Siku hizi Wadada wanaenda kupiga picha na mabegi Airport

Siku hizi Wadada wanaenda kupiga picha na mabegi Airport

Teko Modise

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2017
Posts
2,331
Reaction score
7,733
Yaani ukipita huko Instagram ndio utajua matatizo ya ajira pamoja na afya ya akili ni makubwa sana.

Wadada wa mjini a.k.a Maslay Queen wameibuka na kamtindo ka kwenda airport na mabegi makubwa kupiga picha na kupost Instagram ili kutafuta attention na aonekane yeye ni wa hadhi ya juu ili shughuli zake za ujasiriamali (kudanga) ziwe rahisi.

Mdada anatoka zake Kigogo sambusa au Buza kwa lulenge na begi lake kubwa kwenye daladala mpaka Kipawa airport anashuka anaenda pale nje Terminal 3 anapiga picha zake za kutosha anageuza zake nyumbani na kuedit picha zile kisha anazipost mtandaoni.

Afya ya akili ni tatizo kubwa sana linalokua kwa kasi hivi karibuni hasa kwa dada zetu hawa wa mjini.
 
Yaani ukipita huko Instagram ndio utajua matatizo ya ajira pamoja na afya ya akili ni kubwa sana.



Afya ya akili ni tatizo kubwa sana linalokua kwa kasi hivi karibuni hasa kwa dada zetu hawa wa mjini.
Wadogo zetu wakiona hizo picha plus picha za kwenye mahoteli wanachanganyikiwa na shule wanaona zinawachelewesha wakati watu wanakula maisha.

Mitandao inaweza kukufanya uhisi wewe ndiye umefail maisha peke yako unasubiri kamshahara ambako mtu ananunulia vocha
 
Kuna watu hua wana hekaheka jaman, mie tu kupiga picha kwa simu yangu ibaki tu kwenye simu naona hata siwezi. Kuna wakati hadi mtu akiniomba picha za wanangu inabidi nipige simu wanitumie. Nawaza huo muda wa kupanda daladala na begi kwenda kupiga picha ili tu nipost
 
Unaweza ona wajinga ila kuna mambwiga wanakamatika kipuuzi kama hivyo.

Jinga jinga na vihela vyake akiona mdada yupo airport anaongeza dau la kuhonga hivyo hivyo akidhani ni matawi ya kimataifa kumbe kuku ya kienyeji.

Pia huyo unaemuona mshamba ukute keshakunja mpunga wa maana toka kwa zee moja lipenda dogo dogo kwa ajili ya kwenda kufunga mzigo wa biashara ambayo haipo.
Hapo hapo ikiwa mmoja keshatoa hela ya mzigo kuna mwingine kupitia picha hizo hizo anatoa pesa ya kugombolea mzigo, ikimaanisha kwa bwana mmoja anakwenda safari na kwa mwingine karudi toka safari.

Wazungu wana kamsemo kao 'The end justifies the means'. Ikiwa mwisho wa siku dhamira ya kupata pesa imetimia, haijalishi ni njia gani ilitumika kupata pesa hizo. Mjinga hasa ni ile midume inayohonga kijinga jinga.
 
watu wa buza hawana mambo hayo kwanza wao ndio wapo karibu na eapoti

dada wa kigogo ashavaa kijora chake cha elfu sita hana muda huo

hao maslay queen wanakaa tabata kigamboni kinondoni

chumba kimoja wapo 17 chakula jitegemee high school
 
watu wa buza hawana mambo hayo kwanza wao ndio wapo karibu na eapoti

dada wa kigogo ashavaa kijora chake cha elfu sita hana muda huo

hao maslay queen wanakaa tabata kigamboni kinondoni

chumba kimoja wapo 17 chakula jitegemee high school
Hao kwa kupiga picha majumba ya watu sasa. Ukifanya kosa ukamualiaka kwako kumuondoa uje na grader.
 
Yaani ukipita huko Instagram ndio utajua matatizo ya ajira pamoja na afya ya akili ni kubwa sana.

Wadada wa mjini a.k.a Maslay Queen wameibuka na kamtindo ka kwenda airport na mabegi makubwa kupiga picha na kupost Instagram ili kutafuta attention na aonekane yeye ni wa hadhi ya juu ili shughuli zake za ujasiriamali (kudanga) ziwe rahisi.

Mdada anatoka zake Kigogo sambusa au Buza kwa lulenge na begi lake kubwa kwenye daladala mpaka Kipawa airport anashuka anaenda pale nje Terminal 3 anapiga picha zake za kutosha anageuza zake nyumbani na kuedit picha zile kisha anazipost mtandaoni.

Afya ya akili ni tatizo kubwa sana linalokua kwa kasi hivi karibuni hasa kwa dada zetu hawa wa mjini.
Marketing strategies mkuu
 
Back
Top Bottom