Sikuchagua Mkoa wa Kagera lakini wamenichagua Kagera ndiko nitafanya Oral interview Nauli 100,000

Sikuchagua Mkoa wa Kagera lakini wamenichagua Kagera ndiko nitafanya Oral interview Nauli 100,000

Habari

Kutoka kibaha Mpaka Bukoba nauli Laki Moja, kwenda kurudi Laki Mbili. Kula na Kulala tufanye elfu 60. Sikuchagua Kagera lakini wamenichagua kusudi ili nisiende. Nitatoa Wapi Laki tatu Mimi. Halafu hakuna uhakika kama nitapata au vipi. Nimekata tamaa
Wasiliana nao wakubadirishie ila kama current address yako ni Bukoba sahau kubadirishiwa.....
 
Pole kwa changamoto,ila uli update taarifa zako mapema katika Portal??na kama ulishafanya hivyo kwa wakati jaribu kuwasiliana na Utumishi Mapema pengine unaweza kupata msaada,pia kama utashindwa kupata msaada na una uhakika kuwa umejiandaa vyema jaribu kupambana kwa namna yoyote upate nauli ya kukuwezesha kufikahuko pengine inaweza kuwa nafasi yako.All the best
Hiyo huwa haibadiliki mkuu, hata uwasiliane!!!


. UTUMISHI hii kazi ya afya na walimu naona imewashinda... Wailudishe tu TAMISEMI
 
Kama kweli wewe ni candidate .

Pia jaribu kuwa unapitia nyuzi zako za nyuma ulizokuwa unaandika na kuponda walimu ambao wanajiandaa na usahili.



Gharama ya 300k ni kubwa Sana Ila naamini unaweza kusaidiwa na ukafikia lengo.

Next time jifunze kutumia mitandao vizuri hasa Kama kijana msomi .
Laki 3 nauli sawa hio kazi anayoenda kuipambania analipwa millioni ngapi?
 
Habari

Kutoka kibaha Mpaka Bukoba nauli Laki Moja, kwenda kurudi Laki Mbili. Kula na Kulala tufanye elfu 60. Sikuchagua Kagera lakini wamenichagua kusudi ili nisiende. Nitatoa Wapi Laki tatu Mimi. Halafu hakuna uhakika kama nitapata au vipi. Nimekata tamaa
Pole na hongera kwa kachaguliwa kufanya usaili.

Changamoto kama hii ilitokea kwa wale wa kada ya afya na ndio maana utumishi wakatoa wiki mbili za walimu kuthibitisha (confirm) mikoa husika ya machaguo yao.

Swali ni je wewe ulihakikisha kwamba mkoa husika uliochagua ndio wenyewe wakati ule fursa hiyo ilipotolewa?

Kama ulifanya hivyo na imetokea tofauti labda ujaribu kuwasiliana nao.
 
Back
Top Bottom