Simba na Yanga ni uchawi unaotumiwa kupumbaza akili za vijana Watanzania

Simba na Yanga ni uchawi unaotumiwa kupumbaza akili za vijana Watanzania

Naona wengine wanatanguliza hasira badala ya kujenga hoja tatizo huu upenzi wa hivi vilabu umeteka akili za vijana wengi badala ya kutumia muda mwingi kuwaza na kuongelea changamoto za maisha yetu, unakuta wanakesha na kuongelea changamoto za simba na yanga.
 
Hivi wanasiasa mnapo preach uhuru mnakuwa mnalenga uhuru upi?Leo hii mtu kuchagua kujadili mpira imekuwa kikwazo kwa maendeleo ya taifa?

Unataka wajadili siasa za Membe na ACT au Membe na CCM,Zitto na CHADEMA au Zitto na ACT.Hivi mtu akae ajadili vitu vya hivi?wanasiasa mnabadilika kama vinyonga, hakuna anayeweza kuaminika, kwa hiyo acha vijana wajadili kitu wanachopenda kwa maana nyie ndio kila kukicha mnapreach uhuru.

Kikubwa,tafuta pesa ukipata tumia ni zako na ukikosa pia ni juu yako.Achana na vijana katika chaguzi zao na msipende kuwa madikteta kabla ya kupewa mamlaka
Huwezi kukwepa kuongelea siasa kwa sababu wanasiasa hawaaminiki sababu kwa kadri wasivyoaminika ndivyo wanavyofungua fursa ya kujadiliwa. Kukimbia mijadala ya mustakabali wa maisha yetu ni sawa na kumsusia nyani shamba la mshindi mabichi
 
Naona wengine wanatanguliza hasira badala ya kujenga hoja tatizo huu upenzi wa hivi vilabu umeteka akili za vijana wengi badala ya kutumia muda mwingi kuwaza na kuongelea changamoto za maisha yetu, unakuta wanakesha na kuongelea changamoto za simba na yanga.
Miaka ya 1960s ushabiki wa mpira haukuwa na nguvu sana ndio maana ata uhuru ulipatikana kwa urahisi maana watu wengi walijihusisha na tatizo moja tu...mkoloni.

Leo hii mtu ana arsenal kichwani,simba,yanga nk.ukimuambia katiba mpya inatakiwa hakuelewi...tumerudi nyuma saana
 
Kwa wenye IQ ndogo ndo wanapoteza focus..na nahc hata ww upo kweny hili kundi....mpira ni kujifurahisha tu as long as hakuna sheria inayovunjwa pale unaposhabikia mpira mimi sion haja ya kuanza kupangiana ni stareh gan nifanye na ipi nisifanye
Kwamba mpira ni burudani hilo kiko wazi lakini kwa nn hiyo burudani ipewe umuhimu mkubwa hivyo!? Na kwa taarifa tu ni kwamba kwa simba na yanga ni zaidi ya burudani inakaribia kuwa ibada
 
Naona wengine wanatanguliza hasira badala ya kujenga hoja tatizo huu upenzi wa hivi vilabu umeteka akili za vijana wengi badala ya kutumia muda mwingi kuwaza na kuongelea changamoto za maisha yetu, unakuta wanakesha na kuongelea changamoto za simba na yanga.
Kama sasa hivi Simba tunachangamoto ya number 10, Bwalya bado haja adapt vizuri na Kibu Denis ana papara tungepata mtu dizaini ya Chama au tukizidi kumuamini Sakho tunaweza kufika mbali.

Kiufupi Mwl Pablo aelewe timu yake vizuri na kutuletea defensive midfielder mkata umeme mzuri wa kusaidiana na Mkude. Tutakua wa moto sana katika ligi na mashindano ya Kimataifa
 
Kama sasa hivi Simba tunachangamoto ya number 10, Bwalya bado haja adapt vizuri na Kibu Denis ana papara tungepata mtu dizaini ya Chama au tukizidi kumuamini Sakho tunaweza kufika mbali.

Kiufupi Mwl Pablo aelewe timu yake vizuri na kutuletea defensive midfielder mkata umeme mzuri wa kusaidiana na Mkude. Tutakua wa moto sana katika ligi na mashindano ya Kimataifa
Then utapata maendeleo gani binafsi?

Abudu Mungu,usikeshe unaabudu mpira
 
Miaka ya 1960s ushabiki wa mpira haukuwa na nguvu sana ndio maana ata uhuru ulipatikana kwa urahisi maana watu wengi walijihusisha na tatizo moja tu...mkoloni.

Leo hii mtu ana arsenal kichwani,simba,yanga nk.ukimuambia katiba mpya inatakiwa hakuelewi...tumerudi nyuma saana
Uko sahihi mkuu najaribu kupata picha kama mkoloni ndio angekuwa anatawala leo kwa kweli anayetawala kwa raha sana, maana angefanya mchezo mdogo tu angeziwezesha simba na yanga kutengeneza matukio yanayovutia hisia za vijana, wakati wao wakiendelea na hizo hoja yeye anaendelea kujiimarisha.
 
Ila mimi binafsi huwa nahisi Simba na Yanga zikifutwa tutakuwa na maendeleo kwenye soka kuliko sasa.
 
Hata mimi mpira ilishakuwa kama addiction ,sifuatilii habari nyingine zaidi mpira nikoradhi nikose vyote lkn siyo mechi ya timu yangu au mechi kali yeyote hata kama nina kazi za msingi za kufanya kwa muda huo .Nikafikiria nikasema jambo ambalo haliwezekani lote haliachwi lote nikadhamiria kupunguza sasa faida nimeiona concentration Ktk mambo ya msingi na ufanisi umeongezeka ila kuacha kabisa sidhani.
 
We bhana tuachie timu zetu! Walau zinatufariji na kutuongezea siku za kuishi. Au unataka tuchanganyikiwe zaidi kutokana na hizi siasa tunazo fanyiwa na ccm kila sehemu?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
We bhana tuachie timu zetu! Walau zinatufariji na kutuongezea siku za kuishi. Au unataka tuchanganyikiwe zaidi kutokana na hizi siasa tunazo fanyiwa na ccm kila sehemu?
Kweli kabisa Mkuu, Mpira unasaidia ku refresh mind.
 
Kwasehem naungana na mtoa mada,ukienda Mbeya-Uyole,NJIA panda wanapouza magazeti,utakuta vijana KWA wazee tangu sa nne asubuh hadi sa nne usiku wapo wanajadiri mpira,celebrities kama diamond,Alikiba,Harmonize n.k Wengi wao ni jobless.Kinachoumiza zaid Wengi wao ni vijana ukiwauliza sera ya vijana kitaifa inasemaje?hawajui!Panahitajka elimu pana ktk hili
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom