Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?

Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Leo ni Siku ya Wanawake Duniani, katika safari ya kuelekea usawa wa kijinsia, kuna wanawake wengi wenye sifa na uwezo, lakini wamenyimwa fursa za kushika nafasi za juu kisiasa kutokana na nyingi ya nafasi hizo, kuhodhiwa na wanaume, katika kitu kinachoitwa "mfumo dume!"

Swali ni je, nafasi hizo za juu kisiasa zimeshikwa na wanaume kwa sababu hatuna wanawake wenye sifa, au zimeendelea kushikwa na wanaume kwa sababu ya mfumo dume tuu, nikimaanisha wanawake wenye sifa wapo, lakini hawajateuliwa kushika nafasi hizo?

Kufuatia kilio cha muda mrefu cha wanawake kunyimwa fursa, je ni kweli tunao wanawake wenye sifa na uwezo wa kutupeleka kwenye 50/50?. Hebu na tuanzie na wanawake wenye sifa za urais, je tunao?

Hebu tuwakumbuke the top ten female politicians in Tanzania, na nafasi wanazoshika! Je, wamefikaje hapo, kwa kupanda wenyewe, au wamebebwa ndipo wakafika hapo? Je, wana sifa za urais?
  1. Top No.1 ni Mhe. Samia Suluhu Hassan.
    Huyu mama ni very powerful in Zanzibar na miongoni mwa wanawake wachache wa shoka kutoka Zanzibar. Ni Mjumbe wa CC na NEC wa CCM.
    Very high profile woman from Zanzibar, baada ya kuhudumu kwa miaka 10 kwenye Baraza la Wawakilishi, ameingia Bunge la JMT for 5 years sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais. Ndiye alikuwa Makamo Mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Huyu ni presidential material, sasa ni kumuandaa kwanza kuwa rais wa Zanzibar kwa kumpumzisha Dr. Shein kipindi chake cha pili, kisha 2020 aje urais wa Muungano, ili hili ifanyike, itabidi, CCM iachane na ule utaratibu wake wa two terms za urais, kwasababu kusubiria 2025, kwa huyu mama itakuwa too little too late, age itakuwa imemtupa mkono.
  2. Gutrude Mongela-Huyu alikuwa Mwenyekiti wa ule mkutano maarufu wa Wanawake wa Beijing, na Spika wa Kwanza wa Bunge la Afrika. Huyu pia ni Mwanamke wa shoka. Yeye alifika kote huko kwa deserving. Ni presidential material, ila kwa siasa zetu za Tanzania, she is already a spent force!, age sio rafiki.
  3. Mhe. Anna Makinda- Huyu ni Spika wa Bunge la Tanzania- ameupata usipika kwa kubebwa na mbeleko ya jinsia, ukimlinganisha na spika Sitta aliyemtangulia, Mama Makinda anaonekana wazi amepwaya kwenye Uspika!, lakini likija suala la Urais wa JMT, Mama Makinda ni presidential material, anauweza sana urais, kwa sababu ni mtu mwenye msimamo usioyumba!. Maamuzi ya ki Raisi wa nchi, hayahitaji mijadala kama maamuzi ya Bunge, hivyo Mama Makinda ni predidential material.
  4. Dr. Asha Rose Migiro- Huyu ni top most high profile woman from Tanzania kwenye International arena, ni mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya Deputy SG wa Umoja wa Mataifa akimsaidia Ban Ki Moon, kwa sasa ni mjumbe wa CC ya CCM, na waziri wa sheria wa Tanzania. Amefika kote alikofika kwa deserving ya brain power, ndio the one and only female kupata 1st Class ya Sheria ya UDSM!. Lakini tukija kwenye u presidential material, she is presidential material interms of brain power, but she lack Presidential drive, anachotakiwa kufanya sio kusubiri Chama ndio kimpush, anatakiwa kuonyesha nia na kujitokeza, sio lazima kutangaza kuwa anautaka urais, ili asije kuingia vitani na wasaka urais, bali kujitokeza hadharani kusema yeye ni presidential material, ana sifa na uwezo, wakati wa kutangaza ukifika, atafikia maamuzi au atangaze kujitupa kwenye kinyanganyiro au laa!, na sio kukaa kimya kuisubiria mbeleko ya CCM kubebea watu kwa utaratibu ule wa "sasa ni zamu ya mwanamke!".
  5. Prof. Anna Tibaijuka
  6. Anna Abdallah
  7. Mary Nagu
  8. Hellen Kijo Bisimba
  9. Dr. Stagomena Tax Bamwenda
  10. tuendelee kuwataja wengine.
Natoa pongezi kwa wanawake hawa, na kufuatia wengi kupata nafasi hizo kwa upendeleo uwe ni wa mbeleko ya viti maalum, au affirmative action ya jinsia, kote huko ni kubwebwa! Ule msemo wa wanawake wakiwezeshwa wanaweza, nao ni mbeleko tu, hivyo kuelekea October, 2015, ili wanawake waonyeshe uwezo kuwa wanaweza, sasa ni wakati wa hao wanawake wenye uwezo, wajitokeze hadharani tuwaone kuanzia kwenye kugombea nafasi ya urais!, bado sijamsikia mwanamke yoyote akijitaja anaweza!, na atajitokeza, ukiachilia hawa wanaotajwa tajwa tu, huku wenyewe wamejificha jikoni.

Natoa wito kwa wanawake, kama ni kweli mna uwezo, jitokezeni kwenye urais, ili hata msiposimamishwa, angalau 2015, tuwe na makamo rais mwanamke, au Waziri Mkuu Mwanamke!

Paskali.
 
Kwa Tanzania kuongozwa na mwanamke bado sana jamii hapo inaogopa sio wanaume tu hata wanawake ukiwauliza mwanamke awe rais watakwambia hapana bado jamii haijapevuka vya kutosha kumpa mwanamke nafasi kubwa ya nchi kama rais.

Anagalia dini zetu hizi je zinampa mwanamke nafasi sawa na mwaname jibu hapana, angalia makabira yetu bado sana kumpa mwanamke nasafi sawa na mwanamme.
 
2. Gutrude Mongela-Huyu alikuwa Mwenyekiti wa ule mkutano maarufu wa Wanawake wa Beijing, na Spika wa Kwanza wa Bunge la Afrika. Yeye alifika kote huko kwa deserving. Ni presidential material, ila kwa siasa zetu za Tanzania, she is a spent force!

Pasco
 
Mwanamke amewahi kua kiongozi ktk maandiko yapii? Au mnakiuka misingi na muongozo ya alojuu? So wakuongoze ww nawanao et cku ya wanawake!
 
2. Gutrude Mongela-Huyu alikuwa Mwenyekiti wa ule mkutano maarufu wa Wanawake wa Beijing, na Spika wa Kwanza wa Bunge la Afrika. Yeye alifika kote huko kwa deserving. Ni presidential material, ila kwa siasa zetu za Tanzania, she is a spent force!.

Pasco
pasco
Tunatakiwa tumpime kwa kuangalia nafasi aliyoshika na je amefanya nini kuisaidia nchi

Mfano asha rose migiro huyu alipata nafasi kubwa sana ya kumsaidia katibu mkuu wa umoja wa mataifa lakini je huyu mama kafanya lipi la maana kwa nchi yake au kwa majukumu yake kama naibu katibu mkuu?jibu unakuta hapana hana lolote ni just empy sasa mtu kama huyu mkimpa kisa ni mwanamke unategemea nini?

Makinda ameziba mijadala yenye masilahi ya taifa hata hivyo hiyo nafasi kabebwa tu hana analofanya zaidi ya kulinda interest za waliomuweka
 
3. Dr. Asha Rose Migiro- Ni mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya Deputy SG wa Umoja wa Mataifa akimsaidia Ban Ki Moon, kwa sasa ni mjumbe wa CC ya CCM, na waziri wa sheria wa Tanzania. Amefika kote alikofika kwa deserving, tukija kwenye u predidential material, she is presidential material, anachotakiwa kufanya sio kusubiri Chama ndio kimpush, anatakiwa kuonyesha nia na kujitokeza, sio lazima kutangaza kuwa anautaka urais, ili asije kuingia vitani na wasaka urais, bali kujitokeza hadharani kusema yeye ni presidential material, ana sifa na uwezo, wakati wa kutangaza ukifika, atafikia maamuzi au atangaze kujitupa kwenye kinyanganyiro au laa!, na sio kukaa kimya kuisubiria mbeleko ya CCM kubebea watu kwa utaratibu ule wa "sasa ni zamu ya mwanamke!".

Pasco
 
"Wanawake wenye sifa za presidential material?" Duh kweli waandishi wa habari Tz ni janga kama cream ndio hii.
 
tukiangalia mwanamke ambaye amesimama mwenyewe bila kubebwa ni halima mdeee ni juhudi zake ndo zimemfikisha hapa alipo
Mkuu JME, nakubaliana na wewe, Mhe. Halima Mdee, amesimama mwenyewe, japo mwanzo alianza kwa kubebwa na mbeleko ya jinsia kupitia viti maalum, ukibebwa bebeka! alibebwa, akabebeka na sasa anajijeba mwenyewe which is very good! Na nikimuangalia pia ni presidential material, ila kwa mfumo dume uliomo Chadema, CUF na NCCR mageuzi, does she stand any chance kuchaguliwa kuwa mgombea wa UKAWA?!

Pasco
 
"Wanawake wenye sifa za presidential material?" uh kweli waandishi wa habari Tz ni janga kama cream ndio hii.
Mkuu Mautumbo, fault finding ni sehemu ya mjadala katika kuuboresha kuelekea kwenye perfection!, mentioning tuu faults, haisaidii, toa na corrective options.

Karibu.

Pasco
 
Mkuu JME, nakubaliana na wewe, Mhe. Halima Mdee, amesimama mwenyewe, japo mwanzo alianza kwa kubebwa na mbeleko ya jinsia kupitia viti maalum, ukibebwa bebeka!, alibebwa, akabebeka na sasa anajijeba mwenyewe which is very good!. Na nikimuangalia pia ni presidential material, ila kwa mfumo dume uliomo Chadema, CUF na NCCR mageuzi, does she stand any chance kuchaguliwa kuwa mgombea wa UKAWA?!

Pasco
Ni kweli kwa mfumo uliopo ni vigumu kwa halima kusimama hasa kwa sasa maana hata umri wake unamnyima fursa ya kuwa mgombea labda kwa chaguzi zijazo.
 
Pasco hao wanawake uliowataja kwa nafasi ya urais hawatoshi, labda kama tunataka kuandika historia kuwa Tanzania imewahi kuwa na rais mwanamke hapo sawa. Hii nchi ilivyo kwa sasa hao wanawake watapelekeshwa na mafisadi hadi utawaonea huruma na wao watabaki kulalamika tu.
 
Mwanamke amewahi kua kiongozi ktk maandiko yapii? Au mnakiuka misingi na muongozo ya alojuu? So wakuongoze ww nawanao et cku ya wanawake!

Kabla ya kuchangia sana huu uchache, tujiulize maaskofu, mapadre, Masheikh na Imam ni wangapi katika hawa mama zetu!? Tukipata majibu yake basi ndo tujadili kwa undani!

Dunia ina wakuu wa majeshi wangapi, tukipata majibu hapa ndo tujadili!
 
Mkuu Mautumbo, fault finding ni sehemu ya mjadala katika kuuboresha kuelekea kwenye perfection!, mentioning tuu faults, haisaidii, toa na corrective options.

Karibu.

Pasco

Wanawake wenye sifa za kuwa Rais wa Nchi.

Wakati mwingine tujaribu kuandika kwa lugha nyepesi inayoeleweka na wengi.
 
Wanawake wenye sifa za kuwa Rais wa Nchi.
Wakati mwingine tujaribu kuandika kwa lugha nyepesi inayoeleweka na wengi.
Mkuu Ngarna, presidential material sio sifa tuu za urais ni zaidi ya hapo!, na kuwa na sifa tuu za urais hakukufanyi uwe presidential material!.

Mfano sisi tumeweka sifa 5 kuu za urais
(a) Ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) Nmetimiza umri wa miaka arobaini;
(c) Ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(d) Anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe
wa Baraza la Wawakilishi,
(e) Katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali

Hivyo mtu yoyote akiishakuwa na sifa hizo, anaweza kuwa rais!, lakini kuwa na sifa hizo, hakumfanya kila mwenye sifa hizo kuwa ni presidential materials, na wakati huo huo tuna watu wenye vigezo vya presidential materials lakini hawana sifa kwa mujibu wa katiba, mfano Zitto ni presidential material lakini hana sifa!, tuna watu kibao ni presidential materials lakini sio wanachama wa chama chochote!

Pasco
 
Back
Top Bottom