Eratosthenes
Senior Member
- Mar 13, 2013
- 102
- 114
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani huyu ni kama wewe tu upande wa mishangaziFamilia nzima Washakuona una uraibu wa mishangazi[emoji38]
Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mkuu naomba link niisome
Mkuu, ya kuandika ni mengi sana. Vuta picha tokea story ya kwanza kuweka hapa JF, mpaka hii ya sasa. Zote zingekuwa ndani ya Uzi mmoja ingekuwaje? 😅😅😅Oya Apposto em endelea acha utan story haijaisha
Stay blessed mkuu 👊👊Asante sana Analyse View attachment 2585607
Ameen apostle [emoji120]Karibu tena mrembo. Tuombeane afya.
Nashkuru kwa baraka zako [emoji120]
[emoji23][emoji23]ilaa Jf uki anzisha story tayari inakua ni ya wana Jf sio yako tena uta pangiwa hadi mda wa kuletaMkuu, ya kuandika ni mengi sana. Vuta picha tokea story ya kwanza kuweka hapa JF, mpaka hii ya sasa. Zote zingekuwa ndani ya Uzi mmoja ingekuwaje? [emoji28][emoji28][emoji28]
Nilichagua kuwa nasimulia kwa vipande, ili nisiwachoshe wasomaji, lakini pia na Mimi niwe napata time ya kufanya mambo mengine kwa Uhuru. Siunajua story ikianza humu JF, msimuliaji hutakiwi kuwa na excuses.
Worry out, next time nitakuja na kipande kingine cha kushare nanyi. [emoji109]
Shukran sana broh Gily . Stay blessed 👊My friend Analyse , this is the best story I have ever read on this forum, especially the last conversation you had with your old man. I am grateful, thankful, amazed, humbled and graced by the events in your life. Well, there is so much to learn on your adventures in life. Behalg, I look forward to the next upcoming tales. Until then stay health and thank you for the tagging. Take care. .
Best, Gily
Daaah...! Hiki kipande kina maneno mazito. Kama naaambiwa ni mimi. Una na mzee mwenye kuijua vema maisha duniani. Una na mzee mwenye busara na hekima sana. Maneno kwenye kipande kipande hiki natamani niyaweke mengi kwenye sehemu fulani,kwenye kipande cha moyo wangu,natamani niyakarili yaishi milele moyoni mwangu. Natamani yawe muongozo pia22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
Nimesoma hii part ya kukimbizana nimecheka kwa nguvu usiku huu hadi nimeamsha kakichanga kangu, apostle tutasaidiana kukesha leo.....niliimiss sana hii story kipindi nipo offline dah finally leo niisome yote15th Portion:
.... Masharti ya zile dawa, ni kwamba, ili mambo yaende kama unavyotaka. Ukikutana na muhusika tu, kabla ya yote, sharti la kwanza lazima umpe mkono wenye ile hirizi. Akiupokea tu, anakuwa chini ya himaya yako.
Na endapo atakuwa katika mazingira ya kushindwa kukupa mkono, mfano amebeba vitu mkononi au hajataka kukupa mkono, basi unachotakiwa kufanya ni kumpiga piga begani mara mbili au tatu na ule mkono wenye hirizi ( in a friendly way, sio kumpiga kwa nguvu).
Ukifanikiwa kufanya kimoja kati ya hivyo (kumpa mkono au kumpiga piga bega), unagain access ya akili yake. Unachomwambia, lazima atekeleze. Kutokana na kutokuwa na uhakika na lile jambo kama ni kweli linawezekana, ndio maana nilichagua kwenda kwa Shani, maana kumshika mkono au kumpiga bega isingekuwa big deal.
Sasa nilivyofika kwa shangazi Shani, alivyoniona, kwanza akashangaa maana sikuwa nimempa taarifa kuwa naenda. Akaniuliza "Mwenzetu vipi, kuja kimya kimya bila taarifa, ndio umekuja kufumania?"
Nikamjibu "Tusalimiane kwanza basi mama". Alaf nikamsogelea na kumshika mabega yote mawili. Kwavile pete ilikuwa kidole cha mkono wa kulia, nikampiga piga kwenye bega lake la kushoto mara mbili, Kisha nikamwambia
Analyse: "Nimekumiss kipenzi"
Shani: "Kwenda huko, hakuna cha kunimiss wala nini, ni lile game ndio linakuzuzua, huishi kuja"
Analyse: "Wala sijaja sababu ya ilo game. Alaf afadhali umeliongelea, naomba basi leo niende nalo, hapa kwako halitumiki, mwishowe lijae kutu"
Shani: "Babu eeh, chukua ilo hapo uende nalo, maana unaweweseka kweli. Kila ukija mawazo yapo kwenye ilo dude tu"
Nikajikuta natabasamu tu.
Tukapiga story za hapa na pale huku tunacheck tamthilia pale. Msosi ulivyokuwa tayari nikala, kisha nikamla na yeye. Mida ya saa tano nikaaga niondoke. Nikapewa PS, nikaamsha nayo.
Wakati nipo njiani naelekea ghetto, uso umechanua kwa tabasam, najiuliza How is this possible?. Sema kuna wazo likaniambia, alishachoka kukaa nayo, ndio maana kakupa, wala sio hayo madawa yako.
Usiku wa siku hiyo hiyo, kabla hata sijafika gheto. Mzee Dingi alinipigia simu na kuniambia kuwa kesho inabidi tukutane wote kwa pamoja, lengo ni kuweka mambo sawa, na kukumbushana majukumu ya kila mmoja. Location ya kukutania, ni pale pale kinondoni. Akili ikaanza kuniambia Ili dili ni must win, jamaa hawataki liende mlama hata kidogo.
. . . ***** ****** ****** ******
Asubuhi na mapema, nikajisogeza eneo la kukutania. Tukakumbushiana umuhimu wa kila mmoja kutekeleza jukumu lake, lakini pia Mzee Dingi akatupa mrejesho wa maongezi yake na yule mstaafu, kwamba kila kitu kipo sawa, na hiyo siku ya kuonana nae ni ile ile.
Timu nzima ikawa inanisisitiza nihakikishe nakuwa mtulivu na mwenye kujiamini, maana nafasi yangu (mwenyekiti), ndio nafasi muhimu ya kumfanya mlengwa asiwe na wasi wasi kabisa.
Kikao kilidumu kama dakika 45 tu. Kisha tukatawanyika.
Binafsi kwa upande wangu sikuwa na amani kabisa. Nilikuwa nikiiangalia timu nzima tunaokutanaga, sikuwa na Imani na mgao utakavyokuwa. Nilikuwa nimeshaanza kutawaliwa na mawazo ya kudhurumiwa tu.
Sasa tulivyotawanyika, wazo likanijia nimfatilie Mzee Dingi hadi anapokaa. Nikishapajua kwake, itakuwa rahisi kudeal nao endapo watataka kunidhurumu, maana familia yake walikuwa hawajui ukweli kuhusu mishe zake kwahiyo ingekuwa rahisi kumtaitisha akiwa kwake. Maana alichowaambia nyumbani, ni tofauti na anachofanya.
Nikadhamiria kumfungia tela. Pale kinondoni Mimi na Mzee Dingi tukapanda wote gari za kwenda kariakoo. Tulivyofika, tukaachana. Nikawa kama naondoka, ila nikajibanza nimuangalie. Akapanda gari ya Mbagala, nikachukua pikipiki na kuanza kumfatilia. Alivyofika mivinjeni, akashuka, akapanda tena gari ya kurudi Kkoo. Nikaanza kujiuliza, huyu Mzee kasahau kununua kitu town au?. Alivyofika kkoo, akapanda gari za gongo la mboto, zikampeleka hadi bungoni, pale pia akashuka, akachukua gari za Tabata. Kumbe jamaa anakaa Matumbi pale. Inaonekana ndio mtindo wake kila akitaka kurudi kwake. Siku zote nilikuwa najua amehamia Mbagala, maana kila tukiachana lazima apande gari za kwenda kule.
Kutokea pale Matumbi aliposhukia, kuna kibao kinaonesha Matumbi Street, kipo upande ule ule alioshukia. Akaingia na kibao kilipokuwa kinaelekeza. nilimfatilia mdogo mdogo, akikata kona nipo, akavuka reli nipo. Baada ya mwendo wa dakika kadhaa, ni kama vile machale yalimcheza. Tulikuwa kwenye kichochoro kirefu, ambacho sikutaka kumpa distance kubwa, maana nilihisi akikimaliza naweza nikampoteza, njia ni vichochoro mno. Alivyokimaliza tu kichochoro, anageuka nyuma anakutana uso kwa uso na Mimi.
Alishtuka kinoma, akabana kibegi chake kwapani, nakuanza kukimbia. Sikulaza damu, nikaanza kumkimbiza, baada ya kile kichochoro, kulikuwa na nyumba mbili zimefatana. Akazipita akiwa speed kali, Mimi nilivyoipita ile nyumba ya pili, nasikia kitoto kinaitwa "Baba, baba". Kile kitoto kikaendelea "Mama, njoo umuone Baba kapapita nyumbani anakimbia". Akili ikaniambia kumbe hapa ndipo anapoishi, basi sina haja ya kuendelea kumkimbiza, atarudi tu.
Nilivyoisogelea ile nyumba kwa ukaribu, kale katoto kakanikimbilia "Anko, anko umekuja kwetu". Mama ake nae akatoka nje, tukasalimiana pale, akanikaribisha ndani, ila sikutaka kuingia, nikaomba kistuli nikae nje. Baada ya kama robo saa hivi, namuona Mzee Dingi anakuja kinyoonge. Alivyofika akanikata jicho tu, kisha akaingia ndani bila hata ya kunisemesha. Nikamsubiria atoke huku nikiwa natafakari na kupangilia maneno yangu kichwani.
Alivyotoka tu, nikasimama na kumpa mkono, akashindwa kuukataa japo alikuwa kafura, akaupokea. Alaf akaniambia tutoke nje ya lile eneo, kama vile hataki mtu mwingine aliyepo ndani au karibu na pale atusikie. Nikampiga piga piga begani na kumwambia kwamba asiwe na wasi wasi. Kiukweli, sikuwa na nia yoyote ovu na Mzee Dingi. Nilikuwa najua Mimi na yeye wote tuko sawa, maana mganga wetu ni mmoja. Hata ile kumpa mkono, na kumpiga bega, ni vitu ambavyo vilitokea naturally tu, siku tegemea chochote, na wala sikuwa na wazo lolote. Ila cha ajabu, baada ya kufanya vile, Mzee Dingi ghafla akawa submissive sana kwangu. Ule ukali aliokuwa nao machoni, na sura aliyokuwa kaikunja, vyote vikapotea. Nikabaki najiuliza, how come? Inamaana dawa zangu Mimi ziko strong kuliko zake au ni vipi?
Nakumbuka tulivyotoka nje ya eneo lake, aliniuliza "Unashida gani Apostle, mbona tunafatana mpaka nyumbani?".
Unajua kama nilivyosema hapo awali katika kile kikundi, hakuna aliyekuwa anajua wengine wanakaa wapi, au hata kuyajua majina yao halisi. Ni Mimi tu ndio nilikuwa namfahamu Mzee Dingi kwa jina la mtoto wake, na hii ni kwasababu tulishawahi kuishi nyumba moja. Yani hata ungetokea msala, atakayeshikwa ni ngumu kuwakamatisha wengine.
Nikajaribu kumwambia Mzee Dingi, "Nina matatizo ya kifamilia, nataka nimrudishe wife kijijini, akajifungulie kule, ila sina hata mia"
Mzee Dingi: "Kwahiyo unatakaje?"
Analyse: "Naomba unikopeshe kama 1.5m, utanikata kwenye dili letu likishakamilika"
Mzee Dingi: "Hayo ungeniambia kule kule, sio kufatana mpaka majumbani. Kwanza umepajuaje huku? Au ulinifatilia tokea mjini?"
Analyse: "Ilo la kupajua hapa halina umuhimu mzee, angalia namna ya kunisaidia"
Mzee Dingi: "Sina hiyo hela hapa home"
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje? "
Mzee Dingi: "Nisubirie hapa nakuja"
Akaingia ndani chapu. Baada ya dakika chache akatoka. Akaita pikipiki, ikatupeleka mpaka maeneo ya Tabata T.I.O.T, kwenye ATM ya NMB, akatoa ile amount alaf akanipa. Kabla hatujaachana, Nikajaribu kumuuliza wahusika wote wa ule mchongo tuko wa ngapi?. Je ni wale wale ninaowaona au kuna wengine?
Hakuwa tayari kunipa details za maana, zaidi ya kusema wapo wengine wawili, ila hakutaka kuniambia uhusika wao kwenye ule mchongo.
Tukaachania pale pale, nikaelekea zangu ghetto.
Nikiwa nimebakiza hatua chache kuifikia nyumba niliyokuwa nakaa, Mzee Dingi akanipigia simu. Nilivyoipokea, hakutaka hata kunipa nafasi ya kuongea, alinitukana sana. Alinipa vitisho vya kila aina..
Namuuliza "Kwani kuna shida gani mzee?"
Mzee Dingi: "Unajifanya una akili nyingi sio? Nimeanza kuliona jua kabla yako, nitakuonesha. Usiponirudishia hiyo hela kama ulivyosema, nakuua"
Analyse: "Kwani si tumekubaliana nitakurudishia baada ya dili la yule mama kutiki?"
Mzee Dingi: "Ms*nge wee, huyo mke uliyemtia mimba umemtoa wapi, unadhani kuwa na mke kazi ndogo? We endelea kucheza na akili yangu, nitakuonesha"
Analyse: "Niwe na mke, nisiwe nae, hela yako utapata mzee, kuwa na amani"
Hakutaka kuendelea kunisikiliza, akakata simu.
Hisia zake zilikuwa sahihi, sikuwa na mpango wa kumrudishia ile hela, hata kama wasingenidhurumu.
Nikaingia zangu gheto.
** ***
Baada kuoga, nikaenda maeneo ya Segerea kula vizuri, kisha nikarudi tena gheto. Wakati natoka, simu niliiacha ndani kwenye chaji. Nilivyorudi, nikakuta missed call moja toka kwa Mshua, wakati naendelea kujiuliza nimpigie au la, simu ikaita tena. Mpigaji akiwa ni yeye tena.
Ile hali ya uoga dhidi yake, iliendelea kuwepo. Bado najiuliza, nitamwambia kitu gani?. Nafsi ilikuwa bado inanisuta, natokea nilivyoongeaga na yule Mzee wa Kongowe, sikuwahi kupokea simu ya Mzee wala kumpigia.
Ile simu iliita mpaka ikakata. Ilivyokata, robo saa baadae mama akawa ananipigia. Nikajiuliza, huyu ni Mama kweli ananipigia, au ni Mzee?. Sikuzote Mama akitaka kuongea na sisi, huwa anatubeep tu, na ikitokea umepokea ukala salio lake, basi hiyo ni kesi. So, akipiga badala ya kupokea, huwa tunakata then tunampigia.
Ila siku hiyo nilishindwa kuikata, maana sikuwa na uhakika na mpigaji. Kuikata, ni confirmation kuwa nipo karibu na simu. Na kama nipo karibu na simu why sijapokea simu ya Mshua?. Ikaita hadi ikakata yenyewe, then mpigaji akapiga tena. Badala ya kuikata, nikaamua kuipokea.
Nikawahi kujitetea "Mama sina salio ndio maana nimepok.....". Kabla hata sijamalizia, nasikia sauti ya Mshua;
Mshua: "Salimia kwanza"
Analyse: "Samahani Mzee, nilijua ni Mama, shikamoo"
Mshua: "Ni mwili mmoja, hakuna shida. Mbona hupokei simu zangu?"
Analyse: "Kila unaponipigia nakuwa mbali na simu, alafu Sina salio"
Mshua: "Kama vocha ya 500 inakushinda, unafanya nini huko mjini?"
Nikabaki kimya tu. Akaniuliza "Unaendeleaje? Kila kitu kipo sawa huko?". Nikamjibu "Ndio". Akawa kimya kwa muda, Kisha akasema "Sawa, kuwa mwangalifu usije kuwa kibaka huko". Akakata simu.
Msongo wa mawazo ukarudi upya. Ila nikaamua kujipa moyo, huku nikiwaza dili tunaloenda kupiga na hela itakayoingia. Nahitaji mtaji wa biashara, siwezi kurudi nyuma now, liwalo na liwe......
[emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751]
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Pole kwa kutoishi nae, but I believe upo blessed in your own way 👊Ila nyie wenye baba mnapata sana faida kuliko sisi ambao hata hatukuwahi kuishi na baba zetu...kuna hayo maneno ya huyo mzee wako kiukwel yana maana kubwa sana
Kwamba ndo imeisha kweli?22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse