Sikubaliani kabisa na hii Teua Teua ya Balozi kwa kila Mtu, kwani inatuaibisha na inadhalilisha pia Hadhi ya Neno Balozi kwa wenye Akili duniani

Hao wapambe ndio aliowazungumzia Nyerere kipindi anataka kung'atuka wakawa wanamwambia mzee endelea bdo kumbe mitumbo yao ndio walitaka waendelee kushiba
Kabisa. Wengi ni wale walioingia kwenye siasa kwa zali au kwa nguvu ya kupindua matokeo halali. Hawa watu ni nuksi sana hawa kwani wanajua hawawezi ushindani wa halali.
 
Uzi una logic sana
 
Aya ya mwisho ina point iliyoshiba
 
Kwa Kweli inashangaza sana!

Kuna vijana wasomi wamebobea kwenye hizo kazi lakini hawapewi nafasi wanakuja kupewa watu ambao wameshatumika na kuchoka!
 
Watu ambao hawana new vision ndio wanapewa hizo nafasi sijui hao washauri watu wa wanajiita wa system ndio wanaopelekea hali hiyo kweli?

Inamaana gani sasa?!

Totally demotivating!
 
Wanaenda kusoma gazette na kunywa kahawa ofisini. Hii nchi unaweza tukana ukaishia kukabidhiwa kwa kina kingai
 
Kwa hili umegonga ndipo!

Hii teuzi ya juzi.. ya sele dodo..yaani kuleeh..imeacha watu hoi.. .. huyu bi ... Anawajua vizuri anao wateua na Ana sababu zake.. dah!

Tutafika tu ..japokuwa tutakuwa tumechoka Sana..!

Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
 

Naona wana rambishana tu asali
 
Najaribu kuonesha ni aina ipi ya vichwa vinapaswa kuteuliwa kuwa balozi na sio kuzoa yeyote yule ilimradi kuonesha ushkaji na kulindana
Umenena vyema sina pa kukosa. Jingine anawazibia nafasi wakurugenzi walioandaliwa kwa jukumu hilo la kuwa balozi toka wizara ya mambo ya nje. Na hii inashusha hadhi ya 'Balozi' hasa kipindi hiki cha mama, amefanya uteuzi wa mabalozi kwa, kuwaogopa baada ya 'kuwatumbua'.
 
Very true ndio maana vijana wengi wanakulia pale foreign na wanakuwa groomed kisawasawa then wanakuja kupewa hizo nafasi hii inamaana lazima waive na wajue mambo ya kidiplomasia kwa mapana yake, haiingii akilini kila takataka lililoshindikana humu nchini ndio linatupwa kuwa balozi huu ni uhuni wa kiwango cha lami kabisa. Naunga mkono hoja balozi sio nafasi za failures.
 
Mheshimiwa balozi popoma nakuunga mkono katika hili.
Unakuta MTU ana damu mikononi au mbadhirifu kupindukia halafu anakwenda kuchafua nchi kwa ukilaza wake wakati huo huo kule nje anaitwa mheshimiwa balozi.
Kule nje tukipeleka Malaya, wezi, wauaji na vilaza, raia wa kule wanajua kwamba if this is their best, then waliobaki huko tz ni over vilaza.
 
Kumbe una bwama mightier
 
Ubalozi wa TZ ni wa kupeana michongo na ulaji tu.

Kuna watu wanapewa ubalozi baada ya kuonekana hapa nchini hawawezi fanya chochote.
 
Ubalozi umegeuzwa maficho ya wale wenye nafasi nono ambao wakibakia hapa idle bila jambo la kuwakeep busy wanaweza leta tatizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…