Simba hakuna usajili ni kurundika wachezaji tu.

Kwa sehemu kubwa uko sahihi, japokuwa hapo kwenye Power Dynamo hauko sahihi.
Msimu uliokwisha wa 2023/24 msimamo ulikuwa hivi:
Power dynamo 3
Asante kotoko 6
River united 8
Stella Abidjan 5
Power Dynamo 3
Geita gold 15 (imeshuka daraja)
 
Kwa sehemu kubwa uko sahihi, japokuwa hapo kwenye Power Dynamo hauko sahihi.
Msimu uliokwisha wa 2023/24 msimamo ulikuwa hivi:
Power dynamo 3
Asante kotoko 6
River united 8
Stella Abidjan 5
Power Dynamo 3
Geita gold 15 (imeshuka daraja)
Asante Kwa masahihisho
 
Lakini hawasajili timu nzima, bali wanachukua wachezaji waliofanya vizuri huko walipotoka.
Angalia na ushindani wa ligi zao walipotoka ulinganishe na ligi yetu, mchezaji anaweza kuwa Bora kwenye wabovu uwezi shangaa, na ligi mbovu lazima zipate pia ma MVP wake Kama hao ambao unaambiwa na MVP wa Ivory coast lakini timu yake imeshika namba 6 kwenye msimamo, uyo mwingine unaambiwa kawa MVP wa Nigeria lakini timu yake imeshika namba 8 kwenye msimamo, Sasa unawaleta Tanzania kwenye ligi ngumu na Bora yetu ni macho ngoja tusimalize maneno
 
Kama hiyo ndio sababu yako, basi haupo sahihi mkuu.

Kuna wachezaji wanasajiliwa baada ya timu zao kushuka daraja. Kwahiyo usikariri.
Hull city ilimuuza Andy Robertson kwenda Liverpool mpaka leo Andy Robertson ni moja ya Maleft back bora pale EPL, Na timu ya Taifa na Captain. Mleta mada bado hawezi na haelewi namna timu zinavyosajili.
 
Hull city ilimuuza Andy Robertson kwenda Liverpool mpaka leo Andy Robertson ni moja ya Maleft back bora pale EPL, Na timu ya Taifa na Captain. Mleta mada bado hawezi na haelewi namna timu zinavyosajili.
Angalia na ligi alotoka.
Kama Simba wangekuwa wanatoa wachezaji wa nafasi ligi za South Africa, Tunisia au Morocco tungesema angalau kidogo.
Yaani utoe mchezaji team namba 16 Zambia umlinganishe Na Robertson au Xhaqir aliyetoka Stock city za EPL
 
Hivi wachezaji wa Yanga wote wametoka vilabu vilivyoshinda ligi kuu? Vipi kuchezea tim za Mataifa yao.. Inye Guede Guede anachezea timu ipi ya Taifa, Pacome, Zengeli nk, vp hao pia
 
Angalia na ligi alotoka.
Kama Simba wangekuwa wanatoa wachezaji wa nafasi ligi za South Africa, Tunisia au Morocco tungesema angalau kidogo.
Yaani utoe mchezaji team namba 16 Zambia umlinganishe Na Robertson au Xhaqir aliyetoka Stock city za EPL
Hoja yako bado dhaifu na unatoka kwenye kauli uliyoiandika hapo juu
 
ngara23 kiwango cha mtu ni kiwango tu hakilinganishwi na ubora wa ligi, kama mchezaji anajua anajua tu. Yule Hamad Bacca wa Yanga alikotoka kule Zanzibar timu yake ni ya ngapi Kwenye rank za CAF.
 
Wanayanga wenzangu tuache wivu na hoja nyepesi. Messi alitokea Barca B. Kitasa chetu Ibra Bacca kilitokea Zanzibar. Mimi nasikitika timu yetu kujaza mizee na injury prones.
 
ngara23 kiwango cha mtu ni kiwango tu hakilinganishwi na ubora wa ligi, kama mchezaji anajua anajua tu. Yule Hamad Bacca wa Yanga alikotoka kule Zanzibar timu yake ni ya ngapi Kwenye rank za CAF.
Hivi ushawahi kuona team ya EPL inasajili mchezaji wa Djibouti, Somalia, Tanzania, Moja Kwa Moja.
Yaani Arsenal aje Yanga amsajili Dickson Job
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…