Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #61
ASALI HAITIWI KIDOLE
SEHEMU YA KUMI NA SITA
MTUNZI: edgar MBOGO
WHATSAPP: 0717924403 au 0743632247.
ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI NA TANO: Tuanze na huko ndani, ambako mama Zuhura aliwaita wakina Mariam, ambao aliingia nao chumbani kwake, “nimewaita wote wawili, kuna kitu nataka tuongee” alisema mama Mariam kwa sauti ya chini, kiasi kwamba, ata kama kunamtu alikuwa amekaa nje ya chumba iki yani mlangoni asinge sikia. ENDELEA….
Wakina Mariam wakatega masikio kwa umakini, kumsikiliza mama yao ambae ni kama rafiki yao linapokuja swala la upinzani na mke mwenzie, ya ni mama Radhia.
Mama riam aliwaimulia kikao chake na mzee Abeid na mama Radhia, akiwaeleza jinsi baba yao alivyo kataza kumsimanga Radhia, “lakini kama akiwachokoza wala msimwache msemeni kama kawaida, kwani uongo siyo mjane, yeye alipoolewa si aliwaona nyie amfai na kwamba yeye ndie mwenye bahati sana, na yeye peke yake ndie anae faa kuolewa, sasa kikowapi?” alisema mama Mariam, na kuwafanya watoto wake wazibe midomo wakizuwia vicheko, kuogopa baba yao asije kusikia.
“alafu sijuwi amepata kibwana gani, kinashindwa ata kununulia nguo” alisema Mariam, na kumfanya mama Mariam aache mdomo wazi kwa mshangao, “weee! Usiniambie, au ndio huyo alie mpa hiyo ela mnayosema?” aliuliza mama Mariam, huku anwatazama watoto wake kwa hawamu, “mh! sizani kama ni huyo, amtoe wapi mwanaume mwenye fedha kiasi hicho, si ange mnunulia nguo za siku kuu, baada ya kuwapa ela wakina Mu, wachezee” alisema Mariam, kwa sauti yenye mashaka na zarau, lakini kumbuka kuwa, Mariam na Radhia wamepishana mwaka mmoja tu wakuzaliwa.
Wakati ndani maongezi ya kiwa hayo, huku nje nako, mambo yalikuwa hivi, “vipi tena mbona kama wamechukia?” anauliza mama Radhia, ambae aliona hali ya Mariam na Zuhura, wakati anapishana nao, “ata siwaelewi, walikuwa wanajiongelesha hapa, nashangaa ghafla wamebadirika” alisema Radhia, ambae uso wake ulikuwa ujawa na furaha.
Mama Radhia anaona hali ya furaha ya Radhia, anakosa uvumilivu, maana nikawaida yao kushiriki furaha kwa pamoja, “vipi mwenzetu, naona ume amka naunyonge ghafla umapatwa na furaha” anaongea mama Radhia kwa sauti iliyojaa utani, “walaaa hakuna kitu” anasema Radhia na wakati huo anaonekana Mukhsin akiwa anakuja kwa mwendo wa haraka, huku amebeba mifuko mitatu mikubwa na zuri, maalumu toka kwenye maduka ya nguo.
Wote wanamwona, Zahara anatimka mbio kumfwata kaka yake, maana anajuwa zile ni nini, na zinatoka wapi, maana anakumbuka jana waliahidiwa na Edgar, ambae alisema kuwa wanamtoko wa pamoja, “he! Radhia huyu nae ametoa wapi hivyo vitu” anauliza mama Radhia, huku anamtazama Radhia kwa macho ya udadisi.
Radhia kabla ya kujibu anacheka kidogo, huku anamtazama Mukhsin, ambae alikuwa amesha mfikia, “rafiki yake Mu, amesema leo tumealikwa sehemu, hivyo akasema ata nunua nguo kwaajili yetu” alisema Radhia kwa sauti ya chini, yenye aibu ya kike, aibu ambayo ilimfanya mama yake ahisi kitu, lakini anashindwa kusema maana Mukhsin na Zahara waliwepo pale.
“dada wewe wakwako huu na Zahara huu hapa, amesema saa sita gari linakuja kutuchukuwa” alisema Mukhsin, akiwa katika hali ya furaha, huku anampatia Radhia mifuko miwili, kisha akaingia ndani.
Radhia akiwa ameshikilia mfuko mwili, anatulia kusubiri swali toka kwa mama yake, “unasubiri nini sasa, ebu twendeni ndani tukajionee hivyo vilivyomo ndani, au mpaka waje hao wenye maneno mengi” anasemama Radhia huku anainuka na kuchukuwa ile mifuko miwili na kuingia nayo ndani, akifwatiwa na Zahara kisha Radhia.
Mpaka wanaingia ndani, bado Mariam Zuhura na mama yao walikuwa awajatoka, chumbani walikokuwa wanakikao cha muda, kikao ambacho ata mama Radhia alikuwa anakifahamu.
Aliekuwa anatoa nguo kwenye mfuko ni mama Radhia mwenyewe, akiwa ameanza na mfuko ambao ulisemekana kuwa ni wa Zahara, ambao ulikuwa na nauni zuri sana lenye rangi ya blue, na nakshi za mauwa ya rangi ya silver, na dhahabu, pia hijab na mtandio wa rangi ile ile, ya blue na nakshi kama ilivyo kwenye gauni, viatu zuri vya mikanda, vyenye rangi nyeusi na fito za blue.
Hakika zilikuwa nzuri sana, japo hawa kujuwa gharama yake, lakini zilivutia sana machoni pa kila mmoja wao, na kuwapa hapa hamu ya kuangalia mfuko wa Radhia, ambao pia licha ya kuwa na nguo iliyofanana na lile gauni la Zahara, na viatu kama vyake, ila pia, kulikuwa na pea gauni jingine, lenye rangi nyekundu ya kung’aa, huku likiwa na nakshi za bulue na silver, hijab na viatu pea mbili, zilizo fanana rangi na nguo zake, kama ilivyokuwa kwa Zahara.
Licha ya vitu hivyo vyote, lakini pia bado kuna vitu ndani ya mfuko, mama Radhia anaingiza mkono na kutoa rangi ya mdomo wanja na manukato mbali mbali, pia kimkebe cha mkufu mzuri wenye kipambo cha rubi, lakini bado kuna vitu vingine ndani ya mfuko.
Mama Radhia anaingiza mfuko na kuibuka na komkoba mpya wakike, uliotuna kweli kweli, anaufungua na kuingiza mkono ndani yake, anaibuka na kubunda cha nguo, wote wanatoa macho ya mshangao.
Zilikuwa ni nguo za ndani, yani chupi na sidilia, kiwa ni tatu tatu kwa rangi tofauti, nyeupe pink na nyekundu, zenye maua tofauti tofauti, zikiwa zinafanana na kwa pea ya chupi na sidilia, “Radhia umesema ni rafiki wa Mu?” anauliza mama Radhia kwa mshangao, “ndiyo mama, ni rafiki yake Mu, niyule alie mnunulia viatu vya mpira, mwulize ata Zahara” anasema Radhia kwa namna ya kujitetea.
Mama Radhia anatulia, lakini bado anamashaka, anatumia sekunde kadhaa kuwaza jambo, kabla ajamtazama binti yake mdogo, “aya nenda kaoge si mmeambiwa saa sita mna kuja kuchukuliwa” anasema mama Radhia akimtazama Zahara, ambae haraka sana aanza kujiandaa, anatumia dakika tatu, mpaka kutoka nje na kwenda bafuni.
Chumbani sasa wamebakia wawili, “Radhia auna aja ya kunificha lolote, ebu niambie, huyo mwanaume ni yupi na anakazi gani?” anauliza mama Radhia, kwa sauti tulivu huku anamtazama Radhia usoni, ambae akuonyesha wasi wasi wowote, zaidi ni nijiaibu kwambali, “mama huyu ni rafiki yake Mu, anaitwa Edgar, wala sijuwi lolote kuhusu yeye” alisema Radhia, kisha akamsimulia kuhusu kukutana kwao, na jinsi iilivyokuwa, mpaka kuletewa nguo leo hii.
Radhia alimweleza mama yake kila kitu, kwamba yeye alitoka kwa lengo la kuwapeleka wakuna Zahara, wakakutane na kijana huyo, ambae ata yeye anamfahamu, “lakini nilipotaka kuondoka Edgar akasema nibakie kwanza, maana pake yake asingeweza kukaa na wakina Zahara” alieleza Radhia, na pia akaeleza kuhusu mwaliko, “nilimweleza kuwa mimi sitoweza kwenda, akauliza kwanini, ndio Zahara akamweleza kuwa sababu sikuwa na nguo, nae akasema kuwa atatnunua nguo za kila mtu” alieleza Radhia.
Mama Radhia alisikiliza kwa umakini maelezo ya binti yake, kisha akamweleza, “Radhia, wewe ni mkubwa sasa, na wala ukataliwi kufanya unacho taka, lakini angalia thamani yako na usalama wako” alisema mama Radhia, kisha akamweleza kuhusu maongezi yao na baba yake jana usiku.******
Naaaaaaam!, saa sita na nusu, Mariam na Zuhura wakiwa kibarazani, wakisubiri kula chakula cha mchana, ili wakatembee wanako kujuwa wao, wapo pamona mama Radhia na mama yao, ambae ndie alie kuwa anapika, huku wakina Khadija wanacheza pale mbele ya nyumba yao, hakuwepo Radhia wala Zahara.
“kwahiyo nyie leo mnatoka wenyewe, watoto mtawaacha na nani?” anauliza mama Mariam, “watacheza na wakina Zahara” anajibu kwa haraka Mariam, “Zahara ana toka na Mukhsin na dada yao” anajibu mama Radhia, na kuwafanya Mariam na Zuhura watazamane kwa mshangao. ENDELEA…. KUFWATILIA HADITHI HII YA #ASALI_AITIWI_KIDOLE, HAPAHAPA JamiiForums
SEHEMU YA KUMI NA SITA
MTUNZI: edgar MBOGO
WHATSAPP: 0717924403 au 0743632247.
ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI NA TANO: Tuanze na huko ndani, ambako mama Zuhura aliwaita wakina Mariam, ambao aliingia nao chumbani kwake, “nimewaita wote wawili, kuna kitu nataka tuongee” alisema mama Mariam kwa sauti ya chini, kiasi kwamba, ata kama kunamtu alikuwa amekaa nje ya chumba iki yani mlangoni asinge sikia. ENDELEA….
Wakina Mariam wakatega masikio kwa umakini, kumsikiliza mama yao ambae ni kama rafiki yao linapokuja swala la upinzani na mke mwenzie, ya ni mama Radhia.
Mama riam aliwaimulia kikao chake na mzee Abeid na mama Radhia, akiwaeleza jinsi baba yao alivyo kataza kumsimanga Radhia, “lakini kama akiwachokoza wala msimwache msemeni kama kawaida, kwani uongo siyo mjane, yeye alipoolewa si aliwaona nyie amfai na kwamba yeye ndie mwenye bahati sana, na yeye peke yake ndie anae faa kuolewa, sasa kikowapi?” alisema mama Mariam, na kuwafanya watoto wake wazibe midomo wakizuwia vicheko, kuogopa baba yao asije kusikia.
“alafu sijuwi amepata kibwana gani, kinashindwa ata kununulia nguo” alisema Mariam, na kumfanya mama Mariam aache mdomo wazi kwa mshangao, “weee! Usiniambie, au ndio huyo alie mpa hiyo ela mnayosema?” aliuliza mama Mariam, huku anwatazama watoto wake kwa hawamu, “mh! sizani kama ni huyo, amtoe wapi mwanaume mwenye fedha kiasi hicho, si ange mnunulia nguo za siku kuu, baada ya kuwapa ela wakina Mu, wachezee” alisema Mariam, kwa sauti yenye mashaka na zarau, lakini kumbuka kuwa, Mariam na Radhia wamepishana mwaka mmoja tu wakuzaliwa.
Wakati ndani maongezi ya kiwa hayo, huku nje nako, mambo yalikuwa hivi, “vipi tena mbona kama wamechukia?” anauliza mama Radhia, ambae aliona hali ya Mariam na Zuhura, wakati anapishana nao, “ata siwaelewi, walikuwa wanajiongelesha hapa, nashangaa ghafla wamebadirika” alisema Radhia, ambae uso wake ulikuwa ujawa na furaha.
Mama Radhia anaona hali ya furaha ya Radhia, anakosa uvumilivu, maana nikawaida yao kushiriki furaha kwa pamoja, “vipi mwenzetu, naona ume amka naunyonge ghafla umapatwa na furaha” anaongea mama Radhia kwa sauti iliyojaa utani, “walaaa hakuna kitu” anasema Radhia na wakati huo anaonekana Mukhsin akiwa anakuja kwa mwendo wa haraka, huku amebeba mifuko mitatu mikubwa na zuri, maalumu toka kwenye maduka ya nguo.
Wote wanamwona, Zahara anatimka mbio kumfwata kaka yake, maana anajuwa zile ni nini, na zinatoka wapi, maana anakumbuka jana waliahidiwa na Edgar, ambae alisema kuwa wanamtoko wa pamoja, “he! Radhia huyu nae ametoa wapi hivyo vitu” anauliza mama Radhia, huku anamtazama Radhia kwa macho ya udadisi.
Radhia kabla ya kujibu anacheka kidogo, huku anamtazama Mukhsin, ambae alikuwa amesha mfikia, “rafiki yake Mu, amesema leo tumealikwa sehemu, hivyo akasema ata nunua nguo kwaajili yetu” alisema Radhia kwa sauti ya chini, yenye aibu ya kike, aibu ambayo ilimfanya mama yake ahisi kitu, lakini anashindwa kusema maana Mukhsin na Zahara waliwepo pale.
“dada wewe wakwako huu na Zahara huu hapa, amesema saa sita gari linakuja kutuchukuwa” alisema Mukhsin, akiwa katika hali ya furaha, huku anampatia Radhia mifuko miwili, kisha akaingia ndani.
Radhia akiwa ameshikilia mfuko mwili, anatulia kusubiri swali toka kwa mama yake, “unasubiri nini sasa, ebu twendeni ndani tukajionee hivyo vilivyomo ndani, au mpaka waje hao wenye maneno mengi” anasemama Radhia huku anainuka na kuchukuwa ile mifuko miwili na kuingia nayo ndani, akifwatiwa na Zahara kisha Radhia.
Mpaka wanaingia ndani, bado Mariam Zuhura na mama yao walikuwa awajatoka, chumbani walikokuwa wanakikao cha muda, kikao ambacho ata mama Radhia alikuwa anakifahamu.
Aliekuwa anatoa nguo kwenye mfuko ni mama Radhia mwenyewe, akiwa ameanza na mfuko ambao ulisemekana kuwa ni wa Zahara, ambao ulikuwa na nauni zuri sana lenye rangi ya blue, na nakshi za mauwa ya rangi ya silver, na dhahabu, pia hijab na mtandio wa rangi ile ile, ya blue na nakshi kama ilivyo kwenye gauni, viatu zuri vya mikanda, vyenye rangi nyeusi na fito za blue.
Hakika zilikuwa nzuri sana, japo hawa kujuwa gharama yake, lakini zilivutia sana machoni pa kila mmoja wao, na kuwapa hapa hamu ya kuangalia mfuko wa Radhia, ambao pia licha ya kuwa na nguo iliyofanana na lile gauni la Zahara, na viatu kama vyake, ila pia, kulikuwa na pea gauni jingine, lenye rangi nyekundu ya kung’aa, huku likiwa na nakshi za bulue na silver, hijab na viatu pea mbili, zilizo fanana rangi na nguo zake, kama ilivyokuwa kwa Zahara.
Licha ya vitu hivyo vyote, lakini pia bado kuna vitu ndani ya mfuko, mama Radhia anaingiza mkono na kutoa rangi ya mdomo wanja na manukato mbali mbali, pia kimkebe cha mkufu mzuri wenye kipambo cha rubi, lakini bado kuna vitu vingine ndani ya mfuko.
Mama Radhia anaingiza mfuko na kuibuka na komkoba mpya wakike, uliotuna kweli kweli, anaufungua na kuingiza mkono ndani yake, anaibuka na kubunda cha nguo, wote wanatoa macho ya mshangao.
Zilikuwa ni nguo za ndani, yani chupi na sidilia, kiwa ni tatu tatu kwa rangi tofauti, nyeupe pink na nyekundu, zenye maua tofauti tofauti, zikiwa zinafanana na kwa pea ya chupi na sidilia, “Radhia umesema ni rafiki wa Mu?” anauliza mama Radhia kwa mshangao, “ndiyo mama, ni rafiki yake Mu, niyule alie mnunulia viatu vya mpira, mwulize ata Zahara” anasema Radhia kwa namna ya kujitetea.
Mama Radhia anatulia, lakini bado anamashaka, anatumia sekunde kadhaa kuwaza jambo, kabla ajamtazama binti yake mdogo, “aya nenda kaoge si mmeambiwa saa sita mna kuja kuchukuliwa” anasema mama Radhia akimtazama Zahara, ambae haraka sana aanza kujiandaa, anatumia dakika tatu, mpaka kutoka nje na kwenda bafuni.
Chumbani sasa wamebakia wawili, “Radhia auna aja ya kunificha lolote, ebu niambie, huyo mwanaume ni yupi na anakazi gani?” anauliza mama Radhia, kwa sauti tulivu huku anamtazama Radhia usoni, ambae akuonyesha wasi wasi wowote, zaidi ni nijiaibu kwambali, “mama huyu ni rafiki yake Mu, anaitwa Edgar, wala sijuwi lolote kuhusu yeye” alisema Radhia, kisha akamsimulia kuhusu kukutana kwao, na jinsi iilivyokuwa, mpaka kuletewa nguo leo hii.
Radhia alimweleza mama yake kila kitu, kwamba yeye alitoka kwa lengo la kuwapeleka wakuna Zahara, wakakutane na kijana huyo, ambae ata yeye anamfahamu, “lakini nilipotaka kuondoka Edgar akasema nibakie kwanza, maana pake yake asingeweza kukaa na wakina Zahara” alieleza Radhia, na pia akaeleza kuhusu mwaliko, “nilimweleza kuwa mimi sitoweza kwenda, akauliza kwanini, ndio Zahara akamweleza kuwa sababu sikuwa na nguo, nae akasema kuwa atatnunua nguo za kila mtu” alieleza Radhia.
Mama Radhia alisikiliza kwa umakini maelezo ya binti yake, kisha akamweleza, “Radhia, wewe ni mkubwa sasa, na wala ukataliwi kufanya unacho taka, lakini angalia thamani yako na usalama wako” alisema mama Radhia, kisha akamweleza kuhusu maongezi yao na baba yake jana usiku.******
Naaaaaaam!, saa sita na nusu, Mariam na Zuhura wakiwa kibarazani, wakisubiri kula chakula cha mchana, ili wakatembee wanako kujuwa wao, wapo pamona mama Radhia na mama yao, ambae ndie alie kuwa anapika, huku wakina Khadija wanacheza pale mbele ya nyumba yao, hakuwepo Radhia wala Zahara.
“kwahiyo nyie leo mnatoka wenyewe, watoto mtawaacha na nani?” anauliza mama Mariam, “watacheza na wakina Zahara” anajibu kwa haraka Mariam, “Zahara ana toka na Mukhsin na dada yao” anajibu mama Radhia, na kuwafanya Mariam na Zuhura watazamane kwa mshangao. ENDELEA…. KUFWATILIA HADITHI HII YA #ASALI_AITIWI_KIDOLE, HAPAHAPA JamiiForums