Gily Gru
JF-Expert Member
- Jul 4, 2016
- 8,632
- 23,673
Hupashagi viporo safi sana😀Sina ambae nakutana nae. Nikileta story za love life, naweza ongelea mmoja wao au wote 😅😅
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hupashagi viporo safi sana😀Sina ambae nakutana nae. Nikileta story za love life, naweza ongelea mmoja wao au wote 😅😅
Hutaki Playstation mpya😀Pasha uumwe tumbo 😅😅
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] yaani nimecheka ulipokutana na Mama mwenye nyumba wako licha yakuwa umehama.17th Portion:
.... Mzee Dingi alimtumia msg Mzee KY kumtaarifu kuwa ndio wanakaribia, so tujiandae.
Plan ilivyokuwa ni kwamba, wakishafika pale center, Mzee Dingi alitakiwa kumpigia simu Mzee KY ili aje awapeleke kwenye eneo lake analouza. Wakishafika kwenye hiyo eneo, Mzee KY anatakiwa kuwaita majirani zake aliopakana nao kwenye ilo eneo analouza, ili waje kutambua na kuthibitisha mipaka.
Wakishaoneshana mipaka, na kuelewana katika kila kitu, hapo ndio wanatakiwa kuniita mwenyekiti, niende mpaka pale site, ili kuona eneo linalouzwa na mipaka yake. Nikishajiridhisha kuwa kila kitu kipo sawa, hapo wote kwa pamoja tunatakiwa kwenda ofisini ili kuandikishiana na kukabidhiana hela.
Kuhusu ofisi, Mzee KY angeshauri twende tukaandikishiane nyumbani kwake. Nyumba hii ambayo tulikuwa tumefikia, na ilikuwa na muonekano kuwa inakaliwa na familia so ni rahisi kuaminika. Pia mihuri yote muhimu nilikuwa nimeshapewa, hadi nyalaka za mauziano zilizoandaliwa na Mzee KY nilikuwa nimekabidhiwa. Kiufupi, nyalaka zote sahihi zilikuwepo na baada ya mauziano, yule mstaafu angepewa. Kasoro pekee iliyokuwepo, ni kwamba eneo linalouzwa sio letu.
Takribani nusu saa tokea atume ile msg, Mzee Dingi akapiga simu. Baada ya salamu na maongezi kidogo, Mzee KY akaenda kuwapokea. Kisha akaenda nao hadi eneo linalotakiwa kuuzwa.
Wakiwa pale, majirani wakapigiwa simu. Akaanza kwenda yule mwanasheria feki, robo saa mbele, huyu Mzee Kidevu nae akaenda. Nikabaki mwenyewe, mwenyekiti ndani ya ile nyumba.
Baada ya kama dakika 45 tokea yule Mzee Kidevu aniache kwenye ile nyumba, Mzee KY akanipigia simu niende. Moyo ulikuwa unadunda kuliko kawaida, ila kila nikifikiria mgao wangu nitakaopata, nikajipa moyo. Nikawafata walipo.
Wale wengine wote, hakuna aliyekuwa kabeba begi lake pale site, ni Mimi peke yangu ndio nilienda na kibriefcase changu pale site. Nilivyofika tu site, nikapatwa na mshangao baada ya kumuona mtu tunayetakiwa kumliza.
Unajua katika maisha, coincidences zipo, lakini kuna baadhi ya coincidences hata ujielezee vipi, ni ngumu watu wengine kukuamini.
Alivyogeuka yule mama tunayetaka kumuuzia eneo, nikajikuta nipo uso kwa uso na Mama mwenye nyumba niliyohama siku iliyopita. Binafsi kutokea moyoni, sikuwa nafahamu kama mlengwa ni yeye. Na hata sababu iliyonifanya nihame pale kwake, wala haikuhusiana na yeye kuwa target yetu.
Ila unadhani ni nani angeweza kuamini maelezo yangu?. Yani leo nimehama, then kesho tunaenda kumpiga tukio, alaf niseme nilikuwa sijui kitu? Mtu yeyote mwenye akili timamu na reasoning capacity ya kawaida tu, asingekubali.
Yule mama alivyoniona kwa mbali, akanitambua. Nikawasogelea mpaka pale. Akanipokea kwa bashasha sana.
"Mwanangu ni wewe? Siamini macho yangu, kumbe ndio umepata kazi huku?". Nikamjibu ndio. Akanichangamkia sana, "Mungu mkubwa, na wakati wa Mungu ndio wakati sahihi, angalia ulivyoinuliwa mwanangu". Muda huo anaongea yote, wale washirika wangu wote wapo kimya, kila mmoja kapigwa butwaa kivyake, kasoro Mzee KY, yeye alikuwa neutral.
Yule mama akaendelea, "Unaona mwanangu kuishi na watu vizuri ilivyo ni jambo jema? Mfano ungeondoka kwa ugomvi, leo hii tungetizamana usoni? Nadhan hata jambo langu leo lingekuwa gumu". Mzee Dingi ikabidi aingilie yale maongezi yetu, "Kwani nyie mnafahamiana?". Mstaafu akamjibu, "Ndio, huyu ni kijana wangu kabisa, nimefahamiana nae miaka mingi, na leo ona Mungu amenikutanisha nae tena, ili aweze kuwa msaada wangu kwenye huu ununuzi"
Mzee Dingi: "Ni jambo jema, basi hapa shughuli yetu itaenda kwa urahisi sana"
Mstaafu: "Yani hapa Sina mashaka kabisa, nipo kwenye mikono salama ya kijana wangu"
Yule mstaafu akanigeukia Mimi na kuniambia "Tena tukitoka hapa unikumbushe nikurudishie Kodi yako iliyokuwa imebaki, maana ulivyotoka tu, dalali akaleta mtu mwingine atakayeingia leo. Ilikuwa halali yako kuhama pale. Huku ni mbali mwanangu."
Akili ikaanza kunizunguka kuliko kawaida, hapa nisimame upande wa nani?, wa huyu mama, au wa ile timu?. Upande wowote ambao ningechagua lazima kuna consequences ningekutana nazo. Nikisema nisimame na kina Mzee Dingi, basi uhaminifu kwa huyu mama ningekuwa nimeuvunja. Nikisema nisimame na huyu mama, basi nijiandae kuingia kwenye vita na kina Mzee Dingi, maana nitakuwa nimewaingiza kwenye hasara kubwa sana. Dili za hela ndefu kama hizi, huwa zinamaandalizi mengi, na gharama kubwa inatumika, mfano ile nyumba ambayo tungeenda kuandikishiana, ilikuwa imekodiwa, na iliwekwa vitu vyote vya ndani ili ionekane kama ni makazi halisi.
Kufanikiwa Kwa Ili dili, ndio hela ya kucover hizi gharama zote ingepatikana. Kufeli Kwa Ili dili ni hasara, hasara ambayo hakuna aliyekuwa anataka itokee, na ndio maana maandalizi yake yalikuwa deep. Mpaka kufikia muda ule, hatma ya kufanikiwa au kufeli Kwa lile dili zilikuwa mikononi mwangu. Nikawa najiuliza, hawa watu watanielewa kweli??. Wote nikiwaangalia, they mean business, hakuna aliyekuwa na mzaha. Katika ile timu yote, nilikuwa namuhofia sana yule Mzee KY, ukiachana na yeye kuwa kiongozi, ila pia ni mtu fulani aliye serious sana muda wote. Macho yake yameingia kwa ndani, alafu makali sana. Akikuangalia sana unaweza hisi anachuki na wewe.
Wakati naendelea kuwaza hayo. Mzee KY akaamua kuchukua nafasi yake kama muuzaji wa ile ardhi, akamgeukia Mzee Dingi na kumwambia:
"Hebu tumalize ili swala, kuna sehemu natakiwa kuwahi"
Mzee Dingi: "Haya mama, twende mkaandikishiane, ila tufunge ili swala"
Mstaafu: "Sawa hakuna shida"
Mwanasheria feki na yule Mzee Kidevu kama wanaweza kuondoka, maana kazi yao ya kutambua mipaka wameshaifanya. Mzee KY akawazuia kuondoka, kwamba wao kama majirani na mashahidi, watatakiwa kuweka Saini zao kwenye zile nyalaka za mauziano.
Baada ya kuwaambia hivyo, akashauri twende nyumbani kwake tukasainishane. Nikamkatisha, kwamba kuna shida kidogo imejitokeza.
Wote wanne kasoro yule mama mstaafu, walinigeukia kwa mshangao, maana nilienda nje ya script. Yule Mzee KY alinikata jicho, ambalo lilinipa tafsiri kwamba nikizingua nimekufa.
Akili ikaanza kunizunguka kwa haraka, maana nilitakiwa kufanya maamuzi ndani ya muda mfupi, uhamuzi ambao ungeweza kuwa na impact kwangu, kwa muda mrefu ujao...
Baada ya kufikiria kwa haraka, kuna wazo likanijia kichwani. Wazo ambalo niliona lingesaidia kudelay ile process kwa siku chache. Nikawashirikisha nilichokuwa nawaza
Analyse: "Wazo la kwenda kuandikishiana kwako muuzaji, ni zuri, ila sio sahihi. Kiofisi zaidi, inatakiwa kila kitu kikafanyikie ofisini, ili baada ya hapo niweze kuacha nakala za haya mauziano pale, sitakiwi kuzunguka nazo"
Aisee wale jamaa walinikata macho ya chuki, hadi nikaingia ubaridi. Unajua nature ya hii kazi, maandalizi yake hayakutakiwa kuhusisha ofisi. Ndio maana hata ofisi feki haikuwa imeandaliwa. Kitendo cha kusema tuandikishiane ofisini, maana yake hizo ni gharama zingine za haraka ambazo tutaziingia.
Ajabu ni kwamba, Mimi wakati najaribu kitengua lile zoezi lisifanyike siku ile, yule Maza ambaye tunataka tumpige hela akaanza kunibembeleza nifanikishe mauziano siku ile ile.
Mstaafu: "Mwanangu hebu nisaidie Mama ako, nipate ili eneo siku ya leo, nimelisumbukia sana"
Analyse: "Naelewa mama, lakini haya ni maswala ya kiofisi, leo mkiuziana alaf nikapoteza nyalaka. Inaweza kuniweka hatiani huko mbeleni"
Kesho Yetu: " Kwanini upoteze nyalaka, serikali imekuamini kukupa hiyo nafasi, mbona unashindwa kujiamini?"
Mstaafu: "Wewe mbona ni kijana smart sana, acha kuniangusha bhana"
Mzee Dingi: "Kama wasiwasi ni huo, basi tukishaandikishiana, tutaenda kuzipitisha chini ya mlango wa ofisi. Jumatatu utawahi mapema ili uziweke kwenye mafaili"
Mstaafu: "Hela ya soda ipo kijana wangu, naomba sana unisaidie"
Huyu mama ndio alikuwa anazidi kunipa ugumu. Najaribu kutaka kumsaidia. Lakini yeye anazidi kuniwekea ugumu. Baada ya majadiliano ya dakika kadhaa, Mzee KY ikabidi aingilie kati;
Mzee KY: "Nakubaliana na mwenyekiti, yupo sahihi kwa anachokisema. Ili ni jambo nyeti sana, halitakiwi kupelekwa kiholela."
Wote tukabaki tunamwangalia kwa mshangao, sikutarajia kama angeniunga mkono. Inamaana huruma imemuingia au kuna kitu kingine anafikiria?
Akaendelea:
Mzee KY: "Nashauri tufanye mambo kiofisi zaidi, Jumatatu mpaka Jumatano sitokuwa na nafasi, ila naomba wote kwa pamoja tukutane ofisini siku ya Alhamisi ili tumalize ili swala. Na kuhusu gharama zenu za usumbufu nitazirudisha, wala msiwe na hofu"
Tukawa tumekubaliana hivyo, lakini sisi wengine wote tulibaki na maswali kichwani, Mzee KY anawaza nini?. Mbona tumeenda nje ya plan lakini hajapanick?
Kiukweli nilishindwa kabisa kumuelewa. Ikabidi nimwambie yule mstaafu anipe lift mpaka Dar, maana kuna mambo yangu nilitakiwa kuyaweka sawa kule. Mzee KY akaniangalia jicho lenye kuuliza "Huondoki na sisi?". Nikampotezea.
Kwenye gari ya yule mstaafu, nikapanda na Mzee Dingi. Wale wengine wakarudi kivyao. Tukiwa njiani yule mstaafu alinibembeleza sana nisimamie swala lake lifanikiwe ile. Nikamwambia asijali. Mzee Dingi akawa anachombeza hapa na pale, lakini tukikutanisha macho yake yananiambia "ntakuua apostle". Pamoja na jicho la chuki alilokuwa ananiangalia nalo, lakini alikuwa haruhusu nimguse hata kidogo. Kiufupi alikuwa ananitisha, lakini at the same time ananiogopa.
Baada ya kufika mjini, kila mmoja alienda na njia yake. Yule mama mstaafu alitaka kunipa lift ila nikahofia Mzee Dingi anaweza kutufatilia nyuma nyuma alafu apajue ninapoishi, so nikakataa. Wote akatushushia sehemu moja. Kabla hatujaachana Mzee Dingi akaanza kunipa makavu;
Mzee Dingi: "Apostle Unazingua sana ujue? Dili ilikuwa imeshaisha hii"
Analyse: "Ila kumbuka huyu mama Mimi ananifahamu vizuri tu, dili likiisha msala unabaki kwangu"
Mzee Dingi: "Msala ubaki kwako, kwani bado unaishi kwake? Tanzania mapori mengi sana, nenda hata Mtwara huko, sio lazima wote tuendelee kuishi mjini".
Analyse: "Nirahisi kwa wewe kusema hivyo, lakini pia tambua yule mama.....". Kabla sijamalizia kauli yangu, akanikatisha.
"Acha useng* apostle, kwani Mama ako yule?". Aliongea kwa nguvu na jazba kiasi kwamba watu waliokuwa karibu wote wakatugeuzia sisi macho. Ukimuona Mzee Dingi alivyokuwa kavaa na yale maneno aliyoongea, ilikuwa halali wapita njia kutushangaa.
Nikaamua kuondoka, nikachukua uelekeo wangu, Mzee Dingi nae akaeleka upande wake.
**************
Kuna jambo moja ngoja niliongelee japo wakati naanza kusimulia, sikuplan kabisa kuweka details zake.
Nilivyokuja kuzinguana na kina Mzee Dingi hadi ikafikia kuachana nao (nitasimulia mbeleni) niliendelea kuwa na mawasiliano na Mzee KY kwa muda kidogo. Katika huo muda, ndio alikuja kuniambia vitu ambavyo hata kwangu havikuwa clear. Tokea mwanzo nimekuwa nikisema tu, tukapiga dili ili au lile, lakini sikuwahi kusema how. Ngoja walau nielezee dili la huyu mstaafu ilikuwaje mpaka ikafikia hatua ya kwenda kuuziana ardhi kule vigwaza.
Mzee KY anawatu anaofahamiana nao sehemu kadhaa, kuna mtu alimpa tip kuhusu huyu mama mstaafu na mafao yake. Yeye siku zote huwa anahitaji info hiyo tu, kwamba pale kuna hela kiasi kadhaa inaweza kupatikana, then mengine yote anafanya mwenyewe.
Alivyopewa hiyo info, akaja kuoneshwa muhusika mwenyewe alivyo. Baada ya hapo akaandaliwa mtu wa kumfatilia na kukusanya taarifa zake za kutosha. Zikishapatika, analetwa mtu wa kuja kukuvuta kwenye himaya yao. Kama unayetaka kutapeliwa ni mtu mzima sana, basi katatumwa katoto, kama wewe ni kijana, atatumwa mtu mzima au mzee nk. Kwa huyu mstaafu, kalitumwa katoto kakiwa na sare za shule ya msingi. Mtoto alipewa namba ya simu imeandikwa kwenye kikaratasi, akaambiwa amfate yule mama mstaafu kisha amuombe simu ili ampigie mama yake, maana amechanganya magari (just imagine unakutana na mtoto wa primary maeneo ya kkoo, alafu anakuomba umpigie mama yake, huwezi chomoa. In reality hako katoto kanakuwa sio mwanafunzi, au hata kama ni mwanafunzi basi anakuwa planned).
Sasa ile namba ukiipiga, haitokaa ipokelewe. Itaita sana mpaka ukate tamaa wewe. Kinachofatia, utamsaidia yule mtoto kupanda gari za kumfikisha kwao. Itakapofika mida ya usiku, mwenye ile namba itakupigia na kusema amekuta missed call yako. Ukikumbuka tukio na kumuelezea, atakushukuru, Kisha atakwambia nilikuwa sehemu fulani ndio maana sikuweza kupokea. Hii sehemu fulani atakayoitaja, lazima iwe inaendana na wewe maana taarifa zako za kutosha zinakuwepo. Anaweza kusema nilikuwa kwenye ibada kwa Mwakasege, Kakobe au Mwamposa, or chochote ambacho ukikisikia kitaendana na wewe. Hapo ndio utamwambia "Ooh kumbe na wewe unapata huduma kwa huyo mtumishi?".
So kutokea hapo, hamtojadili habari za mtoto tena. Next mtajikuta mnaanza kukutana physically huko kwenye huduma za kiroho. Atazidi kuwa karibu na kujenga uhaminifu, mpaka kuna siku utaongea kitu kitakacho kuja kukuliza. Haya yote yanachukua muda mrefu sana, na ndio maana Mzee KY kwa mwaka alikuwa hafanyagi dili nyingi.
Sasa kwa huyu mstaafu ilikuwa kama hivi. Alikuja akaongea habari zake za kuhitaji kufanya mradi wa greenhouse na kilimo cha umwagiliaji katika mtindo wa kisasa. Hii ndio taarifa aliyokuwa anaisubiria Mzee KY. Alivyoipata, ndio akaanza kuweka plan ni kwa namna gani akamilishe plan. Wakati anaendelea na kuweka mipango yake sawa, ndio kuna siku aliniona na yule mama mstaafu kabla sijahama kwenye nyumba yake. Na kwavile alishawahi kuniona na kina Mzee Dingi, basi akapendekeza Mimi niwe included ili ku-smoothen the process.
So, kwenye lile dili sikujumuishwa kwavile waliniona smart na mchangamfu, bali ukaribu wangu na yule mama. It was not a coincidence, everything was planned. Na Mzee KY alikuwa ahead of time.
Pamoja na hayo yote, Kunishirikisha Mimi ilikuwa ni plan A, lakini haikuwa plan pekee. Na kitendo cha Mimi kuonekana na yule mstaafu pale site, dili lilikuwa tayari limeshafanikiwa kwa 80%, either niendelee nao au nikatae.
So muda ule nilipoachana na Mzee Dingi baada ya kushushwa kwenye gari na mstaafu, Mimi nilianza kufikiria ni jinsi gani naweza kumsaidia yule mstaafu bila kuingia kwenye utata na kina Mzee Dingi.
Wakati Mimi nafikiria hayo, Mzee KY kwa upande wake alikuwa ashanitoa kichwani kwake. By the moment tumeachana kule site, yeye tayari alisha-execute plan B. Plan ambayo timu nzima hatukuwa tunaifahamu, isipokuwa yeye. Kama ushawahi kuangalia movie, huwa kuna wale extra characters, wanaonekana kwenye vipande kadhaa ili kukamilisha matukio, baada ya hapo hawaonekani tena hadi movie inaisha. Hivyo ndivyo Mzee KY alivyotufanya timu nzima. Yani kipindi Mimi na Mzee Dingi tunatukanana barabarani kisa dili limedelay, kumbe kwenye dili lenyewe wote tumeshatolewa.
Kwa ufupi Mzee KY aliamua kuwa Solo.......
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
[emoji23][emoji23][emoji23] wezi nao wameibiwa ha ha ha nacheka kama mazuri pole kwa mstaafu18th Portion:
Baada ya kuachana na Mzee Dingi, nilirudi gheto direct. Siku hiyo hiyo mida ya jioni, yule mama mstaafu akanipigia simu;
Mstaafu: "Hujambo mwanangu?"
Analyse: "Mzima mama, shikamoo"
Mstaafu: "Marahaba. Vipi utakuwepo mjini mpaka lini?"
Analyse: "Kuna vitu naweka sawa, vikikamilika nitaondoka. Inaweza ikawa Jumatatu au Jumanne"
Mstaafu: " Tunaweza kuonana kabla hujaondoka?"
Analyse: "Sawa hakuna shida, nadhani Jumatatu jioni nitakuja".
Baada ya kuongea na yule mstaafu, jioni hiyo hiyo, Mzee KY nae akanipigia simu, kuniambia tuonane siku ya Jumatatu jioni bila kukosa, ili tuweke sawa mambo kadhaa. So, ndani ya siku moja nikawa na appointments mbili, na zote jioni.
Wa kwanza kuonana nae ni Mzee KY, tulikutana mida ya saa kumi kumi.
Mzee KY: "Umeshaongea na yule mama au kuonana nae tokea ufike mjini?"
Analyse: "Hapana, kwanini?
Mzee KY: "Ulimwambia chochote labda kuhusu huu mpango?"
Analyse: "Hapana, vipi kwani?"
Mzee KY: "Oky Vizuri, sasa shika hizi hesabu" (akatoa hela na kunipa).
Nikahesabu, zikafika laki 3 na nusu. Nikamuuliza za nini hizi?
Mzee KY: "Huo ndio mgao wako, kwenye ili dili haupo tena"
Nikabaki nimeshangaa, sipo Kivipi?. Maana kama sipo basi dili limekufa, ila yeye mbona anaongea as if dili bado lipo?.
Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu, akaniambia "Wewe ulikuwa plan A, haikuwa plan pekee. Kwahiyo kama nilivyokwambia, naomba ukae pembeni, dili litaenda bila uwepo wako. Na usije kumwambia chochote yule Mama"
Nikabaki na mwangalia tu. Hapa ndio alikuja kunipa maelezo ambayo nilikuja kuhitimisha kuwa, uwepo wangu kwenye lile dili haikuwa coincidence, kila kitu kilikuwa planned. Aliifahamu connection yangu na yule mama, na dhumuni la kunifanya Mimi kuplay role ya mwenyekiti, ili niweze kugain trust ya yule mama Kwa urahisi. Na hata kile kitendo cha Mzee Dingi Kuni unblock na kunitaka nipige nao kazi, yote ilikuwa ni maandalizi ya ili dili. Halikuja ghafla kama nilivyodhani. Baadhi ya maelezo aliyonipa, ndiyo niliyaelezea jana. Japo kuna mengine niliyaelezea jana, ila yeye alikuja kuniambia mbeleni kabisa wakati dili limeshafanyika.
Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, tukaagana. Sikuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kule kwa mstaafu, ikabidi nielekee kule.
Nikiwa zangu mdogo mdogo nishakaribia kwa yule, Sina ili wala lile. Kumbe Mzee KY alikuwa ameniungia tela. Sikujua kama dhamira yake ilikuwa kupajua ninapoishi au alitaka kujua nitaelekea wapi baada ya sisi kuachana pale kwenye ile Pub. Naingia tu kwenye ile nyumba, na yeye huyu hapa. Kwa haraka haraka, mtu angeweza kuhisi kuwa tulikuwa tumeongozana wakati tunaenda pale.
Nilishtuka kumuona, japo sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia yeye kuwa pale. Yule Mama mstaafu alipotuona wote alifurahi sana;
Mstaafu: "Naona watu muhimu mmeamua kunijia kwa pamoja, karibuni sana"
Analyse: "Asante sana"
Mzee KY: "Kijana alinipigia simu niungane nae kuja kukuona. Vipi za tokea siku ile?
Mstaafu: "Salama tu, Tunamshkuru Mungu uzima upo kama unavyotuona"
Kisha akanigeukia Mimi;
Mstaafu: "Karibu tena nyumbani, ila this time karibu kama mwenyekiti"
Aliniambia hayo maneno huku anacheka, Mzee KY nae akacheka kidogo. Tukaingia na kukaa sebleni kwake. Maongezi yote kayatawala yule mama tu. Kuna muda akaingia chumbani huko, kisha akatoka na hela;
Mstaafu: "Nilikwambia nitakurudishia hela ya Kodi uliyoacha, chukua laki mbili yako. Sitaki dhulma Mimi, najua kijana ndio kwanza unaanza kujijenga".
Mzee KY akamakinika kuona nitafanya nini. Binafsi nikaamua kuzikataa zile hela;
Analyse: "Hapana mama, nilihama kwa hiari yangu hii hela wala sio deni kwako"
Mstaafu: "Chukua mwanangu, hii haiusiani na kule kusainishiana, maana kule najua huwezi kuniangusha. Nakupa kama kijana wangu tu".
Unajua siku zote wakati nakua, kuna methali ilikuwaga maarufu sana.
"Sikio la kufa halisikii dawa"
Ukikanywa, usiposikia lazima uambiwe. Siku zote nilikuwa naichukulia kama methali tu, lakini in a real sense kwa mara ya kwanza nimekutana na ilo "Sikio la kufa". Unajua ili umuokoe mtu anayezama, sharti awe mtulivu vinginevyo mtazama wote. Au la, basi mpe kijiti, akishike umvute. Sasa huyu mama kila nikimpa kijiti, anakikataa. Kimoyo moyo nikajisemea atajijua mwenyewe.
Analyse: "Usijali mama, hiyo hela wewe Kaa nayo. Nimeondoka kwa amani kabisa, nikiichukua nitajisikia vibaya".
Akabaki na hela yake. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Mzee KY akaomba niwapishe waongee kidogo. Sikuwa na namna, nikatoka zangu nje, wakaongea mambo yao kwa takribani nusu saa au dakika arobaini na tano. Baada ya hapo Mzee KY akatoka nje, tukaondoka wote.
Baada ya kutoka pale, akatafuta sehemu. Akaniweka kikao tena;
Mzee KY: "Sikia kijana, hivi unaweza kukadilia gharama kiasi gani imetumika kuandaa Ili dili?".
Ni kama alikuwa anaongea peke yake, maana kabla sijamjibu akaendelea tena;
"Mlivyokuja kule site, uliwaona wale majirani niliosalimiana nao?. Wale wote nimetoka nao huku. Uliwaona wale watu wanaolima pale?. Sijui hata wanalima nini, ila nao nimewaweka Mimi."
Akaendelea;
"Dili lifanikiwe au lisifanikiwe, hao wote lazima wapate hela yao. Sasa hebu niambie, lisipofanikiwa hela za kuwalipa zinatoka wapi?"
"Kuna watu huwezi kuwasaidia hata ufanye vipi, they are destined to lose. Hata ukisema umuache na hela zake akanunue eneo halali, still zile hela ataenda kuzifukia chini akitegemea zitachipua, ila ataambulia hasara. Najua hukuchukua ile laki mbili yake, sio kwamba huitaki au unamuonea huruma, bali you feel guilty. Nitakupa Mimi ile laki mbili, soon after dili kufanikiwa, ila for now naomba usinizibie njia, maana siwezi elezea nitakachokufanya. Umenisikia..........?'' Akataja jina langu halisi.
Nikashtuka, amelijuaje jina langu?.
Mzee KY: "Wote mliopo kwenye Ili dili hakuna nisiyemjua, kuanzia anapokaa au sehemu zake za kwanza kukimbilia hapa mjini, kwahiyo kabla hujafanya jambo utakalokuja kulijutia, ni heri ujifikirie mara mbili"
Nikabaki nimeduwaa tu Kwa muda, sielewi what next. Akaniambia, "Huna haja ya kuendelea kubaki hapa, wahi ukapange vitu kwenye makazi yako mapya, japo nakushauri hama". Hakusubiria jibu langu, akaondoka.
So, he knows me well?. Why nihame wakati ndio kwanza nimehamia au kuna msala unanisubiria? Wazo likanijia, kwanza yule mstaafu tumejuliana mjini hapa hapa, atajijua mwenyewe, ngoja nijihangaikie Mimi.
Nilivyofika ghetto, Yale maneno ya Mzee KY kuwa nihame pale, yakawa yananijia. Nikajikuta njia panda, nipange vitu au nijiandae kuhama?. Ila nimetoka kulipa Kodi ya miezi 6 siku chache tu zilizopita, nahamaje? Mbona ntakuwa nafaidisha wenye nyumba?. Lakini taswira ya Mzee KY ikawa hainipi picha nzuri ya yajayo. Akili ikaniambia nisipange vile vitu, nihame.
Nikampigia simu mwenye nyumba, kumuomba kesho tuonane kama ataweza. Akakubali.
Asubuhi nilivyoonana nae, nikampanga kuwa nimepata dharura natakiwa kusafiri haraka nje ya mkoa, anirudishie hata nusu kodi. Akanijibu "Mwanangu Cha kukusaidia hapa, labda nikuhifadhie vitu vyako kwahiyo miezi 6 utakayokuwa unapambana na hiyo dharura yako"
Nikaona hapa siwezi ambulia hata mia, cha zaidi nitapoteza muda tu kumbembeleza.
Kipindi Mimi nawaza namna ya kuhama pale. Mzee Dingi akanipigia simu na kuomba tuonane.
Nikafikiria huyu nikutane nae maeneo yapi?. Kipindi kile maeneo ya Tabata kuna mashindano ya mpira wa miguu yalikuwa yanaendelea. Viwanja vilivyokuwa vinatumika ni kile Cha Sigara na cha Tabata shule. Nikaona option ya Tabata shule ndio sahihi, maana ni mbali kiasi na ninapoishi. Lakini sababu nyingine iliyofanya nisione shida kukutana nae Tabata, ni kwavile nilikuwa natarajia kuhama.
Nikamwambia tukutane Tabata shule. Mzee Dingi akagoma, na hii ni kwavile pale ni karibu sana mitaa anayoishi yeye. Nilivyóona bado anakomaa tuchange location, nikamwambia basi sitaki kuonana na wewe. Endelea na mishe zako.
Nilipata ujasili wa kumwambia vile kutokana na sababu Kuu mbili, kwanza kwenye dili lao sipo tena, alafu pili sijui anataka tuongee nini. Alivyoona nimekataa kuonana nae, hakuwa na choice zaidi ya kukubali tukutane maeneo yale.
Mida ya jioni nikasogea pale Tabata shule. Mzee Dingi alikuwa ameshafika kabla yangu. Mara zote ambazo tumekuwa tukikutana, vikao vilikuwa vinafanyikia either bar, pub or kwenye mgahawa. Ila this time hakutaka tukutane maeneo hayo. Akapendekeza tukutane kwenye yale majengo ya shule ya Kijapan (kuna shule ilijengwa na Wajapani maeneo yale). Nikajiuliza mara mbili mbili, why kachagua kule?. Ila kimoyo moyo nikajisemea akileta za kuleta, nitamfumua. Hasira zangu zote ziishie kwake.
Akanielekeza alipokuwa amesimama, nikamfata. Kufika pale, navikuta vizee vyote vitatu vipo. Mzee Dingi, Mzee Kidevu na Mwanasheria feki. Nikajiuliza vinanitakia nini?.
Nilivyowaona, sura zao zote ziliakisi shari, ila sikuwa na namna zaidi ya kuwasogelea. Zikapigwa story za hapa na pale, lakini Unaona kabisa hapa kuna jambo litatokea muda sio mrefu. Na Mimi kwa hasira nilizokuwa nazo, nikawa nasubiria kwa hamu ilo jambo litokee. Kwa jinsi tulivyokuwa tumejipanga, Mzee Kidevu alikuwa nyuma kidogo upande wangu wa kushoto, alafu mwanasheria feki na Mzee Dingi walikuwa mbele, tupo face to face. Tukiwa tunaendelea kuongea upande, kwa ghafla sana yule Mzee Kidevu akanirukia horizontally na kunipiga kichwa cha mbavu. Ni kitu ambacho sikuwa nimekitarajia, nikajikuta nayumba yumba. Kitendo cha kuyumba yumba, wale wazee wote wakanivamia kwa pamoja.
Nikajisemea hapa ndio nilikuwa napataka, ngoja nipunguze hasira zangu. Unajua Kwa jinsi nilivyokuwa nawakadiria, nilihisi dakika 10 nyingi wangesanda kwenye lile valangati. Ila yule Mzee Kidevu sijui hata anakulaga nini aisee, maana kuna muda nilimrushia ngumi, lengo nimpige shingoni, ila at the same time nae akanirushia ngumi. Ngumi kwa ngumi zikakutana, nilipatwa na maumivu kiasi kwamba nikahisi nimepiga mti. Kibaya zaidi yule Mzee hata akuugulia chochote, ndio kwanza anakuja tu.
Kipindi hicho chote, Mzee Dingi na Mwanasheria feki wameshasanda, wameniacha Mimi na Mzee Kidevu. Raia wamejaa wanauliza kuna nini?. Mzee Dingi linawajibu "Mambo ya kifamilia, tuachieni wenyewe". Yule Mzee Kidevu kama angekuwa na pumzi ya kutosha, angeniaibisha pale, kitu pekee kilichofanya akachemka ni pumzi. Nilivyóona kazidiwa, nikaanza kumpelekea punch mfululizo. Kumbe bwana vile vizee vilikuja na back up. Muda wote tokea nimewakuta, kuna jamaa kipande alikuwa amekaa kwa pembeni anachezea simu.
Walivyoona hadi Mzee Kidevu kazidiwa, Mzee Dingi akaita "We Beka fanya kazi yako". Aisee nilivyomuona huyo Beka mwenyewe, sikuwa na namna zaidi ya kukimbia. Nilifungua turbo kuelekea kwenye makazi ya watu, yamekaa kama kota hivi. Nilidhani watanipotezea, nashangaa Beka kaniungia tela, Mzee Kidevu na wale wazee wengine nao wakaanza kuja nyuma yetu. Raia nao hawana dogo, baadhi wameacha kuangalia mpira, wametuungia tela.
Nikipiga hatua zangu mbili, ndio hatua moja ya Beka. Sikwenda mbali sana akanishika. Nikataitishwa. Mwanasheria feki akawa anafanyakazi ya kufukuza watu walau wasogee mbali ba tulipo. Nilivyokuwa chini pale, Mzee Dingi akawa anasema;
Mzee Dingi: "Mvue hivyo vitu alivyovaa ndio vinamtia kiburi"
Beka akanichukulia ile pete yangu yenye kihirizi. Kisha akataka kunivua na kacha niliyokuwa nimevaa mkononi
Mzee Dingi: "Hiyo muachie, haina madhara. Yupo nayo hata kabla hajaoneshwa Dunia ilivyo"
Baada ya kuichukua ile pete, akamkabidhi Mzee Dingi, alafu wakaanza kuondoka. Kwenye wallet nilikuwa na 70k, hawakuigusa kabisa. Yani Wazee shida yao ilikuwa ile pete tu. Nilikuwa bado nimekaa chini nikiwa na hasira, maana yule kipande aliniumiza. Ghafla kuna wazo likanipitia kichwani, sikujiuliza mara mbili, nikanyanyuka na kuanza kuwafata. Nilivyowakaribia nikainama chini na kuchota mchanga, Mzee Kidevu akawa ameniaona;
Mzee Kidevu: "Apostle umenichota unyayo, apostle umenichota unyayo?"
Kiukweli nilifanya vile kama kuwatisha tu, ila Mzee Kidevu akalichukulia serious.
Mzee Kidevu: "Apostle unachotaka kukianzisha unakimudu?. Kumbe mtoto mshenzi sana wewe"
Kabla sijamjibu kitu, yule Beka kipande akawahi kunikamata, akaniminya mkono hadi nikaachia ule mchanga. Nikabaki nimesimama tu. Kila Wakitaka kuondoka, natishia kama nainama kuzoa mchanga, wanarudi.
Mzee Dingi: "Huyu mtoto sio wa kumfanyia mzaha kabisa"
Jamaa kila wakipiga hesabu, walipoacha gari yao ni mbali lazima watembee. Lakini hapo hapo wanahofia huku nyuma naweza fanya jambo baya. Ghafla Mzee Kidevu akanirukia, tukaanguka wote chini. Kisha wakamwambia Beka anibebe mpaka kwenye gari yao.
Muda huo wote raia full kucheka, kelele na kuzomea. Jamaa ikabidi wanipe lift kwa lazima, wakaenda kunishushia Ilala Boma.
Nilichokuja kugundua, kumbe ile Jana nilivyoacha na mzee Kesho Yetu, alimpigia Mzee Dingi na kumwambia Mimi sitoshiriki tena kwenye lile dili, nikiendelea kuwepo kuna uwezekano mkubwa sana wa dili kufeli. Ndio maana kina Mzee Dingi wakaamua kuja kunishikisha adabu na kunipora kile kihirizi, maana waliona sihitajiki tena.
Ambacho Mimi na wale wazee hatukujua ni kwamba, wakati sisi huku tunashikana mashati, upande wa pili Mzee Kesho Yetu alikuwa anakamilisha dili. Jana yake wakati tupo kwa yule mstaafu, walivyo baki peke yao sijui hata alimwambia nini, ila chochote alichomwambia ndicho kilichopelekea wao kwenda kukamilisha dili.
Walau Mimi nilishajua kuwa kwenye lile dili sipo tena, ila kina Mzee Dingi wao walikuwa wanasubiria siku mbili mbele wakakamilishe dili.
Wamechukua pete yangu, na kuondoka kishujaa, kumbe upande wa pili Mzee Kesho Yetu anasepa na mkwanja peke yake.
Kibaya zaidi, anaacha msala ambao ni wetu wote, ilhali sisi wengine hatujajiandaa....
Endelea hapa https://www.jamiiforums.com/threads...liyokutana-na-yule-mzee.2079499/post-45996349
Toa connection hiyo mzee kwani shida Iko wapiii ha ha haTokea story imeanza, kila anayeomba namba, akinipigia anaulizia waganga 😅😅😅
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Ili muende kujaa kwenye page yake? Wabongo hamnaga shoo ndogo 😅😅
Wakora sio watu wazuri kabisa, wamekupoteza kijana20th Portion:
... Nikiwa pale kwenye kiti, Mzee Kesho Yetu alibaki ameniangalia kwa muda mrefu, Kisha akaniambia
Mzee KY: "Sikia bwana mdogo, nakushauri upotee mjini kwa muda. Hivi pale ulishahama?"
Analyse: "Ndio"
Mzee KY: "Vizuri, sasa inabidi usionekene Dar kwa kipindi fulani, ili upishe hali ya hewa itulie."
Analyse: "Natamani kufanya hivyo, ila hela ndio sina. Kule kuhama hama, kumenipotezea hela sana. Hata huku kukutafuta wewe nako kumenirudisha nyuma"
Mzee KY: "Enhee Hapo hapo kwenye kunitafuta, naomba tukiachana leo nisikuone tena hata kwa bahati mbaya. Nisingependa unifatilie tena"
Analyse: "Sasa naondoka vipi na Sina hela?"
Mzee KY: "Unapoanza jambo lolote, lazima uwe umepanga namna ya kulimaliza. Vinginevyo utajikuta unaingia matatizoni kama hivi sasa"
Analyse: " Basi nifanyie mpango hata wa kiasi kadhaa walau kiniwezeshe kupotea"
Mzee KY: " Sina hela kwasasa"
Analyse: " Hela zote ulizopiga Mzee?"
Mzee KY: " Hela zote kiasi gani?. Hivi unajua nyuma yangu kulikuwa na watu wangapi hadi dili likafanikiwa?"
Akaendelea, " Nitakupa ile laki mbili niliyokuahidi wakati ule, nitakuongezea na elfu hamsini. Zaidi ya hapo, sina."
Nikabaki nafikiria tu pale, natokaje salama kwenye huu msala?
Akaendelea, "Tena kitu unachotakiwa kukikwepa sana, ni kuonana na wale wazee wengine. Ni rahisi wao kukuchoma, ili wao wajiweke on safe side".
Analyse: " Sawa nimekuelewa, ila nina ombi moja la mwisho"
Mzee KY: "Ombi gani?"
Analyse: "Unajua wale wazee walinipora ile hirizi niliyopewa na yule mtaalam wako, kama inawezekana unidirect kwake akanipatie nyingine"
Yule Mzee aliniangalia kama vile nimeongea kitu ambacho hakukitarajia kabisa.
Mzee KY: "Ilo haliwezekani kabisa. Alafu nilijua utaongea kitu cha maana, kumbe kujichanganya na wazee akili yako ndio ishavurugika hivyo?"
Analyse: "Sina akiba Mimi, alaf natakiwa kujificha. Najifichaje sasa?"
Mzee KY: " Hayo ilibidi uyawaze kabla hujaamua kuingia kwenye hizi kazi"
Analyse: "Ila nyie ndio mlionishawishi kuingia kwenye hizi kazi"
Mzee KY: "Ila hakuna aliyekulazimisha"
Maneno yake yanazidi kunikata moto, maana bila hela ya maana ni ngumu kutoboa mafichoni.
Analyse: "Basi nisaidie jambo jingine?"
Mzee KY: "Lipi?"
Analyse: "Kwavile wewe unabiashara nyingi genuine mjini, basi nifanyie hata mchakato nifanye kazi kwako"
Akanishangaa tena;
Mzee KY: "Bwana mdogo kumbe hauko smart kama nilivyodhani. Umefikiria kabla hujatoa ilo ombi?"
Analyse: "Nimefikiria, ila sina namna ya kusurvive"
Mzee KY: "Sikia, Mimi na ww kitendo cha kufahamiana kwa njia hii, basi hatuwezi tena changamana nje ya hapa. Na kama tungejuana nje ya hapa, basi hakuna uwezekano ungeweza kunifahamu namna hii. Wakati unajiunga ulijua unachokuja kukifanya, na ukaamua kujiunga, tafuta namna ya kujitoa"
Yaliongelewa mengi, lakini hapakuwa na lolote ambalo lingeweza kumfanya either aniongezee hela au hata anipe ajira. So, tukamalizana kwa yeye kutoa hela kwa wakala, na kunipatia. Hakutaka kabisa kunipa namba yake aliyokuwa anatumia pale. Baada ya kunipa hela akaniambia;
"Kubali hasara, badili simu na hiyo line. Usivitumie tena. Narudia, Simu na line, sio line peke yake"
Tukaagana, nikaamsha.
Nikazunguka, upande wa parking. Nika nakili namba za lile gari lao, kisha nikadandia usafiri wa kurudi Dar. Nikiwa ndani ya coaster, Mzee Kesho Yetu akanitext kwa ile namba yake ya siku zote, "Nimeambiwa umenakili plate namba za hii gari, fikiria mara mbili kabla hujafanya ulichokusudia, maana hakuna kurudi nyuma baada ya hapo".
Nikajifikiria kwa muda, ila nikaamua kumpotezea. Maana hata Mimi mwenyewe sikujua kwanini nimenakili ile namba, ila nilipata hisia inaweza kuja kuwa na msaada mbeleni.
Sababu iliyosababisha nirudi Dar, kwanza sikuwa nimeplan niende wapi, pili sikuwa nimejipanga vizuri namna ya kuondoka.
Nilivyokuwa ndani ya gari, ile simu nikaamua kumuuzia abiria aliyekuwa pembeni yangu. Niliiuza kwa bei ya hasara, ila sikujali. Line nikafuta majina yote, kisha nikaitupa mle mle ndani ya gari.
Nikanyoosha moja kwa moja mpaka gheto. Naanza kutafakari wapi nitaenda. Kesho yake nikanunua simu ndogo ya batani na kusajili line mpya, kisha nikarudi ghetto. Sikuwa napenda kushinda sana nje. Giza likishaanza kuingia, ndio nilikuwa nautumia huo muda kutembea tembea.
Zilipita kama wiki mbili, bila kash kash yoyote au kukutana na mtu yeyote wa kunipa mashaka. Nilivyohisi kama kumetulia, kuna jamaa yangu nikaenda kuonana nae maeneo ya Mikocheni, sasa muda narudi nimefika pale mwenge mataa. Nilisimama karibia robo saa nzima, natafuta timing ya kuvuka barabara, maana gari zilikuwa speed sana.
Zilivyopungua nikawa navuka. Sasa wakati navuka, kuna Mzee nae akawa anavuka kutokea upande opposite na wangu. Ikatokea ile hali ya kugonganisha njia. Yani wewe ukitaka kupita upande wa kulia, wa mbele yako nae anakua kaamua kupita upande huo. Ukisema ushift kushoto, unakuta na yeye karudisha mawazo ya kupita upande huo. Mpaka mnajikuta mnagongana. Icho ndicho Kilichotokea kwa yule Mzee.
Kila nikimkwepa na kwenda kulia, nae anakuja huko, nikirudi kushoto nae huyo kushoto. Binafsi nikikutanaga na situation kama hiyo, huwa nasimama, ili huyo mtu mwingine apite, ila Cha ajabu kwa yule Mzee, nilivyosimama na yeye akasimama. Alafu muda huo huo, kuna gari ipo kibati inakuja upande wetu. Nilivyóona simuelewi yule Mzee, nikaamua liwalo na liwe, kwa nguvu zangu zote nikaamua kumpush ili tuangukie anapotoka yeye. Cha ajabu, nilitumia nguvu nyingi sana, ila nikajikuta napush hewa, hapakuwa na mtu mbele yangu. Nikaangukia upande wa pili, ile gari ikapita speed bila hata kusimama.
Haya yote yalitokea ndani ya muda mchache sana. Cha kushangaza, watu waliokuwa jirani, wao walichukulia kile kitendo kama nimejirusha ili kulikwepa lile gari, kumbe mwenzao niliona vitu tofauti. Na kati yao waliokuwa wanaongea, hakuna aliyezungumzia habari za kumuona mtu mwingine mbele yangu. Waliishia kunipa pole, wengine hongera kuwa siku yangu ya kufa bado nk. Lile tukio lilinifikirisha sana. Kwanini limetokea? Linahusiana na issue tuliyofanya kwa yule mstaafu?. Au ndio ndugu zake wameamua kunifanya kama alivyofanya Kisauti?. Kama ni hivyo, why Mimi niwe napataga adhabu tu, alaf wanaofaidika ni wengine?. Najitoaje kwenye Ili?
Akili ikaanza kuniambia niondoke mjini haraka sana. Ila naenda wapi?. Home nikienda, lazima niulizwe kwanini nimeenda, maana wao wanahisigi nikishazingua ndio huwa naenda. And this time ni sahihi, nishazingua, je niende au nisiende?
Ila hata nikienda, kama jamaa wameniamulia, wanaweza kunidhuru nikiwa kule kule. Nikaanzr upya vurugu za kwenda kwa waganga na Mshua?. Mawazo yakanijia nimpigie Kisauti, dhumuni ikiwa walau anipeleke hata kwa mtaalam wake nikajikinge kwanza. Ila kuna sauti ndani yangu ikawa inanikumbusha maonyo ya mtaalam kuwa nisije kumtafuta tena Kisauti. Ila nitafanyaje?. Namtafuta vipi huyo Kisauti
wakati namba yake sikuwa nayo, niliifuta nilivyouza simu?.
Na kusema niende mpaka kule walipo kabla sijaongea nae itakuwa uongo. What if hasira zao hazijaisha? Na zinaishaje ikiwa hawajapata hela zao?.
Ndani ya wiki nilishaanza kukonda kwa mawazo, maana pia hela Nazo zinaisha tu Kwa matumizi, ila siingizi hata 100.
Wiki mbili tokea lile tukio la pale mwenge litokee, sister akanipigia simu kuwa Mama anaumwa sana, alafu sijawahi hata kuwajulia hali. Ofcourse kichwa changu kisipokuwa na utulivu, huwa kuwatafuta watu inakuwaga issue sana. Na mtu asiponielewa, tutagombana mara kwa mara, ndio maana mahusiano yangu mengi yanavunjikaga kwa mtindo huu. Tokea nibadilishe simu na line, nilivyowapigia ndugu zangu kuwataarifu kuhusu namba yangu mpya, sikuwahi kuwatafuta tena.
Na hapo ulishapita karibia mwezi mzima. Baada sister kunipigia na kunipa ile taarifa, nikajiona nishapata sababu ya kwenda home. Nikaamua kumpigia Mama home, simu alipokea Mshua. Baada ya salamu za hapa na pale, ikiwa ni pamoja na kunielezea hali ya Mama. Nikamwambia kuna kazi ya watu naiweka sawa, kisha baada ya wiki moja nitaenda kuwaona. Hakunipinga.
Sikuwa na kazi yoyote, ila Mshua namjua hivyo sikutaka maswali mengi. Ningemwambia kesho yake naanza safari, angetaka kujua kwamba Sina mishe huku mjini? Maana haiwezekani taarifa upewe leo, then kesho upo ndani ya bus. Sikuwa nimejiandaa namna ya kudanganya, nilihofia ningebabaika alaf akahisi kuna jambo haliko sawa.
Ile wiki nzima ya kusubiria safari, sikutaka hata kutoka nje na pale nilipokuwa naishi. Muda wote nipo ndani, au chooni. Ndani au dukani. Kiufupi niliishi kama digidigi.
Baada ya wiki, nikafunga safari kwenda home. Punch alizoenda kunipa Mshua, zilikuwa ni mara mia ya alizonipa Mzee wa Kongowe.
Walau Mzee wa Kongowe alikuwa ni mtu baki, maana kuna baadhi ya maneno ukiambiwa na mtu wa karibu sana, yanachoma kuliko hata msumari. Mzee wa Kongowe alinifanya nikaanza kumuangalia Mshua kwa namna ya tofauti. Ila maneno ya Mshua yalinibadili mtazamo wangu kabisa.
Kauli za Mshua Ziliniumiza sana, ila naweza kusema zilinisaidia sana kurudi kwenye mstari. Zilinifanya nikaanza kuyaangalia baadhi ya mambo kwa mitazamo tofauti sana. Au kuwachukulia watu kwa namna ya kipekee pia.
Niliufurahia uhamuzi wa kurudi nyumbani kipindi kile. Maana niliondoka nikiwa mtu wa tofauti ....
Endelea hapa https://www.jamiiforums.com/threads...liyokutana-na-yule-mzee.2079499/post-46015399
Yaani ikifika sehemu ya maongezi na mshua wako na enjoy sana ni mzee mmoja hivi matata pia jeshi sijui inaharibu [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]21st Portion:
...Nyumbani nilipokelewa vizuri tu, tena kwavile safari walijua nimekuja kuwaangalia sababu ya ugonjwa wa Mama, hivyo Mshua hakuwa mkaksi kwangu. Hali ya Mama ni kweli haikuwa nzuri, alikuwa haishi kulalamika maumivu na vichomi vya mara kwa mara. Mwanzoni walivyompeleka hospitali, alipewa tu dawa ambazo walidhani zingeweza kulitatua tatizo lake. Ila alitumia mpaka zikaisha, ila tatizo likaendela.
Nilivyofika ikabidi nishauri turudi tena hospital kwa uangalizi zaidi. Na kweli tulivyoenda tena, wale madaktari baada ya vipimo vyao, wakasema Mama anasumbuliwa na appendix na kwa stage iliyofikia, inatakiwa afanyiwe upasuaji haraka sana. Binafsi nikishasikia habari za upasuaji, huwa naichukulia kama habari nzito hata kama ni upasuaji mdogo. Ikabidi tushauriane kama familia nini kifatie, maana Kwa mazingira ya hospital ya pale kijijini, haikunipa amani kabisa kuwaruhusu wamfanyie upasuaji Mama. Mshua akabisha bisha sana pale, Mama nae asivyopenda kusafiri, akawa anasisitiza tufanyie pale pale. Kwavile watoto tuko wengi kuliko wazazi wetu, mawazo yetu ndio yakapita, kuwa upasuaji usifanyikie pale kijijini.
Baada mjadala huo kuisha, ukaibuka mjadala wa hospital gani aende. Nikashauri twende Bugando Mwanza, kwanza ni karibu lakini pia pale Mama atakuwa chini ya uangalizi mzuri wa Dada. Mshua akashauri twende Dar, kule huduma ni nzuri na kuhusu sehemu ya kufikia atafikia kwangu.
Analyse: "Kule Mama hawezi kuwa comfortable tofauti na kwa Dada"
Mshua: "Kwanini asiwe comfortable?"
Analyse: "Sasa unadhani Mimi na wewe tutaweza kumpa uangalizi mzuri kuliko Dada?"
Mshua: "Kwani mpaka tumuangalie Mimi na wewe?"
Analyse: "Sasa nani mwingine atamuangalia?"
Mshua: "Mkeo"
Analyse: "Mke yupi Mzee?. Sina mke mjini Mimi"
Mshua: "Huna mke, au huwa anakuja na kuondoka?"
Mama: "Nyie mkishaanza kubishana hapo, mpaka apatikane mshindi Mimi ntakuwa nishajifia hapa"
Ikabidi mazungumzo na Mshua yakome kwa muda. Tukaadhimia Mama aende Bugando. Tulisafiri nae mpaka kule, Mshua yeye alibaki. Kufika Bugando tukawaelezea tuliyoambiwa hospital kule kijijini, tukawapa na makaratasi ya vipimo vyao walivyofanya. Wakayasoma, kisha wakashauri afanyiwe vipimo upya, baada ya hapo ndio taratibu zingine zifatie.
Majibu ya vipimo vyao pale Bugando yaliporudi. Mama akaonekana hana tatizo appendix, isipokuwa kwenye mifupa ya nyonga uloto ndio umepungua (sababu ya umri), hivyo mifupa inasagana na kumletea maumivu. Akapewa dawa na ushauri wa baadhi ya vyakula anavyotakiwa azingatie, Kisha tukaruhusiwa. Hakufanyiwa upasuaji. Tukaendelea kukaa Mwanza, tukishangaa Jiji kidogo. Mshua akawa anataka turudi;
Mshua: "Ameshapewa dawa, fanya mpango arudi sasa"
Analyse: "Ngoja walau tufanye utalii kidogo kwa wiki hii kisha tunarudi"
Mshua: "Umenisikia vizuri nilichokwambia?. Nimesema fanya mpango Mama arudi, wewe hata ukiendelea kukaa mwaka, Sina tatizo"
Sister: "Lakini Baba, ungemuacha hata siku chache, huko anawahi kufanya nini?"
Mshua: "Hivi nyie sijui hata kama mnanielewa. Yani mnanipangia juu ya mtu ambae mmezaliwa mkanikuta nae?. Nimesema namuhitaji mke wangu"
Tulianza tunajadiliana kawaida tu, ila Mshua akaenda anabadilika mdogo mdogo. Kesho yake tukarudi nyumbani. Home Sweet Home.
Mshua: "Kwahiyo hawa madaktari wa hapa kijijini walikuwa wanataka kufanyia mazoezi mwili wako?"
Mama: "Yameshapita hayo, makosa hutokea"
Mshua: "Ni kwavile huo upasuaji haukufanyika tu, ila nadhani wangeomba uhamisho. Lakini hata hivyo lazima niwafate tukaambizane ukweli"
Analyse: "Hata ukiwafata itabadili nini, acha tu yapite"
Mshua: "Ili limepita, lakini maradhi hayaishi kuja, nataka siku nyingine wakiiona hii sura, wakumbuke notsi zote walizosoma hadi wakahitimu"
Nikamkubalia tu, then nikaingia jikoni kutaka kusaidia kupika maana hatukula njiani. Mshua akaniambia nijipikie mwenyewe tu, maana chakula cha Mama ameshakipika. Nilijua asingeniruhusu kula kile chakula, ila nikamjaribu tu;
Analyse: "Lakini wote tumetoka safari"
Mshua akacheka kwanza, "Yani ninunue mahitaji yote humu ndani, pia nikupikie. Huyu ni mke wangu"
Analyse: "Na Mimi ni mwanao"
Mshua: "Nani kakwambia?. Una uhakika gani wewe ni mwanangu?. Ukiachana na sisi kufanana maana hata Mimi na Mama yako tunafanana, una ushahidi gani mwingine?. Huyu ni mke wangu, ukitaka cheti Cha ndoa kipo, wasimamizi wapo. Wewe unachochote cha kuthibitisha wewe ni mwanangu?.
Mama yeye anacheka tu, wala hachangii chochote. Mshua najua alikuwa katika mood ya utani, lakini kwenye mood ile ile ya utani, nilikuwa na uhakika kile chakula siwezi kula, otherwise mood yake ingechange. Maana nakumbuka kipindi niko O level, Mshua alikuwa na kawaida ya kutupikia. Tukitoka shule tunakuta chakula tayari. Ilitokeaga nikasingiziwa mimba, Mshua alimaindigi kwamba anatupikia chakula (Mimi na mdogo wangu), tukishiba tunaenda kusumbua watoto wa watu. Alisema hatokaa atupikie tena maana tushakuwa vidume. Japa lile soo, baada ya mtoto kuzaliwa iligundulika sihusiki, ila Mshua aliendelea kunimaindi, yeye msimamo wake siku zote ilikuwa mwanamke hawezi kukusingizia mimba kama hujalala nae.
Nikaingia zangu jikoni kupika.
***** ****** *****
Siku zilisogea sana, nilikaa takriban mwezi na nusu. Mpaka jioni moja Mshua aliniomba tuongee mida ya usiku shughuli za nyumbani zikiwa zimepoa.
Siku hiyo hiyo, baada ya kula chakula cha usiku, tukaenda kukaa nje kwenye bustani. Tukiwa pale nje akaniuliza "Vipi unashida gani safari hii?"
Nilikaa kimya kwa muda, nilikuwa najaribu kutafakari, nianzie wapi kumuomba msamaha? Au nifunguaje haya mazungumzo?
Alivyoona nipo kimya sana, akabaki ananiangalia tu bila kusema chochote. Kisha akanyanyua simu yake, na kuniuliza:
Mshua: "Najua unatatizo, vipi niende ndani, alaf tuongee kwa njia ya simu?
Nikatabasam tu.
Analyse: "Nilionana na yule Mzee"
Mshua: "Aliniambia kuwa ulienda shambani kwake"
Analyse: "Kwanini hukuwa niambia yeye ni nani, au mipango uliyokuwa nayo juu yangu?"
Mshua: "Unadhani hiyo ingeweza kubadili kitu?"
Analyse: "Sio kubadili kitu tu, bali ingebadili maisha yangu yote"
Mshua: "Kwani sasa hivi huwezi kubadili hayo maisha yako?"
Analyse: "Sio kiwepesi kama ambavyo ingekuwa mwanzo"
Mshua: "Unapenda kufanya mambo kiwepesi au kwa njia ulizochagua wewe?
Analyse: "Hakuna anayependa kupita njia ngumu, ni matokeo tu ya machaguo yetu ndio yanaweza kutupitisha huko"
Akakaa kimya kwa muda. Alaf kabla hajaongea chochote, nikaona niutumie ule ukimya kumuomba msamaha.
Analyse: "Najua nimeku disappoint sana, nimefanya maamuzi mengi ambayo yameuvunja sana moyo wako na wangu. Ila...."
Kabla sijamalizia, akanikatisha.
Mshua: "Mimi ndio mwenye makosa hapa. Kama kuna anayetakiwa kuomba msamaha kwa kuivunja mioyo yetu, basi ni Mimi"
Akaendelea:
"Unajua katika maisha yangu, sikuwahi kabisa kufikiria kujiunga na jeshi. Ndoto na mipango yangu mingi ilikuwa sehemu nyingine kabisa. Mimi kujiunga na jeshi, ilikuwa ni ndoto ya Babu yako, yeye ndiye aliyenipush sana kuingia kule, japo nilikataa kwa nguvu zangu zote.
Kama ilivyokuwa kwako, nilivyomalizaga kidato cha nne, sikutaka kuendelea zaidi, nilitaka kuwa mfanyabiashara, ila Babu yako alitaka niendelee zaidi, ila kwa kupitia jeshini. Palitokea sintofahamu nyingi kati yetu, hadi ikapelekea Mimi kuondoka nyumbani na baadhi ya mifugo yake
Siku niliyorudi nyumbani, japo nilirudi na zaidi ya nilichoondoka nacho, ila Babu yako hakutaka kunipokea. Ilibidi wazee wa Kijiji wahusike katika kutupatanisha. Pamoja na adhabu ya bakora nilizopogwa mbele yao, Babu yako aliweka sharti la Mimi kujiunga na jeshi, hapo ndio ataweza kunisamehe kabisa na kunichukulia tena kama mwanae.
Sikuwa na jinsi, ilibidi nikubali, japo kutoka moyoni nilijenga chuki na yeye, kwa kunilazimisha kitu nisichotaka. Nilivyoingia jeshini, baada ya muda nikachaguliwa kwenda kozi Urusi. Hapo kidogo ndio nikaanza kulipenda jeshi. Kabla sijaondoka nchini, Babu yako akataka niache nimeoa kabisa. Hapo ukatokea ugomvi mwingine, maana sikuwa tayari kwa jambo lile kwa muda ule.
Nikaambiwa kama sipo tayari kuoa, basi inabidi niache nimechumbia. Pia nikakataa. Wakati najiandaa na safari, Babu yako akaniambia atamchumbia mwanamke kwa niaba yangu. Nikamwambia sitomtambua. Nikaondoka tukiwa hakuna maelewano mazuri.
Nilivyohitimu na kurudi Tz, nilikuwa sitaki kwenda kusalimia nyumbani, maana ningekabidhiwa mke ambae sio chaguo langu. Nilikuja kupata matatizo ya kiafya jeshini, kwa mara nyingine tena Babu yako akaingilia kati kinyume na matakwa yangu, nikajikuta rasmi nimetoka jeshini. Nilivyorudi nyumbani, mwanamke niliyechaguliwa na Babu yako, ndio akapewa jukumu la kuniuguza kwa ukaribu. Kitendo cha kuwa nae karibu kwa muda mwingi, kikajenga mazoea kati yetu. Nikajikuta naanza kumkubali."
Kufikia hapo nikaanza kujiuliza maswali, huyu mwanamke anayezungumziwa hapa ndio Mama yetu au? Ikabidi nimuulize,
Analyse: "Huyo mwanamke aliyekutafutia Babu, ndio Mama?"
Mshua: "Ndio. Kwani vipi?"
Analyse: (nikacheka kidogo) "Kumbe ulitafutiwa mke na Babu?"
Mshua: (akanikata jicho) "Acha dharau kijana, kuna baadhi ya mambo yako nje ya upeo ,huwezi kuelewa sawa?"
Nikawa, mpole, Kisha nikawa najizuia kucheka. Mwisho wa siku tukajikuta wote tunacheka [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].
Akaendelea na story:
"Kabla afya yangu haijatengamaa vizuri, ile biashara aliyopanga kunipa Babu yako, ikapata ajali ya moto. Nikajikuta sina kazi, Sina kiwanda. Hapo ndio hasira juu ya Babu yako zikazidi. Nikaamua kuondoka pale kijijini, na kwenda mbali nao kuanzisha maisha yangu mengine, kivyangu, bila wao. Mwaka 82 nikaamua kumuoa rasmi Mama yenu, kipindi ana ujauzito wa dada yenu.
Majukumu yalipozidi kuongezeka, ikabidi nisogee sehemu za mbali zaidi ili kutafuta kipato. Niliamini umri niliokuwa nao, ndio wakati sahihi wa kupambana. Hakuna sehemu katika hii nchi ambayo sijafika. Nimenusulika kufa mara kadhaa huko migodini, nilishawahi kufukiwa hadi na kifusi. Huu mguu niliomia kipindi nipo jeshini, katika harakati za utafutaji, umeshavunjika tena mara kadhaa. Lakini pamoja na yote hayo, sikufikiria ku-make peace na Babu yako.
Sikuwahi kuwasiliana nae wala kurudi tena pale kwake. Kwa muda mrefu nilikuwa nikimchukia kwa maamuzi aliyoyafanya juu yangu, maana ni kama yaliniharibia maisha. Nilitamani sana angesimama upande wangu, au kusimamia yale niliyojipangia, na sio kunilazimisha kuwa vile anavyoona yeye inafaa.
Ila Mwenyezi Mungu ana njia nyingi sana za kutuonesha mambo ambayo sio rahisi kuelezeka. Hata uwe na moyo mgumu kiasi gani, akiamua kukufikishia ujumbe wake, basi jua atakufikishia tu, hata kwa namna ambayo hukuitarajia
Baada ya miaka mingi kupita, chuki na hasira juu ya Babu yako zikiendelea kuwepo. Alikuwa akinitafuta na kunitumia barua kupitia kwa wafanyabiashara waliokuwa wanatembea vijiji kwa vijiji, ila sikuwahi kumuandikia chochote. Ujumbe wangu nilikuwa naurudisha kwa mdomo tu, japo wahusika waliufikisha.
Mwenyezi Mungu akaamua kunionesha jambo. Mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru wa nchi hii, ila macho yangu yangu yaliendelea kuwa gizani kwa muda mrefu.
Ile siku ambayo wewe uliyozaliwa, ndio siku ambayo macho yangu yalianza kuona. Ujio wako, ulifanya hasira zote nilizokuwa nazo juu ya Babu yako kufutika. Pengine usingezaliwa, ningeendelea kuwa kipofu, japo macho yangu hayakuwa na tatizo. Ningeendelea kuamini nipo sahihi"
Sikuelewa anamaanisha nini, ikabidi niendelee kumsikiliza. Hapo ndio akanifunulia kurasa za kitabu ambacho sikuwahi kukisoma kabla. Kurasa ambazo zilikipa thamani kubwa sana kile kitabu. Kurasa zilizofanya niyatazame baadhi ya mambo, kwa mtazamo tofauti kabisa....
Endelea hapa https://www.jamiiforums.com/threads...liyokutana-na-yule-mzee.2079499/post-46025799
Yule mama mwenye nyumba(mstaafu) mlipata kuonana au mmepoteana mazima? Mzee dingi/Kidevu/Mwanasheria feki na Kesho yetu nao ulipata kugongana nao?Mkuu, ya kuandika ni mengi sana. Vuta picha tokea story ya kwanza kuweka hapa JF, mpaka hii ya sasa. Zote zingekuwa ndani ya Uzi mmoja ingekuwaje? 😅😅😅
Nilichagua kuwa nasimulia kwa vipande, ili nisiwachoshe wasomaji, lakini pia na Mimi niwe napata time ya kufanya mambo mengine kwa Uhuru. Siunajua story ikianza humu JF, msimuliaji hutakiwi kuwa na excuses.
Worry out, next time nitakuja na kipande kingine cha kushare nanyi. 👊
Mwenzio anamiliki English medium skuli DaslamMkuu baada ya hapo ulifanikiwa kutoboa au bado ngoma ngumu?
Safi, nimepanda familia yenu inavyoishi hasa wewe na Mshua. Nimejifunza asante mkuu Analyse22nd Portion (Portion Finale)
.... Tuliongea mengi sana usiku ule. Ngoja nikusimulie machache ya alichonisimulia. Alisema hivi;
"Mpaka wewe unakuja kuzaliwa, kiuchumi walau nilikuwa vizuri kwa kiasi fulani. Yale maisha ya kwenda sehemu za mbali kukaa muda mrefu sababu ya utafutaji nilikuwa nishaachana nazo. Mimi kama mzazi, sikutaka kabisa kuwa kama alivyokuwa Babu yenu, sikutaka kuwa mkoloni na kulazimisha mfanye vitu ambavyo havikuwa kwenye maono yenu.
Nilikuwa naamini kama nitawasupport kwenye vitu mnavyotaka, basi kuna uwezekano mkubwa sana wa kupiga hatua nzuri kwenye maisha. Nilikuwa naamini nimepitia njia ngumu za utafutaji sababu ya kumsikiliza Babu yenu. Laiti ningefatisha njia zangu tokea awali basi nisingepitia msoto kama niliopitia.
Ulipoamua kukimbilia Dar es salaam, pale ndio alarm ililia kichwani kwa mara ya kwanza, ila nikaamua kuipuuzia, kwa kuangalia hata Mimi kuna kipindi kwenye maisha nilishapitia hali ile.
Kwa namna zangu ninazozijua Mimi, niliamua kukusupport katika njia uliyochagua. Kukupa Uhuru ndio jambo ninalojutia mpaka sasa. Niliamini utakuwa unajua kitu unachohitaji, na ndio maana niliamua kukusupport.
Nilikuja kushtuka ikiwa too late, kwamba upo kwenye harakati ambazo hata wewe mwenyewe hujui nini hasa unahitaji. Kibaya zaidi, ukajiingiza kwenye mapenzi. Mapenzi na utafutaji ni vitu ambavyo kamwe haviwezi kwenda pamoja, hata ungejaribu vipi. Ndio maana hata baada ya miaka michache ya kupambana kwako, bado ulirudi nyumbani mikono mitupu, kama ulivyoondoka.
Ile hela niliyokupaga kama mtaji, ilisababishwa na majuto niliyokuwa nayo. Sikujua nini nifanye kwa wakati ule, ndio maana nikakupa ile hela walau ukaendeleze ulichokuwa umeanza. Mimi kama Baba nilitakiwa kuwa mwongozo wako katika kila kitu, kitendo cha kukuachia mtoto uongoze, kimetuingiza wote shimoni.
Niliishi muda mrefu nikiwa na hasira na chuki kwa Babu yako, niliamini yeye ndio alivuruga maisha yangu na kuyafanya yawe magumu. Ila ujio wako, ulionesha ni Kwa kiasi gani sikuwa sahihi. Na pia ikawa wazi Babu yako alikuwa sahihi kwenye mengi.
Hakuwa perfect, ila kwa kiasi chake palikuwa na jema katika kila alilokuwa ananifanyia. Mfano mdogo angalia maisha yangu sasa hivi, vitu vingi nilivyofanya na kuhangaikia, sipo navyo. Hata nyie watoto, wote mmetawanyika, kila mmoja yuko anapojua yeye. Hata hizi mali pengine mpo mnazipigia hesabu, na pia sitokuwa na namna zaidi ya kuwarithisha. Nimebaki na kitu kimoja tu, ambacho hakuna anayefikiria kukichukua toka kwangu, nacho ni Mama yenu. Nimebaki na Mama yenu tu hapa. Cha kustaajabisha ni kwamba, Mama yenu nilichaguliwa na Babu yenu, ambae siku zote niliishi nikimlaumu. Sijui kama unanielewa?.
Nikatikisa kichwa tu kukubali.
Akaendelea:
"Siku niliyokutana na wewe ukiwa kama kibarua kule kwenye tangawizi, ndio siku niliyotambua ni Kwa kiasi gani nilimkosea Babu yenu. Maumivu niliyoyahisi moyoni mwangu,siwezi kuyaelezea. Na ndio yalinipa picha, ni kiasi gani nilimuumiza Babu yenu. Hakuna maumivu makubwa, kama pale unapochukiwa na mtu ambae upo tayari kufanya lolote kwa ajili yake.
Nasikitika jaribio la mfumo wa maisha niliokuwa nautamani, limefeli, kibaya zaidi limefeli katika hatua ambayo hatuwezi kurekebisha. Sasa ndio naamini, unaweza ukampenda sana mtu, ila katika namna ya kumuonesha upendo wako ukajikuta unaharibu. Na ubaya ni kwamba jamii haiangaliagi nia, inaangalia matokeo. Watahukumu kulingana na matokeo ya ulichofanya, hata kama nia yako ilikuwa njema.
Mpaka kufikia ile siku tunakutana kule, japo ukaribu na Babu yako ulikuwa umerudi, ila nilijihisi mkosefu upya. Ukaribu uliokuwa umerudi, ilikuwa ni ile naturally tu kama watu wazima tuliamua kusahau yaliyopita. Ila kwa jinsi nilivyojisikia siku ile nilipokuona, nilitambua kuwa natakiwa kumuomba msamaha Mzee wangu, namshukuru Mungu kwa kunipatia ile nafasi, sijui kama Babu yenu angekuwa ameshafariki ningejisikiaje. Hakuna mzazi anayependa kumuona mtoto wake akiteseka"
Kufikia hapa, Mshua akanyamaza kidogo. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilishuhudia Baba yangu akitokwa na machozi. Tulikuwa tumeangaliana, akainama chini, na Mimi nikaangalia pembeni. Hata kwenye misiba ambayo nilishawahi kuhudhuria na yeye akiwepo, sikuwahi kumuona akilia. Ila usiku ule Baba alilia mbele yangu.
Siwezi elezea nilijisikia vipi, ila itoshe kusema I felt so bad. Akaniambia "Kuwa strong haimaanishi hatuumii, ila pia chozi kutoka sio symbol ya udhaifu. Tuna wengi tunaowaangalia, ila ni wachache wanaotuangalia na kuyaelewa yale tunayoyabeba, hata kama hatujawaambia"
Baada ya ukiwa wa dakika kadhaa. Nikauvunja ule ukimya
Analyse: "Nadhani hata Mimi natakiwa kukuomba msamaha Mzee. Maamuzi yangu mengi ndio yametufikisha hapa Mimi na wewe"
Mshua: "Sio Kweli. Maamuzi yangu Mimi mengi ndio yametufikisha hapa. Mimi ndio niliamua uje duniani, Mimi ndio nilitakiwa kuendelea kukusimamia mpaka pale utakapokuwa kuwa tayari kuanzisha maisha yako. Sikutakiwa kukusikiliza, hakuna ubishi juu ya ilo. Niliteleza, na nimegundua nikiwa nimeshachelewa sana, sema wewe bado hujachelewa. Una nafasi kubwa ya kuweka mambo vizuri. Hasa yale yaliyonishinda Mimi."
Akaendelea;
"Unajua unapokuwa mtoto, unakuwa sharp katika vitu vingi sana, kasoro vision tu. Upeo na maono yanakuwa wazi kulingana na umri unavyoongezeka Kadiri unavyokua, ndivyo unavyong'amua makosa uliyokuwa ukiyafanya katika umri uliopita. Usikubali maono ya siku chache mbele, watakayokuwa nayo vijana wako, yaharibu mipango yako juu yao ya miaka mingi mbele. Ndio maana jukumu la mzazi ni kumsimamia na kumuongoza mtoto mpaka akue. Niliweza kukusimamia, ila nikashindwa kukuongoza"
Analyse: "Sawa nimekuelewa Mzee. Naamini kila kitu kitakaa sawa siku moja"
Mshua: "Sawa. Vipi huko mjini, mambo yako yanaendaje?"
Analyse: "Mambo ni magumu sana Mzee, kila siku napiga hatua moja mbele, mbili nyuma"
Mshua: "Na hivyo ndivyo maisha yalivyo siku zote, ugumu wa maisha upo ili kutukumbusha namna ya kuishi na watu au kuwa na shukrani pale tunapofanikiwa. Yakiwa mepesi sana tungejisahau"
Analyse: "Ni kweli, lakini, hao watu tunaotakiwa kuishi nao vizuri, mbona hawanijali kabisa?"
Mshua: "Hawakujali kivipi?"
Analyse: "Hata yule unayeona anaweza kukusaidia, nae hakupi kabisa ushiriakiano"
Mshua: "Bwana mdogo, siku zote nakwambia hakuna aliyezaliwa kwa ajili ya matatizo yako. Mtangulize Mungu siku zote. Hata yule unayeona anatakiwa akusaidie, na yeye kuna sehemu anahitaji kusaidiwa. Usipolielewa ilo, utamchukia kila mtu"
Akaendelea, "Hivi huwa unasali?".
Kwa macho makavu kabisa, nikamjibu "Ndio"
Akacheka, "Tabia ya mwanadamu huwa haijifichi, tokea umekuja hapa, hakuna siku ambayo hukukumbushwa na Mama yako kwenda kanisani. Unajiweka mbali sana na Mungu, hivi hizi Baraka anazokuombea Mama yako kila siku zitakufikia vipi?".
Nikabaki kimya. Akaendelea na punch zake;
"Jitihada bila Nuru, utazidi kupotea. Jiweke karibu na Mungu, kisha fanya mambo yako, ongea na watu, wapigie simu, omba kuonana nao hata kama hawataki, maana kwenye haya maisha tunawahitaji hata wale ambao hawatuhitaji"
Analyse: "Nimefanya hivyo sana Mzee, lakini hata wale waliokuwa rafiki zangu, hawapo tena karibu na Mimi kama zamani. Maisha yao yanaenda ila yangu yapo vile vile"
Mshua: "Ukisema hivyo unakosea sana, alafu utaonekana kama ni mbinafsi. Vipaumbele vinabadilika kadiri umri unavyosogea. Kama kuna watu ulikuwa unashinda nao siku nzima mkiongea na kufurahi, usitarajie wakishaoa/kuolewa au kuwa na watoto/familia, wataendelea kukupa uzito kama ilivyokuwa zamani."
"Hao unaowasema, jaribu siku kuwapigia simu alafu uone kama kuna atakayekukatia, mtaongea vizuri tu, na hata wasipopokea, waelewe. Hawajakutenga, ila kawaida umri unaambatana na majukumu. Ukilielewa ilo, hutoumia juu ya ukimya wao"
"Maisha yetu hayana tofauti na safari, mliopo kwenye safari moja ndio mtakutana ndani ya bus. Kuna bus la elimu, bus la kazi, bus la semina nk. Na kwenye hayo mabus, kila mmoja atashukia sehemu yake. Ikitokea mtu ameshuka, mtakie kila la kheri huko aendako maana safari yenu ya pamoja inaishia hapo. Ila ukitaka aendelee kuwepo, utajikuta unashukia njiani au unamlazimisha apitilize vituo. Huko mbeleni lazima hamtoelewana, kuna mmoja kati yenu hiyo safari ya kulazimishana itamchosha, maana utajaribu kumuonesha uzuri wa mandhari nje ya dirisha, ataangalia lakini mawazo yake yatakuwa kwingine, mwishowe atashuka. Sasa kwanini usingeacha ashuke wakati ule?"
"Mliyenae safari moja, hawezi kushukia njiani. Na atakayeshukia njiani huyo hampo safari moja."
"Unakumbuka kipindi mnakua jinsi wewe na ndugu zako mlivyokuwa na furaha hapa nyumbani?"
Analyse: "Ndio?"
Mshua: "Mbona siku ya harusi ya dada yako ulikuwa unacheza mziki kwa furaha sana, ingali ukijua sherehe ikiisha hatokuwa hapa tena?"
Analyse: (Kimya).
Mshua: "Kuna muda unatakiwa ufurahi pindi uwapendao wakiwa wanaondoka"
Akakaa kimya kidogo kisha akaniuliza: "Hivi ishawahi kutokea umekutana na mtu katika jambo fulani, mkapoteana, baada ya muda mkaja kukutana tena sehemu nyingine?"
Analyse: "Ndio, ishawahi kutokea Kwa watu niliosoma nao"
Mshua: "Nadhani walau utakuwa umenielewa sasa, mnaweza mkawa ndani ya bus moja, ila safari zenu ni tafauti. Uliyekutana nae shuleni, usilazimishe aendelee kubakia kwenye maisha yako, wakati kusoma mmeshamaliza."
Akaendelea; "Kwahiyo unapokuwa huko mjini, basi jitahidi sana unapokuwa kwenye mihangaiko yako. Japo unahitaji watu, lakini pia uwe selective kwa kiasi fulani. Pia usijiweke mbali sana na Mungu, kuna wakati anatushindia magumu mengi pasipo sisi kujua, jitahidi usifanye mambo yasiyompendeza".
Analyse: "Sawa Mzee, me nimekuelewa, nitajitahidi kubadilisha baadhi ya vitu na mitazamo yangu pia"
Mshua: "Itakuwa ni jambo la kheri, maana usipokuwa makini utashangaa miaka inaenda ila mambo yako yamesimama."
Analyse: "Ila Mzee, umeniambia nina wahitaji hata wale wasionihitaji. Ila hapo hapo unaniambia sitakiwi kulazimisha watu wabaki kwenye maisha yangu"
Akasikitika kidogo kisha akaniambia, "Kuna tofauti kubwa kati ya sehemu ya kujiegesha, na sehemu ya kuegemea. Usichanganye hizo sehemu mbili".
Nikabaki kimya tu namsikiliza huku najaribu kuabsorb maneno yake.
Tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha, lengo ikiwa ni kucatch up with our past. Mwisho wa siku nikamuuliza:
Analyse: "Ulisema nikirudi bila mwanamke, utaniozesha binti yeyote wa hapa kijijini, vipi kuna yeyote uliyenichagulia?"
Mshua (akatabasamu kidogo): "Siwezi kukuchagulia mke"
Analyse: "Kwann? Huoni utakuwa unaenda kinyume na alivyofanya Babu?"
Mshua: "Babu yako alijua naweza kurudi na mzungu, ndio maana akafosi kunitafutia mke. Ila wewe leta yeyote tu, sisi fresh" (Alafu akageuka nyuma kuangalia kama Mama yupo karibu)
Nikajikuta nacheka. Alaf akaniuliza
"Au unawaogopa wanawake huko mjini? Ukihitaji msaada wewe niambie"
Analyse: "Hao wote ambao niliokuwaga nao nimewapata vipi?
Mshua: "Siwezi jua, labda unatanguliza hela je?. Alafu zikiisha wanakuacha, unarudi huku kupumzika, tunajua unastress za maisha kumbe wanawake"
Wote tukaishia kucheka tu.
Mama akawa amekuja mpaka mlangoni, alafu akatuuliza "Mnahitaji chai?". Baba akajibu "Ndio"
Mama: "Analyse, njoo uchukue vikombe na chupa"
Mshua: "Siwezi kuandaliwa chai na huyu, haitokuwa tamu kama ikiandaliwa na wewe mke wangu"
Mama(akacheka) : "Sawa , basi ngoja niwaletee"
Mshua: "Ngoja tuje huko huko ndani, huku mazungumzo yameshaisha"
Mama: "Sawa"
Analyse: "Yani Mama na umri huo unakubali Baba anakuhadaa na vimaneno vyake?"
Mama: "Uongo wa mganga, ndio nafuu ya mgonjwa mwanangu" (Akacheka kisha akaingia ndani)
Nikafikiria kwa muda kidogo alafu nikamuuliza Mshua; "Kwahiyo chai isipoandaliwa na yeye haiwi tamu kwako?"
Mshua: "Mbona ulichofikiria, ni tofauti na ulichoniuliza?"
Nikastaajabu, anaongelea nini huyu Mzee? Amejuaje kama nilichomuuliza sicho nilichofikiria?. Ila kabla sijafungua mdomo wangu akaniwahi:
"Kuna muda binadamu wote ndivyo tulivyo"
Nikabaki namwangalia tu. Akanyanyuka, akanisogelea kidogo. Alivyofika usawa wangu, akaniambia "Unapokuwa mtoto, unatakiwa kumsikiliza mzazi wako. Unapokuwa mtu mzima, mnatakiwa kusikilizana wewe na mzazi wako, maana upeo wako pia unakuwa angavu na umekomaa. Ila kadiri miaka inavyozidi kusogea, wazazi wanatakiwa wakusikilize wewe mtoto wao, maana akili yao inakuwa tayari imechoka. Uwe umejiandaa au hujajiandaa, kuna siku nitatakiwa kukusikiliza mwanangu"
Akanipiga piga kwenye bega, kisha akaingia ndani.
Niliendelea kubaki pale nje kwa dakika kadhaa, nikifanya marejeo ya mazungumzo yetu. Kuna kitu nikagundua alikiongea kwa uwazi, ila nilichelewa kuking'amua. Kilivyokuwa wazi kwangu, nikajikuta nasikitika kwa tabasamu.
Nikanyanyua vitu na kuelekea ndani, tayari kwa kuanza chapter mpya ya maisha yangu.
*******************************************
Wakuu, kama ilivyo ada ya simulizi zangu. Lengo la hii story ilikuwa ni kuelezea mazungumzo yangu na yule Mzee wa Kongowe, niliamua kujumuisha na matukio yangu mengine walau kuweka uzito. Nashkuru kwa uwepo wenu tokea mwanzo mpaka sasa. Panapo majaaliwa, tukutane tena kwenye simulizi zijazo.
Wasalaam,
Analyse