Simba alikataa ofa na kuwakebehi Azam. Je, Azam kalipa kisasi kwa kuipa yanga dau nono?

Watu hawajui kuhusu procedure za dividend, wanazani kampuni ikiingiza mapato ghafi wanagawana hapohapo. Mjikumbushe tu kuwa Kitakachotakiwa kugawanwa ni net profit, yaani Ile baki ya juu baada ya Simba kufanya matumizi yote. Je matumizi ya Simba mnayajua?
 
Naona watu wengi wanapata shida kati ya udhamini na umiliki. Sioni shida ya uwekezaji wa MO wa 20B kwa 49% tukumbuke kuna 51% za wanachama na wawekezaji wengine so definately thamani itakua way higher.

Engagement ya MO kwa Simba sasa hivi ndio imewezesha timu kuwa pale kuwa na quality players, mafanikio uwanjani na kuwa katika ranking za timu bora Africa, so whoever comes kufanya udhamini Simba offer lazima iwe imechangamka, do you think kutokana na fan base, mafanikio na brand ya Simba Azam hawawataki? Simba kwa sasa ana competitive advantage in every sponsorship or investment negotiations.

I believe kama hakuna mikwaruzano ya personal Azam atawafata Simba with best offer or somehow similar to ya Yanga. Uwekezaji wa MO ni muhimu na unafaida sana, asibezwe kisa tu huo udhamini wa Yanga.

Better is yet to come1
 
Na wakumbushe pesa hizo b20 hazitakiwi kuwa allocated kwenye mishahara Bali kwenye investments ili faida za hizo investments ndio ziendeshe timu.
 
Watabaki vinywa wazi Azam akitia 100B simba kutumia content rights kwa miaka 10
 

Nadhani wewe ndiye unapaswa kufunguliwa akili kwa kuangalia Makubaliano ya 2014 v/s Simba ya 2021.

Simba ya 2021 ni kweli Brand kubwa lakini je MO aliingia Makubaliano na Simba hii inavyotaka kushiriki Super League?

Hebu rudi miaka 6 nyuma Simba iliyokuwa ikiitwa Wa Matopeni ambayo ndiyo MO aliyoingia nayo makubaliano halafu utambie kama ilikuwa na thamani hata ya 10B.

Liverpool FC iliuzwa kwa FSG kwa £300M kwa wakati huo lakini sasa thamani yake ni £2.5B je washabiki waanze kulalamika kuwa FSG warudishiwe £300M zao ili wauziwe kwa 2.5B?

Jifunzeni biashara vijana ili mujue kuwa bidhaa kupanda thamani haibadilishi makubaliano ya awali hata kama yalikuwa na thamani ndogo.

Musijadili mambo kwa Mihemko bali jengeni hoja.
 
Yupo tena sana na tunamkubali, hata sasa kigoma nakuhakikishia Yanga 41B itapanda ADVENTURE
 

Acha kudanganya Wenzako Kijana unaonesha hujawahi kufanya biashara hata ya kuuza nyanya 🍅.

Umeona wapi biashara au Kampuni kugawana Mtaji?
Ndugu Kampuni au Biashara wanachogawana ni Faida (Net Profit) hivyo unaposema Simba wakipewa Bilioni 60 zinakuwa shared hapo unadanganya kwa kuto kujua uendeshaji wa biashara.

Labda nikueleweshe tu! Hizo 60B zinaingia kwenye Akaunti ya Timu, baada ya gharama za uendeshaji wa Timu pamoja na Manunuzi ya Wachezaji, Mishahara ya Wachezaji, Viongozi na Watumishi wote wa Simba, kitakachobakia kama Faida ndiyo kinagaiwa kati ya wenye 49% na 51%.
Hivyo upo uwezekano mkubwa wakaishia kugawana hasara na si Mihela kama unavyotaka kudanganya Watu kwani gharama za uendeshaji wa hizi Timu ni kubwa zaidi.
 
Utopoloni shule hamna unategemea nn
 

Tazama na huyu alivyolishwa Matango pori! Anadhani Watu wanagawana tu hela kama ESCROW.

Jifunzeni biashara ndugu musitie aibu hapa.
 
Kwa kwenye hyo b 20 ya mo we umepata sh ngapi?
 
Kuuza maudhui kwa 41 billion kwa miaka 10 ni njaa, lakini kuuza karibu nusu ya klabu kwa 20 billion forever ndo akili sio?!
Unadhani wakati ule MO anaitaka Simba Kwa 20 B ilikua na Thamani hiyo?!!....Sasa hivi Simba ina Thamani kubwa zaidi kutokana na mafanikio yake!!...Yanga wameeza maudhui yake,Simba wanajiendesha wenyewe mnataka Simba nao wauze?!!!...
 
Mbna stori yako ni ya kuunga unga kama ilivyo timu yenu.
 
Halafu kumbukeni bila huyo Mwamedi kuifikisha mahali ilipo Simba,ikafanya vizuri mashindano ya kimataifa,hata huyo Azam asingekuwa na mvuto alio nao sasa.
Mimi nimeanza kutazama mpira wa kibongo baada ya Simba kuanza kufanya vizuri kimataifa.Vinginevyo sikuwa na interest kabisa na huu mpira wa akina Mzee Mpili
 
maswali machache mkuu Chige ,

1. mudi hizo 20b anazilipa kwa installment ngap?

2. je, 20b at per (kama analipa kwa inst moja) zinafanana thamani na say 50b inayolipwa kwa inst 10 (10yrs)?

3. ukiwa mfanyabiashara, kati ya cash na hilo la iende irudi bora lipi?
 
Jifunze namna coy zinavyoendeshwa achana na lile debe tupu (kitenge)
 
Usilazimishe kutoelewa.

Ili kuvutia mtaji mkubwa inabidi uji-brand vizuri na uwe na profit au hasara ndogo. Hicho ndiyo kinachozungumzwa.
Yanga itapunguza hasara, itazidi kukuza brand na hivyo kuvutia mtaji mkubwa na kuna uwezekano mtaji huo ukawa mkubwa kuliko wa Simba.
Just because wanachama na wapenzi wamewekeza to the point, Azam media wamewapa deal la kiasi hicho kabla ya kuingia ubia na mwekezaji yeyote.

Wangepata deal hili wakati wameshaingia ubia na mwekezaji, wanachama na washabiki (ambao most likely watakuwa na holding company yao) wangekuwa relatively short-changed ukilinganisha na sasa.

Hiyo ndiyo point muhimu. Wanachama walipitisha bakuli na wakaita kubwa kuliko ikawaingizia 1.6bn, wakacheza ligi wakapata exclusive media deal na imewaongezea thamani wanachama na washabiki as a "partner". That's the main point.
 
kwenye biashars hakuna kukomoana
huwa tunaangalia maslahi zaidi
huwezi kuuza haki zako zote za matangazo wakati kuna super league inakuja
utatazamwa afrika nzima kila wiki
Mkuu, samahani kama hautojali naomba muundo wa hiyo Super league. Itahisisha team ngapi, kwa vigezo vipi, mshindi atapata nini, itendeshwa kwa mfumo wa ligi au makundi na vinginevyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Haya ulioandika yapo kwenye mkataba wa Mo na Simba?
Je unaweza kutuwekea huo mkataba tusome wote?
 

Nimegundua wewe jamaa ni KIAZI na hakuna unachoongea ambacho ni CONVINCING.

Ni bora ufiche UJINGA wako .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…