita wakawa kama wamesimama nyuma yangu. Kumbe wakati nageuka, nae alikuwa ameplan kunipiga kofi, kwahiyo kile kitendo cha kugeuka, nilikutana na kofi Kali la uso, hadi nikachanika kidogo mdomo wa chini.
Hata Head Master hakuwa ametarajia lile swala, akawa ameshtuka, akamuuliza "We Mzee unafanya nn? Hebu tulia, usije kusabisha majanga hapa"
Yule mchaga akamkunjia sura Head Master "Huyu ni mwanangu, Nina haki ya kufanya lolote". Head Master akavunga. Mchaga akaomba taarifa kamili ya kilichotokea, akakaribishwa ofisini kwa Mkuu. Kikao kikaanza, Mchaga, Mkuu, Mwalim wa nidham, pamoja na Mwalim aliyetushika siku ile. Muda huo nimepigishwa magoti. Mchaga akaelezwa issue nzima ilivyokuwa. Alikuwa amekaa, akasimama kwanza, akawa kama anataka kutoka nje ya ofisi, alafu akarudi. Walim wanamtuliza "Mzee hebu tulia kwanza" alaf mkuu akamuagizia maji walau yamsaidia kupunguza presha. Yule dingi baada ya kunywa maji, aliinama kama dakika 5 yupo kimya tu. Baada ya hapo akaomba fimbo. Alininyuka hadi fimbo ikaisha, akaanza kunipiga makofi. Walim wanafanya kumzuia.
Sijawahi kupatwa hasira kama niliyopata siku ile, maana alinibutua sana, alaf sikuwa na lolote ninaloweza kufanya. Maana ningemdindia, maana yake msala wa kuleta mzazi ungeendelea kuwepo. Mwisho wa siku wakayaongea pale, nikapungiziwa adhabu, badala ya miezi mitatu, nikaambiwa nirudi baada ya mwezi mmoja na nusu alaf siku ya kuripoti nije na 150k kama faini.
Tukatoka nje ya shule, mdogo mdogo tukaizunguka shule, tukachukua uelekeo zilipo hostel za nje. Kwenye zile hostel ng'ambo ya barabara kulikuwa na bustan, tukaenda kukaa pale. Hapo njia nzima tupo kimya, hakuna anayeongea, maana nilitaka kuongea akaniambia nitulie, tutaongea tukifika. Sasa tumefika pale, cha kwanza kuniambia "Pole sana kijana, wale ni watu wazima, kugain trust yao sio kazi ndogo"
Nikawaka, "hata kama, sio unipige vile". Mchaga nae akawaka "Kwanza uliniongopea, ulisema kesi ya uzushi, kumbe umeiba mahindi ya shule? Sasa unataka wenzako wafe njaa?" Nikaanza kujiuliza huyu jamaa vipi, mzima kweli? Mchaga akaendelea "Watoto kama wewe ndio wanasababisha watoto wetu wanafeli, mnaenda shule kusumbua wengine, kama hutaki shule acha, ila usiwape wakati mgumu watoto wa wengine, kwanza naomba hela yangu iliyobaki".
Yani kunipiga kote kule, Bado unataka hela nyingine? Akaniambia "Dogo sijaja Tanga kusoma kama wewe, nimekuja kutafuta hela, usijitoe akili, ntarudi shule nikakuharibie". Nikaona isiwe kesi, nikatoa 20 nikampa akate 15k, mchaga akasema hapa hairudi chenji, ile 25k ilikuwa ni makubaliano kwavile ulisema wamekusingizia kesi, ila ungeniambia ukweli, dau lingepanda.
Nikataka kubisha, ila sikuona dalili za kuipata hiyo elfu 5, so ikabidi nipigie kimya tu. Akaniambia "Usihudhunike sana, nimekusaidia sana, tena next time nitakupunguzia, sitokufanyia Bei kubwa, tushakuwa wana". Nikaona huyu Mzee mbona kama ananichulia? Next time ipi?. Akaniuliza shule unamaliza lini kwani? Nikamjibu mwakani. Akatabasam kidogo, Kisha akaniambia "Kwa jinsi ninavyokuona, ni mbali sana, tunza namba yangu utanihitaji tena kabla hujamaliza shule". Akaamsha.
Alivyoondoka, nikaanza kujiuliza huo mwezi mmoja na nusu naumaliza vipi bila sehem rasmi ya kuishi? Maana sikutakiwa kuonekana hostel. Na kwavile Mzee ameshakuja, hivyo walim wanaamini nitaondoka nae, hakuna mzazi anayeweza kumuacha mwanae arande rande tu. Nakusema kukaa kwa mwanamke mwezi na nusu, bila kuwa na hela, isingekuwa rahisi.
Nikafikiria kwenda kwa ule mshangazi wangu wa buguruni sokoni, ila nikaona nitapoteza. Nikajikuta out of options, ikabidi niamue kurudi Dar kwa muda. Dar sikuwa na sehemu ya kufikia zaidi ya kwake. Hata hivyo sikuwa na mpango wa kukaa sana pale, baada ya kama siku 4 nikapanda bus kwenda Mbeya, kuna jamaa yangu nilikuwa nafahamiana nae mtu wa migodini, sema sio mchimbaji, yeye anafanya biashara ndogo ndogo kama kuuza sigara, bangi, mirungi, boxer n.k
Kitu ambacho najilaumu mpaka sasa, ule muda niliokuwa nimepewa suspension, walau ningeutumia kupiga pindi mchikichini, au hata kujisomea, ndio kwanza nazurura. Nikafika mpaka Mbeya, then nikachukua gari za kunifikisha Songwe, kule nilienda sehemu moja inaitwa Ngwala, jamaa ndio alikuwa kule. Nilivyofika, sikukaa siku nyingi, jamaa akasema kwa kipindi kile, pale hakuna hela, akasema twende kwenye migodi mingine tucheki harakati. Tulikuwa tunazunguka na kukaa sehemu kutegemeana na movements za wachimbaji. Ukiachana na uuzaji wa zile bidhaa, lakini pia sometime nasi tulikuwa tunajumuika na wadau wengine waliokuwa wanachambua chambua mabaki ya mchanga wa madini, au pia kufanya kazi zingine zinazojitokeza. Makapi makapi tuliyokuwa tunaokota na kuuza, yalikuwa yanatupa vihela viwili vitatu vya kusogeza siku.
Ubaya wa migodini, kuna watu tangia wameenda kule, hawajawahi kurudi makwao, kibaya zaidi wengine hata hawajulikani kwa majina yao halisi, ni mwendo wa nicknames tu. Nakumbuka kuna mwamba mmoja aliugua hadi akafa, ila hakuna aliyekuwa anamjua ndugu yake hata mmoja. Jamaa ilibidi azikwe kule kule tu, unaweza kuta ndugu zake mpaka leo wanaimani ndugu yao kaenda kutafuta, atarudi, kumbe jamaa hadi kuoza ameshaoza tayari. Lile tukio lilinifikirisha sana, itakuwaje likinitokea Mimi? Ndo yale mambo, unaangalia zako taarifa ya habari, unasikia kifusi kimefunika watu machimboni, mzazi unachukulia kawaida, unawapa pole wafiwa, ukiamini mwanao yeye yupo shule, kumbe ni miongoni mwa majeruhi au waliofukiwa.
Katika uokotaji kwenye yale mabaki, kuna siku jamaa yangu alibahatisha kajiwe fulani hivi kadogo. Kwavile Giza lilikuwa lishaanza kuingia, tukaamua kwenda kumcheki yule anaeyanunua, tupate hela ya kula then tulale. Jamaa kale kajiwe alikachukua kwa milioni mbili na nusu. Nikamwambia jamaa silali huku leo, naamsha usiku huu huu. Tukachukua pikipiki zikatupeleka mpaka center, lengo ni tulale pale, alaf asubuhi tuchukue gari za kutupeleka mjini. Mpaka muda huo, ile hela tulishagawana pasu kwa pasu, kila mtu anayake.
Kufika center, tukachukua room moja kwenye bar tuliyofikia. Jamaa yangu ni mtu wa tungi, so after kuoga, akashauri tuchukue bia kadhaa tunywee room. Binafsi sikuwa mnywaji pombe, ila nikaona sio kesi, jamaa kaagiza Serengeti, Mimi nikachukua safari 5 tu maana sikuwa mzoefu, tukarudi gheto. Ila binafsi sikuwa na amani kabisa, maana yule jamaa ni mzoefu, nikahisi naweza nikalewa, alaf akapita na hela zote nisijue nampatia wapi. Maana tumefahamiana kwenye harakati tu, tena niliunganishwa na jamaa mwingine ambae ndio alikuwa rafiki yetu wote. Nikawa namtegea jamaa anywe, ila nae akauchuna. Ananiuliza "Mbona hunywi?", Namjibu nitakunywa. Kiufupi mpaka kunakucha, hakuna aliyegusa bia hata moja, kulala yenyewe ilikuwa unasinzia kidogo, then unashtuka. Kulivyokucha, Mimi ndio nilianza kuondoka, maana safari yangu ilikuwa ndefu, nilitaka niunge Dar moja kwa moja, bia zote nilimuachia yeye.
Mbeya mjini, nikaweka kiasi cha zile hela kwenye account, then nikachukua chuma ya kwenda Dar. Hapo ni mwezi mzima unaenda kuisha tokea nitoke Tanga. Baada ya kufika Dar, plans zangu ilikuwa nikanunue materials alaf hizo siku chache nikazimalizie Galanosi kwa jamaa yangu. Nikiwa ndio bado nazunguka kwenye centers tofauti tofauti kununua past papers, Mshua akanipigia simu. Tukaongea fresh, akaniuliza maendeleo, nikamjibu kila kitu kinaenda vizuri, baada ya story mbili tatu tukaagana.
Usiku huo huo, akanipigia simu head prefect kwamba kuna usajili unaendelea pale shuleni kwa wanafunzi wa kidato cha 6, hivyo nifanye mpango niende haraka. Akaniambia pia kuhusu suspension, kwavile siku zimebaki chache, niende na mzazi wangu tena pale shuleni na hela ya fine, atafanya mpango nitapokelewa tu.
Nikaona wazo zuri, kumpigia simu yule Mchaga, akasema aina noma, kesho yake nirudi Tanga, then siku inayofatia twende wote shule akamalizie msala.
Ambacho Mimi na yeye hatukukijua, kumbe Mshua wangu akiwa kwenye kufatilia biashara zake, aliamua aje pale shule kuniangalia kabla hajarudi kijijini. So, muda wote tulioongea na simu Jana yake, tayari alikuwa na taarifa zangu full.
Mimi na yule Mchaga tulikuwa tumeandaliwa mtego. Kilichoenda kutokea, Mchaga alisema hatonisahau........
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Apostle...6th Portion:
.... I was a bit disappointed. Tukaongea story zingine mbili tatu, alafu tukaagana. Niliendelea kulifikiria lile swala, mwisho wa siku nikadhamiria nijipange Kisha niende mpaka kijijini, walau nipate kuongea nao ana kwa ana, maana dhamira yangu ilikuwa thabiti. Tofauti na wao walivyohisi, Mimi sikuwa napanga kuoa shangazi, kuna binti nilikuwa nae kwenye mahusiano ambayo kwa kiasi fulani yalikuwa serious.
Wiki moja baadae, sister angu akawa ameniita niende kumtembelea Mwanza, lakini pia aweze kuniunganisha na mchongo fulani. Nilivyoenda akafanikisha kuniunganisha na ilo deal, japo halikuwa na muda mrefu, maana nilikaa kule takriban mwezi mmoja.
Kumbe ukiachana na huo mchongo, sister alikuwa na mission nyingine. Nyumbani, wazazi walimpa jukumu la kumfahamu mwanamke wangu, Kisha awape taarifa. Sister nae alichokosea, badala walau aniulize, akawa anapitia simu yangu kimya Kimya. Simu yangu haikuwa na password, fingerprint wala patterns, so ilikuwa rahisi kuaccess information.
Katika mapenzi kuna muda wapenzi huwa wanachatig ujinga ili kusogeza siku. Sasa kuna chatting fulani nilikuwa nachat na shangazi, kiutani utani nilimwambiaga "Yani wewe ningefanikiwa kukuoa, ningekuwa na raha sana", ilikuwa ni chatting za kupoteza muda tu, ila sister akaichukulia serious. Na kwenye gallery alikuta picha zake kadhaa, akajirushia Kisha akakausha, maana hakuwa na namna ya kuniambia, kwasababu info amezipata kwa njia isiyo halali.
Siku zikaenda, na ule mchongo ukafika tamati, nikarudi Dar. Sasa kuna siku yule shangazi alitaka nimpost kwenye status, baada ya kuvutana sana, nikaona isiwe case, nikawahide watu wote muhimu, Kisha nikampost nakuweka caption ya kawaida tu. Sasa kumbe sister alikuwa ameinstall Whatsapp mbili kwenye simu yake, na Mimi sikugundua. Akaiona ile status. Nashangaa kuona amereply "Mdogo wangu ndio maana hata uleje haunenepi, mzigo wote huo kweli?"
Ikabidi nijaribu kumkataa:
Analyse: "Huyo ni Mama wa rafiki yangu"
Sister: "Kwenda huko, niliona picha zenu kwenye simu yako, nikahisi ni yaliyopita, kumbe ndiyo yaliyopo?
Analyse: "Haipo hivyo dad... "
Sister: "Huyo ndio mwanamke unataka kumpeleka nyumbani bila aibu? Hivi akili zako zipoje lakini?"
Ikabidi nikaushie msg zake, akaamua kunipigia simu, alinisema sana siku hiyo, hadi nikahisi kizungu zungu. Nikaanza kujihisi sasa hapa nilipofikia pashakuwa pabaya, wanaonizunguka wote hawana utulivu wala amani, inabidi niachane na haya mambo sasa.
Hata lile wazo la kumpeleka yule binti home, ikabidi nilisimamishe kwa muda. Maana mazingira hayakuwa supportive tena, na Kwa jinsi ninavyomjua Mshua, panaweza pakatokea ngumi nikienda, alaf sikutaka tufikie huko.
Huyu manzi, kipindi namwambia nataka nikamtambulishe nyumbani, alikuwa anasita sita, mara aseme nivute subira kidogo, muda bado. Alivyosikia nimesitisha kumpeleka nyumbani, ukawa ugomvi sasa, maana akawa ana push sana nimpeleke, hadi nikawa najiuliza, hiyo subira aliyokuwa anasema niivute, imekatika au?.
Fast forward kidogo. Niliendelea kufanya mishe zangu za kuunga unga mjini, huku nikipata nafasi, nazungusha bahasha maofisini. Pale gheto nilipokuwa nimepanga, kuna Mzee fulan smart, amechomekea muda wote, ni mtu mzima, ila hana mvi hata moja, panki lake muda mwingi limepakwa super black, nae alikuwa amepanga pale. Sema tofauti yetu, Mimi nilikuwa nimepanga chumba kimoja, yeye alichukuwa vyumba viwili na sebule, maana alikuwa na familia.
Mzee sikuwa na mazoea nae sana, hata jina lake halisi nilikuwa silifahamu, nilizoea kusikia mkewe anamuita baba fulani (jina kapuni), au vijana wengi pale mtaani walipenda kumuita Mzee Dingi (na Mimi humu nitapenda kutumia ilo ilo jina la Mzee Dingi). Huyu Mzee kwa mtazamo wa nje, alikuwa na muonekano fulani wa kimamlaka, yani ukimuona tu kwa mara ya kwanza, unahisi atakuwa mtu mzito au yupo kitengo nyeti somewhere. So, kutokana na mambo yangu kuwa magumu, nikapata wazo la kuongea nae, pengine anaweza akaniunganishia mchongo wowote hapa mjini. Siku ya siku nikamkabili, ilikuwa siku ya jumapili, maana huwa anashindaga home tu.
Nilivyomuelezea shida yangu, kabla ya yote akaniuliza kwanini nimemfata yeye?. Nikamjibu nimejaribu tu, maana siwezi jua nani anaweza nisaidia, maana mjini Sina connection ya maana. Mzee Dingi akaniuliza elimu yangu na taaluma niliyonayo. Nikajielezea vizuri pale. Tukaongea mambo mengi, mwishowe akaniambia, kesho nivae vizuri, Kisha nimpigie simu anielekeze nitakapomkuta. Tukabadilishana namba za simu, nikarudi ghetto kwangu.
Kesho yake nikajiandaa vizuri, Kisha nikampigia simu anipe direction. Akanielekeza niende mpaka city center, maeneo ya Samora, kuna bustan fulani ipo opposite na NBC, nimsubirie pale. Nikabeba copy za vyeti vyangu kwenye bahasha, nikaanza safari ya kuelekea town. Nilivyofika, nikamjulisha, akaniambia nimsubirie atakuja. Nikatulia.
Nilikaa sana pale, karibia masaa mawili, Mzee hajatokea, wala hajanicheki. Sema sifa kubwa ya jobless ni uvumilivu, nikaendelea kuvumilia. Baada ya muda, pembeni yangu alikuja akakaa jamaa, ambae alionekana kama Yuko stressed hivi. Kila muda anapiga simu, na ukimuangalia vizuri kama anataka kulia. Sasa katika kupoteza time maana nilikuwa bored, nikajikuta namuuliza kilichomsibu. Jamaa ndio kunipa story kuwa huwa anafanya biashara ya mkaa, analeta na kuuza kwa jumla, kisha anarudi mkoani. Hii ilikuwa ni trip yake ya kwanza tokea aanze biashara kwa upande wa Dar, mzigo wote umekamatwa na maliasili maana pia alikuwa amebeba vitu ambavyo hakuwa na vibali navyo, So upo kituo cha polisi. Haelewi afanye nini, na wale waliomshika, wanataka mpunga mrefu ili aachiwe. Ndani ya muda ule mfupi, alijikuta tu ananiamini, tukawa tunaongea kama watu ambao tumefahamiana kwa muda mrefu.
Binafsi sikuwa na cha kumsaidia, nikabaki nampa pole na kumtia moyo tu. Ghafla Mzee Dingi akawa amefika, nikanyanyuka kumsalimia, alafu nikawa nasubiria anioneshe direction tunayoenda, ila yeye akawa amemakinika sana na yule jamaa niliyekuwa naongea nae. Akaniuliza "Huyu mwenzako ana Nini?". Nikashangaa kwann amemuita mwenzangu, ila sikujali sana, nikampa briefly tu.
Baada ya kuisikia story ya jamaa, pale pale Mzee Dingi akasema anafahamiana na mwanasheria ambae alishamsaidiaga rafiki yake kwenye mzozo na maliasili. Akamwambia yule jamaa aongozane na sisi wakati yeye anampigia simu mwanasheria. Kilichonishangaza, wakati tunaondoka, ile simu aliyopiga, ikaita kwa Mzee mwingine ambae alikuwa eneo lile lile anakunywa kahawa, sema kakaa benchi jingine. Yule jamaa wa mkaa hakuusoma mchezo, sijui ni stress au vipi.
Mzee Dingi aliongea huku simu kaiweka loudspeaker wote watatu tunasikia, mwisho wa siku mwanasheria akasema yupo maaneo ya stesheni,kuna mgahawa anapata chai, so tumfate pale. Tukaongozana Mimi, Mzee Dingi na jamaa wa mkaa. Stesheni kuna mgahawa upo unaface stand direct, ndio tukaingia hapo. Tukamkuta huyo mwanasheria, nilivyoiangalia ile sura, ni Mzee ambae tokea nilivyofika kwenye bustan pale Samora, nilimkuta, muda wote alikuwa anasoma gazeti, story kidogo huku anakunywa kahawa. Yani kiufupi hakuwa na haraka yoyote. Ila tulivyomkuta hapo kwenye mgahawa, akatwambia tuongee tunachotaka kuongea, hana zaidi ya dakika 15, anawahi mahakamani.
Kuna kengele Fulani ikalia kichwani mwangu. Zilipigwa sound za kutosha pale, sound nyingi sana. Mpaka ikafikia hatua, yule jamaa wa mkaa akahitajika kutoa laki 5 ili issue yake iwe solved siku ile ile. Jamaa wa mkaa akawa anajaribu kubargain yule mwanasheria feki akanyanyua briefcase yake akatishia kuondoka, Mzee Dingi akawahi kumtuliza kuwa amsaidie jamaa issue yake, jamaa nae kwa kuhofia kupoteza mtu wa kumsaidia, akakubali kutoa hiyo 500k. Pale pale akili ikaniambia, kuna mtu anatapeliwa muda sio mrefu.
Kati ya wote pale, yule jamaa wa mkaa, alionekana kuniamini Mimi kuliko wengine. Hata ile 500k waliyokubaliana atoe, akanitupia Mimi jicho fulani kama vile kuomba ushauri au kuuliza atoe au asitoe?. Kwa mazingira yalivyokuwa, nikajikuta nampa ishara atoe hela, asiwe na wasi wasi, ila nafsi ilikuwa inanisuta sana.
Wote wanne, tukatoka nje ya ule mgahawa, tukapanda gari ya yule mwanasheria, mpaka ATM, jamaa wa mkaa akatoa hela. Kisha tukarudi mpaka karibu na jengo la mamlaka ya bandari, kufika pale, yule mwanasheria na jamaa wa mkaa wakashuka na kuingia ndani, Nia ni kwenda kuandikishiana hela walizipeana, then ndio waende polisi. Baada ya dakika kama 15, yule mwanasheria akarudi peke yake, akazama kwenye gari haraka, Mzee Dingi akang'oa.
Akili yangu ikawa wazi, kuwa Mzee Dingi ni tapeli tu, yeye na mwenzie. Ikabidi nivunje ukimya ndani ya gari, kwamba kilichafanyika haikuwa haki. Hakuna aliyenijibu, Mzee Dingi akapaki gari kituo cha mnazi mmoja pale, then Mzee Dingi akawa ananiambia "Bahasha wanazunguka nazo vijana wanaotafuta kazi, wewe umeshapata kazi tayari, tafuta briefcase au begi la kubeba mkononi, kesho usije tena kazini na hiyo Bahasha". Nikamwangalia yule Mzee, hana hata chembe ya huruma au kujutia. Yule mwanasheria feki, akaniuliza "Kwani bwana mdogo unachotaka hasa ni nini?". Nikamjibu " Tumrudishie jamaa hela zake". Mzee Dingi akadakia "Sikia apostle, Ungetaka kumsaidia, ungemsaidia kipindi tupo pale mgahawani, acha kutia huruma wakati hela unaitaka"
Nikajikuta hasira zinazidi, hasa alivyoniita apostle, maana ilikuwa ni kama kebehi fulani hivi. Yule mwanasheria feki kwenye ile 500k, yeye akachukua 200k, Mzee Dingi akapewa 200k, alafu akachukua 100k na kunikabidhi Mimi,kisha akanipa na namba ya simu kwenye kikaratasi. Akaniambia "Hiyo ndio namba ya yule jamaa, hiyo 100k ndio mgao wako, mtafute umrudishie walau nusu hasara"
Nikabaki nimetoa macho tu.....
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Sekeseke la Kisauti.....8th Portion:
.... Mtaji wa hela taslim aliokuwa nao Mzee Dingi ni milioni 3, japo tulivyopiga mahesabu tulitakiwa walau tuanze na milioni 5. Akasema hakuna shida, tunaweza anzia hiyo, then million mbili ataiongezea baadae. Nilitamani kumuuliza ataitoa wapi hiyo hela ya kuongezea, ila nikaamua kukausha.
Biashara ikaanza. Mkaa nikawa nachukulia Iringa, Mufindi, kuna Kijiji kinaitwa Usokani, huko ndio nikawa nachukulia mzigo. Nikiufikisha town, Mzee Dingi anaukabidhi kwa madalali wake, Kisha anasimamia makusanyo ya hela mpaka mzigo uishe. Ukiisha, narudi tena porini.
Mwanzoni wakati tunaanza, ilikuwa tunaleta trip moja, ila biashara ilivyo changanya, ikawa trip moja ikishafika town ikapokelewa na Mzee Dingi, kule kijijini naanza kukusanya mzigo mwingine. Sometime demand ikiwa kubwa, nilikuwa naenda hadi vijiji vingine kukusanya mzigo, mara nyingi nilipendelea kwenda maeneo ya Nyololo, kuna Kijiji kinaitwa Mzizi. Kutokana na kuzoeleka, ikafikia wakati tunaweza kusanya mzigo wa gharama kubwa hata kama hatuna hiyo hela. Mwanzoni usafiri tulikuwa tunatumia fuso moja ambayo ilibeba gunia 170, ila ikafikia wakati tukawa tunatumia kipisi chenye kubeba gunia 280, na sometime trip moja ingeweza kuwa na vipisi viwili.
Waliosemaga Ex ni kama furushi la miba, hatakiwi kurudiwa hata akija analia, maana ukimpa nafasi lazima atakuchoma tena, hawakukosea. Biashara ikiwa imenoga, vipisi viwili vipo town vinafaulisha mzigo, muda huo nipo kijijini najaza kipisi kingine nacho kiende mjini, Mzee Dingi akanipigia simu, kuwa uhitaji umekuwa mkubwa, hivyo nifanye mchakato wa kipisi kingine (Yani jumla viwe viwili) Kisha niviagize mjini. Kwavile hela ilikuwa haitoshi, iki kipisi nilichokuwa nasimamia muda huo, na kingine ambacho nimeambiwa nikiongeze, vyote ukiachana na gharama za usafirishaji na gharama za barabarani (ushuru, mizani,nk), gharama zingine zote hasa za mkaa wenyewe, kujaza, kushona na kupakia, zikawa ni Kwa Mali kauli, nikiwa naimani tutazilipa pindi mzigo ambao ushafika mjini utakapoisha.
Ila Cha ajabu, mzigo mwingine hadi nao unafiki mjini, ule wa mwanzo hela haijatumwa. Nikimchek Mzee Dingi, sound zinakuwa nyingi. Sikutilia mashaka kabisa. Kwavile hapakuwa na cha kufanya kule kijijini, nikawa nimesogea maeneo ya Mafinga ili kupumzisha mwili. Ila zikapita siku mbili bila kupewa feedback yoyote na Mzee Dingi. Nikimpigia, anasema nitulie atanipigia muda sio mrefu. Ila nikikaa kimya, hanitafuti.
Kule kijijini nao wakaanza kunipigia simu, wanataka hela zao. Nikimpigia Mzee Dingi, akawa hapokei simu zangu. Nikaamua kumfata Dar. Mpaka nafika, bado alikuwa hapokei simu zangu. Kesho yake mapema sana nikaamkia nyumbani kwake. Kufika pale naambiwa pale alishahamaga, kuuliza alipohamia, wanasema hawajui.
Nikajaribu kumpigia kwa namba ngeni. Alivyopokea na kujua ni Mimi, akanikatia simu. Akili ikaniambia nishapigwa!. Kule kijijini nao hawaishi kunipigia simu, na vitisho vikaanza kuwa vingi. Nikaona isiwe kesi, kwavile Mzee Dingi hapokei simu zangu, basi ngoja nianze kumsaka manually kwenye vijiwe vyake vyote. Kote nilimkosa, ila inaonekana kuna mtu akamfikishia taarifa za Mimi kumtafuta.
Akaamua kunipigia simu. Kupokea, namuuliza inakuwaje anafanya mambo ya ajabu kama yale?.
Mzee Dingi: "Sikupanga iwe hivi, ila kuna changamoto ilijitokeza, sikuwa na jinsi"
Analyse: "Hukuwa na jinsi? Wale jamaa wenye mkaa wao kule kijijini nawaambiaje?"
Mzee Dingi: "Wewe ni msomi mjanja apostle, wanakijiji hawawezi kukushinda. Tafuta namna yoyote ya kuwaelezea, au la, wapotezee, maana kule ushaondoka"
Analyse: "Tuachane na wanakijiji, kwahiyo Mimi sina mgao kwenye hela ambayo nimeisotea kule porini?"
Mzee Dingi: "Matatizo yaliyonikuta yanahitaji hela nyingi sana apostle, hii yenyewe unayoiona, bado haijatosha"
Analyse: "Kwahiyo unaniambiaje?"
Mzee Dingi: "Mungu ni wetu sote apostle, riziki yako haiwezi kupotea, itachelewa tu. Nitakuja kulipa, Alafu wewe bado kijana, nguvu na akili unavyo, pambana tu"
Aisee lilinitoka povu la kutosha, mpaka akaamua kukata simu. Nikapiga, akakata. Nikapiga, akakata. Kupiga tena nakuta kaniblock. Sijakaa sawa, yule jamaa mwenye mkaa wake akanipigia simu kutaka kujua kama nimewadhurumu au vipi?. Kila nikimpanga, haelewi. Huyu jamaa alikuwa mrefu, ana shingo ndefu pia. Alaf shingoni kwenye koromeo pamevimba kiasi. Huyu jamaa alikuwa na sauti ndogo/nyembamba sana japo ni mwanaume, hivyo watu wengi walipenda kumuita Kisauti, japo jina lake halisi ni Mbwana. Na Mimi humu nitakuwa natumia jina ilo la Kisauti. Sasa nikataka kuweka ahadi kwa Kisauti ya kulipa, ila nikifikiria hela wanayodai, nikaona sitoweza, maana Mzee Dingi ndio kaamua kunikataa. Kisauti alivyoona nipo kimya, akaamua kuniambia "Umeyataka mwenyewe mdogo wangu, sitolaumiwa kwa lolote nitakalofanya". Nikamuuliza utanifanya nini? Akajibu "Sikwambii, ila nataka ujionee". Kabla sijamjibu, akakata simu.
Nikampotezea!. Zikapita kama wiki mbili, nikiwa naendelea kumtafuta Mzee Dingi bila mafanikio. Nikaanza kupatwa na tatizo la mwili kuchoma choma. Yani inakuwa kama mtu yuko ndani ya mwili wangu, kashika sindano au pini, alafu ananichoma kwa kutokea ndani kuja nje. Ile hali ilianza taratibu sana, ila baada ya muda ikawa mwili mzima nausikia hivyo. Yani inaweza kunitokea kwa mfululizo ndani ya masaa matatu au manne, alafu inapoa kwa nusu saa au zaidi kidogo. Na hapo ikipoa, nakuwa nachomwa kidogo kidogo kwa mbali.
Yani kuna muda naweza kuwa nimelala au kupumzika, ghafla mwili unaanza kuchoma choma mfululizo, najikuta nasimama naanza kuzunguka tu gheto bila kujua nijikune wapi, inabidi nivue nguo,kisha nitumie ukuta kujikuna. Na ubaya yale maumivu yanatokea ndani kuja nje, sina namna ya kuyadhibiti. Kwa hali hiyo nikawa nashinda ndani tu, na ikitokea nahitaji kitu nje, basi mwendo ni kukimbia tu, tena nilikuwa naenda dukani na chenji kamili, ili nisipoteze muda dukani, na nikifika naanza kutoa hela kabla hata sijapewa nilichofata. Maana nilifikiria what if muuza duka kanipa bidhaa kabla sijampa hela alaf mwili ukaanza kuchoma, nikikimbia si wataniitia mwizi?. Just imagine nje watu wanakupiga, na ndani mwili unachoma, nitadeal na maumivu yapi, ya nje au ya ndani? Sikutaka hizo fedhea.Yani kiufupi nikiwa natoka dukani alaf ikatokea nikakutana na mtu anayenidai, angeweza hisi namkimbia yeye, kumbe mwenzie wala nawahi zangu ndani nikajikune ukutani.
Hali ilivyozidi kuwa mbaya, ikabidi niwajulishe home. Mama akaniambia niende. Aisee, sijawahi kusafiri safari chungu kama ile, maana bus ilikuwa ikipita kwenye matuta, hasa yale ya rasta, kwangu inakuwa mateso tupu. Maana narushwa rushwa, huku kwa ndani mwili unachoma.
Mpaka nafika destination ya lile bus, nilikuwa hoi hoi. Alafu kutokea pale, nikapanda kihiace cha kunifikisha kijijini kwetu. Njia nzima nailaani CCM Kwa kutotengeneza barabara, maana hapakuwepo na matuta, ila njia nzima kihiace kinatingishika, kokoto hazina uwiano.
Hali niliyofika nayo nyumbani, hadi bi mkubwa alijikuta chozi linamlenga lenga. Maana sikuwa hata na wiki tokea tatizo lianze, ila tayari uso ulishaanza kupoteza nuru.
Kijijini kwetu kuna zahanati kubwa tu ya kanisa, palivyokucha nikapelekwa pale. Fanyiwa vipimo vyote, ila halikuonekana tatizo lolote. Nikapelekwa hospital nyingine, nako majibu yanaonesha Sina tatizo. Ikabidi nirudishwe nyumbani, Mama muda wote majonzi tu.
Nikiwa nimelala kwenye kiti pale sebleni Kisauti akapiga simu. Kwavile sikuwa na hali nzuri, Mama hakuruhusu niongee na simu, akaipokeka yeye.
Kisauti akaulizia mwenye simu yuko wapi? Mama akamwambia nimelala. Kisauti akamuuliza Mama "Hali yake ipoje lakini?". Mama akamjibu kuwa hajisikii vizuri, amelala. Kisauti akacheka sana, alaf akamwambia Mama "Huyo ndio basi tena, hata msisumbuke nae, mtapoteza hela zenu bure". Ile kauli ikamchanganya Mama, ikabidi atake kujua sababu ya Kisauti kusema vile. Kisauti akamjibu "Sikutishi Mama angu, ila kama mna mashamba nyie uzeni tu, maana akiba mliyonayo haitotosha". Na kile kisauti chake, anazidi tu kumpanikisha Bi Mkubwa. Mwisho wa siku akamwambia "Nyie muulizeni mwenyewe anajua vizuri alichofanya, ila nawashauri msijisumbue nae". Akakata simu. Jamaa maneno anayoongea, na kile kisauti chake lazima ukereke.
Kipindi hayo mazungumzo yanaendelea, simu ilikuwa loudspeaker. Baba, Mama na Mimi wote tulikuwa tunayasikia yale mazungumzo, japo ni Mama pekee ndio alikuwa anaongea nae.
Simu ilipokatwa, wote wakawa wamenikodolea macho. Mama akaniuliza "Umefanya nn tena safari hii mwanangu? Mbona wewe huishiwi hizi sekeseke lakini?". Baba akanifyonya, alafu akasema "Mimi sio mtabiri, ila hapa lazima mwanamke anahusika, Yani kama hajatembea na mke wa mtu huyu, sijui"
Nikabaki kimya, namuwaza Kisauti na Mzee Dingi....
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Vp mstaafu bdo yupo hai?vp huyo mc haofii kutafutwa na mstaafu au ndugu wa mstaafu??Yeah, alafu Yuko kauzu as if nothing happened. Hii Dunia haitaki uwe na aibu kabisa
Watu wanatagiana wenyewe tuu mkuu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ha ha ha ..[emoji4]Watu wanatagiana wenyewe tuu mkuu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
[emoji38][emoji38][emoji38]nmecheka balaa“Naam jembe langu"
Mchaga kaupiga mwingi Sana[emoji1787]Mchaga alikuwa serious sana na kazi yake. Muda wote kakomaa na script tu [emoji28][emoji28]
Mchaga Alikua serious na kazi[emoji38]Baada ya ule msala, Mchaga alikuwa anataka hela ya ziada, vinginevyo atanifanya kitu mbaya. Makubaliano ilikuwa akanitetee shuleni, na sio kwenda kupigana[emoji28][emoji28]
Mchaga kauzu Sana[emoji1787]Hii story tamu hasa mzee mchaga alivomzibua analyse [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Tizama hapaSi kweli mjomba, Theluthi kubwa kuliko Robo.
1/3 > 1/4... Ama 0.667 > 0.25 ukiiweka kwenye desimali.
Kama ulimaanisha 1/6 ama 1/8 moja wapo katika hizi inaitwa Sumuni. Sikumbuki vizuri ni ipi kati ya hizo mbili ndio huitwa Sumuni ila hizo ndio ndogo kuliko robo i.e 1/4.
Kwa kifupi tu thaman iliyo ndogo kuliko robo ni kuanzia yenye kigawo kikubwa kuliko 4 ambayo ni 5 na kuendelea tukiwa na maana ya 1/5, 1/6, 1/7 en so sooo ila sio zenye thaman ndogo kuliko 4 kama 3 na 2 napo tukiwa na maana ya 1/3 (theluthi), 1/2 (nusu).