Simba waziponda Sh milioni tatu za GSM, zilikuwa ndogo sana, wataja lengo la mkataba

Simba waziponda Sh milioni tatu za GSM, zilikuwa ndogo sana, wataja lengo la mkataba

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amefunguka mambo kadhaa kuhusu udhamini uliositishwa.

Ni kuhusu GSM kutangaza kuvunja mkataba wa kuwa mdhamini mwenzake wa Ligi Kuu Bara:

“Simba hatukukubaliana na mkataba huo, tulipambana lakini wenzetu hawakuona kama tuko sahihi, tulionyesha njia, tulionyesha ujasiri wetu, wakati ule hawakutuelewa, hatimaye wametuelewa.

“Tunawapongeza TFF kwa kupambana kutuletea mdhamini, haikuwa jukumu lao ni jukumu la klabu, lakini hiyo isitumike kama fimbo ya kuleta kila aina ya mdhamini, ifike hatua nionyeshe thamani ya kile ambacho tunatakiwa kukipata.

“Kuipa timu shilingi milioni tatu kwa mwezi, timu ya Ligi Kuu ni thamani ndogo, kuna wakati inakulazimu kuonyesha thamani yako.

“Anayetoa hela ndogo anapata nafasi kubwa ya kutangazwa, msimu uliopita hatukuvaa nembo ya mdhamini mwenza.

“Shida ni kwenye klabu zenyewe pia, huu ulikuwa mwezi wa pili unaenda wa tatu lakini hakukuwa na hela zilizoingia, kwa nini klabu hazikulalamika? Kwa nini Bodi ya Ligi yenyewe hailalamiki?

“Walitangazwa na timu zote lakini unavunja mkataba kisa tu Simba, basi lengo lao lilikuwa Simba, unataka kukuza soka kisha unasitisha udhamini sababu ya timu moja!”
 
[emoji1313][emoji1313]
IMG-20220207-WA0147.jpg
 
Kwanza mazingira ya mkataba yenyewe yalifanyikia gizani huku walipokuja kuwasilisha makubaliano yao wakaweka komeo la siri na kuweka kauli za vitisho watu wasihoji na kwamba makataba huo ni kati ya TFF na GSM

Fact ya Simba kukataa kuvaa nembo ya GSM kwenye jersey yake ilikuwa nyepesi sana na logically, kama mkataba unahusu GSM na TFF basi hakuna sababu ya Simba kuvaa nembo ya GSM au kuweka mabango uwanjani yake kwenye mechi za Simba na badala yake hizo nembo zivaliwe na viongozi wa TFF na hayo mabango yapelekwe pale karume kwenye ofisi zao

Ile mikwara ya bumbuli kumvagaa dauda kumwambia kwenye nchi hii yanga akitaka kufanya kitu hakuna wakuzuiliwa na sasa watake wasitake watavaa tu yuko wapi?

Saizi naona wamebadili msemo kwamba club zinazoumia ni hizi ndogo, lakini hapo hapo pia tunaambiwa katika kipindi hicho cha mkataba huo kusainiwa hakuna timu ambayo ilipokea chochote. Sasa ni mjinga gani anaweza akaamini kuwa uwepo wa GSM kama co sponsorship una impact kwa club hizo?
 
Kwanza GSM afunguliwe kesi ya udanganyifu na uhujumu uchumi, aweke rehani hata vile vigodoro akili imkae sawa
Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja
 
Hoja hizi nzito za Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally zinaonyesha jinsi alivyo very Intelligent kuliko Morons Haji Manara na Hassan Bumbuli ( Wasemaji wa Yanga SC ) na kwamba amesoma na Kuelimika vyema Kitaaluma hivyo Simba SC hawakukosea Kumuajiri hapo.
 
Hoja hizi nzito za Msemaji wa Simba SC Ahmed Ally zinaonyesha jinsi alivyo very Intelligent kuliko Morons Haji Manara na Hassan Bumbuli ( Wasemaji wa Yanga SC ) na kwamba amesoma na Kuelimika vyema Kitaaluma hivyo Simba SC hawakukosea Kumuajiri hapo.
Sijaona hoja ya maana pale!
 
Kwanza GSM afunguliwe kesi ya udanganyifu na uhujumu uchumi, aweke rehani hata vile vigodoro akili imkae sawa
Maskini siku zote mnatamani kuona matajiri wakishindwa, na hivyo kuwa maskini kama nyinyi.

Ulichokiandika hapa ni sawa tu na dua la kuku. Kamwe haliwezi kumpata mwewe.
 
Aliyetaka mkataba usihojiwe ni nani? Ni gsm au ni tff? Unaona sasa uelewa wako umeegemea kwenye ushabiki napoteza mda hapa kubishana na wewe
Mkataba ulikuwa na makubaliano hayo, kwamba hiyo ifanyike siri watu wengine wasijue na ndio maana hukumuona GSM kuipinga TFF kwamba ameenda kinyume na makubaliano

Tff wangetoa tamko ambalo lilikuwa na madhara kimkataba linalopingana na makubaliano ya mkataba na GSM unafikiri GSM angekaa kimya kwasababu ni TFF?

Kwanini GSM hakutoka public kama alivyofanya leo kukemea TFF kwa kitendo cha kutoa kauli ya kudhibiti watu wasiweze kuhoji mkataba wao ambao haikuwa makubaliano kuwa watu wasihoji?

Huoni kwamba kwa ukimya wake na namna ambavyo wapambe wake walivyokuwa wanatamba ni dhahiri kabisa kua kilichofanywa na TFF kilikuwa na baraka ya GSM
 
Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja
Mkuu, mbona povu kama lote! Acha GSM awajibike kuwalipa waliotumikia mkataba kwa miezi mitatu. Si mlisema mmeinunua ligi nzima pamoja na kombe la mapinduzi, kumbe hata 200M tu hamuwezi kutoa!
 
Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amefunguka mambo kadhaa kuhusu udhamini uliositishwa.

Ni kuhusu GSM kutangaza kuvunja mkataba wa kuwa mdhamini mwenzake wa Ligi Kuu Bara...
Walitangazwa na timu zote lakini unavunja mkataba kisa tu Simba, basi lengo lao lilikuwa Simba, unataka kukuza soka kisha unasitisha udhamini sababu ya timu moja!”
 
Maskini siku zote mnatamani kuona matajiri wakishindwa, na hivyo kuwa maskini kama nyinyi.

Ulichokiandika hapa ni sawa tu na dua la kuku. Kamwe haliwezi kumpata mwewe.
GSM bado ni mpambanaji kama mimi na ana safari ndefu ya kujiimarisha kiuchumi na wala sioni maajabu yeyote ya wewe kumfanya aonekane tajiri kiasi cha watu kuogopa kusema madhaifu yake.

Hilo la dua la kuku halimpati mwewe lilizungumzwa sana kipindi kile babra ameweka msimamo wake wa kutotambua udhamini wa GSM na tuliposema kwamba ipo siku huu mkataba utapolomoka kwa aibu mkasema dua la kuku halimpati mwewe.

Yes huwenda ni kweli dua la kuku halimpati mwewe ila cha kujiuliza ni kweli upande uliosimama wewe unawakilishwa na "mwewe" au panzi tu ambaye kwa kuku ni mboga inayolika kirahisi bila ubishi?
 
Kwanza GSM afunguliwe kesi ya udanganyifu na uhujumu uchumi, aweke rehani hata vile vigodoro akili imkae sawa
Hatimaye umeonesha uhalisia wako. mtu kama wewe eti ndio unapingaga uwepo wa mungu kumbe jinga tu
 
Hatimaye umeonesha uhalisia wako. mtu kama wewe eti ndio unapingaga uwepo wa mungu kumbe jinga tu
Utagundua vingi sana, utanibashiria mambo mengi kuhusu mimi, utaongea mambo lundo mabaya just to irritating me lakini utasahau kua moja ya sifa yangu kubwa ambayo huijui ni kua hata mimi sifa hiyo siijui

Umejua?
 
Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja
matusi ya nini 😂😂😂
dawa imewaingia tayar
 
Yaan hua tunalaumu serikali pale inapoingilia Mambo ya soka ila kwa hili la Gsm walipaswa kufungwa, Mambo hayapaswi kuisha namna hii....
Naipenda sana Yanga ila sipendi makandokando katika soka, nasikia saev wanamtaka Morrison , tunapiga hatua moja mbele tunarudi hatua kumi nyuma
 
Back
Top Bottom