Simba fans ni kichekesho kumponda Kocha Saed wa Yanga wakati Fadlu wenu aliishusha timu yake daraja Afrika Kusini

Simba fans ni kichekesho kumponda Kocha Saed wa Yanga wakati Fadlu wenu aliishusha timu yake daraja Afrika Kusini

Makavuli

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2024
Posts
1,425
Reaction score
1,829
Ni vichekesho kwa mbumbumbu eti wanaiponda cv ya kocha mpya wa yanga wakati ajawai kushusha timu daraja kama ilivyo kwa kocha wao fadlu ambae aliishusha Martizburg na akatimuliwa!

Kama cv zinakufanya kazi basi Simba wasingemchukua fadlu kwakuwa cv yake ilikuwa ni ya ovyo!

Unapochukua kocha Kuna vitu vingi vinavyoangaliwa kuanzia mifumo yake, uweledi wake, mbinu zake za kiufundi je vinaendana na utamaduni wa klabu husika, na sio kuangalia cv tu peke yake!

Kocha Nabi alichukuliwa na yanga akitokea El merekh ya Sudan ambako alifukuzwa kwa kufanya vibaya lakini alichokuja kujifanya akiwa yanga Kila mtu mwenye akili timamu anajua na kukumbuka!

Alivyoondoka wachambuzi uchwara na vibaraka wao wakasema ndio mwisho wa yanga but Engineer akamwibua Tena gamond aliyekuwa hana timu takribani mwaka mzima na alichokuja kukifanya Kila mtu aliufyata!

Sasa amechukuliwa Saed tiyali midomo isiyokuwa na breki imeanza na wapiga ramli washaingia kazini kupiga ramli zao, mara yanga inapotea, mara yanga inaanza upya, mara ubingwa awapati Tena kwa kubadili kocha ilimradi tu kukamilisha siku na kutafuta followers mitandaoni!

Yanga ya sasa hivi ata ukimpa Aly kamwe aiongoze kuwa kocha anaweza na ikafanya vizuri, uwepo wa wachezaji Bora wanaojielewa na waliokomaa ndio msingi na uti wa mgongo wa timu, kwa maana iyo yanga aiwezi kuanza upya bali kocha ataendeleza alipoishia gamond kama ambavyo gamond aliendeleza alipoishia Nabi!
 
Utopolo Kazi Mnayo, Ubaya Ubwela umewafemea...!

Huu Mwaka ndo Mwaka Wa Ubaya Ubwela......mtauelewa tu...!

Disemba ikiisha huyo Mzee Said Wenu mpya akinusurika kuendelea kuwepo Basi nitatoa Ofa nendeni baa yoyote Kunyweni mgalagae bili iandikwe jina Langu. !
 
Mbona huyo Side mnamtetea sana jamani, Acheni kazi yake ije imtetee wekeni akiba ya maneno. Kumbuka majirani wana Kampeni kabambe ya UBAYA UBWELA
 
Mb
Mbona huyo Side mnamtetea sana jamani, Acheni kazi yake ije imtetee wekeni akiba ya maneno. Kumbuka majirani wana Kampeni kabambe ya UBAYA UBWELA
Akuna anayemtetea bali tunawarudisha kwenye mstari wanaombeza kabla ajaanza kazi yake wanapiga ramli
 
Hatumpondi huyo kocha wa utopolo ila takwimu zake huko alikotoka ndo zinamponda
 
Back
Top Bottom