Simu za Google Pixel zina shida gani?

Simu za Google Pixel zina shida gani?

Pixel 4 zina tabia ya kufa AC itakuwa yako nayo imekufa. Ichaji alafu washa ikirespond kwa ule mtetemo wa kushtuka ikiwaka ila screen iko off hapo probably ni AC. Mafundi wa uhakika...
pamoja na redmi
 
Nadhani simu nyingi zipo hivyo ukiwa na simu iliyoshika roho umakini unatakiwa sana...
Simu hii ya Pixel nnayotumia haijavunjika kioo na imeangukia Sura zaidi ya mara 3 na sijawahi kuweka screen protector naitumia km ilivyo na ishatumbukia kwenye maji zaidi ya mara 3 Ila Ile Samsung iliangukia sura mara 1 tu kioo kika-bust alafu kuna siku nikakosea nikailalia ndio ikawa kwisha habari yake ikaanza kuchemka nikiichaji yaan km nimeinjika sufuria kwenye jiko la gesi kwenda kuulizia kioo nikaambiwa nikadata ikabidi niiuze tu km spear kwa wale mafundi kuanzia pale sitaki tena Samsung,
 
Simu hii ya Pixel nnayotumia haijavunjika kioo na imeangukia Sura zaidi ya mara 3 na sijawahi kuweka screen protector naitumia km ilivyo na ishatumbukia kwenye maji zaidi ya mara 3 Ila Ile Samsung iliangukia sura mara 1 tu kioo kika-bust alafu kuna siku nikakosea nikailalia ndio ikawa kwisha habari yake ikaanza kuchemka nikiichaji yaan km nimeinjika sufuria kwenye jiko la gesi kwenda kuulizia kioo nikaambiwa nikadata ikabidi niiuze tu km spear kwa wale mafundi kuanzia pale sitaki tena Samsung,
Hiyo Samsung iliharibu inner panel tunaita kioo namba mbili. Hasahasa ikiwa ni replaced second hand wakaweka LED ndio zina cases ikitenguka kidogo inachemka screen na kuisha chaji haraka.
 
Basi hapo ndio ulitakiwa urekebishe pale fanya editing sema sio zote maana ume-generalize kwamba zote
Sibadilishi, huo ndio uzoefu wangu. Nimesema Pixel hazidumu hiyo kauli ni data driven sijakurupuka. Simu yako kudumu haibadilishi msimamo wangu, kwenye statistics kuna outliers.

Ukileta units kadhaa za Huawei, iPhone, Mi, Pixel na Samsung utakuta Samsung na Pixel ndio ziko prone kuharibika hardware. Hii haimaanishi nyingine haziharibiki, ila tunaangalia numbers.
 
Pixel 7 kwa 700,000 miezi mitano iliyopita? Miezi mitano iliyopita pixel 7 ilikuwa inauzwa hadi 1,000,000 kule Amazon.

Alinunua simu iliyotumika au yenye changamoto. Ukitaka ufurahie hizi devices nunua mpya.

Kwa upande wako pia ulinunua Simu iliyotumika, hakuna pixel 4 mpya sokoni so nikawaida sana kupata changamoto kama hizo.

Wauzaji wengi wa Tanzania sio waaminifu, kama unaweza agiza refurbished phone Amazon na wanatoa na warrant ya miezi miwili, ni nafuu kuliko kunua kwa hawa matapeli.
 
Sibadilishi, huo ndio uzoefu wangu. Nimesema Pixel hazidumu hiyo kauli ni data driven sijakurupuka. Simu yako kudumu haibadilishi msimamo wangu, kwenye statistics kuna outliers.

Ukileta units kadhaa za Huawei, iPhone, Mi, Pixel na Samsung utakuta Samsung na Pixel ndio ziko prone kuharibika hardware. Hii haimaanishi nyingine haziharibiki, ila tunaangalia numbers.
Sawa mkuu umeshasema sio zote basi hakuna shida hapo, maana hata iPhone zinalipuka na hio Huawei hata kwa bure sichukui
 
Na pixel 3a hapa toka July 2021 ipo poa tu nilinunua huko huko kariakoo kipind hazijazagaa

Hii miaka miwili iliyopita viduka uchwara vya simu vimekua ving sana hapa mjin nakushauri ukitaka simu jichanhe ununue mpya...

Simu used zilikua reliable before 2022
Mimi ninayo 4xl 128,tangu 2020
 
Back
Top Bottom