Simba sasa wanacheza mpira wa Ligi ya Uingereza

Simba sasa wanacheza mpira wa Ligi ya Uingereza

Simba walikuwa na mapungufu muhimu ya kiufundi ambayo kwa hatua wanayotaka kupiga hasa huko CAF ilihitaji kuyarekebisha.

Pungufu la kwanza lilikuwa ukosefu wa ubunifu katika kupenyeza mipira katika ngome ya timu pinzani. Hii ilisababisha timu kulazimika mara kwa mara kurudisha mipira nyuma, mara nyingi hadi kwa kipa. Mashabiki wengi hawakuwa wanaliona hili au walikuwa wanalimezea, wao walikuwa wanaona tu boli linatembea ila haya yalikuwa madhaifu.

Pungufu la pili ilikuwa kwenye ukabaji na kujituma. Simba alikuwa anacheza mpira wa taratibu sana na morali ya wachezaji ilikuwa chini. Ndiyo kuna game goli zilikuwa zinakuja wakati mwingine nyingi tu halafu mashabiki wanasahau ila zile mechi ambazo game ilikuwa inakataa tuliona wazi hayo mapungufu na watu waliyalalamikia. Ila angalia game hizi mbili za mwisho, wachezaji unaona wanapambana sana. Morali ya timu iko juu.

Simba ya Robertinho haichezi mpira wa Brazil, Spain wala wa Dubai. Huu ni mpira wa English Premiere League. Nashangaa watu wanaangalia kila siku EPL, wengine wanabeti, wengine wamekuwa mashabiki lia lia wa Arsenal, Man U, Man C, nk. ila wanashindwa kutambua mpira wa Uingereza unaochezwa sasa na Simba ambao ni mpira wa kasi na ni kawaida kucheza mipira mirefu. Tofauti kule wachezaji wana control nzuri ya mpira ambayo Simba kiasi wana mapungufu hasa wakitaka kumaintain kasi ya mchezo.

Wachezaji hasa mabeki wanahitaji kutulia maana naona wanacheza kwa pressure sana na pia timu nzima iongeze uwezo wa kucontrol mpira vizuri hata kama ni kwa kucheza mpira wa kasi. Pia safu ya mbele inabidi kuwa inatumia vizuri nafasi inazopata.

NB. Binafsi siyo mpenzi sana wa style inayotumika EPL.
Aina ya wachezaji ambao kocha anawatumia hawana asili ya creativity
 
Shida tunathamini rangi kuliko maarifa
Mgunda a. K. a MAJINZI ni bora kuliko Robetihno A. K. A MIKANDA YA MABEGI
KIDOGO NJE YA MADA...... HAWA JAMAA WANATEGEMEANA SABABU MGUNDA JINZI KUBWA PLUS ROBETIHNO MIKANDA WA MABEGI KILA MMOJA ANAWEZA KUAZIMA KWA MWENZAKe JINZI au mkanda pia Wanafanana kimavazi unaweza kudhani ni walevi chapa chapa[emoji3][emoji3][emoji3]
Wana ni jokes tu
Ila Mgunda ni bora kuliko huyo mbrazil
Sio kila mchina a najua kung-fu
 
Kocha akieleweka na wachezaji vizuri tutashuhudia mazuri mengi sana hasa huko CHAMPIONS LEAGUE... Pia kocha wa fitness anatakiwa aongeze utimamu wa wachezaji ili waweze kumaintain kasi ya mchezo dakika zote uwanjani.
 
Shida tunathamini rangi kuliko maarifa
Mgunda a. K. a MAJINZI ni bora kuliko Robetihno A. K. A MIKANDA YA MABEGI
KIDOGO NJE YA MADA...... HAWA JAMAA WANATEGEMEANA SABABU MGUNDA JINZI KUBWA PLUS ROBETIHNO MIKANDA WA MABEGI KILA MMOJA ANAWEZA KUAZIMA KWA MWENZAKe JINZI au mkanda pia Wanafanana kimavazi unaweza kudhani ni walevi chapa chapa[emoji3][emoji3][emoji3]
Wana ni jokes tu
Ila Mgunda ni bora kuliko huyo mbrazil
Sio kila mchina a najua kung-fu
Acha walimu wafanye kazi zao hizo zingine unaleta ni porojo tu...
 
Mpira wa kasi mwenzetu umeuona wapi? Binafsi sijaona mpira wa kasi bali nimeona mpira roho juu.
Kwani wewe ukiangalia EPL roho huwa haiwi juu? Roho kuwa juu ni "excitement" kwa sababu ya kasi ya mchezo na kwenye kasi kuna kosakosa nyingi.
 
Labda wewe unaangalia mechi nyingine ila kwa mpira wa Leo hakuna cha kusifia.
Hizo changamoto za Simba zimesemwa sana huko nyuma na toka Roberto aje, zimeisha ghafla. Utasemaje hakuna cha kusifia?
 
Kwani wewe ukiangalia EPL roho huwa haiwi juu? Roho kuwa juu ni excitement kwa sababu ya kasi ya mchezo na kwenye kasi kuna kosakosa nyingi.
Roho juu kwa anayepelekewa moto kila mara, unaomba mpira uishe.
 
Hizo changamoto za Simba zimesemwa sana huko nyuma na toka Roberto aje, zimeisha ghafla. Utasemaje hakuna cha kusifia?
Kwa maoni yangu sijaona jipya sidhani kama unaweza nilazimisha niendane na mtazamo wako.
 
Kwa maoni yangu sijaona jipya sidhani kama unaweza nilazimisha niendane na mtazamo wako.
Upande wa pili tumewazoea hamjui kusifia kinachofanywa na wengine
 
Roho juu kwa anayepelekewa moto kila mara, unaomba mpira uishe.
Ndiyo "excitement" yenyewe hiyo na ndiyo raha ya mpira hiyo. Nguvu ya kila timu inabalance, siyo timu inajihakikishia kushinda mechi 10 mfululizo, excitement itatoka wapi?

Simba wakiweza kujenga stamina na fitness nzuri ya wachezaji na kuweza kupossess mpira, hii kasi itasumbua timu nyingi.
 
Mimi nasubiri nione kitakachojili mbeleni kwasasa bado naangalia jinsi kikosi kinavyoendelea kusukwa kama kitafanya kama Mgunda au zaidi ya Mgunda au kitashuka ubora zaidi. Kwasasa maneno yamekuwa mengi wengine wameanza kutoa sifa tokea mechi ya kwanza kuwa kocha anajua kuusoma mchezo, ni mthubutu, ana mbinu nyingi kisa tu katolewa Chama. Ngoja tuendelee kuvuta muda tuone uwezo wake
Ana mapungufu mengi sana hafanyi sub kwa wakati kuna muda sawadogo alinyoosha mikono juu atoke kocha hakujali bdae ilimbidi akae chini nikaona anaombwa n bocco aendelee lakini wapi
Sikuona ulazima wa kutolewa baleke nje wakati mbele alikuwa analazimisha mabeki kufanya makosa halafu anamuingiza kyombo huyu kocha sijui
 
Ndiyo "excitement" yenyewe hiyo na ndiyo raha ya mpira hiyo. Nguvu ya kila timu inabalance, siyo timu inajihakikishia kushinda mechi 10 mfululizo, excitement itatoka wapi?

Simba wakiweza kujenga stamina na fitness nzuri ya wachezaji na kuweza kupossess mpira, hii kasi itasumbua timu nyingi.

Hapana msijenge stamina na fitness ili mbakie kwenye mpira wa excitement. Usiwe kigeu geu
 
robertinho hata me simuelewi mfumo wa 4-4-2 hautulipi. Wachezaj hakai na mpira hata dk 2 jamani ni kubutua tu kwenda mbele
 
robertinho hata me simuelewi mfumo wa 4-4-2 hautulipi. Wachezaj hakai na mpira hata dk 2 jamani ni kubutua tu kwenda mbele
Niambie timu duniani inayokaa na mpira kwa dakika 2. Hayo ni madhaifu ya wachezaji wengi wa kitanzania. Wakitaka kukaa na mpira wanacheza slow sana.

Soma uzi huu niliongelea kuhusu mifumo mbalimbali na kwa nini mfumo wa Uingereza haufai katika ligi yetu.

Tufumue mfumo wetu wa soka kwa kuingia mkataba na Ujerumani
 
Back
Top Bottom