Simba wadhamiria kukamilisha uwanja wao, Mo Dewji achangia Bilioni 2

Jamaa mjanja Sana, kasha wakimbia tayari. Yaani uwanja wa watu 30, 000/= unao karibia thamani ya 40 bilion unachangia 2 bilion kweli?
wewe kweli zuzu.

Watu 30,000/= ndiyo kitu gani hiki Utopolo. Duuuh! Kweli mnaweweseka!
 
Eti nachangia billion 2!

Na mm kwa kutambua mchango wa kuwa na uwanja wetu binafsi kama timu kubwa barani Afrika, naanza kuchangia Milioni Moja
Wewe ni utopolo tunakujua vizuri.

Nendeni mkazuie Yale maji pale jangwani kwanza
 
Mkuu kwa muda mchache niliokuwepo hapa jukwaani, niseme wazi wewe ni KILAZA na uonapo komenti yangu usiiquote. Huna logic, umejaza mafua kichwani.
 
kwanza uwanja wenyewe tayari unaitwa mo - arena!
 
Kama kampuni ni ya MO kwa 49% kwanini hao wengine wenye 51% wasichangie na badala yake unataka MO peke yake achangie?
 
Mkuu kwa muda mchache niliokuwepo hapa jukwaani, niseme wazi wewe ni KILAZA na uonapo komenti yangu usiiquote. Huna logic, umejaza mafua kichwani.
lete logic.

Azam Ni mali binafsi ya Bakhresa ndiyo maana anagharamia kila kitu.

Simba ni timu ya wanachama. Mo ni mwekezaji na ameshaweka dau lake la uwekezaji. Na hapa hatujui kwanini Mo katamka HELA kabla ya analysis.

Kwangu mm Mo katoa km shabiki kwasabab hata analsis haijafanyika.Amepata wapi nguvu ya kutamka kwamba atachangia.Kuchangia maana yake ni mchango wake wa hiari.

Na ishu hapa hatujui mkataba wa simba na Mo unasemaje.

Au weka huo mkataba wa uwekezaji ili tuone terms zake km Mo anatakiwa kujenga uwanja.Kimsingi tuwaachie Simba.

Ukishindwa utakuwa umejaza kamasi kichwani.

Ongea ukweli wako unaoujua kuhusu Mo na Simba, Bakhresa na Azam.Halafu uonyeshe sasa ukilaza wangu.

Nik tayari kuelimisha na kufahamishwa. Elimu ni bahari, tunajifunza kila siku.

Karibu!
 
Kama kampuni ni ya MO kwa 49% kwanini hao wengine wenye 51% wasichangie na badala yake unataka MO peke yake achangie?
Ndio maana nimesema kabla ya yeye kutoa hizo bil 2, ilipaswa kufanyika analysis juu ya gharama ili kila upande utoe pesa kwa % stahiki.
 
Wabongo upande wa kuchangia...... wagumu Simba mwaka jana walikuja na idea nzuri sana wanachama wa Simba wawe na electronic card kila card ada yake kwa mwaka ilikuwa 14000.Mpaka sasa nina uhakika kadi zilizo chukuliwa hazikuzidi,timu hizi mara nyingi, zinaendeshwa na matajiri ili waendelee kupiga hela.
 
UNA ELIMU GANI WEWE??
Nyie mko wanachama 30k mnamiliki 51% na yeye yuko peke yake anamiliki 49% huoni tatizo kabisa??
Aisee
Nina Elimu ya namba iliyonifunza kuwa mwenye 49% amezidiwa na mwenye 51%
 
Mkuu kwa muda mchache niliokuwepo hapa jukwaani, niseme wazi wewe ni KILAZA na uonapo komenti yangu usiiquote. Huna logic, umejaza mafua kichwani.
wewe ni nini Cha maana unachopost humu?

Hapa umeleta hoja ipi kunipinga au kuniprove wrong?

Sluggish!
 
Wewe ni kilaza, pitia hoja zako zote kila uelimishwapo kuhusu SIMBA unajaza mafua kichwani. SIKIA MO NI MMILIKI HALALI WA SIMBA KWA 49% na WANACHAMA WANAMILIKI 51% Kwahiyo KAMA ILIVYO AZAM AMBAPO BAKHRESA ANAMILIKI KWA 100% NA SIMBA INAMILIKIWA KWA 49% NA MO. HIVYO NI JUKUMU LAKE KUJUA GHARAMA ZA UWANJA NA KISHA AKAE YEYE NA WANACHAMA WAGAWANE KULINGANA NA UBIA WAO AMBAO NI 51% KWA 49%.

Unapochangia kitu tuliza akili yako na acha ushabiki wako wa kimpira usio na maana.
Kwa mfano wewe ukichangia hiyo pesa na UWANJA UKAJENGWA hujui kuwa UTAKUWA MALI YA MO KWA 49%?? kwa maana itakuwa ni ASSET ya SIMBA?
Sasa kwanini atake mchangie wakati anajua wazi kuwa yeye ni mmiliki? Anataka tumpe mtaji aongezee kwenye mtaji wa AWALI?
 
Simba Sc ya sasa inauwezo wa kufanya jambo lolote wakiamua kutokana na LEVEL yake kwa sasa AFRICA kama swala la kujenga uwanja ni kitu kidogo sn wakiamua kuingia BANK yoyote AFRICA kuomba LOAN haitachukua hata dakika moja ombi Lao la mkopo litakubaliwa kwa hela yoyote watakayo itaka.

Sent from my SM-G975F using JamiiForums mobile app
 
Si mkiwacheka yanga eti bakuli fc kwahiyo na nyie muitwe kapu fc
 
Kwa bajeti nzuri na kubwa duniani kote, Viwanja hutumia mpaka miaka minne au mitano kukamilika, vile vya kuanza kabisa chini! Hivyo unahitaji resource za kutosha sana, maana kuchanga tu Watu watachoka

Klabu nyingi duniani zimeingia ubia na Makampuni makubwa katika ujenzi wa Viwanja vyao kisha kukubaliana suala la mapatano kuhusu malipo

Mfano Atletico Madrid baada ya kuvunja Vicente Calderon na kujenga uwanja mpya chini ya udhamini wa Kampuni ya wachina wakakubaliana kwenye naming rights

Uwanja unaitwa METROPOLITANO ila kutokana na sababu za kibiashara unaitwa WANDA METROPOLITANO, hii Wanda ni Kampuni ya Kichina

Hivyo Simba wanaweza kuingia ubia na Kampuni moja Tajiri, jumlisha na pesa yao wakapata uwanja mzuri, wa kisasa na wenye kuingiza hata Mashabiki 30,000 sio mbaya sana

Ni ukweli mchungu kuwa huwezi kusimamisha uwanja wa hadhi ya Simba kwa michango tu mfukoni, bali kumeza vidonge vichungu vya kukopa, kuingia ubia na Kampuni Ili kufanikisha!

Pia Simba wajiandae kusacrifice kipindi cha miaka hadi mitano ya kufanya vibaya uwanjani kwasababu watashindwa kufanya vizuri ktk masoko ya usajili wa wachezaji bora wenye gharama kwasababu ya Pesa nyingi imeelekezwa kwenye ujenzi wa uwanja

Waitishe Mkutano Mkuu wa dharura kukubaliana, kujenga uwanja ni Uamuzi wa hasira, sasa ni hatari sana kufanya maamuzi ingali na hasira, hivyo kuzifanya hasira ziwe rasmi wanapaswa kuitisha Mkutano Mkuu wakubaliane, kwenye faida na hasara pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…