Sikuchagua Mkoa wa Kagera lakini wamenichagua Kagera ndiko nitafanya Oral interview Nauli 100,000

Sikuchagua Mkoa wa Kagera lakini wamenichagua Kagera ndiko nitafanya Oral interview Nauli 100,000

Habari

Kutoka kibaha Mpaka Bukoba nauli Laki Moja, kwenda kurudi Laki Mbili. Kula na Kulala tufanye elfu 60. Sikuchagua Kagera lakini wamenichagua kusudi ili nisiende. Nitatoa Wapi Laki tatu Mimi. Halafu hakuna uhakika kama nitapata au vipi. Nimekata tamaa
Hakuna kumwezesha mtanzania ajikwamue. Ni kuwekewa vikwazo tu Ili ashindwe. Inasikitisha sana
 
Nitasema hii kitu.

NGO moja ya kimataifa ilitangaza nafasi za kazi, posts zilikua zipo Arusha, Dom, Dar, Znz na Bunda.

Ofisi niliyokua najishikiza washkaji watano wakafanya test ya kwanza online wakapita kwenda oral. Katika hawa watano 2 walikua wamechagua Znz, mmoja Dom, mmoja Arusha na mwingine Bunda.

Yule jamaa wa Arusha anasema alikutana na binti ana begi la nguo, akamuuliza mbona una begi na hii ni oral tu. Binti akasema posts zishajazwa ni formality tu inafuatwa.

Wa Dom jina halikurudi.

Wa Znz akachaguliwa mmoja.

Wa Bunda anasema wamefika oral wapo 4 wakati posts ni 7, ila selection ilionyesha watafika 40.

Walivyofika waendesha interview wakawaita wote kwa pamoja wakawauliza mtakua tayari kufanya kazi huku? Wakajibu ndiyo wakaambiwa basi mmeshapita.

Mkirudi Dar pelekeni details zenu makao makuu, kama hauna passport katengeneze peleka, wakaomba details za mwajiri wakatuma background check form ya jamaa.

Yaani mshkaji alianza kujaza hizi deals wakati watu wengine wanasubiri majina ya walioitwa kazini. Hata mshkaji wa Znz akaanza kujaza baadaye kabisa wakati mshkaji wa Bunda alishamaliza kitambo.

Kama kuna lolote umeelewa hapa hongera
 
Toa pesa upate pesa.
kama kuna uhakika wa kupata hiyo sio tatizo, kwa scenario ya huyu kijana mimi naona kama kubeti tu, mimi namshauri aendelee kutafuta tu sehemu nyingine.
Siku zote akufukuzae hakuambii toka hiki ndicho nakiona kwenye huu uzi wa kijana
 
Sio roho tuu.. hata michango yake humu ndani ni very constructive ni moja ya vijana ambao wapo vyema upstairs.

🤣😂Sijawai ona mchango wake kwenye nyuzi za kula tunda kimasiara natania TU in JPM VOICE.
Unaroho nzuri sana
 
Ukifika Bukoba mjini pale round about utatembea dk 15 au 10
Mzee Umenikumbusha BK nilisoma kwenye Ile shule kongwe.

Hali ya hewa ya ubaridi nilitesekaga Sanaa.

Kule nilishuhudia radi zinapiga huku jua linawaka..

Kule ndio nilijifunza kula senene na parachichi...

Ooga wa kusafiri na vyombo vya maji ndipo ulinitokaga..kashai,nshambia,rwamishenye, kyaka irabo.
 
Back
Top Bottom