Simba yatambulisha mshambuliaji mpya kutoka Ivory Coast Freddy Michael Kouablan

Simba yatambulisha mshambuliaji mpya kutoka Ivory Coast Freddy Michael Kouablan

Shadeeya Aione kwenye kwenye jalada kwa ajili ya ufuatiliaji.
Musonda alisajiliwa Yanga kwa kuangalia current performance lakini haku click katika eneo la ufungaji. Onana alisajiliwa kwa kuangalia current performance naye amegeuka adui ya wana Simba. Onana alipotoka alikuwa anaongoza kwa magoli, Musonda alipotoka alikuwa anaongoza kwa magoli ila wameshindwa kuonesha makeke yao katika ufungaji wa magoli.

Ondoa matarajio makubwa katika usajili mchezaji anaweza kuwa bora au asiwe bora japo alikuwa na profile kubwa atokako. Au anaweza akawa bora japo hakuwa na profile kubwa hatokako. Angalia profile ya Joseph Guede kwa upana wake hapa.
Alikuwa na magoli 23

IMG_20240116_080035.jpg
 
Uzi unahuzunisha na kuchekesha ...

Unachekesha hapo kwa mwana parokia mpya wa Uto mtakatifu Joseph

Unahuzunisha hapo kwa Baleke na Phiri...yani mm nilikua nampenda Baleke anavyoshangilia mabao ya wenzie kwa moyo wote...sijui nini kilimkumba jamani akawa kama amepigwa zongo..msimu uliopita alikua tishio...
 
Uzi unahuzunisha na kuchekesha ...
Unachekesha hapo kwa mwana parokia mpya wa Uto mtakatifu Joseph
Unahuzunisha hapo kwa Baleke na Phiri...yani mm nilikua nampenda Baleke anavyoshangilia mabao ya wenzie kwa moyo wote...sijui nini kilimkumba jamani akawa kama amepigwa zongo..msimu uliopita alikua tishio...
Kaka wewe una Dvision Zero ya mpira yaani hujui kitu kabisa.
 
Ndugu yake Makonda, anyway hongereni simba tumpe muda maana wabongo tunajikuta wenyewe muda sio mrefu mtaanza kuanzisha uzi hapa
 
kuhusu wanaokuja ni kamari hatuna uhakika, ila kuhusu wanaoachwa naamini ni mapendekezo ya benchika maana haoni wakiifaa simba , ukizingatia simba itahitaji kuwa vizuri kwa mechi zote zilizobaki msimu hii ili kujaribu kutimiza malengo...
 
Uzi unahuzunisha na kuchekesha ...
Unachekesha hapo kwa mwana parokia mpya wa Uto mtakatifu Joseph
Unahuzunisha hapo kwa Baleke na Phiri...yani mm nilikua nampenda Baleke anavyoshangilia mabao ya wenzie kwa moyo wote...sijui nini kilimkumba jamani akawa kama amepigwa zongo..msimu uliopita alikua tishio...
Ishu ya Baleke klabu haijatoa taarifa yyt bivyo bado ni tetesi tu
 
Naona bado hamjajifunza kitu kuhusu usajili. Usajili ni kamari, mchezaji anaweza kuwa top scorer huko alipo ila akaenda timu nyingine aka floppy au mchezaji akatoka timu nyingine akiwa wa kawaida ila akaenda timu nyingine aka shine. Mifano ipo mingi kwenye hili. Hivyo subirini wachezaji muwaone uwanjani.
Kama ni kamari basi hakuna sababu ya ku point finger kuwa mchezaji tuliyemleta ni mbovu.

Kiufupi kwa hoja yako inaonesha hautakiwi ku criticize chochote kwenye usajili mpya
 
Tuwape muda.. wachezaji wageni ....

baleke bado ni bonge la mchezaji, ..mpambanaji .na yule jamaa ni ngumu kumpora mpira mguuni ..kupanda na kushuka Kwa viwango ni kawaida
 
Mt. Joseph parokia ya Ivory Coast

Kutoka kwenye ukurasa wa James Sheka

Mfahamu, Joseph Guede Gnadou ambaye ni mchezaji mpya wa kikosi Cha Yanga SC raia wa Ivory coast, huyu ni mchezaji mwenye umri wa miaka 29 ambaye kazaliwa mwaka 1994 huko nchini Ivory coast.
Screenshot_20240116-113108.png

Mchezaji huyu ameanzia soka lake huko kwao Ivory coast katika Klabu ya USC BASSAM FC mnamo mwaka 2017 hii ilikuwa tarehe 01/08/2017 katika msimu wa 2017/2018. Msimu uliofuata wa 2018/2019 tarehe 01/07/2018 akajiunga na Klabu ya soka ya AFAD DJEKANOU FC ya huko huko kwao Ivory coast.
Screenshot_20240116-113040.png


Baada ya kuhudumu katika kikosi hicho Kwa mida wa msimu mmoja tu akaondoka na kwenda nchini Morocco kujiunga na Klabu ya soka ya Far Rabbat FC ambayo Kwa Sasa inafundishwa na kocha wa zamani wa YANGA SC bwana Mohamed Nabi, huu ulikuwa msimu wa 2019/2020.

Baadae msimu wa 2021/2022 tarehe 07/08/2021 akatolewa Kwa mkopo kwenda kujiunga na Klabu ya soka ya EMIRATES CLUB ya huko nchini Palestina, na baada ya mkopo wake kumalizika akarudi tena Far Rabbat FC ya Morocco tarehe 30/06/2022.

Msimu wa 2022/2023 uliisha akiwa Hana timu yoyote maana yake ni kwamba hakucheza msimu mzima mpaka unaisha Kwa sababu hakuwa na timu. Na msimu uliofuta wa 2023/2024 ambao ndio huu uko nusu Sasa hivo alipata timu huko nchini Uturuki katika ya TUZLASPOR FC hii ilikuwa tarehe 02/08/2023 akiwa kama mchezaji huru maana msimu wa nyuma yake hakuwa na timu.

Katika timu hii alifanikiwa kucheza Michezo 4 tu pekeee na hakuna goli lolote alilofunga Ndani ya timu yake hiyo ya Uturuki inayoshiriki ligi daraja la Pili lakini pia akiwa na Kadi ya njano Moja.

Ndani ya hii timu yake ya Uturuki, hakuweza kudumu Sana, badala yake alidumu Kwa muda wa mwezi mmoja na siku 13 pekee yaani alikaa siku 43 pekee kuanzia tarehe 02/08/2023 hadi tarehe 15/09/2023 Klabu hii ikavunja MKATABA wake kutokana na kiwango kibovu alichokionesha Ndani ya timu hiyo.

Na kuanzia hapo hakuwa na timu tena Kwa muda wa MIEZI 4 hadi hii Leo, Kwa maana hiyo Klabu ya Yanga imemsajili mchezaji ambaye hakuwa na timu yoyote maana yake ni kwamba wamesajili akiwa huru.

Tujiulize kidogo hapa, hivi timu zetu za Tanzania hazina uwezo wa kusajili mchezaji ambaye Yuko ACTIVE yaani ambaye anacheza na ana mkataba na timu yake?. HUYU NDIYE, (JOSEPH GUEDE GNADOU).#HOLYFINGERS
Screenshot_20240116-113129.png
 
Halafu huyu mbona kafanana na yule jamaa alisema kazaliwa mwaka 1990 wakati mama yake alikufa mwaka 1986 au yeye nini!?
 
Shadeeya Aione kwenye kwenye jalada kwa ajili ya ufuatiliaji.
🙏 Mtani hizi mambo zisikutishe hata.

Hata Mayele kipindi anakuja zilizagaa maneno za kutosha lakini mwisho wa siku akawa gumzo ndani ya Soka la TZ.

Hivyo subiri makubwa Uwanjani na hapo ndo uwezo wake utaongea na sio kwenye makaratasi.
 
Back
Top Bottom