Simba waziponda Sh milioni tatu za GSM, zilikuwa ndogo sana, wataja lengo la mkataba

Simba waziponda Sh milioni tatu za GSM, zilikuwa ndogo sana, wataja lengo la mkataba

Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja
Povu la kutosha[emoji1787][emoji1787]
 
Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja

Acha mkwara mkuu!! Jibu hoja za wadau Wewe ni mdau wa mpira unaona ni Sawa simba kupewa milioni3 kwa mwezi? Kwakufanya matangazo kwenye kila mechi ya simba na jenzi kuwa na lebo ya GSM?
 
Kwanza mazingira ya mkataba yenyewe yalifanyikia gizani huku walipokuja kuwasilisha makubaliano yao wakaweka komeo la siri na kuweka kauli za vitisho watu wasihoji na kwamba makataba huo ni kati ya TFF na GSM

Fact ya Simba kukataa kuvaa nembo ya GSM kwenye jersey yake ilikuwa nyepesi sana na logically, kama mkataba unahusu GSM na TFF basi hakuna sababu ya Simba kuvaa nembo ya GSM au kuweka mabango uwanjani yake kwenye mechi za Simba na badala yake hizo nembo zivaliwe na viongozi wa TFF na hayo mabango yapelekwe pale karume kwenye ofisi zao

Ile mikwara ya bumbuli kumvagaa dauda kumwambia kwenye nchi hii yanga akitaka kufanya kitu hakuna wakuzuiliwa na sasa watake wasitake watavaa tu yuko wapi?

Saizi naona wamebadili msemo kwamba club zinazoumia ni hizi ndogo, lakini hapo hapo pia tunaambiwa katika kipindi hicho cha mkataba huo kusainiwa hakuna timu ambayo ilipokea chochote. Sasa ni mjinga gani anaweza akaamini kuwa uwepo wa GSM kama co sponsorship una impact kwa club hizo?
Well said bro, huu ni mkataba wa kihuni, Kwanza TFF walikubali vipi utekelezwaji kabla ya pesa yoyote kuingia? Tff wamekosa umakini kiasi hiki au ndio tuamini viongozi walihongwa na GSM?
 
Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amefunguka mambo kadhaa kuhusu udhamini uliositishwa.

Ni kuhusu GSM kutangaza kuvunja mkataba wa kuwa mdhamini mwenzake wa Ligi Kuu Bara:

“Simba hatukukubaliana na mkataba huo, tulipambana lakini wenzetu hawakuona kama tuko sahihi, tulionyesha njia, tulionyesha ujasiri wetu, wakati ule hawakutuelewa, hatimaye wametuelewa.

“Tunawapongeza TFF kwa kupambana kutuletea mdhamini, haikuwa jukumu lao ni jukumu la klabu, lakini hiyo isitumike kama fimbo ya kuleta kila aina ya mdhamini, ifike hatua nionyeshe thamani ya kile ambacho tunatakiwa kukipata.

“Kuipa timu shilingi milioni tatu kwa mwezi, timu ya Ligi Kuu ni thamani ndogo, kuna wakati inakulazimu kuonyesha thamani yako.

“Anayetoa hela ndogo anapata nafasi kubwa ya kutangazwa, msimu uliopita hatukuvaa nembo ya mdhamini mwenza.

“Shida ni kwenye klabu zenyewe pia, huu ulikuwa mwezi wa pili unaenda wa tatu lakini hakukuwa na hela zilizoingia, kwa nini klabu hazikulalamika? Kwa nini Bodi ya Ligi yenyewe hailalamiki?

“Walitangazwa na timu zote lakini unavunja mkataba kisa tu Simba, basi lengo lao lilikuwa Simba, unataka kukuza soka kisha unasitisha udhamini sababu ya timu moja!”
Ukiangalia sababu zilizotolewa na GSM kufikia uamuzi wa kusitisha mkataba wa udhamini wa ligi kuu ya NBC, asilimia 99 zimechangiwa na ukaidi wa Simba katika kutekeleza ma..
Soma zaidi hapa : Kwa hili TFF, Bodi ya Ligi wajitafakari
 
Tatizo watu weng wana shindwa kujua kuwa GSM NA TFF/BODI YA LIGI waliingia mkataba, na huo mkataba una vipengele ambavyo walikubaliana kuvi telekeza na vipo ambavyo vina weza kuvunja mkataba bila hata ya kutokea pande moja kusema.
1.GSM wao wametangaza kujiondoa kweny mkataba baina yao kwa kuangalia nature ya vipengele vyao walivyo pangiana.
2. GSM wakatoa na vipengele vilivyo vunjwa

Hivyo tunaomb TFF/BODI YA LIGI wao nao wa angalie jins ya kuvitetea hivyo vilabu

Note: mpira wetu umejaa siasa Sana na uyanga na usimba
 
Mo analipa Bei gani kwa kila tangazo kwenye jezi za Simba!?
Mo ni mdhamnini wa ligi?

Mo ana hisa kwenye club ya simba, yaani kile alichokuwa anakifanya GSM kwa yanga kabla ya mkataba huu ndicho anachokifanya MO kwa kuifadhili simba
 
Well said bro, huu ni mkataba wa kihuni, Kwanza TFF walikubali vipi utekelezwaji kabla ya pesa yoyote kuingia? Tff wamekosa umakini kiasi hiki au ndio tuamini viongozi walihongwa na GSM?
They didnt see it coming wali underestimate msimamo wa CEO wakidhani hawezi kuwa na madhara kwasababu wao ndio wakubwa wameahaamua

Hiyo dhana ilitengeneza kiburi kwa GSM na crew yake pamoja na mashabiki wa yanga, zilitumika lugha za kishujaa sana baada ya TFF kuidhinisha rasmi huo mkataba

Utakumbuka kua hasani bumbuli alimfata chamber shafii dauda na kumwambia kua Yanga ndio kila kitu kwenye hii nchi, hakuna kitu yanga itatala halafu kukawepo kikwazo cha kuzuia

Na akidai sasa hakuna namna Simba itaepuka mkono wa GSM (hiyo baada ya zile jersy za Simba ku leak zikiwa zina chata ya GSM)
 
They didnt see it coming wali underestimate msimamo wa CEO wakidhani hawezi kuwa na madhara kwasababu wao ndio wakubwa wameahaamua

Hiyo dhana ilitengeneza kiburi kwa GSM na crew yake pamoja na mashabiki wa yanga, zilitumika lugha za kishujaa sana baada ya TFF kuidhinisha rasmi huo mkataba

Utakumbuka kua hasani bumbuli alimfata chamber shafii dauda na kumwambia kua Yanga ndio kila kitu kwenye hii nchi, hakuna kitu yanga itatala halafu kukawepo kikwazo cha kuzuia

Na akidai sasa hakuna namna Simba itaepuka mkono wa GSM (hiyo baada ya zile jersy za Simba ku leak zikiwa zina chata ya GSM)
GSM amezungukwa na watu wenye uwezo mdogo Sana na wanaoendeshwa kwa mihemuko. Amekosa watu Makini wa kumshauri. Ngoja aingie hasara atajifunza tu.
 
Yanga hawakuwa tayari kudhaminiwa na Vodacom kisa rangi ya logo, Vodacom walikubali kubadili rangi
The same happened kwa NBC
 
Kwanza GSM afunguliwe kesi ya udanganyifu na uhujumu uchumi, aweke rehani hata vile vigodoro akili imkae sawa
Haya maneno ya sisi masikini, ni maneno ya kwenye kanga.

Mwenye pesa hawezi ongea utumbo kama huu!
 
Haya maneno ya sisi masikini, ni maneno ya kwenye kanga.

Mwenye pesa hawezi ongea utumbo kama huu!
Utofauti unakuja tunapo tofautiana kwenye SI Unit ya kupima kujua yupi mwenye pesa na nani mpambanaji anaye fight kujiweka sawa

Mwenye pesa hawezi badilisha jina la kampuni ili kukwepa kodi
 
TBC ana mabango yake na ametoa Mil 300 tu mbona Makolo hawajasema ni ndogo
 
Unakazwa wewe sio bure, unaelewa nini juu ya masuala ya mikataba! Wewe ni nani ameshakuja kuhoji mkataba wako na mwajiri wako? Mbona umemficha ata mkeo/mmeo mshahara unaopokea? Unapata wapi nguvu ya kuhoji mikataba ya wenzako, funga bakuli kwa vitu usivyovijua utakuja kuvalishwa dela siku moja
Fisadi mkubwa wewe,nenda ZAKO unatuhalibia ligi yetu
 
TBC ana mabango yake na ametoa Mil 300 tu mbona Makolo hawajasema ni ndogo
TBC hawekwi kwenye jezi ya timu yoyote, na kama timu zimekubaliana na TBC kwenye matangazo ya redio na ikiwa ni redio ya taifa haina shida.
TBC hawakua na mikwara yoyote ya kusema mtake msitake tutatangaza.
 
Simba wana viherehere style yasitaki mbichi hizi
 
Licha ya timu 15 za ligi kuu, isipokua moja tu, kuvaa logo yake na kuweka mabango yake viwanjani, muuza magodoro, ambae ni bwana wa yule mchumia tumbo, ameona magodoro yake hayauziki bila kutangazwa na chama kubwa Afrika mashariki na kati Simba Sc, ndio mana ameshindwa hata kuwalipa hizo timu 15 kwa kazi waliyoifanya ya kumtangaza kwa kipindi hicho cha miezi 3.
 
Licha ya timu 15 za ligi kuu, isipokua moja tu, kuvaa logo yake na kuweka mabango yake viwanjani, muuza magodoro, ambae ni bwana wa yule mchumia tumbo, ameona magodoro yake hayauziki bila kutangazwa na chama kubwa Afrika mashariki na kati Simba Sc, ndio mana ameshindwa hata kuwalipa hizo timu 15 kwa kazi waliyoifanya ya kumtangaza kwa kipindi hicho cha miezi 3.
Uhuni tu, Kama kawaida vyura washaanza kukalamika huko.
 
Barbara amesema atachukua nafasi ya udhamini ulioachwa na GSM ila iko siku sisi Simba tutakuja kuwakumbuka GSM na siku yenyewe haipo mbali
 
TFF ndiyo imefeli usimamizi wa soka hapa bongo,huo mkataba wao na GSM viongozi walitanguliza matumbo yao mbele bila kuangalia maslahi ya vilabu
Siyo mbaya kwa TFF kutafuta wadhamini wa ligi ishu ni kuwa hawakuweka mambo wazi leo yanavurugika inaonekan GSM amefeli kumbe shirikisho letu ndiyo lilikubal masharti ya kinyonyaji na kutaka vilabu visihoji mambo
Me naona Tff wawajibike kulipa vilabu vilivyovaa logo ya GSM..
Kwani hao GSm wameshindwaje kupitia mlango ambao NBC walipitia
 
Back
Top Bottom