Simba yaachana na Haji Manara, Ezekiel Kamwaga ateuliwa kukaimu nafasi ya Msemaji wa Simba

Simba yaachana na Haji Manara, Ezekiel Kamwaga ateuliwa kukaimu nafasi ya Msemaji wa Simba

View attachment 1871232

======

View attachment 1871250

Hajj Manara mwisho wake ni leo, Gsm poleni sana yuda iskarioti is out, Ezekiel ni kama vile anapewa miezi miwili ya transition ili kuendeshwa kitofauti na kusafisha u snitch ulisababishwa na tamaa za kuchukua mahela ya kuishi kifahari mjini.
Nichukue nafasi hii adhimu kabisa Kumpongeza Kaka yangu katika Fani ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma Ezekiel Kamwaga kwa Kuteuliwa huku Kukaimu hii nafasi.

Ni Mwandamizi Kwangu, Mweledi, Msikivu, Mwelewa na Kubwa kabisa Ezekiel Kamwaga ameiva si tu Kimaadili bali hata kwa Hekima na Busara.

Ana Shule (Elimu) nzuri na pia ni Mzungumzaji mzuri mwenye kujua wapi aseme nini na wapi pia asiseme. Hata alipokuwa na nafasi hii huko nyuma kabla Simba SC haijaiingia katika Mabadiliko aliitendea Haki hiyo (hii) nafasi tuliokuwepo tuna Ushahidi nalo.

Na Kitu pekee ambacho GENTAMYCINE nakipenda kwa Kaka Ezekiel Kamwaga hata akiwa 'Newsroom' kote alikopita ni Mtu asiyependa Makuu Wala Sifa za Kijinga kama si za Kipumbavu kama za Mtangulizi wake aliyekuwa Mnafiki na Chawa.

Tafadhali sana Kaka (Comrade) Ezekiel Kamwaga nimekumwagia Sifa zote hizi kwakuwa GENTAMYCINE nakujua vyema kwani katika Tasnia ya Uandishi wa Habari (hasa za Michezo) nchini Tanzania Wewe si tu ni Mwandamizi bali pia ni Nguli hivyo usiniangushe nikaja Kuumbuka na Kuchekwa hapa.

Yale mema (mazuri) ya Mtangulizi wako Haji Manara yaboreshe Kiufanisi zaidi ila yale yake mengi ya Kipuuzi tafadhali nakuomba mwachie nayo Mwenyewe ili akayaendeleze huko kwa waliokuwa wakimtumia 'Kutuumiza' wana Simba SC kila inapocheza na Yanga SC hasa katika Mechi za Ligi Kuu ya Tanzania (VPL)

Mwisho kabisa nichukue nafasi hii pia Kuupongeza Uongozi wa Simba SC kwa Kumteua Kaka yangu katika Fani Ezekiel Kamwaga Kukaimu nafasi hii na GENTAMYCINE ambaye najua hata nyie ( Viongozi wa Simba SC huwa mnaniheshimu ) niwaombeni tu hata msipoteze muda wenu mwingi Kumthibitisha kuwa Msemaji wetu Mkuu wa Simba SC kwani ana Sifa zote 'tukuka' ya Kushika hicho Cheo na hapa kwa Ezekiel Kamwaga Klabu ya Simba imefanya Usajili wa Thamani Kubwa katika Uongozi na Utendaji wa Klabu.

Ezekiel Kamwaga Mungu akakusimamie.
 
Wapi picha ya Kamwaga tumuone?
Yupo kushoto kwa January 🤣👇
20210728_105451.jpg
 
Pamoja na kweli kua Simba imempatia jina kubwa na kuanza kupata deals nyingi nyingi,

lakini ukweli ni lazima usemwe pia Haji Manara alijitahidi kwa dhati kuchochea ukuaji wa jina la Simba kuimaridadisha na niukweli ameongeza washabiki ambao hawakupenda sana mpira kuichagua Simba kama timu yao rasmi.

Umaarufu ulimzidi, ukaanza kumpa kibri,ndio kosa kubwa alilolifanya na hapo ndipo ukawa mwisho wake.
 
Nichukue nafasi hii adhimu kabisa Kumpongeza Kaka yangu katika Fani ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma Ezekiel Kamwaga kwa Kuteuliwa huku Kukaimu hii nafasi..
sasa muraaa haiwezekani kwenye hayo mabadiliko kukawa na kitengo cha amshaamsha cha mtandaoni? chawa kama mwijaku wapiga kelele ila wasitambulike kimuundo wa ajira hapo klabuni, lopolopo lao liwe kupewa posho zisizo rasmi
 
Watani zetu Simba SC wameamua kuenenda KIPROFESHENI....

Wamesema ndg.Haji Manara ameomba kuachana nao na sikuona neno kuwa AMEONDOLEWA katika nafasi yake 🤣🤣🤣

#DaimaMbeleNyumaMwiko
Umesoma vizuri wamesema wanamshukuru kwa maneno yake ya kuwaaga, kwa kiufupi wamemchukia sana, ni nafasi yake sasa kuomba nafasi ya kudumu Gsm
 
Kwahiyo ombi la Mwijaku kutaka nafasi ya Manara simba hawajaiona[emoji81][emoji81][emoji81]
 
Mchukueni sasa mbona mnalialia baada ya kitendea kazi chenu kunyofolewa.
Manara hakua na msaada wowote kwetu amini nakuambia, mmetafuta tu sehemu ya kummwaga, jamaa alikua honest sana, tena kwa taarifa yako ushawishi wake uliwafanya hadi aweze kuwashawishi wachezaji baadhi waje kwenu,pale mmepoteza jembe mnajikaza tu
 
Niseme tu Idara ya Usemaji ya Simba SC sasa inaenda Kuheshimika si tu ndani ya Tanzania bali hata Nje ya nchi na kwa 'Corporates' mbalimbali kuliko ilivyokuwa hapo awali ambako ilikuwa chini ya Muhuni, Mpuuzi na Mswahili aliyepigwa chini rasmi.
🤣🤣Genta unatisha.

Usiku wa manane umebipu asubuhi SSC WAMEIPIGA NGOMA...🤣🤣

Tabia ya Komredi mwenzangu Haji Manara akiwa SSC imeacha alama za FUNZO kwake mwenyewe na kwa kila kijana....

FUNZO kuwa KUJITAMBUA ,ADABU ,NIDHAMU ,HEKIMA NA KUJISHUSHA KIBUSARA ndio nguzo ya MAFANIKIO........

#DaimaMbeleNyumaMwiko
 
alishawahi kuwa simba msemaji zamani pia ni mwandishi mzoefu sema nimekumbuka kisa kimoja nimecheka sana, simba ilikuwa inafanya vibaya miaka hiyo ikatokea vurugu pale msimbazi jamaa alitimuka mbio vibaya sana akaruka ukuta huku nyuma kawaachia manyoya ila ilikuwa ile simba yenye shida za pesa hata mshahara ilikuwa shida
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Manara pamoja na sifa zake,kajitahidi Sana kuitangaza Simba
Acheni Upuuzi na Upofu wa Akili hata wakati wa akina Seydou Rubeya, Juma Nkamia na Clifford Ndimbo Simba SC ilitangazika vyema kuliko mnavyopotosha hapa.

Halafu acheni kuwa Wapumbavu ( Fools ) Simba SC haijatangazika kwa sababu ya uwepo wa Haji Manara bali ni Mafanikio ( Performance ) ya Simba SC Uwanjani ndiyo imeitangaza zaidi.

Barcelona FC, Liverpool FC, Bayern Munich na PSG zimetangazika ( zinajulikana ) kutokana na Maafisa Habari wao? Umeshawajua Maafisa Habari wao tokea uanze Kufuatilia Masuala ya Mpira?

Mnatukera na huyo Mpuuzi Mwenzenu.
 
Back
Top Bottom