Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

halafu bado kuna watu wanashabikia eti kiswahili kiwe lugha ya kufundishia kindergatten mpaka chuo kikuu(ngazi ya PhD) AIBUUU
 
Hizi ishu za kingereza nakumbuka zile SR za udsm zishawahi nitoa jasho kwenye presentation za LT
 
Hizi ishu za kingereza nakumbuka zile SR za udsm zishawahi nitoa jasho kwenye presentation za LT
Halafu hizo kozi za LT zinakuwaga na mabinti wazuri ajabu, kijeba unaongea broken ili uonekane bab kubwa lakini katikati inayeyuka.
 
Halafu hizo kozi za LT zinakuwaga na mabinti wazuri ajabu, kijeba unaongea broken ili uonekane bab kubwa lakini katikati inayeyuka.
Mkuu we acha tu yaan mabinti wazuri halafu huyo Lecturer wa hyo kozi pia alikua ni seminar leader mwenyewe mama mmoja mzungu wa marekani, cku hyo moyo ulinidunda acha kabisa. Cku hyo ilikua ni vicheko coz wote ilikua mara yetu ya kwanza kupresent tukiwa first year
 
Mkuu we acha tu yaan mabinti wazuri halafu huyo Lecturer wa hyo kozi pia alikua ni seminar leader mwenyewe mama mmoja mzungu wa marekani, cku hyo moyo ulinidunda acha kabisa. Cku hyo ilikua ni vicheko coz wote ilikua mara yetu ya kwanza kupresent tukiwa first year
Bora unge-opt kozi za KISWAHILI (Vishazi & Vielezi) na mashairi ya kutosha.
 
hiz kura pia noma, kama kuna ticha mmoja wakati tupo o level walikuja wazungu kutoka marekani walileta vitabu, walimu wakawa wanajitambulisha paredi, maadam mmoja alisema 'my name is madaam sanga, am married by two childrens'
 
Kiingereza si mchezo wandugu,pale UDSM kuna Dr. Juma Kiduanga huwa anafundisha DS 101 kwa kweli Sijui huwa anafundisha nini darasani. Full kujing'ata haeleweki hata lugha gani huwa anaitumia.
Isinti tii
 
H⃟i⃟ h⃟i⃟ h⃟i⃟i⃟i⃟i⃟i⃟i⃟i⃟ #
K⃟i⃟t⃟h⃟u⃟n⃟g⃟u⃟ n⃟o⃟m⃟a⃟
 
Mimi first year nilikuwa sivaagi nguo nyeupe usiku za presentation ni mwendo Wa nyeusi tu , maana jasho linakuwa jingi balaa.
 
English ni lugha ya maigizo, ukitaka kuijua badilisha mwonekano wako yaani assume kama wewe ndo trump au ubama then unamwaga lecture vile, ila uwe na kijikaratasi cha kuibia pionti.
Mbona wale wamasai pale wanaongea kama wapo ulaya
 
yaani nikikutana na mtu ambae anataka tuongee kiingereza asee ni kama napewa adhabu
 
hiz kura pia noma, kama kuna ticha mmoja wakati tupo o level walikuja wazungu kutoka marekani walileta vitabu, walimu wakawa wanajitambulisha paredi, maadam mmoja alisema 'my name is madaam sanga, am married by two childrens'
hahahah mkuu nimecheka sana
 
Hatari sana....achana na kithungu cha mbele ya kadamnasi!!!.…..mbaya zaidi class kuwepo na wapenda sifa wasioelewa na maswali lukuki...patamu hapo unaweza omba ardhi ipasuke
 
Nakumbuka jamaa yangu aliniambia kwenye miaka ya 1990 waliomba kazi ya udereva kwenye shirika fulani la kimataifa hapa nchini, nafasi waliyokuwa wanataka ni mbili tu. Wakaitwa watu 6 kwenye interview, sasa jamaa mmoja akaitwa wa kwanza, hakuchukua muda akatoka...akawaambia wenzake huko ndani ni kingereza kitupu na kuna wazungu, jamaa yangu akaitwa wa pili, sema yeye alikuwa anajua kujieleza kiasi, anasema alipotoka nje hakukuta mtu hata mmoja, ina maana wale madereva walitimua mbio baada ya kusikia ndani ni English kwa kwenda mbele. Hivyo jamaa yangu akapata kazi kiulani peke yake, kwani hata yule wa kwanza alishindwa kabisa kuongea kingereza. Jamaa yangu akafanya kazi kwa miezi sita wakaridhishwa na utendaji wake, wakampa kazi ya kutafuta madereva wanaojua kingereza waajiriwe...

Kujua kingereza kuna raha yake....
hahahah mkuu yaani hapa mbavu sina
 
Kwa hiyo tumekubaliana kuwa [HASHTAG]#HAPA[/HASHTAG] KISWAHILI TU# hata wakija wageni wasijua kiswahili?
 
Enzi hizo Makongo high school pale, kulikuwa na kibao Speak English or French. Sasa ukifika pale getini unakutana na Ma-mp wanoko kishenzi,hapo ushachelewa,hakuna namna lazima utafute namna ya kujinasua vinginevyo kichura chura,kufyeka vitakuwa ni sehemu ya masomo yako siku hiyo,basi wajanja wakagundua njia,wala mamp walikuwa weupe,hawana shule,wakikukomalia unafunguka sentensi yoyote ile ya kiingereza na ujanja wao ulikuwa unaishia hapo. Basi kuna siku wakamdaka jamaa yetu kipindi hiko form njuka unajua definition na importance za masomo, MP :Aroo kwanini umechelewa? JAMAA : Transportation is a process of moving goods and services from one place to another MP : Hay kwenda ndani na kibao juu,hiyo ndio ilikuwa salama yake na hapo akawa katufungulia njia pale getini,ukiulizwa we unadefine chochote kile mpaka kuna denti alijisahau akatoa definition ya kemia bahati mbaya pembeni kuikuwa na mwalimu wa zamu,kilichomkuta yule dogo hawezi kusahau maisha yake yote [emoji23] [emoji23]
 
Enzi hizo Makongo high school pale, kulikuwa na kibao Speak English or French. Sasa ukifika pale getini unakutana na Ma-mp wanoko kishenzi,hapo ushachelewa,hakuna namna lazima utafute namna ya kujinasua vinginevyo kichura chura,kufyeka vitakuwa ni sehemu ya masomo yako siku hiyo,basi wajanja wakagundua njia,wala mamp walikuwa weupe,hawana shule,wakikukomalia unafunguka sentensi yoyote ile ya kiingereza na ujanja wao ulikuwa unaishia hapo. Basi kuna siku wakamdaka jamaa yetu kipindi hiko form njuka unajua definition na importance za masomo, MP :Aroo kwanini umechelewa? JAMAA : Transportation is a process of moving goods and services from one place to another MP : Hay kwenda ndani na kibao juu,hiyo ndio ilikuwa salama yake na hapo akawa katufungulia njia pale getini,ukiulizwa we unadefine chochote kile mpaka kuna denti alijisahau akatoa definition ya kemia bahati mbaya pembeni kuikuwa na mwalimu wa zamu,kilichomkuta yule dogo hawezi kusahau maisha yake yote [emoji23] [emoji23]
[emoji133] [emoji122] [emoji133] [emoji122] [emoji141] [emoji130] [emoji133] [emoji130] [emoji134] [emoji130]
 
Back
Top Bottom