Simu za 5G ni utapeli tu hazina tofauti na 4G

Simu za 5G ni utapeli tu hazina tofauti na 4G

Upo sahihi mkuu kitu chengine kuongezea ukiwa na speed ya kasi unaperuzi page nyingi zaidi, mtu mwenye internet slow kuna muda anasubiria ili page ifunguke hivyo Ina limit page ngapi atafungua kwa siku, ila mwenye internet yenye speed anaserereka tu akigusa inafunguka hivyo anafungua page nyingi zaidi.
Hivi humu ndani naomba nieleweshwe NADHARIA ya kua 5G inatumia bundle kubwa kuzidi 4G, maanake naona hiki kitu watu wengi wanakiamini, mimi akili yangu imegoma kuamini.

How????????
Yaani una file la 10Mb, ukili download kwa 4G litatumia data chache mfano hio hio 10Mb,
Na ukili download kwa 5G litatumia data zaidi mfano 15Mb?, Logic iko wapi hapaa?

Nijuavyo 4G & 5G it's just Internet Speed,
i.e how fast your going to download/stream e.t.c file/content at a given time...

Labda iwe hivi...
Kwanza achana kabisa na file la ku download, hapo sijui utumie technolojia gani kunielewesha..
Twende kwenye streaming hapa unaweza ukanishawishi.

KIVIPI??
Ukiwa unaangalia lets say Movie Neflix au YouTube mfano katika resolution ya 1920×1080(FULL HD) kwa kutumia speed ambayo inacheza, yaani kuna mda inakua 4G mda mwingine 3G/H+, hizo sites zina sifa za ku detect data speed yako na ku adjust resolution ya Movie yako, mfano kutoka kwenye 1920×1080(FHD) kwenda kwenye 1280×720(HD), ili angalau kukusaidia movie isisimame kabisa, ndio maana mda mwingine unaona inakuja na ukungu ukungu na ku stack, labda data zikishuka sana ndio itasimama kabisa.

Kwahio basi, matumizi ya data yanapanda na kushuka kulingana na Connection yako, (Naamini as long umeweza ku login Jf unajua, Resolution = Data kubwa, and vice versa).

Lakini ukiwa katika Connection iliyoko JUU na ipo STABLE (mfano hio 5G sasa) Video yako yote utaiangalia katika resolution ya FHD, na hapo ndipo matumizi ya data yataonekana makubwa..
Kwa hilo ndio nitakubali Hoja yenu, otherwise mnipe nisichokijua.
Chief-Mkwawa .
Depal yupo tayari kunyongwa kuliko kuamini mliyoyaandika.
 
5g ni hardware, so kuipata ni mpaka waje wafunge vifaa vya 5g kwenye mnara wako wa karibu au eneo lako. So kwa kuwa 5G husoma LTE kwa simu nyingi, wasa na inavyosoma 4g, ni ngumu kuitofautisha 5g na 4G kama eneo lako halina 5g. Ila ikiwepo tofauti utaiona.
 
Tz hakuna 5G, wanatudanganya tuu.
Bro sio kweli 5G ipo kuwa na device sahihi na uwe sehemu sahihi utaona balaa lake. Ukisema 5G ipo sehemu chache mno nita kuelewa. Airtel 5G na push mpaka 500mbps mzee ni moto sana ahhhahahhaaha. Tatizo Posta yenyewe hamna ipo Kigamboni pale ferry tu ukiwa kwenye waitinh lounge na kwa mbali ukiwa Ferry magogoni
 
5G ya simu inatakiwa pia laini unayotumia iwe 5G , ukitumia simu 5G halafu sim card 4G bado haileti mabadiliko.

Ila kwa Tanzania mtandao wenye kasi vizuri ni Vodacom
𝐊𝐢𝐛𝐨𝐧𝐠𝐨 𝐛𝐨𝐧𝐠𝐨 𝐡𝐚𝐦𝐧𝐚 𝐥𝐢𝐧𝐞 𝐲𝐚 5𝐆 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐭𝐮𝐦𝐢𝐚 𝐡𝐢𝐲𝐨𝐡𝐢𝐲𝐨 𝐲𝐚 4𝐆 𝐧𝐢 𝐬𝐚𝐰𝐚?
 
Makampuni yanatumia vitu vidogo sana kutupiga hela, ukichukua simu ya 4g na 5g kwa internet ya tz download vitu kwa pamoja kwa mtandao mmoja utaona hazipishani

Utakuta mtu simu kuwa na 5g anauza milioni moja yenye 4g laki 5, yaani 5g imekula laki tano[emoji23][emoji23]
Sio utapeli tatizo la watoa huduma kwenda na wakati wa vifaa vyao vya kukupa 5g PESA HAKUNA.
INABIDI WAINGIE BAJETI KUBADILISHA MINARA YOTE VIFAA
 
𝐊𝐢𝐛𝐨𝐧𝐠𝐨 𝐛𝐨𝐧𝐠𝐨 𝐡𝐚𝐦𝐧𝐚 𝐥𝐢𝐧𝐞 𝐲𝐚 5𝐆 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐭𝐮𝐦𝐢𝐚 𝐡𝐢𝐲𝐨𝐡𝐢𝐲𝐨 𝐲𝐚 4𝐆 𝐧𝐢 𝐬𝐚𝐰𝐚?
Hapo uongo, laini iwe 4G halafu simu iwe 5G na isapoti 5G any way sijui zaidi wataalam wa IT wanaweza kutusaidia
 
Back
Top Bottom