DIFFENDA
Senior Member
- Jun 23, 2013
- 124
- 53
DuDoctor shedy, kazingua
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
DuDoctor shedy, kazingua
mimi sitohi hata mia kama hutoposti tena baci stohi hata shilingi mojaSIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI[emoji15][emoji24] 39&40
"Mr Brighton[emoji848] hivi unadhani kama Clara ana mimba yangu nitakubali akahukumiwe, yani nikubali tu kirahisi mtu ahukumie hali ya kuwa ana kichanga changu tumboni[emoji16] haiwezekani kabisa" alisema Mr. Michael. "Kwa maana hiyo unataka kusemaje[emoji848]?" Nilimuuliza. "Ah mimi naona tu uachane na hizi habari za kumpeleka Clara kwenye kambi ya jeshi la marekani kwasababu kwa sasa Clara ni mama mtoto wangu mtarajiwa" alisema Mr. Michael "Wewe una uhakika gani kwamba mimba ya Clara ni ya kwako?" Nilimuuliza, wakati huo Clara alikuwa anacheka tu [emoji23] kwa jinsi tunavyobishana. "Sasa unataka tufanyaje?" Aliniuliza Michael. "Mi naona katika zile bilioni 20 ambazo ilitakiwa tugawane unipatie bilioni 10 nirudi zangu Tanzania kuhusu mimba mtajuana wenyewe iwe yako mama isiwe yako mimi sitaki kujua" Nilimwambia Mr. Michael. "Sasa kwani hizo bilioni 20 unazotaka tugawane ni zakwako ama ni za Clara alitoa kwenye account yake na kunipatia nifanye biashara kipindi nipo Oman?" Aliniuliza Michael na kuzidi kunipandisha hasira[emoji3525] "Sililiza Mr. Michael izo bilioni 20 tulizipata kwa kuuza meli ya mizigo ambayo tuliiteka, tena katika hizo bilioni 20 ilitakiwa tugawane watu watano, mimi Clara pamoia na watu wake watatu sasa inakuaje leo hii unaingilia suala ambalo hulijui kiundani?" Nilimuuliza Mr. Michael. "Wewe kwanza unazitaka hizi pesa za wizi ili zikusaidie nini, jipange urudi Tanzania laa sivyo nitakupa kesi kwanza upo kwenye nchi yangu huna pasport ya kusafiria halafu unataka kukoroma kwenye nchi za watu, tafuta kazi upate pesa za kurudi nchini kwako , mambo ya nchi yangu yaache kama yalivyo" alisema Michael, moyoni nikasema huyu hanijui, nilimpiga ngumi[emoji109] ya jicho la kushoto, kabla hajakaa sawa nilimrukia teke la tumbo alibamiza ukutani na kudondoka chini[emoji3525] nilimfuata palepale chini na kuanza kumshindilia ngumi za uso, damu zilianza kumtoa puani na masikioni, kwa hasira[emoji3525] alinisukuma kwa nguvu sana nikaanguka pembeni yeye akasimama, ile nataka kunyanyuka pale chini alinishindilia teke nzito la mbavu mpaka nikahisi bandama zimeoka, nilirudi tena chini, wakati najizoazoa pale chini ili nisimame tena alinirukia teke la uso kwa bahati nzuri kabla teke lile halijatua usoni kwangu nilifanikiwa kulidaka, alidondoka chini kama mzigo wa kuni.
Haraka nikamrukia juu yake, na kumkaba shingo yake kwa nguvu sana[emoji123] huku nikiichomoa pingu yake aliokuja nayo kwenye Luksi ya suruali yake nikafanikisha kunfunga mikono yake na ile pingu aliokuja nayo kisha funguo ya pingu nikaweka mfukoni kwangu, wakati huo Clara alokuwa amenitolea macho ya mshangao[emoji15] baada ya kuona nimefanikisha kumdhibiti Michael. "Nisikilize Michael haijalishi Clara ana mimba yako ama sio yako, Clara ni muhalifu na ni lazima ahukumiwe kwa mujibu wa sheria, lakini sasa naona na wewe unataka kumtetea muhalifu mtu aliyeua mamia ya watu kisa eti unahisi ana mimba yako, hapa brother umeyakanyaga lazima wewe na Clara wote wawili muhukumiwe" Nilimwambia Mr. Michael. "Ni sawa lakini unadhani ukitupeleka kwenye kambi ya marekani ndio utapata sifa kwa viongozi wa nchi, sasa kwa taarifa yako nchi ya marekani, mwafrika ama black amerika yoyote hata afanye vipi hawezi kuthaminiwa, wewe unadhani viongozi wa jeshi ni wapumbavu kiasi hicho wakubali wewe muafrica utangazwe shujaa kwa kumkamata jambazi aliyetesa nchi ile hali wao wapo?, kwanza watadharaulika na hata kuachishwa kazi kwa kigezo kwamba wanajeshi wa taifa kubwa kama la marekani wanashindwaje mbinu na mtu ambaye ni mtu mweusi isitoshe sio hata mwanajeshi brother kwa taarifa yako hutatangazwa popote zaidi ya kusifkusifiwa tu palepale kambini na kupewa kifuta jasho chako kisha watakuaga halafu wao ndio watajimwambafai kwa viongozi wa nchi kwamba wao ndio wamefanikisha kumkamata Clara, mimi naona uachane tu na hizi habari , nitakupa bilioni moja urudi nchini kwako hizo ni pesa nyingi pia" alisema Michael. "Acha janja janja wewe kwasababu nimeshakufunga pingu ndio unasema utanipa bilioni moja, lengo lako nishalijua unataka nikufungue pingu ili upate namna nyingine ya kunigeuka hilo haliwezekani acha nifanye mpango niwafikishe wewe na Clara marekani mengine tutajulia huko mbele[emoji848]" Nilimwambia Mr. Michael.
Nilifanya mpango wa kuwatafuta polisi wa palepale station ya treni na kuwaelezea kila kitu, lakini wao wakadai hawawezi kufanya lolote kwasababu Michael ni usalama wa Taifa na cheo chake kipo juu yao wenye mamlaka ya kumkamata Michael ni mahakama ya kijeshi pekee endapo Michael anahatia, hivyo labda kwa kunisaidia wapige simu makao makuu ya kambi ya jeshi la marekani niongee nao wao ndio watajua wapi waanzie, "Sawa hata kwa msaada huo nitashukuru" niliwaambia, basi wakapiga simu[emoji336] niliongea na viongozi wa kambi ya jeshi la marekani na kuwaeleza kwamba nimemkamata gaidi Clara na nipo station ya treni mjini Mexico hivyo nilihitaji msaada wao, sikuwaambia chochote kuhusu Michael maana ningewaambia kwamba nipo na Michael wangesema Michael atumie pesa ambazo alipewa kama adivansi ya kufanya upelelezi ili jambazi Clara apatikane, jambo ambalo Michael asingekubali sasa nikatumia mbinu huzo ili wakija wakute na Michael ninemfunga pingu, endapo wataniuliza sababu nitawajibu kwamba Michael alitaka kunigeuka ili ashirikiane na Clara kisa anahisi mimba aliyonayo Clara ni ya kwake. Basi waliahidi ndani ya masaa mawili watakuwa wamefika, nikakaa kusubiri. "Mr Brighton hii ni vita umeanzisha dhidi yangu na wewe, nitaachishwa kazi lakini na wewe sitakuacha salama" alisema Mr. Michael kwa kunipa maneno ya vitisho, sikumjibu kitu zaidi ya kumkalia kimya, hatimaye baada ya masaa mawili na dakika kadhaa kupita helicopter[emoji576] ya jeshi la marekani iliwasili, kwanza wanajeshi walishangaa sana baada ya kushuka kwenye helicopter na kukuta nimemfunga pingu mr Michael, walipouliza kulikoni niliwapa sababu kwamba Michael alitaka kunigeuka ili ashirikiane na Clara baada ya kuhisi Clara ana mimba yake hivyo nikamdhibiti Michael kwa kufanya vile ili Clara afikishwe kwanza kwenye vyombo vya dola maana ni muhalyeye "Hongera sana kijana wewe ni shujaa, Mr Michael kwanza umeenda kinyume na sheria za kuwa askari wa usalama wa Taifa, kwanz hutakiwi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na muhalifu, nafikiri suala hili litashughulikiwa na mahakama ya kijeshi tuondokeni" alisema mkuu wa kikosi kile cha jeshi kilichokuja kutoa msaada, tulipakia kwenye helcoper na safari ya kuelekea marekani ilianza, siku hiyohiyo, maamuzi juu ya Clara na Michael yalitolewa baaada ya kufika marekani. Ilitakiwa Clara ateswe kwa siku saba ndipo auwawe kwa kunyongwa lakini ilipobainika kwamba anamimba aliswekwa gerezani kwa miezi tisa mpaka ajifungue ndipo atasomewa tena mashtaka yake na atahukumiwa tena kwa mujibu wa vifungu vya sheria, Michael aliachishwa kazi kabisa kwa kujihusisha kimahusiano na muhalifu, hivyo mimi nilibaki kwenye kambi ya jeshi nikila bata tu[emoji16] huku nikisubiri Clara ajifungue ahukumiwe nipewe mavumba yangu nirudi TZD, Miezi tisa si haba Clara alishikwa na uchungu na kujifungua, ajabu Michael alituma barua za maombi kwenye ofisi kuu ya kambi ya jeshi akidai kwamba anataka tufanye vipimo vya DNA kati yangu na yeye ili ijulikane ni nani baba wa mtoto kati yangu na yeye, "[emoji848] Mh mara pap vipimo vya DNA vinaonyesha mtoto wa Clara ni wangu itakuwaje?" Niliwaza sana wakati huo tulikuwa tunasubiri majibu kutoka kwa daktari, baada ya lisaa daktari alituita wote ndani[emoji32]
Nyieeee! Nyieee acheni tu itakuwaje ? Like coment nije chaaaaap
SIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI[emoji15][emoji24] 40.
Baada ya daktari kukamilisha kufanya vipimo vyake ndani ya ofisi yake, alitoka nje na kutuita tuingie ndani kwa ajili ya kupokea majibu ya vipimo vya DNA, tuliingia ndani wote wanne, mimi, Clara, mr Michael pamoja na mtoto ambaye bado alikuwa hajapewa jina mpaka ajulikane baba yake[emoji17] tuliingia ndani na kukaa kwenye viti vilivyokuwa mbele ya meza ya doctor wakati huo mapigo ya moyo wangu yalikuwa yanapiga kite kuliko kawaida yake, nilisali kimoyomoyo matokeo ya DNA yaonekane mtoto sio wangu, Doctor yule mwenye asili ya kiafrika aliniangalia machoni na kuniuliza "Mbona wewe kama unatetemeka sana shida nini" nilimwangalia sura yake nikagundua doctor yule ni mpare nikamjibu kwa kipare "Henaicho ivyo vipimo vitidhe[emoji23]" Nilimuuliza kwa kipare nikimaanisha kwahiyo vipimo vinasemaje?. "Avae mwana ni wako[emoji16]" Doctor alinijibu kilugha kwamba mtoto ni wa kwangu "[emoji32]Weeee mvwire uu mndu iti mwana ni wake, ambu wekimvira iti ni wangu henevuka vita ambu uu jamaa emanje iti mwana ni wake nivonia huruma ili ni isanga la vandu[emoji24]" Nilimwambia doctor amwambie Mr. Michael kwamba mtoto ni wake, maana Mr Michael anajua mtoto ni wake ili tu niepushe shari na nipokee maokoto yangu mengine yatafuata baada ya kushika maokoto yangu. "Daktari mbona siwaelewi mnaongea kilugha halafu nasikia maneno kama huruma mnamaanisha nini sasa[emoji3525]" aliuliza Michael kwa ukali sana kwasababu kiswahili alikijua na isitoshe kuna maneno ya kilugha ambayo niliyatamka kiswahi kwa kutojua yanatamkwaje kilugha. "Ahhh unajua huyu jamaa kule kwetu Tz kimakabila ni mtani wangu sasa nimemwambia mtoto sio wake anasema eti nimuonee huruma maana anampenda sana Clara hivyo nikisema mtoto ni wake wewe utamuacha Clara hivyo atafanikiwa kuwa na Clara, na mimi siwezi kumwambia mtoto ni wake kamwe maana kwenye kazi hii nilikula kiapo" Doctor alimlaghai Mr. Michael kwa maneno ili mr. Michael asigundue chochote lakini ukweli ni kwamba mtoto alikuwa ni wangu ila nilicheza mchezo na Doctor na kumuahidi atapata malipo yake baada ya mimi kulipwa fungu langu.
Basi bwana Mr. Michael alifurahi sana [emoji16] baada ya kuambiwa mtoto ni wake, walikumbatiana na Clara kisha askari jela wa kike akamchukua Clara na kuondoka naye, akampeleka kizuizini ambapo alipewa muda wa kumlea mtito kwa miaka minne ili akuekue ndipo akabidhiwe baba yake Mr. Michael na ndiposa Clara ahukumiwe kwa mujibu wa sheria. Basi ilikuwa ni siku ya jumamosi kambi ya jeshi iliamuamua kunifanyia sherehe kubwa sana [emoji3059] kunipongeza kufanikisha kupatikana kwa Clara, na pia licha ya Mr. Michael kuachishwa kazi lakini alialikwa kwenye sherehe hiyo kusudi apewe pesa za mishahara yake ya huko nyuma ili aache kazi rasmi, hata hivyo kwa furaha ya moyo wangu nilimwalika Doctor shedy ambaye tulikula naye njama aseme mtoto ni wa Mr. Michael. Sherehe ilienda vizuri makomando wa kimarekani walionyesha uwezo wao wa kimazoezi mbele yangu mithili ya makomando wa kitandania wanavyoonyesha mbwembwe zao mbele ya muheshimiwa raisi[emoji16] wapo walioruka sarakasi, wapo waliolalia ncha za misumari kwa migongo yao, hakika walikomaa migongo kama ngozi ya mamba maana misumari ilikuwa mikali sana, hata hivyo wapo waliotua chini kwa kamba helcopter ikiwa angani juu sana, kiufupi bwana [emoji16] nilienjoy, tulikula na kusaza kwani sherehe ile ilihusishwa wanajeshi tu na hapakuwa na kiongozi wa serikalini na sijui kwanini walifanya vile hata hivyo sikutaka kuuliza nilichotaka ni kupata maokoto[emoji389][emoji385] yangu kwanza na sio vinginevyo, basi mkuu mpya wa vikosi vya jeshi akasimama kuhutubia kisha mbele ya halaiki ya watu niliwekewa bilioni 50 kwenye account yangu pesa ambayo ningekula mpaka kifo changu na bado ikabaki[emoji16], si hiyo tu pia kuna wanajeshi waliungana na kuchanga bilioni ishirini nayo ikawekwa kwenye account yangu, yani kiufupi wengi walifurahishwa na ushujaa wangu kutokana na kwamba sikupitia mazoezi yoyote yale ya jeshi hivyo waliona kama ni kipaji ambacho ninacho na ilistahili kupongezwa
Basi, baada ya kukabidhiwa pesa zangu, mr Michael naye alilipwa pesa zake na kuachishwa kazi paleple, alipewa siku tano awe amerudisha sare ya jeshi pamoja na maganbuti ya jeshi kwani kutoka wasaa ule yeye ni raia kama raia wengine, pia mkuu wa jeshi alinieleza kwamba iwapo kesho yake nitasafiri kurudi Tanzania basi nisisahau kuacha mawasiliano yangu maana mimi kwao ni kama ndugu na iwapo baada ya miaka minne kupita kama watanihitaji kwa ushahidi zaidi juu ta hukumu ya Clara basi nitatakiwa nirudi tena marekani nitoe ushahidi. Nilikubaliana naye na kumueleza kwamba nitatoa ushirikiano kadri ya uwezo wangu endapo watanihitaji, basi mchana tulikula na kusaza hatimaye usiku tukakusanyika kwenye bwalo kubwa la kijeshi ambapo wanajeshi walitakiwa kunywa na mimi vinywaji ili waniage kwa mara ya mwisho kwani kesho yake nilipanga kurudi TzD, Ndani ya bwalo pia Mr, Michael alikuwepo, hata Doctor shedy naye alikuwepo , watu walikunywa pombe balaa ila mimi nilikuwa soda, kwa kawaida wanajeshi vichwa ngumu sana hawalewi walikunywa mpaka saa sita usiku lakini bado walikuwa fiti, mimi nilikunywa tu maji kwa siku hiyo sikutaka kulewa lakini doctor Shedy alilewa mithili ya mlevi wa mataputapu, mara akaanza kuropoka mbele ya Mr. Michael na wanajeshi wengine [emoji15]...........
Kiruuuuuuuuuu je itakuwaje sasa hili nalo ni Tatizo[emoji23] acheni kwanza nimeze funda la soda niliyokuwa nakunywa maana imekwama kooni baada ya doctor Sheddy kuanza kubwabwaja.Nyieeee nyieeee acheni nirudi[emoji2099][emoji419]
Malizia kwa 500
Sitaendelea Tena kuipost lipia 500
Number 0784468229 Airtel money jina neema alafu njoo whatsp kwa namba hii hiii
Tatizo huwa hamumalizii story hadi inatia uvivu kuisomaSIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI[emoji15][emoji91]
Sehemu ya Kwanza ( 1 )
***************
KILA Mtu
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
Ilikuwa takribani siku nne zimekatika tangu nianze kumuona mwanaume kichaa nje ya jumba langu akiwa ameketi na makorokoro yake, siku ya kwanza niliogopa kidogo kwani alilala hapo na makorokoro yake mpaka kukakucha, siku ya pili pia alifanya hivyo lakini siku ya tatu nilianza kumuhisi vibaya maana vichaa wengi wamekuwa wakitumiwa na majambazi katika kazi zao atakuja karibu na nyumba yako atapiga kambi wewe utajua ni kichaa kumbe ni msoma ramani. Basi nikataka kwenda kunfukuza lakini roho yangu ilisita kwa woga kwani sura yake ilikuwa inatisha vibaya mno, rundo la nywele chafu lilijikusanya kichwani mwake na isitoshe alikuwa anavuta mamisokoto sijui ni bangi au ni gonzo mwenzenu nikajihami hata kumsogelea.
Basi bwana usiku wa siku hiyo kulinyesha mvua kubwa sana, mvua ilipokatika nikatoka nje na tochi kuzunguka nyumba yangu niangalie usalama maana sikuwa na mlinzi bali nilikuwa naishi mimi tu na mke wangu Clara ambaye ni mzungu, naye tulikutana tu hotelini miezi miwili iliyopita nikiwa kwenye safari zangu za kikazi nikamtongoza akaubali basi nikamkaribisha kwangu na mabegi yake niishi naye wakati tukiendelea kufanya mchakato wa kwenda kutambulishana kwa wazazi. Sikukagua mabegi yake kwani sisi waafrika mila zetu ni mwiko kukagua mabegi ya mgeni japo yalikuwa chumbani kwangu.
Basi bwana wakati nazunguka nyumba yangu huku nikitembeza mwanga wa tochi huku na kule ghafla nikamuona yule kichaa akiwa amekaa palepale anapopenda kukaa na alikuwa amenyeshewa na mvua vibaya mno, nikasema potelea mbali hata awe jambazi siwezi kuruhusu binadamu mwenzangu ateseke vile mimi nimelala ndani, kama anaiba aibe tu, mali hizi ni za kutafuta na tutaziacha duniani. Kwanza angekuwa jambazi asingekubali anyeshewe vile yule ni mwendawazimu" Nilijisemea nafsini mwangu na kwa huruma nikaenda kumchukua, lakini kuna kibegi chake chakavu na kilikuwa kimeloana sana aliking'ang'ania licha ya kumtaka akitupe lakini alikataa katakata, nikaona kubishana na chizi ni kujipa kazi nikamchukua vile vile na kibegi chake, nilienda kumuogesha vizuri bila kujali kwani wote ni wanaume, nilimpa nguo zangu safi avae usiku ule kisha nikamuonyesha chumba alale, aliingia chumbani na hakutaka kuachia kibegi chake nilijiuliza "Kwani hicho kibegi kina nini mbona huyu kichaa hataki kukiachia" nilijiuliza sana lakini mwisho niliona ni tabia ya vichaa kung'ang'ania vitu wanavyovipenda.
Basi nilipohakikisha yule kichaa Kalala na mimi nikarudi chumbani kwangu alipo Clara mke wangu ambapo alikuwa amelala tangu mchana, nilipoingia chumbani nikamkuta anajiandaa maana kuna baadhi ya siku alikuwa akitoka usiku kwa madai ya kwamba anaenda kumpa kampani rafiki yake wa kike kule hotelini asibaki mpweke nami sikuwa namkatalia maana huyo rafiki yake ambaye walikuwa wanakaa naye hotelini ndiye aliyeniruhusu niishi naye na hata siku nilipotoka safarini na Clara tulikuja na rafiki yake lakini yeye alifikia hoteli ya mtaa wapili na kwangu. Alidai ana mtu wake mara kwa mara anamtembelea hivyo anataka amkute hotelini na si kwa mtu.
Basi Clara alipoondoka usiku ule nikabaki na maswali kichwani mwangu." Huyu mwanamke licha ya mvua yote hii kunyesha lakini hajaona haja ya kulala hivi ni kweli huwa anaenda kwa rafiki yake? Na begi lake dogo kabeba mbona hili kubwa limetiwa kufuli kuna nini ndani yake? Mh[emoji848] huku kukaribisha watu usiowafahamu vizuri ndani na mabegi huku hapana?" Niliwaza kisha nikaenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli kitaalam maana kazi hizo niliziweza.
Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka, ile natupia macho ndani ya begi[emoji15] ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka [emoji15] kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nika.....
Niliyenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli kwenye begi la Clara ili nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli la watu kitaalam maana kazi hizo niliziweza. Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka mithili ya mtu aliyeshika kambale ambaye bado yupo hai, basi ile tu natupia macho ndani ya begi[emoji15] ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka [emoji15] kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nikaanza taratibu za kulirudishia lile kufuli kwa utaalam zaidi lakini wakati huo mtungo wa mawazo yalikuwa yakipenyeza kichwani kwangu sio kawaida.
"Mh huyu mwanamke anafanya kazi gani, mbona ana silaha kali hivi? au ni jambazi lakini mbona ni mpole vile na sura yake imejaa utashi wa kimahaba kiasi kile, hapana pengine kuna mtu anamtumia lakini jambazi hawezi kuwa na sura tamu kiasi kile" Niliongea mwenyewe kimoyomoyo na kujijibu mwenyewe kiufupi nilikuwa nimepagawa. "Lakini pengine huyu Clara ni jambazi nisijipe moyo kwa upole wake na mapenzi anayonipa kitandani nikamuona ni mwema laaaa hasha ! Hata simba ni hatari sana lakini kwenye mapenzi anatulia kama maji mtungini, hapa nisijipe moyo Brighton nimeangukia kwenye penzi la jambazi yani nimeyakanyaga kama sio kuyatimba" nilijisemea baada ya kumaliza kurudishia kufuli kwenye lile begi.
Nikakaa kitandani kisha nikavuta pumnzi ndefu na kushusha huku mkono ukiwa shavuni kwa mawazo "Mh na huyu kichaa ni kichaa kweli au geresha, kichaa gani anakubali kuogeshwa na apewe nguo nyingine avae bila kuleta utata wowote, sasa mbona na kile kibegi chake chakavu kilichonyeshewa na mvua ameking'ang'ania? kina nini ndani yake? Mbona sura yake ni kama mzungu chotara?
Kuna kitu si bure[emoji848] huenda ikawa huyu kichaa ni mpelelezi maana ndio kawaida yao unalikuta jitu linajidai chizi kumbe lipo kazini usione minywele ile ukasema chizi hapana ni askari wa usalama aliambiwa afuge manywele na mandevu maana kuna kazi anatakiwa kupewa miaka miwili badae hivyo anatakiwa awe katika muonekano wa kichaa. Inawezekana kabisa na huyu ni mpelelezi, anampeleleza Clara. Jamani Bryhton mimi si nitaambiwa nashirikiana na Clara wakati sijawahi kuiba hata kuku?" Niliwaza huku moyo ukinidunda vibaya mno.
Basi usiku huo wa manane nikatoka chumbani kwangu taratibu kwa mwendo wa kinyonga, nikaenda kusimama mlangoni mwa yule kichaa na kuaikilizia, nilimsikia akkoroma hapo nikabaini Kalala, basi nikajaribu kufungua mlango ajabu mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani na funguo, kidogo nikashangaa na kujiuliza " kichaa gani anafunga mlango kwa ndani au kuna taarifa gani anaficha zisijulikane?" Hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu. Basi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo.
Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu. Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile..... Jamani Nyieeee..... Nyiee acheni tu kwani baada ya kuzama ndani haraka nika.
" Mh kichaa gani anaetambua kwamba muda wa kulala mlango unatakiwa ufungwe kwa ndania? [emoji848]Hapana huyu si kichaa bali kuna kitu au ama taarifa anaficha zisijulikane?" Niliwaza na hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu na kujifanya kote ni kichaa si kichaa bali pale yupo kazini. Basi mimi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo. Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu.
Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile, huku nikitetemeka. Mara ghafla akaacha kukoroma[emoji15] haraka nikakichukua kile kibegi na kutoka nacho nje taratibu kisha nikasimama pale mlangoni kwa muda kidogo nikisikilizia kama ataamka ama laa, mara akaanza tena kukoroma, taratibu nikaufunga ule mlango kwa nje na funguo. Haraka nikaelekea chumbani na kile kibegi chakavu ambacho hata mtoto wa fukara hawezi kubebea madaftari maana kilichakaa mno.
Basi nilipofika chumbani nikaketi Kitandani na kukifungua kile kibegi, kwanza nilikuta mfuko wa plastick uliofungwa, hapo nikagundua mfuko ule ni kwaajili ya kuzuia mvua isiloanishe vitu vilivyopo ndani yake. Nikautoa ule mfuko nje na kuufungua, kwanza nilishangaa [emoji15] kukuta simu na vitabu viwili, kimoja likiwa ni cha katiba ya America. Nikaikagua ile simu ilikuwa na paswed na iliwekwa vibration, bado tomaso nikaendelea kukagua zaidi ndani ya kile kitabu cha katiba, nilikuta picha ya yule kichaa akiwa amevalia gwanda la Marekani lenye nyota tano, na alikuwa nazifu huwezi kumdhania.
Tomaso niliendelea kukagua huku mikono ikinitetemeka mithili ya mgonjwa wa degedege, nikakuta vitambulisho vingi, usalama wa Taifa na vitengo vingi ambavyo yule kichaa alipitia akiwa kama mtumishi Marekani, nikakuta pasport ya kusafiria na nakala kadhaa. "Mh Mungu wangu yani vitu vyote hivi muhimu asiwe na hata bastola ya kumlinda je akivamiwa maana vyote ni Orginal na sio copy[emoji848] au bastola kaitoa akaweka uvunguni? Inawezekana" Niliwaza huku nikiendelea kupekua pekua.
Na ndipo ghafla[emoji15] nikakutana na picha ya Clara imewekewa X na kwa nyuma iliandikwa "most wanted" yani anatafutwa kwa udi na uvumba, pia nikaona karatasi inayomuelezea Clara, macho yalinikodoka [emoji15] huku nikisoma, looo kumbe Clara ni jambazi kuu lililoua mamia ya watu nnchini Marekani yeye na mwenzake, pia akavunja mabenki mengi na kuiba pesa nyingi lakini haitoshi akamuua mtoto wa mbunge wa jimbo la California na ndipo akamua kutoroka yeye na mwenzake na inasemekana walitoroka na silaha kali walizoziiba kwenye kambi ya jeshi la kimarekani, Dah hakika nilikosa nguvu maana ni dhahiri zile silaha kwenye begi la Clara ndizo zilizoibiwa kwenye kambi ya jeshi la kimarekani.
"Mh Bryhton mie sasa nimeingia mkenge huku kushobokea wazungu hovyo na kukaribisha watu nisiowafahamu kwa undani nyumbani kwangu sasa kumeniweka pabaya sijui nifanyaje?[emoji848]" Niliwaza na hapo nikaamua nirudishe taratibu vitu vya yule kichaa chumbani kwake maana alionekana ni mtu hatari sana, kabla sijaamka kitandani pale nilipoketi ili nirudishe vitu vya watu mara [emoji15] nikamsikia akiongea kwa jazba chumbani kwake tena kwa kingereza "aaaa! Nimeibiwa aaaa hapana haiwezekani" aliongea mwenyewe huku akifungua ule mlango wa chumba chake kwa ufunguo kwani alikuwa na funguo yake tofauti na ile yangu ya ziada niliyotumia kwenda kuchukua kibegi chake ili nimpekue.
Wakati anafungua mlango wake, haraka nikakitupia kile kibegi uvunguni kwangu huku nikitetemeka mpaka meno. Mara nikamsikia akitembea kwenye korido ya kuja chumbani kwangu. Mweee! Mweee ! Mweee Nilizidi kutetemeka na kuhisi haja kubwa ghafla, mara mlango wa chumba changu ukagongwa [emoji15] hapo nika...
Acheni nirudi maana ingekuwa ni wewe tayari ungeshajinyea walahi?
Unajua nini kiliendelea hakikisha unapomaliza kusoma unalike na kucoment ili usipitwe na moto huu[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
Muendelezo soma: Sikujua kichaa anayelala nje ya jengo langu ni mpelelezi anayemtafuta gaidi wa Kizungu niliyemuoa bila mimi kujua ni gaidi
PamokoooooooSIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI[emoji15][emoji24]
Sehemu ya 43,44&45 MWISHO[emoji3578]
Nikiwa tayari nimekwishavalia baibui langu na nikabu ambayo iliyonifunika uso wote na kuacha sehemu ya macho🥷 nikajilaza kitandani huku nikiwaza ni kwa namna gani nitachomoka marekani nirejee tanzania bila jeshi la polisi la marekani kunitia nguvuni, wakati naendelea kujadiliana na serikali pamoja na bunge la kichwa changu mara ghafla[emoji15] nikasikia huko nje polisi wakiongea na muhudumu wa vyumba, walimueleza kwamba kuna muhalifu wanamtafuta hivyo wakamuomba CCTV camera [emoji327] ambayo ingenasa picha za watu wote waliowasili hotelini hapo, kwa bahati nzuri muhudumu aliwaeleza kwamba CCTV camera iliyokuwa inatumika hotelini hapo imeharibika, basi wakamwambia "basi sawa sio tabu hebu waamshe wateja wako wote tukague chumba hadi chumba" niliposikia kauli hiyo mwili wote ulianza kunitetemeka mpaka utumbo, kwani niljua ni lazima tu nitiwe nguvuni.
Basi nikakaa kimya nikingoja kitakachojiri, niliwasikia wakikagua chumba hadi chumba huku wakiwauliza wateja majina yao na sehemu walipotoka pamoja na kazi zao, waliuliza chumba hadi chumba walipofika kwenye chumba changu wakagonga mlango [emoji15] hapo nikajidai nimelala na ninakoroma kama paka aliye usingizini[emoji3] wakapiga mpaka simu ya mezani[emoji338] iliyokuwa mule chumbani, simu iliita mda mrefu lakini bado nilizidi kujikausha. "Mh huyu mtu vipi ni usingizi gani huo yani pamoja na kubamiza kote mlango kiasi hichi manusura uvunjike lakini bado yupo usingizini hapana huenda ndiye muhalifu mwenyewe kwani kwenye daftari na mteja wa chumba hichi ameandika jina gani" Askari alimuuloza muhudumu wa vyumba. "Ameandika George Nicholus" muhudumu alijibu. "Na ameandika ametoka wapi? Askari alimuuliza tena muhudumu. " Washngton Dc " muhudumu alimjibu askari kwamba natokea jiji la washton Dc lililopo hapohapo marekani, "Ni sawa lakini kama ni mwema kwanini ajikaushe asifungue mlango, je alikuwa ni mzungu au ni mwafrica" askari alizidi kumdodosa muhudumu. Swali hilo likawa mwiba kwangu kwani wakati naingia mpaka napewa chumba nilikuwa bado sijavalia yale mavazi tangu ya kujificha yani baiubui na nikabu🥷. "Ni mwafrica na anadai yeye ni mfanyabiashara wa madini" alijibu muhudumu. "Je ni huyu hapa kwenye picha" askari aliendelea kumuuliza muhudumu huku akimuonyeshea picha yangu. "Sina uhakika maana hapa nahudumia watu wengi na kuna vyumba zaidi ya mia mbili ishirini hivyo ni vigumu kukariri kila sura ya mteja anayeingia na kutoka" alisema muhudumu.
"Sawa kama ni mwafrica tunaomba tuvunje mlango, tutalipa gharama za mlango na ikiwa sio yeye tunayemtafuta pia tutamlipa gharama za usumbufu" alisema askari. Basi sawa" muhudumu alikubaliana nao. Moyoni nikasema "Kishanuka sasa hapa natembeza mkong'oto [emoji109]bila kujali ni nani atapita mbele ya macho yangu" niliongea kimoyomoyo huku nikiwa bado nimejilaza pale kitandani wakati huo mlango wakiendelea kuvunja mlango, mlango ulipofunguka nikajifanya nimekurupuka kitandani mfano wa mtu aliyekuwa anaota ndoto mbaya akashtuka na kupiga kelele. Tena nilipiga kelele kwa kuigiza sauti ya kike[emoji32] "Heee mbona sasa ni mwanamke yupo na kwenye daftari amejiandikisha mwanaume. Aliuliza askari na nilikuwa hodari wa kuigiza sauti ya kike haswa yani Joti wa kutokea Tanzania akasome. "Wewe dada kulikoni umejiandikisha jina la kiume ile hali wewe ni mwanamke" askari alianza na swali hilo. "Mimi nilikuwa na mume wangu tulikuja hapa kuenjoy kama wapenzi ila ameitwa kazini maana yeye ni mfanyabiashara wa madini na yeye ndiye aliyejiandikisha kwenye kitabu" Nilijibu. "Hebu kwanza toa hiyo nikabu yako sisi tunataka tuongee na mtu ambaye tunaona sura yake" alisema askari. "Kaka dini yangu hairuhusu" nilijibu kwa kulegeza sauti. "Dada acha kuleta mambo ya udini kwenye serikali toa nikabu yako haraka sana[emoji17] usituletee udini wako hapa kila mtu ana imani yake lakini tuwapo kwenye mambo ya kiserikali wote tuwamoja na pia wewe unaonekana ni muhalifu tu kwasababu utalalaje na hizo nguo [emoji848]"
Alisema askari. Kabla hajakaa sawa nilimchopu ngumi[emoji109] ya kidevu, alianguka pembeni haraka nikashika kiti kilichokuwa mule chumbani, nikaanza kuwatembezea wenzanzake kwa kuwatwanga nacho vichwani, yani kila aliyejileta aliambulia kiti cha kichwa, nilipopata tu kaupenyo sikutaka kung'oja nnzi wajae[emoji12] nilichomoka mbio na kuanza kukimbia, baadhi walinikimbiza lakini walishindwa kunipata, asubuhi yake nilienda uwanja wa ndege nilikata pasport ya kusafiria ambayo ilikuwa na jina la kike, nilisafiri mpaka uturuki na huko nilobadili sura yangu na kuwa ni ya mwanaume ambaye ni chatara mwenye asili ya kizungu na africa kisha nikakata pasport tena ya kusafiria na kurudi Tanzania, iliniwia vigumu ndugu za kunielewa lakini sauti pamoja na kuwatambua ndugu wote wa ukoo pamoja na kuwatajia majina yao hadi waliokufa viliwafanya waniamini, hata hivyo nilihama nilipokuwa naishi kuhamia kijijini kabisa ambapo kwa sasa nimejiwekeza katika biashara mbalimbali ila kiuhalisia natumia sura ambayo sio yangu. Yote yote pia nimejifunza kutokuwakaribisha watu nisiowafahamu vizuri nyumbani kwangu .
MWISHO SEASON 02!!!
Title ya story tu inabore. Hakuna ubunifu ni ya kitoto. Haina mvuto.SIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI😳🔥
Sehemu ya Kwanza ( 1 )
***************
KILA Mtu
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Ilikuwa takribani siku nne zimekatika tangu nianze kumuona mwanaume kichaa nje ya jumba langu akiwa ameketi na makorokoro yake, siku ya kwanza niliogopa kidogo kwani alilala hapo na makorokoro yake mpaka kukakucha, siku ya pili pia alifanya hivyo lakini siku ya tatu nilianza kumuhisi vibaya maana vichaa wengi wamekuwa wakitumiwa na majambazi katika kazi zao atakuja karibu na nyumba yako atapiga kambi wewe utajua ni kichaa kumbe ni msoma ramani. Basi nikataka kwenda kunfukuza lakini roho yangu ilisita kwa woga kwani sura yake ilikuwa inatisha vibaya mno, rundo la nywele chafu lilijikusanya kichwani mwake na isitoshe alikuwa anavuta mamisokoto sijui ni bangi au ni gonzo mwenzenu nikajihami hata kumsogelea.
Basi bwana usiku wa siku hiyo kulinyesha mvua kubwa sana, mvua ilipokatika nikatoka nje na tochi kuzunguka nyumba yangu niangalie usalama maana sikuwa na mlinzi bali nilikuwa naishi mimi tu na mke wangu Clara ambaye ni mzungu, naye tulikutana tu hotelini miezi miwili iliyopita nikiwa kwenye safari zangu za kikazi nikamtongoza akaubali basi nikamkaribisha kwangu na mabegi yake niishi naye wakati tukiendelea kufanya mchakato wa kwenda kutambulishana kwa wazazi. Sikukagua mabegi yake kwani sisi waafrika mila zetu ni mwiko kukagua mabegi ya mgeni japo yalikuwa chumbani kwangu.
Basi bwana wakati nazunguka nyumba yangu huku nikitembeza mwanga wa tochi huku na kule ghafla nikamuona yule kichaa akiwa amekaa palepale anapopenda kukaa na alikuwa amenyeshewa na mvua vibaya mno, nikasema potelea mbali hata awe jambazi siwezi kuruhusu binadamu mwenzangu ateseke vile mimi nimelala ndani, kama anaiba aibe tu, mali hizi ni za kutafuta na tutaziacha duniani. Kwanza angekuwa jambazi asingekubali anyeshewe vile yule ni mwendawazimu" Nilijisemea nafsini mwangu na kwa huruma nikaenda kumchukua, lakini kuna kibegi chake chakavu na kilikuwa kimeloana sana aliking'ang'ania licha ya kumtaka akitupe lakini alikataa katakata, nikaona kubishana na chizi ni kujipa kazi nikamchukua vile vile na kibegi chake, nilienda kumuogesha vizuri bila kujali kwani wote ni wanaume, nilimpa nguo zangu safi avae usiku ule kisha nikamuonyesha chumba alale, aliingia chumbani na hakutaka kuachia kibegi chake nilijiuliza "Kwani hicho kibegi kina nini mbona huyu kichaa hataki kukiachia" nilijiuliza sana lakini mwisho niliona ni tabia ya vichaa kung'ang'ania vitu wanavyovipenda.
Basi nilipohakikisha yule kichaa Kalala na mimi nikarudi chumbani kwangu alipo Clara mke wangu ambapo alikuwa amelala tangu mchana, nilipoingia chumbani nikamkuta anajiandaa maana kuna baadhi ya siku alikuwa akitoka usiku kwa madai ya kwamba anaenda kumpa kampani rafiki yake wa kike kule hotelini asibaki mpweke nami sikuwa namkatalia maana huyo rafiki yake ambaye walikuwa wanakaa naye hotelini ndiye aliyeniruhusu niishi naye na hata siku nilipotoka safarini na Clara tulikuja na rafiki yake lakini yeye alifikia hoteli ya mtaa wapili na kwangu. Alidai ana mtu wake mara kwa mara anamtembelea hivyo anataka amkute hotelini na si kwa mtu.
Basi Clara alipoondoka usiku ule nikabaki na maswali kichwani mwangu." Huyu mwanamke licha ya mvua yote hii kunyesha lakini hajaona haja ya kulala hivi ni kweli huwa anaenda kwa rafiki yake? Na begi lake dogo kabeba mbona hili kubwa limetiwa kufuli kuna nini ndani yake? Mh🤔 huku kukaribisha watu usiowafahamu vizuri ndani na mabegi huku hapana?" Niliwaza kisha nikaenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli kitaalam maana kazi hizo niliziweza.
Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka, ile natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nika.....
Niliyenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli kwenye begi la Clara ili nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli la watu kitaalam maana kazi hizo niliziweza. Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka mithili ya mtu aliyeshika kambale ambaye bado yupo hai, basi ile tu natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nikaanza taratibu za kulirudishia lile kufuli kwa utaalam zaidi lakini wakati huo mtungo wa mawazo yalikuwa yakipenyeza kichwani kwangu sio kawaida.
"Mh huyu mwanamke anafanya kazi gani, mbona ana silaha kali hivi? au ni jambazi lakini mbona ni mpole vile na sura yake imejaa utashi wa kimahaba kiasi kile, hapana pengine kuna mtu anamtumia lakini jambazi hawezi kuwa na sura tamu kiasi kile" Niliongea mwenyewe kimoyomoyo na kujijibu mwenyewe kiufupi nilikuwa nimepagawa. "Lakini pengine huyu Clara ni jambazi nisijipe moyo kwa upole wake na mapenzi anayonipa kitandani nikamuona ni mwema laaaa hasha ! Hata simba ni hatari sana lakini kwenye mapenzi anatulia kama maji mtungini, hapa nisijipe moyo Brighton nimeangukia kwenye penzi la jambazi yani nimeyakanyaga kama sio kuyatimba" nilijisemea baada ya kumaliza kurudishia kufuli kwenye lile begi.
Nikakaa kitandani kisha nikavuta pumnzi ndefu na kushusha huku mkono ukiwa shavuni kwa mawazo "Mh na huyu kichaa ni kichaa kweli au geresha, kichaa gani anakubali kuogeshwa na apewe nguo nyingine avae bila kuleta utata wowote, sasa mbona na kile kibegi chake chakavu kilichonyeshewa na mvua ameking'ang'ania? kina nini ndani yake? Mbona sura yake ni kama mzungu chotara?
Kuna kitu si bure🤔 huenda ikawa huyu kichaa ni mpelelezi maana ndio kawaida yao unalikuta jitu linajidai chizi kumbe lipo kazini usione minywele ile ukasema chizi hapana ni askari wa usalama aliambiwa afuge manywele na mandevu maana kuna kazi anatakiwa kupewa miaka miwili badae hivyo anatakiwa awe katika muonekano wa kichaa. Inawezekana kabisa na huyu ni mpelelezi, anampeleleza Clara. Jamani Bryhton mimi si nitaambiwa nashirikiana na Clara wakati sijawahi kuiba hata kuku?" Niliwaza huku moyo ukinidunda vibaya mno.
Basi usiku huo wa manane nikatoka chumbani kwangu taratibu kwa mwendo wa kinyonga, nikaenda kusimama mlangoni mwa yule kichaa na kuaikilizia, nilimsikia akkoroma hapo nikabaini Kalala, basi nikajaribu kufungua mlango ajabu mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani na funguo, kidogo nikashangaa na kujiuliza " kichaa gani anafunga mlango kwa ndani au kuna taarifa gani anaficha zisijulikane?" Hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu. Basi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo.
Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu. Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile..... Jamani Nyieeee..... Nyiee acheni tu kwani baada ya kuzama ndani haraka nika.
" Mh kichaa gani anaetambua kwamba muda wa kulala mlango unatakiwa ufungwe kwa ndania? 🤔Hapana huyu si kichaa bali kuna kitu au ama taarifa anaficha zisijulikane?" Niliwaza na hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu na kujifanya kote ni kichaa si kichaa bali pale yupo kazini. Basi mimi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo. Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu.
Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile, huku nikitetemeka. Mara ghafla akaacha kukoroma😳 haraka nikakichukua kile kibegi na kutoka nacho nje taratibu kisha nikasimama pale mlangoni kwa muda kidogo nikisikilizia kama ataamka ama laa, mara akaanza tena kukoroma, taratibu nikaufunga ule mlango kwa nje na funguo. Haraka nikaelekea chumbani na kile kibegi chakavu ambacho hata mtoto wa fukara hawezi kubebea madaftari maana kilichakaa mno.
Basi nilipofika chumbani nikaketi Kitandani na kukifungua kile kibegi, kwanza nilikuta mfuko wa plastick uliofungwa, hapo nikagundua mfuko ule ni kwaajili ya kuzuia mvua isiloanishe vitu vilivyopo ndani yake. Nikautoa ule mfuko nje na kuufungua, kwanza nilishangaa 😳 kukuta simu na vitabu viwili, kimoja likiwa ni cha katiba ya America. Nikaikagua ile simu ilikuwa na paswed na iliwekwa vibration, bado tomaso nikaendelea kukagua zaidi ndani ya kile kitabu cha katiba, nilikuta picha ya yule kichaa akiwa amevalia gwanda la Marekani lenye nyota tano, na alikuwa nazifu huwezi kumdhania.
Tomaso niliendelea kukagua huku mikono ikinitetemeka mithili ya mgonjwa wa degedege, nikakuta vitambulisho vingi, usalama wa Taifa na vitengo vingi ambavyo yule kichaa alipitia akiwa kama mtumishi Marekani, nikakuta pasport ya kusafiria na nakala kadhaa. "Mh Mungu wangu yani vitu vyote hivi muhimu asiwe na hata bastola ya kumlinda je akivamiwa maana vyote ni Orginal na sio copy🤔 au bastola kaitoa akaweka uvunguni? Inawezekana" Niliwaza huku nikiendelea kupekua pekua.
Na ndipo ghafla😳 nikakutana na picha ya Clara imewekewa X na kwa nyuma iliandikwa "most wanted" yani anatafutwa kwa udi na uvumba, pia nikaona karatasi inayomuelezea Clara, macho yalinikodoka 😳 huku nikisoma, looo kumbe Clara ni jambazi kuu lililoua mamia ya watu nnchini Marekani yeye na mwenzake, pia akavunja mabenki mengi na kuiba pesa nyingi lakini haitoshi akamuua mtoto wa mbunge wa jimbo la California na ndipo akamua kutoroka yeye na mwenzake na inasemekana walitoroka na silaha kali walizoziiba kwenye kambi ya jeshi la kimarekani, Dah hakika nilikosa nguvu maana ni dhahiri zile silaha kwenye begi la Clara ndizo zilizoibiwa kwenye kambi ya jeshi la kimarekani.
"Mh Bryhton mie sasa nimeingia mkenge huku kushobokea wazungu hovyo na kukaribisha watu nisiowafahamu kwa undani nyumbani kwangu sasa kumeniweka pabaya sijui nifanyaje?🤔" Niliwaza na hapo nikaamua nirudishe taratibu vitu vya yule kichaa chumbani kwake maana alionekana ni mtu hatari sana, kabla sijaamka kitandani pale nilipoketi ili nirudishe vitu vya watu mara 😳 nikamsikia akiongea kwa jazba chumbani kwake tena kwa kingereza "aaaa! Nimeibiwa aaaa hapana haiwezekani" aliongea mwenyewe huku akifungua ule mlango wa chumba chake kwa ufunguo kwani alikuwa na funguo yake tofauti na ile yangu ya ziada niliyotumia kwenda kuchukua kibegi chake ili nimpekue.
Wakati anafungua mlango wake, haraka nikakitupia kile kibegi uvunguni kwangu huku nikitetemeka mpaka meno. Mara nikamsikia akitembea kwenye korido ya kuja chumbani kwangu. Mweee! Mweee ! Mweee Nilizidi kutetemeka na kuhisi haja kubwa ghafla, mara mlango wa chumba changu ukagongwa 😳 hapo nika...
Acheni nirudi maana ingekuwa ni wewe tayari ungeshajinyea walahi?
Unajua nini kiliendelea hakikisha unapomaliza kusoma unalike na kucoment ili usipitwe na moto huu🔥🔥🔥🔥🔥
Muendelezo soma: Sikujua kichaa anayelala nje ya jengo langu ni mpelelezi anayemtafuta gaidi wa Kizungu niliyemuoa bila mimi kujua ni gaidi
Kweli naona umejanjaruka. Wewe ulikuwa huishi kuandika nyuzi za kutusema wapemba.... Na ukasimulia kile kisa cha mpemba kukutunuku gari. Leo unaona kutukana ndo ujanja wa mjini? Hewallah sheikh. Inshallaah... Ila kumbuka bado hujamaliza safari sheikh.... Wewe mjini tumekuingiza sisi, tumekupokea na kukupa hadi gari.... Leo hii umekuwa mjanja wa matusi? Nawe eti unajua kitu.... Umesahau kuwa umekaa home kwa Ami Yusufali ukimhudumia? Na ulisema humu mwenyewe? 😁Bado unataka Mwanzi?
Nimekuuliza UMEUMISS MWANZI?Kweli naona umejanjaruka. Wewe ulikuwa huishi kuandika nyuzi za kutusema wapemba.... Na ukasimulia kile kisa cha mpemba kukutunuku gari. Leo unaona kutukana ndo ujanja wa mjini? Hewallah sheikh. Inshallaah... Ila kumbuka bado hujamaliza safari sheikh.... Wewe mjini tumekuingiza sisi, tumekupokea na kukupa hadi gari.... Leo hii umekuwa mjanja wa matusi? Nawe eti unajua kitu.... Umesahau kuwa umekaa home kwa Ami Yusufali ukimhudumia? Na ulisema humu mwenyewe? 😁