Simba ilishawahi kupigwa 9 na Yanga

Simba ilishawahi kupigwa 9 na Yanga

Mbona sisi wenzako tumekubaliana na hizo takwimu zote!! Kwa nini wewe unapinga? Kwani hiyo timu iliyokuwa inaitwa Sunderland, si ndiyo hii hii simba ya sasa!!

Kubali basi ili twende pamoja.
Katika hizo 9-0 magoli alifunga nani na nani
 
unajua buana makolo yanajivunia rekodi ya magoli 6 bila, sawa,ngoja tuachane na magoli yetu yale 9 ya mwaka 1938 tuje kwenye rekodi ambazo hazizungumzwi sana, kale ka rekodi ketu ka kufunga goli 3 kipindi cha kwanza kisha makolo kipindi cha pili hayatokei, mala mbili tunafanya hivo, vipi mngekuwa mnatokea kpnd cha pili ktk mechi hzo...! au tuseme mna hyo rekodi ya ku2funga sita,lakini je ktk mechi zote tulizokutana tangu mkiitwa QUEEN mnatuzid magoli? hata kwenye idadi ya ushindi tulioupata dhidi yenu mnatupata? MZEE RAGE ajengewe sanamu pale posta
 
Ndio asili ya uswahili wetu, tunapenda sana kukuza mambo ambayo hata hayafai kukuzwa. Kuna muda tuige hata wamagharibi
Kwakweli aisee..najua kuna watu huko Yanga wanakwazika sana...maana haikutakiwa kumfunga Simba iwe story kubwa hivi...mngeona kawaida tuu...
 
Kwakweli aisee..najua kuna watu huko Yanga wanakwazika sana...maana haikutakiwa kumfunga Simba iwe story kubwa hivi...mngeona kawaida tuu...
Kwenye mpira ni kawaida sana ila wamegeuza story ya kumalizia nayo mwaka
 
Hiyo post ya simba kupigwa 9 nimeiona,kwa great thinker sidhani kama ni sahihi kuandaa uzi kuhusu hayo matokeo kwasababu ni kushusha ukubwa wa JF au lah basi ungeupeleka uzi huu kwenye jukwaa la vichekesho.

Hebu jiulize
1. 1938 kulikuwa na ligi kuu tz?maana ile post imeandikwa TPL yani Tanzania Premier League, miaka hiyo hatujawa tanzania bado,na wala hakukuwa na ligi kuu...
2. Imeandikwa Simba vs Yanga....miaka hiyo simba anaitwa sunderland
3. Wameweka logo ambazo zimebuniwa juzi tu hapo hasa ile ya simba
4. Miaka ya 1938 hakukuwa na technology ya kutengeneza post kama ile.

Kwa minajili hiyo,huu uzi haupaswi kuwa humu,bali upelekwe jukwaa la vichekesho.


SHUKRANI
 
𝗩𝗜𝗣𝗜𝗚𝗢 𝗩𝗜𝗞𝗨𝗕𝗪𝗔 𝗭𝗔𝗜𝗗𝗜


Matukio na vipigo vikubwa zaidi kuanzia (5+) kwenye derby ya Kariakoo:

FT: Yanga SC 9-0 Simba SC (1938)
FT : Yanga SC 5-0 Simba SC (1968)

⚽⚽ Maulid Dilunga 18' Pen, 43'
⚽⚽ Salehe Zimbwe 54', 89'
⚽ Kitwana Manara 86'

𝗠p𝗶𝗿𝗮 𝗸𝘄𝗮𝗽𝗮𝗻𝗶:

Tarehe 3 Machi 1969:

Simba SC waligoma kurejea Uwanjani kipindi cha pili baada ya kufungwa (3-0). Yanga SC walipewa pointi (3) na mabao (3) mezani.

FT: Simba SC 6-0 Yanga SC (1977)

⚽ Selemani Sanga OG 20'
⚽⚽⚽ King Kibadeni 10', 42', 89'
⚽ ⚽Jumanne Masimenti 60'

𝗦𝗵𝗶𝗸𝗮 𝗺𝗸𝗼𝗻𝗼:

Mwaka 1988, Yanga SC waliwasaidia watani zao Simba SC wasishuke daraja. Mchezo wa mwisho wa ligi kuu Yanga wakishinda wanatwaa Ubingwa, Simba wakisare au kupoteza wanashuka daraja. Yanga hawakumkaba kwa makusudi, Hamisi Shikamkono ili afunge goli Simba wasalie ligi kuu.

Shikamkono akafunga goli, Simba wakasalia ligi kuu na Yanga wakaukosa Ubingwa. Msimu huo Simba SC walikuwa na mgogoro mkubwa baina ya katibu mkuu, Jimmy David Ngonya na wazee wa klabu hiyo.

Mpaka sasa Simba na Yanga ndio klabu pekee ambazo hazijawahi kushuka daraja ligi kuu Tanzania tangu ianzishwe.

𝗬𝗮𝗻𝗴𝗮 𝘄𝗮𝗮𝘇𝗶𝗺𝗮 𝘄𝗮𝗰𝗵𝗲𝘇𝗮𝗷𝗶 𝗦𝗶𝗺𝗯𝗮 𝗦𝗖:

Mwaka 1998, Yanga SC waliazima wachezaj kutoka Simba SC ili waongeze nguvu kikosini kwao kwenye michuano ya CAF champions league ambapo Yanga ndio walikuwa klabu ya 1 East Africa kuingia group stage.

Wachezaji walioazimwa ni:
  • Monja Liseki
  • Shabani Ramadhani
  • Alphonce Modest
Zamani hawakuwa maadui 🙌

FT: Simba SC 5-0 Yanga SC (2012)

⚽⚽ Emmanuel Okwi 2', 62'
⚽ Felix Sunzu (Penati) 56'
⚽ Juma Kaseja (Penati) 67
⚽ Patrick Mafisango (Penati) 72'

FT: Simba SC 1-5 Yanga SC (2023)

⚽️ Kibu Denis 🅰️ Ntibazonkiza 9'
⚽️ Musonda 🅰️ Yao 3'
⚽️ Nzengeli 🅰️ Aziz Ki 63'
⚽️ Stephanie Aziz Ki 🅰️ Mzize 73
⚽️ Maxi Nzengeli 🅰️ Mzize 77'
⚽️ Pacome (Penati) 86'

©Tom Cruz-Mchambuzi.View attachment 2812260
Taarifa yako ina viashiria vya majini
 
Umetumia utaratibu wa kutaja majina ya wafungaji kwa mechi zote ,naomba utaratibu huo huo uendeleze kuorodhesha majina ya wafungaji wa hayo magoli 9 mwaka 1938.
Putin.jpg
 
Mananihii ya kale hayanuki; sisi tunaangalia miaka mitano iliyopita tu kujua nani aligusa mwiko akadungwa akagungwa sindano ya 5G na bado ananuka dawa.
 
Back
Top Bottom