Barbiedoll
JF-Expert Member
- Apr 7, 2023
- 772
- 2,150
Nice😍
Big up analyse
Big up analyse
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Santeee
22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
Hii sentensi imenifanya nifikirie kuwa single Kwanza"Mapenzi na utafutaji haviendi pamoja" hii kauli ngumu kumeza ni ya kweli ila kuiishi ndo mziki, kweli ujana una mambo
Amen 🙏🙏I've read stories on this forum and off, I still have reason to say that your story is superb, I have learnt a lot about all aspects of life, spiritual issues, social issues, etc.
I have kept this last part for my future use.
May God bless your struggles.
Kuna kipindi niliwachukia watu na kuwa-block kisa walikuwa wananiletea miyeyusho ya kutoa support kipindi nipo kipindi cha mpito! baada nikajiona mwenye shida ni mimi hivyo sina haja ya kumchukia mtu kwa kushindwa kunitatulia shida zangu hata kama niliwahi kuwa support. Nilivyoona hizi nondo zimekumbusha mbali sanahakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
This is really deep.
Ushaanza kuwa mchawi sasa jamani! Ila pole sana14th Portion
... Nilivyofika kwake, nilipokelewa vizuri kama vile hatukuwa na ugomvi. Nikala, Kisha nikala tena. Zikafatiwa story za hapa na pale. Kutokana na mishe niliyotakiwa kuifanya kesho yake, sikuweza kulala pale. Muda ulivyosogea, nikamwambia inabidi niondoke. Hakunizuia, maana alijua muda wowote anaweza kunipata. Kabla sijaondoka, nikaomba ile PS niondoke nayo.
Hapo ndio kama nilimtibua nyongo, maana sio kwa maneno aliyonitolea. Kana kwamba dakika chache zilizopita, sio sisi tuliokuwa tunafurahi. "Yani wewe unapenda kupokea, kutoa hutaki, haya nenda kaiombe ruhusa familia yako kuwa nataka kukupa zawadi, wakikubali, njoo uchukue, maana maamuzi yako wanafanya wao". Kiufupi alisema kama sipo tayari kukubali takwa lake, basi nisahau kuhusu ile PS. Nikakubaliana na hali. Nikaondoka.
Wakati nipo gheto nawaza dili la kesho tu. Mfano tukipata million 60, pale mgao wangu sio chini ya 10m. Nikaanza kuipangia matumizi kabisa, hapo ndio nikaona Mzee Dingi alikuwa sahihi, dili likifanikiwa naweza survive mwaka mzima bila stress. Baada ya mawazo ya hapa na pale, nikaamua kulala nitulize kichwa.
***** ***** ******* ** **
Niliamka mapema sana, asubuhi ya siku iliyofuata. Ili niwahi pale maeneo ya kisutu, ile njia inapandisha kuelekea mtaa wa Lumumba. Lengo la kwenda pale ilikuwa ni kununua begi lenye muundo wa briefcase. Wakati nipo njiani naelekea pale, Mzee Dingi akanipigia, na kunitaarifu yule mstaafu amepata dharura, hivyo zoezi halitoweza fanyika siku hiyo, tutaenda kesho yake.
Baada ya kuongea nae, niliendelea na safari yangu, maana kivyovyote vile. Lile begi lazima niwe nalo. Baada ya kulininunua, nikaendelea na mishe zangu kama kawaida, kisha nikarudi ghetto. Kesho yake pia dili likabuma. Safari hii likasogezwa mbele wiki nzima.
Ikabidi tukutane wote kujadili nini kifanyike katika iki kipindi tunasubiria yule mstaafu mambo yake yakae sawa. Katika yale maongezi wakawa wanasema kuna kitu hakipo sawa ndio maana dili linakuwa gumu. Mzee Dingi akashauri kama timu, inabidi twende tena kwa mtaalam wao tukaangalie tatizo liko wapi (wao walishaendaga na huwa wanaenda sana). Kwavile Mimi nilikuwa ndio mgeni, wakashauri niwepo siku ya kwenda. Ila Mzee Kesho Yetu akakataa lile swala, akawaambia kwa mganga sio sehemu unayoenda enda tu kila ukitaka. Na kwavile wao walishaenda wiki chache zilizopita, basi ni apostle (Mimi) ndio natakiwa niende.
Mzee KY: "Huyu bwana mdogo ndio inabidi kwenda nae kuangalia shida nini, maana kila kitu kilikuwa sawa kabla hajahusishwa"
Mzee Dingi: "Ni wazo zuri pia, kwahiyo anaendaje?"
Mzee KY: "Nitaenda nae Mimi"
Mzee Dingi: "Ungepumzika tu mkuu, acha niende nae"
Mzee KY: "Hapana hakuna haja, nitaenda nae. Maana nataka nimpeleke sehemu tofauti na ile niliyowapeleka last time"
Mzee Dingi: "Sawa hakuna kama ni hvyo"
Nia yao ilikuwa zoezi la kwenda kwa mtaalam lifanyike wik end, ila nikawaomba wik end hiyo waniache nifanye mambo yangu, alafu jumatatu ndio twende huko kwa mtaalam. Baada ya kuelewana, tukasambalatika, kila mtu na uelekeo wake.
Jumapili asubuhi nikawasiliana na yule Mzee wa Kongowe, akaniambia nimsubirie pale pale aliponichukua mtoto wake mara ya mwisho. Mida ya saa nne, tayari nilikuwa pale, alivyofika tukaondoka wote.
Tulivyofika pale shambani, tulizunguka zunguka kwenye mifugo yake huku tunapiga Story. Dhumuni la kwenda kuonana nae safari hii ilikuwa ni kutaka kumuomba kama anaweza kunisaidia kuniunganisha sehemu yoyote ya ajira, maana maisha ya kuunga unga hayanaga dhamana.
Mzee: "Hicho ndicho najaribu kufanya mwanangu, ila sio rahisi kama unavyodhani"
Analyse: "Ila ulikuwa kwenye mfumo wao Mzee, japo ni ngumu, ila huwezi kosa namna"
Mzee: "Mambo hayapo hivyo kijana. Mimi pia nilifanya kuchomekwa tu, kama unavyojua sitokei kwenye familia zenye mashina na mizizi ya kisiasa. Watu wa kupenyezwa wanapigwa vita sana na inner circle. Na kibaya zaidi utawala ni mpya, kila mtu anajaribu kujitengenezea yeye njia, nani atanikumbuka?
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje kijana wako"
Mzee: "Nitaendelea kuangalia angalia, ukipatikana upenyo, nitakwambia. Ila Sasa hivi wamebana sana mianya yote. Na walengwa tunaobanwa ni sisi, sio wao"
Analyse: "Sawa Mzee"
Mzee: "Mlango mmoja ukifungwa, kuna mwingine mahali fulani utafunguliwa kwa ajili yako, unachotakiwa ni kuwa tayari muda wote maana hujui ni lini, wapi au kutoka Kwa nani mlango wako utafungukia. Kwa umri wako hutakiwi kukata tamaa kabisa, siku zote tumaini ni sauti ya Mungu ndani yetu, bila hiyo huna cha maana utakachofanya".
Analyse: " Nimekuelewa Mzee"
Mzee: "Sawa, nitaendelea kuangalizia upenyo sehemu, ukipatikana nitakwambia, ila am not promising you anything"
Analyse: "Sawa, nashkuru sana"
Tukaendelea na shughuli zingine za hapa na pale, mpaka muda wake wa kuondoka ulivyofika, tukaondoka wote.
Niliendelea kujilaumu mpaka basi, kwa nafasi niliyopoteza. Niliipiga teke njia rahisi, nikachagua kuhangaika kusikokuwa na faida. Kesho jumatatu ilibidi asubuhi ninyonge tai, moka nzuri, unyunyu kisha nielekee ofisini, ila sababu ya uzembe, ntaenda kukutana na wazee wasio na hekima, ili twende kwa mganga. Maisha haya [emoji28][emoji28][emoji28]
Kesho yake mapema nikakutana na Mzee KY maeneo ya mbezi stand ya gari ndogo, safari ya kuelekea Moro ikaanza. Baada ya kufika Moro, tulitembea kwa dakika kama 30 kisha tukaachana na mji, na kuchukua njia kuingia ndani ndani huko. Safari nzima, mawazo yangu yapo kwenye mazungumzo yangu na yule Mzee kule Kongowe.
Mimi na Mzee KY hatukupiga story nyingi njiani, ni Mzee ambae sio muongeaji, muda mwingi anasikiliza tu. Na hizo story chache tulizopiga, ni kwamba alikuwa ananiuliza kitu, then ananiacha nibwabwaje.
Baada ya mwendo wa kama lisaa na nusu au mawili, tukafika mwisho wa safari yetu, then tukaelekea kwa huyo mtaalam wake.
Inaonekana alishawasiliana na yule mtaalam, kumjulisha ujio wetu. Maana tulivyofika, baada ya salamu hapakuwa tena na mazungumzo mengi, nikaambiwa niingie kwenye chumba kilichokuwa vyumba vya nyuma. Mzee KY akamwambia mtaalam bwana mdogo atoke kaiva, mganga akacheka tu. Nikaingia kupikwa kwa mara ya kwanza.
Niliambiwa vitu vinavyotakiwa kununuliwa mfano nazi, karatasi nyeupe, wembe, unga nk. Hela ilitolewa, vikafatwa. Palifanyika mambo mengi sana na mazito, tena kwa muda mrefu. Nilianza kwa kusuguliwa na mchanganyiko wa unga wa sembe na tui la nazi mwili mzima. Vikafatia visomo, chale kuanzia unyayoni mpaka utosini. Kiufupi zoezi lilikuwa zito. Kimoyo moyo najiuliza "Huyu ni Mimi ndio nafanyiwa hivi au?''. Baada ya hapo nikatakiwa kutoka nje vile vile na boksa yangu, mpaka katikati ya kiwanja alafu nirudi ndani. Nikamuuliza yule mganga, "Natoka hivi, na wale watu waliopo nje je?". Mganga akanikata jicho, kiasi kwamba nikajikuta nanyanyuka.
Aisee ukiona mtu anahela, wewe muheshimu tu, haijalishi kazipata vipi. Watu wanasuffer mazee, kila njia ni tough.
Mida ya jioni ndio tulimaliza. Nikapewa dawa ambazo nilitakiwa kujifukiza kwa siku kadhaa, na zingine ambazo nilitakiwa kuoga, lakini hizi za kuoga, sikutakiwa kuziogea bafuni au chooni. Kuna dawa ilikuwa mchanganyiko wa unga mweusi, na mafuta mafuta, hiyo nilitakiwa kuichanganya kwenye mafuta ya nazi, kisha niwe napaka viganjani na usoni kabla ya kutoka nyumbani na kwenda kwenye mishe mishe zangu. Lakini pia nilipewa kitu mfano wa hirizi, ambayo upana wake unakaribia kucha ya kidole cha shahada. Hiyo niliambiwa niwe nayo muda wote. Hizi dawa mbili (ya kupaka na hirizi) zilifanya mpaka kesho nina bifu na Mzee Dingi.
Kila kitu kilivyokuwa kimekamilika, tukaaga na kuondoka. Njiani Mzee KY ananiambia, "Bwana mdogo ukiwa serious kwenye maisha utafika mbali sana, ila kwa muda mchache ambao nimespend na wewe, tatizo lako kubwa ni moja tu"
Nikamuuliza tatizo gani??. Akanijibu, "You don't smile easily". Nikatatizika kidogo, "Kuto tabasamu nalo ni tatizo?". Akanijibu "Bado una mengi ya kujifunza". Nikabaki namwangalia tu. Katikati ya story zilizoendelea, nikajikuta namwambia "Sikuwahi fikiria kama siku moja ningeangukia huku". Akacheka.
Mzee KY: "Tukiwa wadogo, ni ndoto ya kila mtoto kuwa rubani. Hii Dunia jinsi ilivyo, ukiteleza kidogo tu inakuchagulia njia"
Hapo ndio akaniambia machache kuhusu yeye. Katika hayo maongezi yetu ndio niligundua kuwa ana masters ya uhandisi wa umeme, lakini pia ana CPA, ana uwezo wa kuzungumza lugha 3 za kimataifa kwa ufasaha kabisa. Chuo alisomeaga Uganda. Na ana ofisi mbili town, lakini just for backup, japo zinafanya vizuri.
Nilimshangaa sana kwanini ameamua kuendelea na njia ile wakati ana uwezo wa kutengeneza decent money?
Mzee KY: "Sikia bwana mdogo, hii Dunia inaweza kukuchapa alafu haikupi kabisa muda wa kujutia. Na hata ukiwa kwenye kujutia, inaweza ikakuchapa tena, kiasi kwamba ukiwa kwenye kujutia kwako, ndani yake ukapata majuto mengine".
Wakati najaribu kujiuliza amemaanisha Nini, akaendelea, "Unatakiwa kujutia huku unaenda nayo, maana muda haukusubiri".
"Sema sijui kwanini wewe umeingia huku, ila binafsi kisasi na kinyongo nilichokuwa nacho juu ya mtu fulani ndio kimeniingiza huku. Nilipima kina Cha maji kwa mguu, sasa nimeshazama tayari".
Hakuongea tena mpaka alivyonishusha mbezi mwisho.
. ****** ******** ********** ** ***
Baada ya pale, nikanyoosha mpaka gheto kwangu. Kwavile sikuwa nimejiandaa sehemu ya kuogea, ikabidi nibebe ndoo yangu hadi kwenye kiwanja cha shule ya msingi (nilikuwa jirani na shule), nikaenda kuogea pale chap, then nikarudi ghetto kujifukiza ile dawa nyingine. Baada ya hapo nikalala.
Kabla ya kwenda kwa mganga, kuna vitu vingi sana nilikuwa sivielewagi, na sivipatii majibu. Nilikuwa nikipishana na vijana (wakike kwa wakiume), unakuta mtu smart, lakini macho mekunduu kuliko kawaida, japo sio mlevi wala mvutaji sigara. Au mkipishana unahisi harufu ya moshi tu. Nilikuwa najiuliza, hivi hapa mjini kuna watu wanapikia majiko ya kuni au?. Kumbe hakuna bhana, vijana wanajifukiza sana. Tena wameanza kuoga moshi kabla hata ya Corona.
Hizo siku tatu za kujifukiza, nilikuwa nanuka moshi muda wote. Kibaya zaidi, zile dawa za kuoga hutakiwi kutumia sabuni.
Kipindi naendelea na ile dozi. Mzee Dingi akawa ametupa taarifa kuwa alipigiwa simu na yule mlengwa wetu, wamekubaliana zoezi litafanyika siku 6 tokea hiyo siku. Maana alikuwa anajipanga, akishanunua lile eneo basi mipango yake mingine iende haraka pia.
Nikamaliza masharti, tukabaki tunamsikilizia yule mstaafu, japo tulipiga dili kama mbili, na zote zilitiki vizuri tu.
Kile kihirizi alichonipaga yule mtaalam, aliniambia kwavile natakiwa niwe nacho muda wote mwilini, basi naweza kukihifadhi kwa namna tatu. Mosi, nikifunge kwenye kamba, alaf nikibane mkononi kama wanavyofanya makepteni wa mpira, Pili, nikizungushie big g, alaf nikienda eneo la tukio, nikibane mdomoni, tatu, nikitengenezee bangili, au pete ya kukibana then niivae.
Mimi nilitengeneza pete za kacha zile, alafu nikakishonea pale. Nikaivaa kwenye kidole cha pete, mkono wa kulia.
Zikiwa zimebaki siku tatu twende kwenye lile dili kubwa. Nilikuwa zangu gheto tu nimekaa, wazo likanijia nikajaribishe zile dawa sehemu. Akili ikanituma niende kwa Shani.
Mida ya jioni, nikaoga, nikapaka mafuta yangu ya nazi yenye dawa, mikononi na usoni. Kisha nikatoka.
Aisee Hii Dunia ni zaidi ya tuijuavyo. Kuna vitu vingi sana vipo beyond our explanations.......
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
🤣🤣🤣🤣🤣Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Hii Mzee umepiga mistari mizito Sana humu ndani bigup22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
Nimecheka pale unamfutilia mzee Dingi zile kona kama zakitonga, halafu umeambiwa angalia usiwe kibaka mshua wako lakini umekaza shingo [emoji25][emoji25][emoji25]15th Portion:
.... Masharti ya zile dawa, ni kwamba, ili mambo yaende kama unavyotaka. Ukikutana na muhusika tu, kabla ya yote, sharti la kwanza lazima umpe mkono wenye ile hirizi. Akiupokea tu, anakuwa chini ya himaya yako.
Na endapo atakuwa katika mazingira ya kushindwa kukupa mkono, mfano amebeba vitu mkononi au hajataka kukupa mkono, basi unachotakiwa kufanya ni kumpiga piga begani mara mbili au tatu na ule mkono wenye hirizi ( in a friendly way, sio kumpiga kwa nguvu).
Ukifanikiwa kufanya kimoja kati ya hivyo (kumpa mkono au kumpiga piga bega), unagain access ya akili yake. Unachomwambia, lazima atekeleze. Kutokana na kutokuwa na uhakika na lile jambo kama ni kweli linawezekana, ndio maana nilichagua kwenda kwa Shani, maana kumshika mkono au kumpiga bega isingekuwa big deal.
Sasa nilivyofika kwa shangazi Shani, alivyoniona, kwanza akashangaa maana sikuwa nimempa taarifa kuwa naenda. Akaniuliza "Mwenzetu vipi, kuja kimya kimya bila taarifa, ndio umekuja kufumania?"
Nikamjibu "Tusalimiane kwanza basi mama". Alaf nikamsogelea na kumshika mabega yote mawili. Kwavile pete ilikuwa kidole cha mkono wa kulia, nikampiga piga kwenye bega lake la kushoto mara mbili, Kisha nikamwambia
Analyse: "Nimekumiss kipenzi"
Shani: "Kwenda huko, hakuna cha kunimiss wala nini, ni lile game ndio linakuzuzua, huishi kuja"
Analyse: "Wala sijaja sababu ya ilo game. Alaf afadhali umeliongelea, naomba basi leo niende nalo, hapa kwako halitumiki, mwishowe lijae kutu"
Shani: "Babu eeh, chukua ilo hapo uende nalo, maana unaweweseka kweli. Kila ukija mawazo yapo kwenye ilo dude tu"
Nikajikuta natabasamu tu.
Tukapiga story za hapa na pale huku tunacheck tamthilia pale. Msosi ulivyokuwa tayari nikala, kisha nikamla na yeye. Mida ya saa tano nikaaga niondoke. Nikapewa PS, nikaamsha nayo.
Wakati nipo njiani naelekea ghetto, uso umechanua kwa tabasam, najiuliza How is this possible?. Sema kuna wazo likaniambia, alishachoka kukaa nayo, ndio maana kakupa, wala sio hayo madawa yako.
Usiku wa siku hiyo hiyo, kabla hata sijafika gheto. Mzee Dingi alinipigia simu na kuniambia kuwa kesho inabidi tukutane wote kwa pamoja, lengo ni kuweka mambo sawa, na kukumbushana majukumu ya kila mmoja. Location ya kukutania, ni pale pale kinondoni. Akili ikaanza kuniambia Ili dili ni must win, jamaa hawataki liende mlama hata kidogo.
. . . ***** ****** ****** ******
Asubuhi na mapema, nikajisogeza eneo la kukutania. Tukakumbushiana umuhimu wa kila mmoja kutekeleza jukumu lake, lakini pia Mzee Dingi akatupa mrejesho wa maongezi yake na yule mstaafu, kwamba kila kitu kipo sawa, na hiyo siku ya kuonana nae ni ile ile.
Timu nzima ikawa inanisisitiza nihakikishe nakuwa mtulivu na mwenye kujiamini, maana nafasi yangu (mwenyekiti), ndio nafasi muhimu ya kumfanya mlengwa asiwe na wasi wasi kabisa.
Kikao kilidumu kama dakika 45 tu. Kisha tukatawanyika.
Binafsi kwa upande wangu sikuwa na amani kabisa. Nilikuwa nikiiangalia timu nzima tunaokutanaga, sikuwa na Imani na mgao utakavyokuwa. Nilikuwa nimeshaanza kutawaliwa na mawazo ya kudhurumiwa tu.
Sasa tulivyotawanyika, wazo likanijia nimfatilie Mzee Dingi hadi anapokaa. Nikishapajua kwake, itakuwa rahisi kudeal nao endapo watataka kunidhurumu, maana familia yake walikuwa hawajui ukweli kuhusu mishe zake kwahiyo ingekuwa rahisi kumtaitisha akiwa kwake. Maana alichowaambia nyumbani, ni tofauti na anachofanya.
Nikadhamiria kumfungia tela. Pale kinondoni Mimi na Mzee Dingi tukapanda wote gari za kwenda kariakoo. Tulivyofika, tukaachana. Nikawa kama naondoka, ila nikajibanza nimuangalie. Akapanda gari ya Mbagala, nikachukua pikipiki na kuanza kumfatilia. Alivyofika mivinjeni, akashuka, akapanda tena gari ya kurudi Kkoo. Nikaanza kujiuliza, huyu Mzee kasahau kununua kitu town au?. Alivyofika kkoo, akapanda gari za gongo la mboto, zikampeleka hadi bungoni, pale pia akashuka, akachukua gari za Tabata. Kumbe jamaa anakaa Matumbi pale. Inaonekana ndio mtindo wake kila akitaka kurudi kwake. Siku zote nilikuwa najua amehamia Mbagala, maana kila tukiachana lazima apande gari za kwenda kule.
Kutokea pale Matumbi aliposhukia, kuna kibao kinaonesha Matumbi Street, kipo upande ule ule alioshukia. Akaingia na kibao kilipokuwa kinaelekeza. nilimfatilia mdogo mdogo, akikata kona nipo, akavuka reli nipo. Baada ya mwendo wa dakika kadhaa, ni kama vile machale yalimcheza. Tulikuwa kwenye kichochoro kirefu, ambacho sikutaka kumpa distance kubwa, maana nilihisi akikimaliza naweza nikampoteza, njia ni vichochoro mno. Alivyokimaliza tu kichochoro, anageuka nyuma anakutana uso kwa uso na Mimi.
Alishtuka kinoma, akabana kibegi chake kwapani, nakuanza kukimbia. Sikulaza damu, nikaanza kumkimbiza, baada ya kile kichochoro, kulikuwa na nyumba mbili zimefatana. Akazipita akiwa speed kali, Mimi nilivyoipita ile nyumba ya pili, nasikia kitoto kinaitwa "Baba, baba". Kile kitoto kikaendelea "Mama, njoo umuone Baba kapapita nyumbani anakimbia". Akili ikaniambia kumbe hapa ndipo anapoishi, basi sina haja ya kuendelea kumkimbiza, atarudi tu.
Nilivyoisogelea ile nyumba kwa ukaribu, kale katoto kakanikimbilia "Anko, anko umekuja kwetu". Mama ake nae akatoka nje, tukasalimiana pale, akanikaribisha ndani, ila sikutaka kuingia, nikaomba kistuli nikae nje. Baada ya kama robo saa hivi, namuona Mzee Dingi anakuja kinyoonge. Alivyofika akanikata jicho tu, kisha akaingia ndani bila hata ya kunisemesha. Nikamsubiria atoke huku nikiwa natafakari na kupangilia maneno yangu kichwani.
Alivyotoka tu, nikasimama na kumpa mkono, akashindwa kuukataa japo alikuwa kafura, akaupokea. Alaf akaniambia tutoke nje ya lile eneo, kama vile hataki mtu mwingine aliyepo ndani au karibu na pale atusikie. Nikampiga piga piga begani na kumwambia kwamba asiwe na wasi wasi. Kiukweli, sikuwa na nia yoyote ovu na Mzee Dingi. Nilikuwa najua Mimi na yeye wote tuko sawa, maana mganga wetu ni mmoja. Hata ile kumpa mkono, na kumpiga bega, ni vitu ambavyo vilitokea naturally tu, siku tegemea chochote, na wala sikuwa na wazo lolote. Ila cha ajabu, baada ya kufanya vile, Mzee Dingi ghafla akawa submissive sana kwangu. Ule ukali aliokuwa nao machoni, na sura aliyokuwa kaikunja, vyote vikapotea. Nikabaki najiuliza, how come? Inamaana dawa zangu Mimi ziko strong kuliko zake au ni vipi?
Nakumbuka tulivyotoka nje ya eneo lake, aliniuliza "Unashida gani Apostle, mbona tunafatana mpaka nyumbani?".
Unajua kama nilivyosema hapo awali katika kile kikundi, hakuna aliyekuwa anajua wengine wanakaa wapi, au hata kuyajua majina yao halisi. Ni Mimi tu ndio nilikuwa namfahamu Mzee Dingi kwa jina la mtoto wake, na hii ni kwasababu tulishawahi kuishi nyumba moja. Yani hata ungetokea msala, atakayeshikwa ni ngumu kuwakamatisha wengine.
Nikajaribu kumwambia Mzee Dingi, "Nina matatizo ya kifamilia, nataka nimrudishe wife kijijini, akajifungulie kule, ila sina hata mia"
Mzee Dingi: "Kwahiyo unatakaje?"
Analyse: "Naomba unikopeshe kama 1.5m, utanikata kwenye dili letu likishakamilika"
Mzee Dingi: "Hayo ungeniambia kule kule, sio kufatana mpaka majumbani. Kwanza umepajuaje huku? Au ulinifatilia tokea mjini?"
Analyse: "Ilo la kupajua hapa halina umuhimu mzee, angalia namna ya kunisaidia"
Mzee Dingi: "Sina hiyo hela hapa home"
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje? "
Mzee Dingi: "Nisubirie hapa nakuja"
Akaingia ndani chapu. Baada ya dakika chache akatoka. Akaita pikipiki, ikatupeleka mpaka maeneo ya Tabata T.I.O.T, kwenye ATM ya NMB, akatoa ile amount alaf akanipa. Kabla hatujaachana, Nikajaribu kumuuliza wahusika wote wa ule mchongo tuko wa ngapi?. Je ni wale wale ninaowaona au kuna wengine?
Hakuwa tayari kunipa details za maana, zaidi ya kusema wapo wengine wawili, ila hakutaka kuniambia uhusika wao kwenye ule mchongo.
Tukaachania pale pale, nikaelekea zangu ghetto.
Nikiwa nimebakiza hatua chache kuifikia nyumba niliyokuwa nakaa, Mzee Dingi akanipigia simu. Nilivyoipokea, hakutaka hata kunipa nafasi ya kuongea, alinitukana sana. Alinipa vitisho vya kila aina..
Namuuliza "Kwani kuna shida gani mzee?"
Mzee Dingi: "Unajifanya una akili nyingi sio? Nimeanza kuliona jua kabla yako, nitakuonesha. Usiponirudishia hiyo hela kama ulivyosema, nakuua"
Analyse: "Kwani si tumekubaliana nitakurudishia baada ya dili la yule mama kutiki?"
Mzee Dingi: "Ms*nge wee, huyo mke uliyemtia mimba umemtoa wapi, unadhani kuwa na mke kazi ndogo? We endelea kucheza na akili yangu, nitakuonesha"
Analyse: "Niwe na mke, nisiwe nae, hela yako utapata mzee, kuwa na amani"
Hakutaka kuendelea kunisikiliza, akakata simu.
Hisia zake zilikuwa sahihi, sikuwa na mpango wa kumrudishia ile hela, hata kama wasingenidhurumu.
Nikaingia zangu gheto.
** ***
Baada kuoga, nikaenda maeneo ya Segerea kula vizuri, kisha nikarudi tena gheto. Wakati natoka, simu niliiacha ndani kwenye chaji. Nilivyorudi, nikakuta missed call moja toka kwa Mshua, wakati naendelea kujiuliza nimpigie au la, simu ikaita tena. Mpigaji akiwa ni yeye tena.
Ile hali ya uoga dhidi yake, iliendelea kuwepo. Bado najiuliza, nitamwambia kitu gani?. Nafsi ilikuwa bado inanisuta, natokea nilivyoongeaga na yule Mzee wa Kongowe, sikuwahi kupokea simu ya Mzee wala kumpigia.
Ile simu iliita mpaka ikakata. Ilivyokata, robo saa baadae mama akawa ananipigia. Nikajiuliza, huyu ni Mama kweli ananipigia, au ni Mzee?. Sikuzote Mama akitaka kuongea na sisi, huwa anatubeep tu, na ikitokea umepokea ukala salio lake, basi hiyo ni kesi. So, akipiga badala ya kupokea, huwa tunakata then tunampigia.
Ila siku hiyo nilishindwa kuikata, maana sikuwa na uhakika na mpigaji. Kuikata, ni confirmation kuwa nipo karibu na simu. Na kama nipo karibu na simu why sijapokea simu ya Mshua?. Ikaita hadi ikakata yenyewe, then mpigaji akapiga tena. Badala ya kuikata, nikaamua kuipokea.
Nikawahi kujitetea "Mama sina salio ndio maana nimepok.....". Kabla hata sijamalizia, nasikia sauti ya Mshua;
Mshua: "Salimia kwanza"
Analyse: "Samahani Mzee, nilijua ni Mama, shikamoo"
Mshua: "Ni mwili mmoja, hakuna shida. Mbona hupokei simu zangu?"
Analyse: "Kila unaponipigia nakuwa mbali na simu, alafu Sina salio"
Mshua: "Kama vocha ya 500 inakushinda, unafanya nini huko mjini?"
Nikabaki kimya tu. Akaniuliza "Unaendeleaje? Kila kitu kipo sawa huko?". Nikamjibu "Ndio". Akawa kimya kwa muda, Kisha akasema "Sawa, kuwa mwangalifu usije kuwa kibaka huko". Akakata simu.
Msongo wa mawazo ukarudi upya. Ila nikaamua kujipa moyo, huku nikiwaza dili tunaloenda kupiga na hela itakayoingia. Nahitaji mtaji wa biashara, siwezi kurudi nyuma now, liwalo na liwe......
[emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751][emoji1751]
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Simulizi nzuri sana. Asante22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse
Yaani kuna siku kidogo wanitapeli tu dola twangu, wale watu sio kumbe walikoanzia kazi mie ndiyo nimeamkia huko niliwaacha mdomo wazi nikaondoka zangu [emoji3][emoji3][emoji3]16th Portion:
... Usiku huo nilitafakari mambo mengi sana. Ila jambo kubwa ni kitendo cha wale washirika wangu wote kunipa false direction ya sehemu wanazo ishi. Tokea nilivyoamua kujiunga nao rasmi, Mzee Dingi nilidhani amehamia Mbagala au maeneo ya huko, ila kumbe sivyo. Tafsiri iliyonijia, hata wale wengine nao nikaanza kuwa na mashaka na makazi yao. Kwa ufupi, wote walijua Mimi napatikana Tabata, ila wao sijui wanapokaa. Na kibaya zaidi, Mzee Dingi anapajua ninapokaa. Ule mshtuko alioupata baada ya kuniona mitaa ya kwake, ulinipa tafsiri ya hatari. Hii kwangu haikuwa nzuri, nikaadhimia kuhama. Nikampigia dalali anifanyie mpango kesho nipate chumba.
******* ****** ****** *****
Palivyokucha, nikaanza pilika pilika na dalali wangu. Baada ya kuzunguka nyumba kadhaa, hatimae nikapata chumba maeneo ya Tabata Segerea, kwa Bibi pale (kwa wale waliosoma story ya fumanizi la mama mwenye nyumba, nyumba yenyewe ni hii). Nilidhamiria kukaa pale kwa miezi michache, alaf ndio niende eneo jingine nje ya Tabata nitakalokaa kwa kutulia.
Nilitafuta usafiri wa kunihamisha siku hiyo hiyo. Mama mwenye nyumba hakuwepo, nilifanya kumpigia na kumtaarifu kwa njia ya simu. Alisikitika kuhama ghafla, akataka kujua kama kuna tatizo, ila nikamtoa wasi wasi nimepata kazi sehemu, hivyo nataka nihamie karibu na nitakapofanya kazi, ili kupunguza gharama za usafiri. Huyu mama nilishakaa kwenye nyumba zake mbili. Ile ya kwanza tulikuwa wapangaji tupu, hii ya pili ambayo nahama, yeye ndio alikuwa anaishi hapo.
Akaniuliza vipi kuhusu kodi yangu iliyobaki, maana ilikuwa imebaki miezi mingi. Nikamwambia asiwe na wasi, maana nimehama kwa hiari yangu, basi kodi nasamehe.Tukamalizana hivyo. Nikahamisha vitu vyangu.
Nilivyoingiza vitu vyote ndani ya makazi yangu mapya, sikutaka hata kuvipanga vizuri. Nilifunga Kitanda tu.
Baada ya hapo, nikaona niende bank kuweka ile hela iliyobaki, toka kwenye hela niliyochukua kwa Mzee Dingi, sikutaka kuendelea kukaa nayo ndani.
Nikajiandaa kama kawaida ili nitoke. Unajua ngozi ya uso wangu ni ya mafuta, nikipaka lotion, walau kuna unafuu. Ila Sasa kile kitendo cha kuwa naongezea na mafuta ya nazi juu yake, kikawa kinaleta changamoto, nikipigwa na jua kidogo, uso unang'aa kama kitumbua, Yani nikiwa kwambali unajua kabisa Analyse yule anakuja. Hiyo hali ikawa inaniboa, ikabidi nibadili namna ya kupaka yale mafuta ya nazi. Nakumbuka mtaalam aliniambia natakiwa kuyapaka kidogo tu maeneo ya usoni na viganjani. Nikaanza kuwa nayapaka kidogo chini ya mdomo wa chini, alaf na sehemu ya ndani ya masikio. Yani mtu ningekutana nae, kwa haraka haraka angeweza kuhisi nimekosea tu kwenye kujipaka, au pengine hata asing'amue, maana nilikuwa nayapaka kidogo sana.
Tokea niwe na yale mafuta na kile kihirizi, route za mjini hakuna siku niliyowahi toa hela yangu kumpa konda. Tena wale ndio wepesi kinoma, ukimgusa bega kidogo, mtapiga story hadi mwisho wa safari. Alaf nikishuka wananiaga kama vile tunajuana miaka mingi sana.
Leo hii nikisikia mtu katapeliwa kimazingara, siwezi mlaumu kabisa. Akili inakuwa sio yake muda ule. Baadae sana ndio ufahamu unamrudia.
***** ****** ***** ** **
Nilitoka mpaka bank, NMB tawi la Mandela. Pale pale alipowithdraw hela Mzee Dingi. Nilichagua tawi lile, maana ndio lilikuwa karibu na Mimi.
Baada ya pale, sikutaka kulala kule kwangu siku ile. Niliadhimia kwenda kulala kwa Shani. Hivyo nilirudi gheto kwangu na kuchukua kibegi changu cha kazi, na nguo nitakazo vaa hiyo kesho siku ya dili, pia nikapitia sehemu na kumnunulia vitu kadhaa vya kupika ambavyo najua angehitaji. Kisha nikaelekea kwake.
Nilivyokuwa mazingira ya pale kwake, walau mawazo ya kazi ya kesho yalipungua. Naweza sema, niliyasahau kwa muda, au tuseme alinisaahulisha kila kitu.
** *** *****
Asubuhi niliamshwa na simu toka kwa Mzee Dingi, akaniambia niwahi kusogea meeting point, ili niweze kuondoka na wale wazee wengine.
Nikajiandaa kama kawaida, Kisha nikapaka yale mafuta. Sikutaka hata kusubiria chai, japo Shani alisisitiza sana.
Ilitakiwa nikutane nao pale mataa ya ubungo. Nilichelewa kidogo, nikawakuta tayari wamefika, wananisubiria Mimi tu. Nikajitosa kwenye gari ya yule Mzee KY, safari ikaanza.
Kila nikiwa na wale wazee, nilikuwa napatwa na mawazo ya kujilaumu sana. Nilimpotezea Mzee wa maana ambae angeweza kubadili maisha yangu, ila nimejikuta naangukia kwenye himaya ya wazee wa ajabu. Nilipata funzo kwa njia ngumu sana, kwamba usiharibu maisha yako kwasababu ya watu wengine. Maana utaacha mambo yako, kwa ajili yao, ila ikifika wakati wa wao kufanya yao, hawatojiuliza hata mara mbili, watakupotezea bila kujali ulijitoa vipi kwao au ulikuwa na mchango gani.
Safari nzima ilitawaliwa na ukimya. Na ungetuona tulivyokuwa serious na tumependeza, ungeweza hisi ni wana familia tunaenda ukweni kutoa mahari. Maana kijana nilikuwa peke yangu, nimezungukwa na wazee tu.
Ndani ya ile gari tulikuwa watu wanne. Mimi, Mzee KY, mwanasheria feki na Mzee Kidevu. Mzee Dingi yeye alitakiwa kuja na yule mlengwa wetu.
Tulisogea hadi eneo la tukio. Gari ikaenda kupack mbele zaidi, kwenye nyumba fulani kuu kuu isiyokuwa na uzio. Mzee KY akasalimiana na majirani pale, kisha akatukaribisha ndani, na kutwambia kuwa pale ni kwake.
Yani jamaa alitafuta na nyumba kabisa, na hata majirani wanamjua na wamemzoea. Kiufupi alikuwa kajipanga. Nilistaajabu sana, huyu Mzee ni mtu wa aina gani?
Wote kwa pamoja tukatulia, huku tukisubiria signal ya Mzee Dingi.
Mzee KY akatukumbushia tena umuhimu wa kila mmoja kuplay part yake bila kutetereka.
Katika zile siku kadhaa nilizokuwa nakutana nao kupanga hii plan, niligundua kuwa Mzee wa KY ndiye aliyekuwa kiongozi wa kile kikosi. Na hata dili nyingi kubwa, yeye ndio alikuwa anatengeneza plan nzima, namna gani iwe, na yupi achukue nafasi ipi.
Tukiwa pale kwenye makazi feki ya Mzee KY, Mzee Dingi akatuma msg ; "Get Ready"
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Shani si ndio aliyekupa plat station 😀😅😅😅 Shani au Mwahija?
Huyo huyo Shani. Tupe mrejesho wake😀 I can see the next storyYeah ,alinibless ile mashine 😅😅