Simpendi na sikumchagua Magufuli lakini naunga mkono 100% msimamo wake kuhusu Korona

Simpendi na sikumchagua Magufuli lakini naunga mkono 100% msimamo wake kuhusu Korona

Korona haina tiba wala haina kinga. Njia zote zinazoshauriwa ili kujikinga na korona ni za dhahania na nadharia tu. Ndiyo maana hakuna mahala popote walipofanikiwa kuiondoa na kuimaliza korona. Hizo chanjo zimekaa kisiasa na kibiashara tu. Mafua yana karne nzima mpaka leo hakuna kinga, ukimwi una nusu karne mpaka leo hakuna chanjo, halafu leo miezi 9 tunaambiwa Kuna chanjo ya korona! Rubbish!!

Njia na mbinu zinazopendekezwa kuchukuliwa kuepuka korona hazitekelezeki na zinaongeza tatizo. Tumeona maandamano na mabishano hata katika mataifa makubwa kama Marekani, Brazil, Ujerumani na kwingineko wananchi wanapinga makatazo na masharti mbalimbali ya kujikinga na korona yanayowekwa na viongozi wao.

Sasa watanzania wenzangu mnaoshinikiza na kumtaka JPM atoe tamko kuhusu korona naombeni mnijibu. Mnatakaje? Alishasema tumuachie Mungu. Sasa kelele za nini?

Hivi mnataka JPM atangaze kitu gani kifanyike hapa nchini ili kuizuia korona zaidi ya kumwachia Mungu?

Awafungie watanzania ndani? Hawa hawa watanzania wanaokula kwa kufanya umachinga na uchuuzi? Hawa hawa wanaolima na kuvuna ndipo wapate mlo? Hawa hawa wanaochunga mifugo yao kwa kuzunguka nayo maporini? Ulaya kuna zero grazing. Hapa Tanzania na nchi zote za Afrika tutauwa watu na mifugo kwa njaa.

Na ndiyo maana South Africa hali ilikuwa tete, na pale Kenya ulifanyika usanii tu wa kuzuia watu kutoka usiku, halafu mchana kutwa wako majiani. Usanii mtupu. Uganda wamejikanyaga wakashindwa. Usiitolee mfano Rwanda. Kale kanchi ni kadogo sawa na kisiwa cha Unguja ndiyo maana wanagawana gunia kumi za unga kwa siku na zinawatosha.

Halafu hii kunawa nawa, nayo pia ni ujinga tu. Unanawa halafu unaingia kwenye daladala kubanana? Mnashea kikombe cha maji ya kunywa nyumba nzima? Mnashea kete za bao, kopo la mbege, komoni na wanzuki? Acheni zenu bhana! BTW, kirusi kinauawa kwa kunawa? Sanitizer inauwa kirusi? Unazijua tabia za kirusi?

Virus is immortal. Why? This is because Virus is the RNA/DNA particle. Na ndiyo maana mpaka leo ukitaka DNA/RNA ya dinosaurs walioishi miaka milioni150 iliyopita utapata.

Mnataka atangaze watanzania wavae barakoa? Hawa hawa wanaokosa hata leso ya kufutia kamasi? Hawa hawa wanao omba mia tano ya kununua kipande cha muhogo?? Hapa tutasababisha mlipuko wa magonjwa mengine. Maana watu wanaweza kuvaa kitambaa mwezi mzima bila kukifua.

Tumuunge mkono JPM (simtaji kama mheshimiwa Rais kwa kuwa ushindi wake katika uchaguzi wa 2020 mpaka siku nakufa sitaukubali), lakini kwenye suala la korona namuunga mkono 100%.

Tuweke pembeni chuki na tofauti zetu zote za kila aina tuangalie uhalisia. Msimamo wa JPM katika suala la korona unaendana na uhalisia na ndiyo njia bora ya kuifuata. Hayo mataifa yanayojitia kuwafungia na kupiga sanitizer watu wake wamefanikiwa kiasi gani kujikinga na korona?

Halafu hivyo vifo Cha mmoja mmoja vinavyotokea mbona ni kidogo sana kuliko vile vya magonjwa kama malaria, TB, ajali, ukimwi, n.k?? Kwann hivi havihesabiwi??

Wewe mwenye unafuu wa maisha kaa ndani tuache walala hoi tuendelee kuzurura na kupengeana makamasi ili miili yetu ijenge kinga asili dhidi ya korona. (Kajisomee types of immunity, kuna natural na artificial).

Nimemaliza.
sikiliza wewee, chanjo ya mafua ipo na inatolewa kila mwaka kwenye nchi za wenzetu wenye miili rojo rojo. Chanjo ya Covid nayo ipo, inafanya kazi kuufundisha mwili namna ya kupambana na corona, aina hii ya chanjo inaitwa RNA vaccine ambayo hutumia njia inaitwa mRNA ( messenger RNA) kuzalisha kinga. Anachokifanya Magufuli japokua kinatucost roho za watu lakini ni sahihi, sisi hatuna uchumi wa kuwalipa watu wasipofanya kazi, marekani huko wana lockdown lakini wananchi wanapewa milioni moja kila mmoja ( dola 600 kila mmoja wa familia), huko uingereza kina rashford wameifanya serikali iwape watoto vyakula vya bure, sosi haya hatuyawezi, korona ni janga ila kwetu janga kubwa ni uchumi wetu wa dola bilioni 50. Kama tutauziwa kinga ya korona kwa bei wanayouziwa afrika kusini ya ~ dola 6 kwa dozi, tutatumia ~dola milioni 390 (~ shilingi bilioni 840) kwa dozi za watanzania wote. Bila msaada hizo hela hatuzipati. TRA wameambiwa wakusanye walau trilioni 2 kila mwezi kuanzia januari, tukifanya lockdown ndo kwaheri uchumi wetu
 
kitu pekee nachojiuliza mpaka sasa, kwa nini tanzania ambao hatuchukui tahadhari yoyote hatujadhurika sana kama wanaochukua tahadhari?
 
kitu pekee nachojiuliza mpaka sasa, kwa nini tanzania ambao hatuchukui tahadhari yoyote hatujadhurika sana kama wanaochukua tahadhari?
Tahadhari inapovhukuliwa inazaa Matatizo mengi.
Mfano lockdown inazaa kushuka kwa kinga, umasikini, msongo wa mawazo n.k

Barakoa huleta magonjwa ktk mfumo wa upumuaji n.k, n.k
 
Blah blah blah

Rais anachukua uamuzi ila nchi nzima ipo kinyume nae...

Ajifikirie mno....

Ana matatizo ya thinking
Siyo nchi nzima wako kinyume na uamuzi wa jpm. Mm pia ni mtanzania. Hao walio kinyume waache mihemko watoe suluhisho la korona kama wanalifahamu
 
Kukiri Corona ipo ndio njia ya kwanza kukabiliana nayo, siku zote huwezi pigana na adui usiemjua.

Rais lazima atoe kauli ili kila mmoja wetu ajue Corona ipo na achukue hatua za kujilinda kwa umakini.

Kauli ya Rais sio sawa na kauli yangu au yako, hiyo itachujuliwa kwa uzito unaostahili na wengi wataanza kuwa serious na huu ugonjwa.

Lakini Rais kuendelea kukaa kimya au kusema Tanzania hakuna Corona ndio kunapelekea watu kudharau kuchukua hatua za kujilinda.

Huko vijijini wengi hawana access ya internet kujua hali halisi tofauti na sisi tuliopo mijini, wao wakisikia Magifuli kasema hakuna Corona wanaamini hivyo, wanaendelea kuchapa kazi.

Hili halihusiani na lockdown au vyovyote, muhimu watu wajue Corona ipo seriously na wajilinde badala ya kuamini haipo wakati wengine wanaugua na hata kufa.
Hii upuuzi mkubwa kuamini tamko la Rais
Kwani wewe wajibu wako wa kiagya
Hacha utoto asee
 
Brother

Jifikirieni sana yaani....

The whole country haiamini anachokisema JPM....

Ugonjwa hauna mjadala,solution ni kunawa,barakoa na distancing,thats it!

Unaongea nini wewe maiti ya JPM?
Mbona wazungu basi wanazidi kufa kwa maelefu pamoja na kuchukua hatua zote hizo?

Hakuna njia hata moja iliyofanikiwa kupunguza corona! Hakuna.
 
Ugonjwa hauna mjadala,solution ni kunawa,barakoa na distancing,thats it!
Mbona kama suluhisho lako limeondoa mambo mengine kama lockdown, kufunga makanisa, kufunga mashule, kuzuia sherehe, na kuzuia mazishi? Haya maigizo yakifanyika korona itaisha? Na maigizo haya mwisho wake lini? JPM is right!
 
Hakuna anayetaka Jpm afungie wat u,ila Tz siyo kisiwa......serikali kuwahamasisha wananchi wake mbinu za kujikinga siyo dhambi.......kama huna mtu wa karibu au ndugu aliyeugua huu ugonjwa huwezi kuelewa mkuu,ni ngumu sana
 
Korona haina tiba wala haina kinga. Njia zote zinazoshauriwa ili kujikinga na korona ni za dhahania na nadharia tu. Ndiyo maana hakuna mahala popote walipofanikiwa kuiondoa na kuimaliza korona. Hizo chanjo zimekaa kisiasa na kibiashara tu. Mafua yana karne nzima mpaka leo hakuna kinga, ukimwi una nusu karne mpaka leo hakuna chanjo, halafu leo miezi 9 tunaambiwa Kuna chanjo ya korona! Rubbish!!

Njia na mbinu zinazopendekezwa kuchukuliwa kuepuka korona hazitekelezeki na zinaongeza tatizo. Tumeona maandamano na mabishano hata katika mataifa makubwa kama Marekani, Brazil, Ujerumani na kwingineko wananchi wanapinga makatazo na masharti mbalimbali ya kujikinga na korona yanayowekwa na viongozi wao.

Sasa watanzania wenzangu mnaoshinikiza na kumtaka JPM atoe tamko kuhusu korona naombeni mnijibu. Mnatakaje? Alishasema tumuachie Mungu. Sasa kelele za nini?

Hivi mnataka JPM atangaze kitu gani kifanyike hapa nchini ili kuizuia korona zaidi ya kumwachia Mungu?

Awafungie watanzania ndani? Hawa hawa watanzania wanaokula kwa kufanya umachinga na uchuuzi? Hawa hawa wanaolima na kuvuna ndipo wapate mlo? Hawa hawa wanaochunga mifugo yao kwa kuzunguka nayo maporini? Ulaya kuna zero grazing. Hapa Tanzania na nchi zote za Afrika tutauwa watu na mifugo kwa njaa.

Na ndiyo maana South Africa hali ilikuwa tete, na pale Kenya ulifanyika usanii tu wa kuzuia watu kutoka usiku, halafu mchana kutwa wako majiani. Usanii mtupu. Uganda wamejikanyaga wakashindwa. Usiitolee mfano Rwanda. Kale kanchi ni kadogo sawa na kisiwa cha Unguja ndiyo maana wanagawana gunia kumi za unga kwa siku na zinawatosha.

Halafu hii kunawa nawa, nayo pia ni ujinga tu. Unanawa halafu unaingia kwenye daladala kubanana? Mnashea kikombe cha maji ya kunywa nyumba nzima? Mnashea kete za bao, kopo la mbege, komoni na wanzuki? Acheni zenu bhana! BTW, kirusi kinauawa kwa kunawa? Sanitizer inauwa kirusi? Unazijua tabia za kirusi?

Virus is immortal. Why? This is because Virus is the RNA/DNA particle. Na ndiyo maana mpaka leo ukitaka DNA/RNA ya dinosaurs walioishi miaka milioni150 iliyopita utapata.

Mnataka atangaze watanzania wavae barakoa? Hawa hawa wanaokosa hata leso ya kufutia kamasi? Hawa hawa wanao omba mia tano ya kununua kipande cha muhogo?? Hapa tutasababisha mlipuko wa magonjwa mengine. Maana watu wanaweza kuvaa kitambaa mwezi mzima bila kukifua.

Tumuunge mkono JPM (simtaji kama mheshimiwa Rais kwa kuwa ushindi wake katika uchaguzi wa 2020 mpaka siku nakufa sitaukubali), lakini kwenye suala la korona namuunga mkono 100%.

Tuweke pembeni chuki na tofauti zetu zote za kila aina tuangalie uhalisia. Msimamo wa JPM katika suala la korona unaendana na uhalisia na ndiyo njia bora ya kuifuata. Hayo mataifa yanayojitia kuwafungia na kupiga sanitizer watu wake wamefanikiwa kiasi gani kujikinga na korona?

Halafu hivyo vifo Cha mmoja mmoja vinavyotokea mbona ni kidogo sana kuliko vile vya magonjwa kama malaria, TB, ajali, ukimwi, n.k?? Kwann hivi havihesabiwi??

Wewe mwenye unafuu wa maisha kaa ndani tuache walala hoi tuendelee kuzurura na kupengeana makamasi ili miili yetu ijenge kinga asili dhidi ya korona. (Kajisomee types of immunity, kuna natural na artificial).

Nimemaliza.
La msingi hapa ni kuwaambia wananchi ukweli ili wajue na kuchukua tahadhari. Malaria ipo na inaua kila siku lakini uwepo wake unajulikana na watu wote na njia za kujikinga zinajulikana. Wenye uwezo wa kuzingatia wanazingatia na kupata matokeo yake. Wasiozingatia nao matokeo wanayaona.
 
Hadi sasa siajajua wanaotaka Rais atangaze janga la corona, je lengo lao ni kitu gani? Sijaona hata mmoja anayetoa njia itakayowezesha kumaliza huu ugonjwa kwa asilimia 100.
Hakuna popote duniani ambapo umedhibitiwa 100%. Kinachofanyika ni kujaribu kupunguza kasi ya maambukizi. Mifano ya nchi zilizofanikiwa kwa hilo ipo na zile zilizodharau na kuacha maambukizi yaongezeje kwa kasi ipo.
 
Wewe hufi? Hapo ulipo umejifungia kwa shemeji yako hujui huo ugali unaokula unapatikana vipi ndio maana akili yako yote inawaza kwamba rais akisema tujifungie ndani corona inaisha.
Nitakufa ila sitakufa kama mjinga! Kwahio akili zote umezipeleka kwenye tumbo, sio? Mitanzania sijui lini mtakua na akili. Ona sisi, kila siku tunapewa updates


IMG-20210127-WA0016.jpg
 
Rais gani? Amefanya nn? Amefanikiwa kwa kiasi gani?
Swala la kufanikiwa au kutokufanikiwa ni lingine, suala la kwamba rais gani amefanya Nini kama hili nalo ni la kukueleza basi Tz mna tatizo
 
Los Angeles hapa tumefungiwa ndani kitu kimekaza watu wanapukutika mpaka wameamua kuachia tu watu waendelee na shughuli zao lakini wachukue tahadhari. Mdudu huyu ni changamoto sana. Wiki chache hapa mahospitali yalikuwa yamefurika maiti mpaka wanakodi masemitrela na kuyageuza ofisi ya Mshana Jr (mochwari)....
Mkuu unachokisema ni kweli kabsa by the way.

Ila kwa nchi kama zetu hizi ikifanya ivyo.

Watu watakfa kwa strees tu ya maisha akiugua tuu kdog hatajua tayar ni korona. So ni stress juu ya stress .
 
Nitakufa ila sitakufa kama mjinga! Kwahio akili zote umezipeleka kwenye tumbo, sio? Mitanzania sijui lini mtakua na akili. Ona sisi, kila siku tunapewa updates
Unapewa updates ndio corona inapungua?

Mbona mnakuwa wapumbavu?

Nikafikiri una kitu kinaonesha mmefanya corona kupungua, kumbe updates kuonesha jinsi waathirika wanavyoongezeka?
 
Back
Top Bottom