Ironbutterfly
JF-Expert Member
- Feb 5, 2023
- 3,042
- 8,227
Siyo mc garabu huyu?🤣🤣Ili muende kujaa kwenye page yake? Wabongo hamnaga shoo ndogo 😅😅
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Siyo mc garabu huyu?🤣🤣Ili muende kujaa kwenye page yake? Wabongo hamnaga shoo ndogo 😅😅
🤣🤣Siyo mc garabu huyu?🤣🤣
Usiende makao makuu njoo tawi la kinondoni. Kudadeki......13th Portion:
... Sikuwa na kitu nilichoweza kufanya kwa wakati ule. Hata kama ningesema nimbembeleze, still isingefanya kazi, maana sijui dhamira yake halisi ni ipi.
Sikutaka hata kulala pale. Nikaamua kurudi gheto kwangu, PS4 yake nikamuacha nayo.
Njia nzima kichwa kimezongwa na mawazo hasa juu ya yale mazungumzo na yule Mzee. Kuna muda unaweza ukawa umezungukwa na watu wengi, alaf wasiwe na faida, na wale wachache wenye faida pia usiweze kuwatambua. Kutwa nalalamika maisha magumu, michongo hakuna, alaf watu wenye uwezo wa kunipa michongo ndio nawapotezea, Kisha nakumbatia wasio na umuhimu.
Usingizi ulinipaa kabisa. Niliwaza mengi sana, kiasi kwamba nikajikuta namtumia msg yule Mzee kuomba kuonana nae tena siku inayofuata. Sikutegemea anijibu muda ule ule, maana ilikuwa ni karibia saa nane kasoro. Niliendelea kuwaza mambo tofauti tofauti mpaka nilipopitiwa na usingizi.
***** ****** ****** ******
Asubuhi niliamshwa na mlio wa simu yangu, iliyokuwa ikiita. Kuiangalia nakuta Mshua ndio anapiga. Sijui kwanini, ila nilishtuka sana. Nikajikuta naogopa kuipokea ile simu, maana najiuliza anataka kuniambia nini?. Yule Mzee amemwambia kama tumeonana? Au nikipokea nitaweza kuongea na comfortable?. Ushawahi kufanya jambo fulani la aibu sana, alafu ukutane na mtu au watu wanaolifahamu, huwa unapoteza ule uchangamfu mbele yao. Hata katika story utakazopiga nao, wakicheka utahisi wanakucheka ile aibu yako. Hiyo hali ndio nilikuwa najihisi muda huo wakati Mshua anapiga. Kwa mara ya kwanza nikashindwa kupokea simu ya Mshua. Ikaita hadi ikakata.
Nikiwa bado nipo pale pale kitandani, simu ikaanza kuita tena. Nilishtuka kana kwamba nimepigwa shoti ya umeme. Nilishusha pumzi za amani baada ya kuona jina la mpigaji. Ni yule Mzee ndio alikuwa ananipigia. Niliipokea, tukaongea mambo kadhaa, ila akaniambia Kwa hiyo siku hatokuwa na nafasi, lakini pia hata siku zinazofata, bado angekuwa busy. Hivyo akashauri kama alivyoniambia jana, kuwa wik end ndio ratiba yake inakuwa wazi. Tukakubaliana niende tena kule kule shambani kwake, siku ya jumamosi.
Baada ya kukata simu, mawazo yakanirudia tena. Picha ikanijia, ni Kwa namna gani masaa 24 yanaweza kubadili kila kitu. Maana ni ndani ya masaa 24, kutoka kuwa mtu anayeongea na Baba yake kwa vicheko na bashasha, hadi kuanza kumuogopa.
Baada ya masaa kadhaa ya kujivuta vuta pale kitandani, nikaanza kutafakari siku yangu niipeleke vipi. Unajua tatizo la kuwa jobless, ni kwamba unakuwa na muda mwingi sana, ila vitu vya maana vya kufanya ndio hakuna.
Baada ya kuwaza sana, nikaona ngoja niende kule maeneo ya katikati ya jiji, nikamtafute Mzee Dingi. Jamaa alitembea na karibia million 15, huku pakiwa na karibia million 6 ya kina Kisauti, ambayo hakuitolea jasho kabisa. Mawazo yakaniambia nimtafute walau nipate mgao wangu, maana tayari nishatumikia adhabu.
Nikasogea hadi maeneo ya Samora, ila hakuwepo. Nikatembelea vijiwe vyake vyote ila nikaambulia patupu, sielewi nampatia wapi. Kwenye simu bado kaniblock. Nikafikiria kwenda kwa Shani, ila nikaona tutaenda kulumbana, alaf ugomvi uzidi kuwa mkubwa. Nikajaribu kumpigia yule mpenzi wangu, nikakuta bado kaniblock. Nikaamua kurudi zangu home.
** **
Zilipita kama siku mbili hivi, Mzee Dingi akanipigia simu.
Mzee Dingi: "Uko wapi Apostle?"
Analyse: "Nipo gheto, vipi?"
Mzee Dingi: "Najua bado una hasira, ila wanaume hatuwekagi vinyongo, njoo tufanye kazi"
Analyse: "Nyie fanyeni tu mtajirike, Mimi Sina mpango na hizo kazi zenu"
Mzee Dingi: "Dogo mambo hayaendi hivyo, hakuna tuzo kwa ajili ya watu wanaopata hela kwa shida. Kazi zipo nyingi, utapata hela, na utasahau habari ya ilo deni unalonidai"
Analyse: "Siwezi fanya kazi alaf nimfaidishe mtu mwingine, nyie fanyeni tu ambao mnawezana"
Mzee Dingi: "Ile ilitokea tu, kwasababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. Safari hii tutakuwa mguu kwa mguu apostle"
Nikajifikiria kwa muda kidogo, nafsi ikawa mguu nje mguu ndani, Sina mchongo town, bills nitazilipa vipi?
Nikamuuliza, "Kuna dili gani sasa hivi?"
Mzee Dingi: "Hayo sio mambo yakuongelea kwenye simu, kesho njoo ofisini tujadiliane kwa kina"
Analyse: "Sina nauli, kama hatuwezi kuongea kwenye simu, Mimi siji"
Hakunijibu kitu, akakata simu. Alafu baada ya kama dakika tatu, ikaingia elfu sabini kwenye tigopesa toka kwa Mzee Dingi, Kisha akaniandikia msg.
"Kesho fanya juu chini uje Apostle. Usiende makao makuu, njoo tawi la kinondoni"
Nikamjibu "Poa"
Unajua kupambana kunaumiza, ila kukata tamaa kunaumiza zaidi. Maana aliyekata tamaa hana dira, anaweza kujikuta anafanya mambo ambayo hakuwahi kutarajia. Story na yule Mzee zilinifanya nikajiona hopeless sana. Nikajikuta nimeridhia kwa moyo mmoja kujiunga na kina Mzee Dingi.
. ***** ***** ***** ******
Kesho yake nikatimba pande za Kino, nikakuta timu ya watu watatu, Mzee Dingi akafanya utambulisho. Nikajiunga nao rasmi.
Tulijadili mipango kadhaa, na tokea siku ile tukaanza kupiga dili kulingana na zinavyokuja. Siwezi elezea in details ni kwanma gani tulikuwa tunafanikisha hizo deals, ni watu gani tuliwapiga au hata kuyataja hayo madili, maana sio lengo la story lakini pia huwezi jua nani anasoma, nisijekuamsha hasira zilizolala.
Tulikuwa tunahama vijiwe kadiri tunavyopiga dili, ili kuepuka kukutana na wale tunaowapiga. Wengi tuliokuwa tunawapiga, michongo yote ilikuwa based on coincidences, ndio maana baada ya kuspend time sana na kina Mzee Dingi, I will never ever believe in coincidence, NEVER.
Baada ya kama miezi miwili au mitatu, Mzee Dingi akaniomba tukutane wawili tu, Mimi na yeye. Tulikutana baa maeneo ya buguruni.
Mzee Dingi: "Apostle kuna mtu anataka kukutana na wewe. Kuna dili limejitokeza"
Analyse: "Ni nani huyo? Na kwanini atake kukutana na Mimi?"atake
Mzee Dingi: "Huyu mtu shoo zake sio ndogo ndogo Apostle. Dili zake zote ni mikia ya kondoo"
Analyse: "Mikia ya kondoo kivipi?"
Mzee Dingi: "Huyu kwa mwaka akipiga dili nyingi ni nne, ila mkwanja unaopatikana hapo, unaweza kwenda likizo muda mrefu, tena kwa mtoto kama wewe, unaweza Kaa hata mwaka bila stress ya kipato, ni matumizi tu"
Analyse: "Duh anaitwa nani huyo Mzee?"
Mzee Dingi: "Jina lake la kazi tunamuita Kesho Yetu"
Analyse: "Kwanini sasa anataka kuonana na Mimi?"
Mzee Dingi: "Wewe fanya mpango kesho tuonane nae pale Kinondoni, kuna dili analeta, linahitaji watu kadhaa, na wewe ametaka uwepo"
Analyse: "Ananijua kwani?"
Mzee Dingi: " Ndio anakujua, ameona kazi kadhaa ulizoshiriki, uchangamfu na usharp wako ndio anautaka"
Nikaguna pale, ila mwisho wa siku tukakubaliana, kesho yake tukutane pale Kino...
***** ****** ****** *****
Kesho yake asubuhi na mapema nikatimba Kinondoni Manyanya. Nikamcheki Mzee Dingi, akanielekeza walipokuwa wamekaa. Yupo yeye, mwanasheria feki, na Mzee mwingine ambae ndio ilikuwa mara ya kwanza namuona, kwa jina la kazi alikuwa anafahamika kama Kidevu.
Kitu kingine nilichonote, hawa jamaa wote hakuna aliyekuwa anafahamika kwa jina lake halisi. Na hiyo ndio sababu ilifanya Mimi niwaache waendelee kuniita apostle. Na kingine hakuna aliyekuwa anajulikana anapokaa. Kiufupi, ingetokea mmoja akakamatwa, angeishia kutaja majina ya apostle, Mzee Dingi, Kidevu au Kesho Yetu. Akiambiwa akaoneshe wanapokaa hao watu, wangezunguka Dar nzima.
Baada ya utambulisho. Mchongo mzima ukawekwa mezani. Kulikuwa na mwalim mstaafu ametoka kuchukua mafao yake. Yule mwalim alikuwa anahitaji eneo kubwa kwa ajili ya mradi wake wa green house aliotaka kuuanzisha. Lakini pia, alikuwa anahitaji vifaa kwa ajili ya umwagiliaji, na kuchimbiwa kisima kwenye ilo eneo atakalo nunua. Sasa mpango ilikuwa apigwe kwenye eneo, alafu dili likisha kamilika, apigwe kwenye vifaa na uchimbaji.
Mzee Dingi yeye alitakiwa kucheza kama dalali wa eneo linalouzwa, mwanasheria feki na yule Mzee Kidevu, wao wawe majirani, Mimi nikaambiwa niwe kama afisa mtendaji au mwenyekiti wa kile Kijiji. Mzee Dingi ananiambia:
"Wewe apostle inabidi uwe mtendaji wa kile Kijiji. Unajua watendaji wengi ni vijana na wasomi. Ni rahisi yule Mama kuamini"
Nikabaki na mwangalia tu. Akaendelea
"Yule Mama tukishamaliza kuuziana nae kiwanja, itabidi hapo hapo wewe (Mimi) kama mtendaji umwambie unaweza kumsaidia kutafuta kampuni ya uchimbaji visima, na kuweka set up nzima ya kila kitu kwa ajili ya project yake".
"Yani inabidi tukimaliza tu kulipana hela za kiwanja, malipo ya hizo process zingine yafatie. Kuna watu tutakuunganisha nao ambao ndio utaendelea nao kwenye hiyo nngwe ya pili"
Wakati tunaendelea kuongea pale. Kuna Mzee mwingine akaja, yuko smart, kabeba begi muundo wa briefcase au zile za kubebea laptop. Yule Mzee sidhani kama kuna mhuri ambao hana. Kibriefcase chake Kiko full, mihuri, Karatasi, Calculator nk. Akatoa mihuri kadhaa akaiweka mezani. Eneo ambalo alitakiwa akauziwe yule mstaafu, lilikuwa vigwaza. Huyu Mzee smart aliyeongezeka, ndio Mzee Dingi akanitambulisha kwake kama 'Kesho Yetu'. Huyu ndio alikuwa mastermind wa huu mchongo wote, na ndiye aliyetakiwa kuact kama muuzaji wa eneo. Na Kwa mujibu wao, tulitarajia kati ya million 50 mpaka 70, kutegemeana na namna tutakavyofatisha maelekezo ya Mzee Kesho Yetu.
Kila kitu kikawekwa sawa, then yule mstaafu akapigiwa simu, na makubaliano yakafikiwa kuwa kesho akalione lile eneo.
Unajua sometime unaweza Sikia story mtu katapeliwa,alafu ukaanza kumcheka na kumuona mjinga, ila huyu Mzee Kesho Yetu alinibadilisha mtazamo wangu. Mtu akitapeliwa, usimlaumu sana, peleka sifa kwa yule aliyemtapeli. Watu wana mahesabu makali sana, jinsi huyu Mzee Kesho Yetu alivyokuwa anapanga mambo, accuracy yake ni almost 100%. Kinachotakiwa ni kufatisha maelekezo yake tu.
Na hata dili nyingi ndogo ndogo tulizokuwa tunafanya na kina Mzee Dingi, zilikuwa zinatoka kwake zikiwa na full deatils ya kuzipush. Yeye alikuwa anapewa percent fulani ya mgao, alikuwa hashiriki. Ukiona kashiriki, basi ilo dili liko very serious, na target sio chini ya million 50. Na hata hii deal nilidhani usharp na usmart wangu ndio ulifanya anielewe na kuniunganisha kama jinsi Mzee Dingi alivyoniambia, lakin kumbe alikuwa na sababu ya tofauti kabisa. Kitu ambacho sikuwahi kukifikiria kabisa, ila yeye kwa upande wake alishakifikiria miezi mingi iliyopita. Na jibu alilipata ni "Apostle". Nilikuwa funguo yake bila hata ya Mimi mwenyewe kujua.
Tulivyoagana, wakati wengine washaanza kuondoka, nikamsimamisha Mzee Dingi.
Analyse: "Mzee hii deal inahusisha sura ngeni nyingi, na pia hela yake ni ndefu, kuna kila dalili ya kudhurumiwa hapa"
Mzee Dingi: "Apostle unaongea nini wewe?. Hakuna wa kukudhurumu hapa"
Nikamsikiliza tu, lakini sikuwa na amani kabisa.
Tukaagana nikaamsha. Mida ya jioni jioni, Mzee Dingi akaniwekea laki mbili kwenye simu. Kisha akanipigia
Mzee Dingi: "Apostle najua utakuwa na uhitaji wa hela, chukua hiyo, piga ua kesho inabidi utokee"
Analyse: "Tunakutania wapi?"
Mzee Dingi: "Wewe na wale wengine mtatangulia asubuhi sana. Mimi nitakuja na yule mlengwa baadae."
Analyse: "Poa poa"
Mzee Dingi: "Maelezo ya ziada utayapata kule kule, hakikisha unakuwa smart sana, usisahau begi lako"
Analyse: "Sawa nimeelewa "
Alivyokata simu tu, Shani akanipigia
Shani: "Uko wapi we Mtu?"
Analyse: "Nipo gheto tu"
Shani: "Naona umenisusa tokea siku ile. Mimi nishakumiss"
Analyse: "Me nipo"
Shani: "Unaweza kuja kwangu muda huu? "
Analyse: "Poa nakuja"
Shani: "Ndio maana nakupenda, huwekagi vitu rohoni. Haya njoo nakusubiri"
Nikaenda kuoga, ili niende.. ..
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Anatakiwa akae na Umughaka waandae script wafanye featuring ya Movie moja kali lililojaa utapeli; ushirikana. Yaani full vimbwangaSema we jamaa umepitia mambo mengi sana [emoji28][emoji28]
Hivi kuna ambacho hukijui kweli
Alikua anajaribu kwenda na scrept kumbe baba wa kweli ame-appear kwenye scene 😂Hahahahahha mzee alikua kazini[emoji23][emoji23]
Ulikua wapi siku zote,watakucheka watu[emoji23]
Stori ni nzuri na ina mafunzo mengi, asante sn mkuu.22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
Santee
22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
KaribuSantee