Simba na Yanga ni uchawi unaotumiwa kupumbaza akili za vijana Watanzania

Unakaa Nyagwa wewe,yaani balala mpiganie klabu zingine zije kuwa na fanbase kubwa kama hii klabu kubwa na zicheze mpira wa kuvutia kama Simba, eti unataka ifutwe,tutwa wewe kwanza

Shubaaat
Kwa hiyo wakicheza vizuri ww unaambulia nini!?
 
Sasa si Bora tushabikie mpira wewe unataka tujadili siasa za mamluki wa CCM
Mi nakuhakikishia kama kelele za kupinga mambo maovu yanayoendelea ndani ya nchi zingekuwa kubwa kama zinavyopigwa kelele za mpira nchi hii mambo maovu mengi yangekuwa yamekwisha kabisa
 
Madhumuni ya uanzishwaji wa Club ni kuwapa wanachama furaha na sio kuwapa profits, so hiyo furaha kama unaweza iweke in monetary form na kuitax ndio mapato yao hayo.
 
Mkuu hebu tofautisha hobi na ishu ya maslahi maana unaweza ukawa na hobi ya kucheza au kupenda mpira then serikali ya ccm unamiliki viwanja vyote na haitaki kuviboresha unategemea utakidhi haja ya hobi yako?
Mfano mwingine unapenda mpira lakini marefa wanakula rushwa ili kuisaidia yanga ishinde kwa namna yoyote hauoni kwamba unahitaji serikali imara kudhibiti rushwa!?
 
mleta mada hoja yako ni ya ukweli kabisa hasa kwa miaka hii ya 2015 kuja mbele ,kutokana na kuzuiwa mikutano ya siasa kwa vyama vya upizani,bunge live kutokurushwa ambapo hoja mbalimbali zinazohusu taifa zilikuwa wazi ,viongozi (whistle blowers ) kufungwa au kufanyiwa figusu za za makusudi wanapokosoa,imefanya vijana wengi kutokujadili siasa kama hapo nyuma.2005 hadi 2015 kujadili siasa ni mada zilikuwa zikitrendi katika mikusanyiko yeyeto hapa tz tofauti na sasa .Media zilikuwa huru kukosoa ,sasa wamefungwa midomo kwa sheria mbalimbali mambo ambayo ni huru kujadlili ni michezo na ndio maana unaona kizazi hichi kipo hivyo
 
Mpk Leo hii Kuna makovu makubwa ambayo yalisababishwa na huruka za jiwe kudhibiti mijadala.

Siku zote tumesema kuwa jiwe angeendelea kuwa hai nchi ingetumbukia shimoni
 
Mkuu kila mtu hawezi kuongelea siasa, ushabiki wa mpira upo kwa kiwango cha juu hata uingereza lakini hakujazuia watu kuhoji mambo ya msingi kutoka kwa wa-twawala.....
 
Uko sahihi, kuna watu ambao hawajui ht mlo unaofuata utatoka wapi lakini utawakuta wamekaza mishipa ya shingo wakitumia nguvu kidogo walizo nazo kubishania Manara, Mo na timu zao, pathetic.
 
Mkuu kila mtu hawezi kuongelea siasa, ushabiki wa mpira upo kwa kiwango cha juu hata uingereza lakini hakujazuia watu kuhoji mambo ya msingi kutoka kwa wa-twawala.....
Wazungu huwa wanashabikia mpira kwa mbwembwe wakiwa viwanjani au wanaangalia mechi tu baada ya hapo wanajikita kufanya mambo mengine ya maendeleo, sio kuendelea na mijadala isiyoisha ya mpira kila mahali.
 
Ni jambo la fedheha mpira wa Simba na Yanga huwa unajadiliwa hadi bungeni!
 
Msipende kumsingizia kila kitu Magufuli. Why mpaka leo mnaishi kwa kivuli chake wakati mtu ameshajifia zake. Watu wameacha kujadili siasa baada ya kuona ni ulaghai mtupu.

Unakuta mwanasiasa wa upinzani anaipinga Serikali kila siku, lakini akipewa nafasi yeye hata ya ubunge tu, hakuna lolote analolifanya zaidi ya kujineemesha yeye na familia yake. Wengine tumewaona wamepata nafasi za kisiasa wanaweka ndugu na mahawara wao huku wananchi wakiendelea na shida zao. Ndo maana watu wameona ni bora wajadili vitu vinavyowapa furaha kama mpira kwasabbu wanasiasa siyo wakweli bali ni wachumia tumbo tu.
 

Wapi ww, Magufuli ndio aliyezuia watu kujadili siasa ili awatawale kwa shuruti. Unasema watu wameamua kujadili mpira maana wameona wanasiasa ni waongo na wanafaidika na familia zao. Kwani huko kwenye mpira ndio wanagawana pesa na wachezaji? Acha Utetezi dhaifu kwenye ukweli.
 
Kwasehem naungana na mtoa mada,ukienda Mbeya-Uyole,NJIA panda wanapouza magazeti,utakuta vijana KWA wazee tangu sa nne asubuh hadi sa nne usiku wapo wanajadiri mpira,celebrities kama diamond,Alikiba,Harmonize n.k Wengi wao ni jobless.Kinachoumiza zaid Wengi wao ni vijana ukiwauliza sera ya vijana kitaifa inasemaje?hawajui!Panahitajka elimu pana ktk hili
 
Mkuu kila mtu hawezi kuongelea siasa, ushabiki wa mpira upo kwa kiwango cha juu hata uingereza lakini hakujazuia watu kuhoji mambo ya msingi kutoka kwa wa-twawala.....
Sio lazima iwe siasa lakini kwa nini mbona tuna changamoto lukuki ambazo wala hazizungumzwi mfumo mbovu wa elimu uhaba wa ajira kupanda bei za bidhaa haya ni baadhi ya mambo ambayo ninadhani yakishupaliwa kwa hisia kali kama ilivyo kwa mpira viongozi wetu lazima wataona kwamba vibarua vyao viko mashakani
 
Watz wengi wamekuwa na wajinga saaana hasa vijana kwa ajili ya mambo ya mpira yasiyo na majibu ya maisha yao.

Hii naiona sana hapa Tz,mambo wanayopaswa kuyafanyia mjadala na kuchukua hatua wanakaa kimya
 
Mapenzi mengine ni ujinga tu,mapenzi na mpira ni umbumbumbu na ulevi mbaya sana
 
Kama unaishi maisha ya kijinga na ya ulevi wa kushabikia mpira kila siku lazima uambiwe kuwa unapotea,huwezi kujua kwa urahisi ila athari ni kubwa kiakili...ni kama nyeto tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…