Simba yatambulisha mshambuliaji mpya kutoka Ivory Coast Freddy Michael Kouablan

Simba yatambulisha mshambuliaji mpya kutoka Ivory Coast Freddy Michael Kouablan

Nenda karikaoo kanuue suruali yenye size 34 ya taiwan au china ukivaa itakutosha.

Halafu mwambie muuzaji akutolee 34 ya German ujaribu kuvaa utaona kuwa ni size ya pepe kale yani haikuenei.

Kwa hiyo utagundua sometimes namba nazo zinaongopa..... na hapo ndipo ilipo hoja yangu

Striker wetu ana mwili wenye asili ya kijerumani yani umri mdogo kwa namba halafu umbile na sura vi vya kiutu uzima.
Hebu huko. Khaaa. 😂😂
 
Naona bado hamjajifunza kitu kuhusu usajili. Usajili ni kamari, mchezaji anaweza kuwa top scorer huko alipo ila akaenda timu nyingine aka floppy au mchezaji akatoka timu nyingine akiwa wa kawaida ila akaenda timu nyingine aka shine. Mifano ipo mingi kwenye hili. Hivyo subirini wachezaji muwaone uwanjani.
Scars vipi somo limeshakukaa au bado? Unafurahia usajili na kumponda mchezaji kabla hata haujaona uwanjani atakuwaje
 
Scars vipi somo limeshakukaa au bado? Unafurahia usajili na kumponda mchezaji kabla hata haujaona uwanjani atakuwaje
Mzize aliyecheza msimu wote ana goli ngapi kumfananisha na Fredy aliyekuja dirisha dogo?
 
Yaani mchezaji wa kimataifa unakuja kumlinganisha na mchezaji wa ndani Mzize. Wewe kweli ikifikia Simba na Yanga akili uweka pembeni.
Kwani wachezaji wa ndani wao wanacheza mpira wenye kanuni tofauti na ambao wanacheza hao wa kimataifa?

Feisal kafunga magoli 19 kuliko Maxi na Pacome so hiyo unaweza kuiwekaje ili kuwatetea wanao hao wakimataifa ambao wamezidiwa na mchezaji wa ndani?

Fredy na Musonda nani mwenye goli nyingi?

Na Musonda kacheza mechi ngapi ukimlinganisha na Fredy?
 
Kwani wachezaji wa ndani wao wanacheza mpira wenye kanuni tofauti na ambao wanacheza hao wa kimataifa?

Feisal kafunga magoli 19 kuliko Maxi na Pacome so hiyo unaweza kuiwekaje ili kuwatetea wanao hao wakimataifa ambao wamezidiwa na mchezaji wa ndani?

Fredy na Musonda nani mwenye goli nyingi?

Na Musonda kacheza mechi ngapi ukimlinganisha na Fredy?
Jibu la swali lako linajibika hapa.
Ni mchezaji yupi iwe Simba au wa Yanga ambaye ni wa ndani anayeliipwa mshahara mkubwa kuliko mchezaji wa kimataifa.
 
Jibu la swali lako linajibika hapa.
Ni mchezaji yupi iwe Simba au wa Yanga ambaye ni wa ndani anayekipwa mshahara mkubwa kuliko mchezaji wa kimataifa.
Mshahara ni maswala ya negotiations

Wote tunajua sababu za wachezaji wa ndani kulipwa mshahara mdogo husababishwa na mambo mengi.

Sababu ya kwanza ni shauku ya wachezaji wenyewe kutamani kucheza katika hivi vilabu vikubwa wakiamini huku ndio sehemu sahihi ya wao kuweza kukuza majina yao.

Hiyo inafutuatia na wao kuridhika na mshahara wowote ambao watakuwa approached na hizo timu.

Lakini pia hata kulingana na mishahara ambayo walikuwa wanaipata kwenye timu zao ambazo ni ndogo.

Mishahara ile ilikuwa ni midogo so inapotokea Simba na Yanga wanapomfuata mchezaji na kumuongezea kiasi kidogo cha juu kutoka kwenye ule mshahara wake, mchezaji anakuwa motivated na kukubali.

Lakini sababu nyingine ni swala la udalali (middle men) kulingana na wachezaji wa ndani kutamani kucheza kwenye hivi vilabu basi kuna wadau ambao wamekuwa wakitumia hiyo fursa kupiga hela.

Mchezaji anaweza kusajiliwa kwenye makaratasi kukaandikwa mshahara mnono pamoja na signing fee lakini kiasi kingi cha pesa kinaishia kwa middle man.

Na ndio maana huwezi kuona wachezaji hao wakiitwa kwenye vilabu vya nje wanaendelea kulipwa mishahara midogo kama ambayo walikuwa wakilipwa huku.
 
Back
Top Bottom