Simba SC yamtangaza Sven Vander Broeck kuwa kocha mpya akichukua mikoba ya Patrick Aussems

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Simba SC ambao ni Mabingwa wa Nchi, leo Desemba 11, 2019, imetangaza Kocha Sven Vander Broeck kuwa kocha mkuu mpya akichukua mikoba ya Patrick Aussems.

Vander Broeck Mbelgiji, amewahi kuifundisha timu ya Taifa ya Zambia pia alishinda ubingwa wa Afrika AFCON akiwa kocha msaidizi katika timu ya Taifa ya Cameroon mwaka 2017.

Klabu ya Simba SC kwenye taarifa yake imesema kwamba, inaamini kocha Sven Vanderbroeck ataleta matokeo chanya na klabu imeahidi kumpa ushirikiano ili kutimiza malengo ya klabu.

This Is Simba SC Next Level.........SimbaNguvuMoja

 
Mkuu hongereni kufanikisha mchakato kwa haraka, vipi mbona hujashusha CV yake au na wewe hujaipata?
 
haka kakocha kachalii kalitimuliwa Zambia kwa aibu, simba kweli mbumbumbu, hakuna kocha hapa, mmeenda kuokota kocha wa bei rahisi na kumfukuza Ausem kwa ajili ya wshahara mkubwa. huyu chalii haifikishi simba kokote, ndio maana kapewa mkataba wa mwaka mmoja maana HAAMINIKI ?
 
kama nyinyi mlivyomwokota Mkwasa ambaye Taifa stars ilivunja naye mkataba baada ya kuwa na maatokeo yasiyoridhisha ikiwemo kufungwa goli 7 na Algeria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…