Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Mnyama Mkali Mwituni, Simba SC kutoka viunga vya Msimbazi jijini Dar es salaam, katika kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya Ligi Kuu, michuano ya Kimataifa msimu wa 2022/23 leo Agosti 3, 2022 imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa kiungo nyota wa Nigeria Nelson Esor Bulunwo Okwa (28) kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya River United ya nchini Nigeria.
Nyota huyu ambaye msimu uliopita kwenye Klabu ya River United ambao ni Mabingwa wa Ligi Kuu nchini Nigeria alicheza michezo 24 na kufanikiwa kufunga mabao mawili huku akitoa pasi za mwisho za mabao manne, amekuja kuongeza ubunifu eneo la katikati ya dimba ndani ya Simba SC.
Okwa pia ana uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji, lakini kwa klabu ya River United walimtumia kama kiungo wa kati ambapo kazi yake kubwa ni kulinda vema nafasi ya ulinzi, kwani ni mwepesi wa kupora mipira kwa wapinzani na kuanzisha mashambulizi kwa haraka na nguvu.
Kwa usajili huu wa Okwa ni dhahiri kuwa Simba SC wamedhamiria kuimarika zaidi eneo la katikati ya dimba, ambapo Kocha Zaron Maki atakuwa na viungo haswa kuamua kuwatumia nani aanze kulingana na mechi...Mkude, Akpan, Okwa, Mzamiru, Kanoute.
...Kulipewa Mwana Kulitaka Mwana....
Nyota huyu ambaye msimu uliopita kwenye Klabu ya River United ambao ni Mabingwa wa Ligi Kuu nchini Nigeria alicheza michezo 24 na kufanikiwa kufunga mabao mawili huku akitoa pasi za mwisho za mabao manne, amekuja kuongeza ubunifu eneo la katikati ya dimba ndani ya Simba SC.
Okwa pia ana uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji, lakini kwa klabu ya River United walimtumia kama kiungo wa kati ambapo kazi yake kubwa ni kulinda vema nafasi ya ulinzi, kwani ni mwepesi wa kupora mipira kwa wapinzani na kuanzisha mashambulizi kwa haraka na nguvu.
Kwa usajili huu wa Okwa ni dhahiri kuwa Simba SC wamedhamiria kuimarika zaidi eneo la katikati ya dimba, ambapo Kocha Zaron Maki atakuwa na viungo haswa kuamua kuwatumia nani aanze kulingana na mechi...Mkude, Akpan, Okwa, Mzamiru, Kanoute.
...Kulipewa Mwana Kulitaka Mwana....