Silaha na askari wamiminika mipakani mwa Israel. Biden ashtushwa. Aenda Israel mwenyewe huku akitaka Palestina wapewe nchi yao



Hii ni documentary au ni kwenye uwanja wa vita?
Kwa sababu hata TZ, Rwanda au Malawi wanaweza kutoa makala kama hiyo ya kuelezea uwezo wa majeshi, vyombo vyao vya ulinzi na usalama ikijumuisha vifaa na silaha zao. Mwisho wa siku vita ni mipango na mikakati.

Narudia Tena, hapa watu wataleta ushabiki kama wa kwenye timu za soka, na kusahau vita inahusisha maisha ya watu. Tuombe amani ipatikane, vita ni ya kuisikia tu Kwa wengine sio jambo zuri hata kama unafikiri unavifaa na vikosi imara.
 
Itazame utaelewa ni nini.

Usingoje kila kitu kufanyiwa, mazowea mabaya hayo kwa kijana wa kiume.
 
Si rahisi, mara ya mwisho Myahudi alitandikwa vibaya sana na Hezbollah wa Lebanon, rudia homework yako.
Rudi darasani hakuna Vita mwarabu aliwahi kumshinda Myahudi.

Siongei ushabiki maandazi coz mwarabu na myahudi si wajomba zangu. Hawana impact yyte ktk maisha yangu.
 
Fata hiyo clip iliyowekwa, usifate yangu.

Wairan wansema kimbembe chao hakiishii kwa myahudi tu, Wamarekani nao wakae sawa.
USA na Israel vinaenda kufutwa kwenye uso wa dunia na Iran. Kazi ipo.
 
Hapo lazima wayahudi waufyate, kama walivyoufyata toka juzi.
Punguza hicho kilevi unachokunywa kwa siri. Pombe ya kificho Ni mbaya sana.

Wewe Ni mtu unahitaji ushauri wa kisaikolojia kuweka akili yako sawa.
 
Watafanya Nini Hawa wanaokimbia na bodaboda kushambulia watu?
Thamani ya kitu ni vile kinavyotumika na kutoa faida kwa mtumiaji.Kifaru kitakuwa na maana gani kitakapokuwa hakiwezi kuvuka vizuizi vya meno ya Dragon.Na kitakuwa na faida gani katika baadhi ya maeneo ambapo hakiwezi kupenya na kina kelele.
Kuna watu wanashindwa kuwaita Hamas wavaa kobazi tena.Walitumia silaha hafifu walizonazo pamoja na matrekta kuvunja uzio waliofungiwa ndani yake.Baada ya hapo haikuwa magari ya kijeshi ni pick up tu kusogea miji ya mbali.
 
Itazame utaelewa ni nini.

Usingoje kila kitu kufanyiwa, mazowea mabaya hayo kwa kijana wa kiume.

Sijasema sijaelewa, nimekuuliza wewe uliyeleta hapa jukwaani. Umewahi kunifanyia kitu Gani hata useme nna mazoea mabaya? Au nimekosea kukuuliza swali, si ungejibu tu nilichokuuliza?
 
Marekani nayo sasa hivi imepeleka wanajeshi wa majini, 2000! Na sasa hivi majeshi yote ya US yamewekwa kama tahadhari kwa ajili ya kupambana na Iran na Hezibollah!
 
Israel wanaungana na chama Cha Fatah cha Muhamud Abass kukabiliana na jitihada zozote kutoka mahali popote duniani za kuitegemeza Hamasi kwa silaha na fedha.

Fatah na Israel wako pamoja kuhakikisha Hamasi inatokomea kabisa katika ardhi ya Ghaza na Palestine kwa ujumla wake.
 
Amani ndiyo inayotakiwa na ndio inayopendeza na kila mtu anaitaka.Haitakiwi amani ya mdomo ambapo unampa mtu amani huku unampiga na kumdhalilisha.Wapenda amani nao lazima wamkemee anayedhalilisha wenzake bila sababu.
Ukiona watu wanapigana mtaani kama ni binadamu mpenda amani basi usiwapite tu.Unachotakiwa ni kwaamua na kuwapa nasaha.
 
Hivi hiyo theory ya kuwa US, huwa hapigani kwake, sioni kama ina mashiko? Sasa mfano, siku US, apigane vita na MEXICO, CUBA na CANADA, atakwepaje hiyo nadharia yako? Kwasababu hawa wana shea mipaka? Ila mala nyingi yeye vita yake huwa na mataifa yaliyo mbali sana na yeye, kitu kinachofanya ugumu wa yeye kushambuliwa. Lakini huwezi niambia eti hiyo ni sababu.
 
si warushe tu mabom wawalipue, wanasubiri nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…