britanicca
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 16,295
- 33,994
Kama kawaida yangu huwa nataka kujua yaliyoendelea Miaka ya Nyuma hasa kutoka kwa watu waliopigania nchi hii na kudai uhuru
Simon Rwamugila Kwa koo za Kihaya ana jina la Omutware yaan mtu au mshauri wa karibu wa Mukama(King)
Ukifika bukoba mjini unaelekea kiziba kwa kutumia njia ya Uganda ,ukifika katoma unachipuka kama unaelekeea Mugana kabla ya Mugana kuna njia ya Kwenda Ishozi, Kiziba unafika Kwa Omutwale Mushaijaki,
Mzee Simon Rwamugila Mushaijaki ni miongoni mwa wazee waliopigania haki nchini Tanzania na kabla ya kuja Tanzania alaikaa na kuiwakilisha Tanzania Nchini Ujerumani, mpaka miaka ya 70 akarejea nchini Tanzania,
Kuna shirika linaitwa TIDESO ni miongoni mwa waanzilishi wa mwanzo wa shirika ilo ambapo alitumia kiinua mgongo chake kuhakikisha wahaya wanaochipukia wanaenda shule, na walioshindwa kuendelea aliwapeleka Uganda, Mchango wake ni mkubwa mno, Hatimaye mwaka 2008 alitangulia mbele ya haki,
Nimewahi kupata kukaa na mzee huyu na akanisimulia mambo mawili kuhusu Nyerere na Dhana ya kupata uhuru
1. HAKI NA NYERERE ALIVYOPENDA HAKI
Anasema wakiwa shule ya sekondari Tabora maarufu kama Tabora Government School bado mchanganyiko, viongozi wa shule walizoea kubagua wanafunzi wengine na kuwapangia kazi ilikuwa ni kwa kubaguana, kuna waliopewa kazi za kunyanyaswa na kuna waliopendelewa, Juliusi Nyerere hakuopenda suala ili kabisa na aliumia mno kuona haki haitendeki kabisa, walipofika kidato cha tatu Bwana Juliusi Nyerere alichaguliwa kuwa Kakaka Mkuu na alikuja na mabadiriko kadha wa kadha.
"Ilikuwa ijumaa tumetoka kumaliza uchaguzi kabla hajafanya suala lolote alipanda juu ya bench ndani ya holi la chakula akatumia kijiko chake akagonga chuma kwa nguvu akasema tangia leo Meza zote za chakula tunapokaa zitapangwa upya na madish ya chakula yote yatagawiwa sawa, maana sisis viongozi tulikuwa tumejitenga tunakula kivyetu na Tunajaza nyama na chukula kizuri alafu wengine hawapati share kama ya viongozi" anaendelea kusimulia
"Ilikuwa vigumu kumuelewa nyerere lakin bwaro zima lilizizima kelele za kushangilia uku viongozi wakijifanya kususa na kununa na kuchukia wakasema tumefanya kosa kubwa sana kumchagua huyu bwana, maana baada ya hapo aliwaambia viongozi kwamba pamoja na kwamba sisi ni viongozi lakini tunapaswa kuongoza kwa kuonesha mfano, ndo maana nataka kila kiongozi awe na kipande chake cha bustani na eneo liliofyekwa vizuri alilofyeka yeye kama mfano kwa wengine. Baadae tuliendana na kasi yake na cha kushangaza utaratibu ulifuatwa bila kuingiliwa na walimu, kwa mwonekano bwana Nyerere alikuwa mdogo ila akija parade kutoa neno tunasikiliza kwa makini maana alikuwa mtu wa ajabu mno na hali ya juu ya ushawishi, hata hayo ya bustani viongozi baadhi walichelewa lakin yeye akaanzisha ya kwaqke kama kaka mkuu na kuwahamasisha, hivyo bwanan huyu alipenda usawa sana." akamalizia point hiyo
2. USAWA WA JINSIA NA RANGI SHULENI
Mutwale anaendelea kusimulia hapa anasema
''Siku moja akapata taarifa kwamba kama kuna ubaguzi hapa shuleni hasa kwa jinsia ya kike na kwa wahindi na waarabu , Kulikuwa kuna utaratibu wa kuwachagua wawakilishi wa madarasa yaan viongozi ambapo aliingilia mchakato kidogo nje ya utaratibu.maaana waafrika waliwanyima uongozi wanawake na waarabu.
Nakumbuka tulienda darasa la form two kuna watu walipendekeza majina ya wagombea ambao watapigiwa kura na Nyerere alisema anataka watu kupiga kura kwa kunyoosha mikono juu si kwakuandika kwenye karatasi ila kwasababu ya undue influence mtanyoosha mikono mkiwa mmeinama chini bila kuona nani kampigia nani. Zoezi likaanza yaliletwa majina matatu mdada mmoja na wavulana wawili, akawaambia tunaanza zoezi na aliyekuwa anahesabu kura alikuwa mzee wanzagi ambaye alitutangulia darasa, akawaambia wanaomtaka fulani. Kwakweli walinyoosha mikono sana kumuunga mkono mvulana mmoja wa kusini walinyoosha kama takribani 40 kati ya 50 na zaidi.
Nyerere akaadika 7 kati ya 50, alafu akauliza wanaomtaka huyu mwingine aliyekuwa chaguo la mwalimu wakanyoosha wawili Nyerere ankumbuka aliandika 29 alafu wanaomtaka wa tatu akaandika alafu zilizobaki kaandika hawakunyoosha maana ilikuwa vigumu kumbishia maana walikuwa wameinamisha vichwa, akawa amefanikiwa kubalance mambo
Tukaenda darasa Jingine ambalo alituma mtu kabla kwamba apendekeze jina la Iqbar muhindi mmoja , baada ya kufika akacheza mchezo ule ule na ukawepo uwakilishi sawa, kwakweli bwana Nyerere alikuwa na Iq kubwa mno,
PIA RWAMUGILA ALINISIMULIA DHANA YA UHURU HURU NA UHURU FUNGWA
Rwamugila Pia akazungumzia tulivyopata uhuru akashangilia lakin mwanasheria mmoja mzungu akamwambia kwamba "Mr. Simon you think Tanganyika gained independence? Rwamugila akamjibu yes, now we are free! Mzungu akacheka akasema "we are just reducing administration costs that’s why every colony will belong to union of previous colonial master, no one granted independence and then we colonize acording to nature time and situation "' mzee Rwamugila akaniambia kumbe haukuwa uhuru kama alivyodhania
Mwalimu Nyerere
Omutwale Mushaijaki Simoni Rwamugila
Ni hayo tu kwa leo
Britanny
Simon Rwamugila Kwa koo za Kihaya ana jina la Omutware yaan mtu au mshauri wa karibu wa Mukama(King)
Ukifika bukoba mjini unaelekea kiziba kwa kutumia njia ya Uganda ,ukifika katoma unachipuka kama unaelekeea Mugana kabla ya Mugana kuna njia ya Kwenda Ishozi, Kiziba unafika Kwa Omutwale Mushaijaki,
Mzee Simon Rwamugila Mushaijaki ni miongoni mwa wazee waliopigania haki nchini Tanzania na kabla ya kuja Tanzania alaikaa na kuiwakilisha Tanzania Nchini Ujerumani, mpaka miaka ya 70 akarejea nchini Tanzania,
Kuna shirika linaitwa TIDESO ni miongoni mwa waanzilishi wa mwanzo wa shirika ilo ambapo alitumia kiinua mgongo chake kuhakikisha wahaya wanaochipukia wanaenda shule, na walioshindwa kuendelea aliwapeleka Uganda, Mchango wake ni mkubwa mno, Hatimaye mwaka 2008 alitangulia mbele ya haki,
Nimewahi kupata kukaa na mzee huyu na akanisimulia mambo mawili kuhusu Nyerere na Dhana ya kupata uhuru
1. HAKI NA NYERERE ALIVYOPENDA HAKI
Anasema wakiwa shule ya sekondari Tabora maarufu kama Tabora Government School bado mchanganyiko, viongozi wa shule walizoea kubagua wanafunzi wengine na kuwapangia kazi ilikuwa ni kwa kubaguana, kuna waliopewa kazi za kunyanyaswa na kuna waliopendelewa, Juliusi Nyerere hakuopenda suala ili kabisa na aliumia mno kuona haki haitendeki kabisa, walipofika kidato cha tatu Bwana Juliusi Nyerere alichaguliwa kuwa Kakaka Mkuu na alikuja na mabadiriko kadha wa kadha.
"Ilikuwa ijumaa tumetoka kumaliza uchaguzi kabla hajafanya suala lolote alipanda juu ya bench ndani ya holi la chakula akatumia kijiko chake akagonga chuma kwa nguvu akasema tangia leo Meza zote za chakula tunapokaa zitapangwa upya na madish ya chakula yote yatagawiwa sawa, maana sisis viongozi tulikuwa tumejitenga tunakula kivyetu na Tunajaza nyama na chukula kizuri alafu wengine hawapati share kama ya viongozi" anaendelea kusimulia
"Ilikuwa vigumu kumuelewa nyerere lakin bwaro zima lilizizima kelele za kushangilia uku viongozi wakijifanya kususa na kununa na kuchukia wakasema tumefanya kosa kubwa sana kumchagua huyu bwana, maana baada ya hapo aliwaambia viongozi kwamba pamoja na kwamba sisi ni viongozi lakini tunapaswa kuongoza kwa kuonesha mfano, ndo maana nataka kila kiongozi awe na kipande chake cha bustani na eneo liliofyekwa vizuri alilofyeka yeye kama mfano kwa wengine. Baadae tuliendana na kasi yake na cha kushangaza utaratibu ulifuatwa bila kuingiliwa na walimu, kwa mwonekano bwana Nyerere alikuwa mdogo ila akija parade kutoa neno tunasikiliza kwa makini maana alikuwa mtu wa ajabu mno na hali ya juu ya ushawishi, hata hayo ya bustani viongozi baadhi walichelewa lakin yeye akaanzisha ya kwaqke kama kaka mkuu na kuwahamasisha, hivyo bwanan huyu alipenda usawa sana." akamalizia point hiyo
2. USAWA WA JINSIA NA RANGI SHULENI
Mutwale anaendelea kusimulia hapa anasema
''Siku moja akapata taarifa kwamba kama kuna ubaguzi hapa shuleni hasa kwa jinsia ya kike na kwa wahindi na waarabu , Kulikuwa kuna utaratibu wa kuwachagua wawakilishi wa madarasa yaan viongozi ambapo aliingilia mchakato kidogo nje ya utaratibu.maaana waafrika waliwanyima uongozi wanawake na waarabu.
Nakumbuka tulienda darasa la form two kuna watu walipendekeza majina ya wagombea ambao watapigiwa kura na Nyerere alisema anataka watu kupiga kura kwa kunyoosha mikono juu si kwakuandika kwenye karatasi ila kwasababu ya undue influence mtanyoosha mikono mkiwa mmeinama chini bila kuona nani kampigia nani. Zoezi likaanza yaliletwa majina matatu mdada mmoja na wavulana wawili, akawaambia tunaanza zoezi na aliyekuwa anahesabu kura alikuwa mzee wanzagi ambaye alitutangulia darasa, akawaambia wanaomtaka fulani. Kwakweli walinyoosha mikono sana kumuunga mkono mvulana mmoja wa kusini walinyoosha kama takribani 40 kati ya 50 na zaidi.
Nyerere akaadika 7 kati ya 50, alafu akauliza wanaomtaka huyu mwingine aliyekuwa chaguo la mwalimu wakanyoosha wawili Nyerere ankumbuka aliandika 29 alafu wanaomtaka wa tatu akaandika alafu zilizobaki kaandika hawakunyoosha maana ilikuwa vigumu kumbishia maana walikuwa wameinamisha vichwa, akawa amefanikiwa kubalance mambo
Tukaenda darasa Jingine ambalo alituma mtu kabla kwamba apendekeze jina la Iqbar muhindi mmoja , baada ya kufika akacheza mchezo ule ule na ukawepo uwakilishi sawa, kwakweli bwana Nyerere alikuwa na Iq kubwa mno,
PIA RWAMUGILA ALINISIMULIA DHANA YA UHURU HURU NA UHURU FUNGWA
Rwamugila Pia akazungumzia tulivyopata uhuru akashangilia lakin mwanasheria mmoja mzungu akamwambia kwamba "Mr. Simon you think Tanganyika gained independence? Rwamugila akamjibu yes, now we are free! Mzungu akacheka akasema "we are just reducing administration costs that’s why every colony will belong to union of previous colonial master, no one granted independence and then we colonize acording to nature time and situation "' mzee Rwamugila akaniambia kumbe haukuwa uhuru kama alivyodhania
Mwalimu Nyerere
Omutwale Mushaijaki Simoni Rwamugila
Ni hayo tu kwa leo
Britanny