Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 69
ASIA DIGITALI
Neno msikiti, lilimjia akilini mwake katika namna ya kushtukiza. Akafanya tabasamu pana na kujishangaa, imekuwaje hadi akauwaza msikiti ilihali hakuwa mtu wa swala tena.
Tabia zake mbovu za kuwalaghai wanaume na kuwaibia mali zao, leo hii anawaza msikiti.
“Au nd’o shetani kuzeeka anakuwa malaika…” Asia alijiuliza huku wazo la msikiti likiwa palepale. Na hapo ndipo alipokumbuka juu ya kijana wa kuitwa Hassan Tembo!!
Ni muda mrefu sana alikuwa ameelezwa sifa zake na uwezo wake kipesa.
Asia hakutaka kitu kingine cha ziada kwa mwanaume zaidi ya pesa. Hakujali juu ya utu wake, lakini zaidi ni kwamba Asia alikuwa akijiuza katika namna ya kidigitali. Hayajui mapenzi wala hajui nini maana ya kupendana…. Anachoamini ni kuwa anatoa penzi nawe umpatie pesa. Tena sio pesa kidogo!!
Anachuma mamilioni.
(MIKASA ZAIDI YA ASIA NI KATIKA SIMULIZI YA ASIA DIGITALI kama hujaisoma wasiliana nami inbox)
Alikuwa anamiliki gari yake, na nyumba nzima ya kupanga….. pesa yote aliitoa kwa wanaume katika njia za ki-digitali.
Asia akiwa na rafiki yake Husna wakaongoza njia kuelekea msikitini Kariakoo…
. . Jua lilikuwa kali, kilammoja alifanya jitihada za kupambana na joto la jijini Dar es salaam.
Hekaheka za hapa na pale Kariakoo ziliufanya mji kuonekana mdogo sana.
Kanzu nyeupe na mabaibui meusi yalitapakaa huku na kule ishara ya sala ya ijumaa.
. . Asia naye alikuwemo katika hekaheka za siku hiyo.
. . Muda wa sala ulipowadia kila mtu alikuwa mahala pake akiswali.
. . Asia naye alikuwa mmoja kati ya waliojumuika kuswali katika msikiti ambao hajawahi kuswali hapo kabla.
. . Asia aliswali huku mahesabu yake yakienda sawa kabisa juu ya mipango yake madhubuti kichwani.
. . Muda wa swala ulipomalizika Asia alitoka nje ya msikiti.
. . Akaangaza macho huku na kule.
. . Aliyategea mawindo yake yaweze kunasa.
. . Hatua kwa hatua Asia alijitembeza, kwa kasi huku akipigia mahesabu makali ya tukio ambalo litatokea.
. . Asia alikuwa akimtazama mwanaume mfupi mweusi ambaye huenda alikuwa amependeza kuliko wote ndani ya kanzu yake yenye thamani ya juu.
Asia alimtazama jinsi alivyokuwa amejikita katika kutumia simu yake. Asia akatumia upenyo ule.
. . Akajipitisha mbele yake, bwana yule pasipokumwona Asia akajikuta amemkanyaga. Asia akajilegeza akatua chini.
. . Aliyemgonga alikuwa ni Hassan Tembo, Munyama mukubwa kamba fedha ambaye alikuwa amevurugwa haswa na tukio lililotokea kwa Mamamia.
Hassan alikuwa anajulikana sana maeneo yale ya msikitini, asingeweza kumkimbia Asia ama kumpuuzia, aliheshimika kutokana na moyo wake wa kujitolea huku akiwa kijana mdogo.
. . Tukio la Asia akalitumia kama nafasi nyingine ya kuthibitisha kuwa ana pesa japo kwa wakati huo alitumia gari la kuazima na hakuwa na kadi yake ya benki japo alikuwa na kiasi fulani cha pesa alichokuwa amehifadhi ndani ya nyumba yake.
Akaamuru apelekwe katika gari lake binti yule.
Wafuasi wakambeba Asia hadi ndani ya gari la Tembo.
. . Akisindikizwa na wanaume wawili Hassan alimchukua Asia hadi katika hospitali ya watu binafsi maeneo ya mnazi mmoja.
Hapa sasa hakuwahitaji wale watu tena, akabaki peke yake.
Uzuri ni kwamba alikuwa na bima ya afya hivyo alifanya utaratibu na pesa kiduchu ikaongea Asia akatibiwa bure kwa kutumia kadi yake.
. . Hassan baada ya kuelezwa kuwa binti yule hakuwa amepata majeraha makubwa sana aliamua kuondoka naye aweze kumrejesha nyumbani.
Wakiwa ndani ya gari Hassan Tembo akakumbuka kuwa alikuwa matatani, na kilichochokonoa kichwa chake ni kisa cha Mamamia, akajiuliza ni lipi lilisababisha yale mambo kutokea. Akakumbuka na kujisahihisha kuwa haukuwa utaratibu wake kulala na msichana mmoja mara mbili.
Mh! Yawezekana ndo tatizo kweli ama?? Alijiuliza bila kupata jibu.
Akilini mwake sasa aliingiwa na ujasiri wa ajabu sana, hakutishika na kilichotokea chumbani akiwa na Mamamia, ile akili yake ya zamani ikarejea tena kwa kasi akaona Asia alikuwa mtu sahihi kabisa wa kumfanyia majaribio.
ASIA DIGITALI
Neno msikiti, lilimjia akilini mwake katika namna ya kushtukiza. Akafanya tabasamu pana na kujishangaa, imekuwaje hadi akauwaza msikiti ilihali hakuwa mtu wa swala tena.
Tabia zake mbovu za kuwalaghai wanaume na kuwaibia mali zao, leo hii anawaza msikiti.
“Au nd’o shetani kuzeeka anakuwa malaika…” Asia alijiuliza huku wazo la msikiti likiwa palepale. Na hapo ndipo alipokumbuka juu ya kijana wa kuitwa Hassan Tembo!!
Ni muda mrefu sana alikuwa ameelezwa sifa zake na uwezo wake kipesa.
Asia hakutaka kitu kingine cha ziada kwa mwanaume zaidi ya pesa. Hakujali juu ya utu wake, lakini zaidi ni kwamba Asia alikuwa akijiuza katika namna ya kidigitali. Hayajui mapenzi wala hajui nini maana ya kupendana…. Anachoamini ni kuwa anatoa penzi nawe umpatie pesa. Tena sio pesa kidogo!!
Anachuma mamilioni.
(MIKASA ZAIDI YA ASIA NI KATIKA SIMULIZI YA ASIA DIGITALI kama hujaisoma wasiliana nami inbox)
Alikuwa anamiliki gari yake, na nyumba nzima ya kupanga….. pesa yote aliitoa kwa wanaume katika njia za ki-digitali.
Asia akiwa na rafiki yake Husna wakaongoza njia kuelekea msikitini Kariakoo…
. . Jua lilikuwa kali, kilammoja alifanya jitihada za kupambana na joto la jijini Dar es salaam.
Hekaheka za hapa na pale Kariakoo ziliufanya mji kuonekana mdogo sana.
Kanzu nyeupe na mabaibui meusi yalitapakaa huku na kule ishara ya sala ya ijumaa.
. . Asia naye alikuwemo katika hekaheka za siku hiyo.
. . Muda wa sala ulipowadia kila mtu alikuwa mahala pake akiswali.
. . Asia naye alikuwa mmoja kati ya waliojumuika kuswali katika msikiti ambao hajawahi kuswali hapo kabla.
. . Asia aliswali huku mahesabu yake yakienda sawa kabisa juu ya mipango yake madhubuti kichwani.
. . Muda wa swala ulipomalizika Asia alitoka nje ya msikiti.
. . Akaangaza macho huku na kule.
. . Aliyategea mawindo yake yaweze kunasa.
. . Hatua kwa hatua Asia alijitembeza, kwa kasi huku akipigia mahesabu makali ya tukio ambalo litatokea.
. . Asia alikuwa akimtazama mwanaume mfupi mweusi ambaye huenda alikuwa amependeza kuliko wote ndani ya kanzu yake yenye thamani ya juu.
Asia alimtazama jinsi alivyokuwa amejikita katika kutumia simu yake. Asia akatumia upenyo ule.
. . Akajipitisha mbele yake, bwana yule pasipokumwona Asia akajikuta amemkanyaga. Asia akajilegeza akatua chini.
. . Aliyemgonga alikuwa ni Hassan Tembo, Munyama mukubwa kamba fedha ambaye alikuwa amevurugwa haswa na tukio lililotokea kwa Mamamia.
Hassan alikuwa anajulikana sana maeneo yale ya msikitini, asingeweza kumkimbia Asia ama kumpuuzia, aliheshimika kutokana na moyo wake wa kujitolea huku akiwa kijana mdogo.
. . Tukio la Asia akalitumia kama nafasi nyingine ya kuthibitisha kuwa ana pesa japo kwa wakati huo alitumia gari la kuazima na hakuwa na kadi yake ya benki japo alikuwa na kiasi fulani cha pesa alichokuwa amehifadhi ndani ya nyumba yake.
Akaamuru apelekwe katika gari lake binti yule.
Wafuasi wakambeba Asia hadi ndani ya gari la Tembo.
. . Akisindikizwa na wanaume wawili Hassan alimchukua Asia hadi katika hospitali ya watu binafsi maeneo ya mnazi mmoja.
Hapa sasa hakuwahitaji wale watu tena, akabaki peke yake.
Uzuri ni kwamba alikuwa na bima ya afya hivyo alifanya utaratibu na pesa kiduchu ikaongea Asia akatibiwa bure kwa kutumia kadi yake.
. . Hassan baada ya kuelezwa kuwa binti yule hakuwa amepata majeraha makubwa sana aliamua kuondoka naye aweze kumrejesha nyumbani.
Wakiwa ndani ya gari Hassan Tembo akakumbuka kuwa alikuwa matatani, na kilichochokonoa kichwa chake ni kisa cha Mamamia, akajiuliza ni lipi lilisababisha yale mambo kutokea. Akakumbuka na kujisahihisha kuwa haukuwa utaratibu wake kulala na msichana mmoja mara mbili.
Mh! Yawezekana ndo tatizo kweli ama?? Alijiuliza bila kupata jibu.
Akilini mwake sasa aliingiwa na ujasiri wa ajabu sana, hakutishika na kilichotokea chumbani akiwa na Mamamia, ile akili yake ya zamani ikarejea tena kwa kasi akaona Asia alikuwa mtu sahihi kabisa wa kumfanyia majaribio.