Simba kufungwa na Raja tumestahili, tujipange msimu ujao

Simba kufungwa na Raja tumestahili, tujipange msimu ujao

Raja waliandika twitter kabla ya match watashinda 3 -0 kweli wamepata hayo magoli. Wanacheza kama wapo kwao wanajiamini sana, wanasoma mchezo halafu wanatumia mapungufu kila dakika.
Inaonekana walishasoma viwango vya Simba huwezi kuwalaumu wachezaji au kocha wa Simba.

Hao wenzetu wameonesha kiwango cha juu sana.
Wametuzidi kila idara, kila kitu kuanzia mitandaoni hadi uwanjani.
 
Lakini kama ni mshabiki wa mpira kweli, ungeweza kutoa kasoro zilizojidhihirisha kwenye mchezo wa leo kwanza kabla ya kuanza kuhukumu historia!

Timu haina short on target ya maana, mipira inapotea kati, Saido anapoteza mipira ovyo, anaesaidia na Kapombe hajulikani, Boko na Baleke hakukuwa na tofauti.

Kongole kwa Shomari kwa kila hali.

Kimsingi, tatizo ni waalimu kwanza, kisha umri wa wachezaji na mwisho makuzi ya wachezaji, kuwa mpira sio jambo lao la kwanza, ni baada ya kufeli shule!
Eeeh Saido tena [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mimi ni shabiki wa mnyama pure.... ila hii ya leo hata umlete pep guardiola original hachomoi.

Hiyo quality ya waarabu umeiona? Umecheki wanavyokimbia? Umecheki wanavyojiamini wakipata mpira?umeona pass accuracy yao?

Men tukubali raja ina wachezaji quality kuliko simba leo hakuna wa kulaumiwa hata mmoja.
Dah wanacheza kama ulaya aisee.
Yule Sufiane aliyefunga goli la pili ana miaka 22.
 
Naungana na wewe mtoa mada. Tuanze project mpya. Mambo ya ghafla hayata tufikisha popote.

Viongozi wa timu wanatufanyia siasa.

Unaanzisha kandarasi na kocha mpya (mwenye falsa tofauti na iliopo) wiki tatu kuelekea mchuano mkubwa na muhimu kama huu, unatarajia nini?

Unamleta Manzoki kuja kufanya maonyesho kwenye uchagu wakati ulishindwa kumsajili dirisha kubwa na ndogo, kama sio siasa za uchaguzi ni nini?
 
Manzoki tuu iliyohitajika ml 400 viongozi waliingia mitini wakaleta kyombo, kapama na the likes ambao ni bei chee na viwango duni. Pale simba kwa squad hii hata umlete mzee wenga hatoboi.
Uko sawa kwenye angle hiyo mkuu ila kumbuka kuwa kwa sasa, sio tu uchumi wa nchi pekee bali kila sekta ni masikini na huku kwenye soka, uwezo wa kusajili mchezaji kwa sh 100m hatuna, ni kulazimisha upuuzi wa kipuuzi tu

Kama hatuna chipukizi wa miaka 16 to 21, hatuwezi toboa kwa wachezaji wa mchongo tunaoambiwa wanasajiliwa kwa 100m na kuendelea.

Waarabu wanatumia wageni kushinda hizi mechi?

TP Mazembe, enzi zake, wageni wangapi walikuwa wanatamba kwenye kikosi?
 
Nakubali, first on target, goli, second on target, goli.

Kipaji hakikuzwi mtaani, Kapombe, Chama, Baleke, Saido, Enock, Mkude, Mzamiru n.k, hawa wameanzia wapi career yao ya mpira wa miguu?
Quality ya wachezaji wa Raja na wa Simba ni mbingu na ardhi....shida kubwa pia ipo kwa viongozi ambao wanasajili wachezaji wachovu kama sawadogo
 
Kiuhalisia simba hatuna timu ya kushindana kwenye ligi wala kwenye mashindano ya kimataifa. Timu iko flop.

Lazima tukubali mpira wa sasa hauchezwi kwa historia eti kwa mkapa hatoki mtu huu ni uzwazwa.

Ni hivi, Simba imekuwa ikisajiri kwa ujanja ujanja, ni kama viongozi hawapo serious huku ukweli wanaujua, mpira ni uwekezaji.

Ni hivi, Simba imewekeza sana kwenye propaganda. Msemaji wa timu anaropoka ropoka tuu kufurahisha genge huku akijua wazi kuwa mpira hauchezwi mdomoni wala kwa slogan.

Ni hivi, viongozi wanatufanya mashabiki wa simba ni mazuzu. Wanaona kwa kuwa watu wanaujaza uwanja basi wao wanafikiri watu ni watumwa wa mpira na hawana shuguli nyingine ya kufanya. Tunaweza tusiwe tunaenda uwanjani kwa kususia kwani simba haileti ugali majumbani kwetu.

Ni hivi, imenyesha tumejua panapo vuja. Tuna wachezaji magalasa kibao ambao hawakutakiwa kuwa simba leo ila wanalindwa kwa kutumia neno uzawa, bloodfckn.

Ni hivi, hii dhana ya kujiona wakubwa kisa tulimfunga ahly ni ya kitoto na ya kuachana nayo. Angalia quality tuliyonayo sasa hivi utaifunga timu gani inayojielewa? Hao utopolo tu ambao tunarogana kila siku hatuwawezi sembuse wanaowekeza mijipesa yao kwenye mpira?

Kiukweli natamani tusipate point hata moja kwenye mashindano haya labda viongozi akili zitawaamka. Ng'ombe hanenepi siku ya mnada viongozi nao waachane na kutoa motisha kwa wachezaji kwani ile ni kazi yao.

Kiufupi msimu ujao wachezaji wanaostahili kubaki simba ni baleke, inonga, saodoo, phiri na chama bhaaasiii. Wengine wote timua. Ni bora timu ikasukwa upya kuliko kujidanganya eti sisi ni wakubwa.
Ww ndyo shabiki kwenye ukweli unasema siyo wengine kazi kukaza mafuvu tu
 
Back
Top Bottom