DYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
★★★★★★★★★★★★★★★★
Zilipita siku mbili baada ya Grace kumweleza Dylan ukweli huo wote. Sasa walikuwa pamoja nyumbani usiku, wakiwa na Jafari, ambaye aliitwa na Grace ili waongelee kuhusiana na mipango yao. Ni hapa ndipo Dylan alipata kujua kuwa Jafari ndiye yule mwanaume aliyekuwa akimwona mara kwa mara akimfatilia kule alikoishi kwa Baraka. Ndiyo huyu aliyemwona kipindi kile saluni, kwenye mechi, na akitokea hapo nyumbani kwa Grace. Alikuwa mpelelezi wake wa kibinafsi ambaye pia alitaka sana kufichua uovu mwingi wa Mr. Bernard.
Jafari alikuwa akieleza mambo mengi ambayo alipata kufahamu kutokana na uchunguzi alioufanya, naye Dylan akawa anapitia baadhi ya vitu ambavyo vilikuwa kama ushahidi wa yale waliyoyaona kuwa ni matendo ya hila kutoka kwa Mr. Bernard. Wote walikuwa wameketi kwenye viti ndani ya ofisi ya Grace ya nyumbani, wakijadiliana na kupanga mambo mengi vizuri kwa kuwa sasa timu yao ilikamilika.
"....uliungua sana ndiyo sababu haikuwezekana kujua mwili ule ulikuwa ni wa nani. Wakauzika wakifikiri ni wako," Jafari akawa anamweleza Dylan.
"Advantage kubwa tuliyonayo ni kifo chako. Hawawezi kuona nini kinakuja ikiwa hawajui ni nani anakuja... ndiyo maana wewe ni wa muhimu sana kwenye hili Dylan," Grace akasema.
Dylan alikuwa anaangalia baadhi ya picha za helicopter ile iliyoanguka, ambazo Jafari alichukua wakati ule anafanyia uchunguzi.
"Boss... umesubiri kwa muda mrefu sana... na najua una uwezo mkubwa wa kumshusha Bernard chini. Kwa nini bado unasubiri?" Jafari akamuuliza Grace.
"Ni muhimu tujue kwanza nani yuko nyuma ya mgongo wake. Na pia ni kwa sababu maumivu nayotaka kumpa siyo kumshusha tu ki-mali... ila kumfanya ahisi maumivu yote aliyonifanya nipitie," Grace akajibu kwa hisia yenye mkazo.
"Usijali, Grace. Tutahakikisha anayapata," Dylan akasema kwa uhakika.
Grace akashusha pumzi kutulia.
"Walisema chanzo ni nini cha helicopter kuanguka?" Dylan akamuuliza Jafari.
"Kwamba iliishiwa fuel kwa hiyo ikapoteza mwelekeo na kuanguka," Jafari akajibu.
"Ni uwongo tu," Grace akasema.
"Ndiyo. Fuel kuisha siyo jambo lililofanya ianguke, kwa sababu inaonekana tatizo lilipotokea bado helicopter iliendelea kukaa juu kwa muda mrefu, bila shaka pilot akijaribu kuirudisha kwenye control," Jafari akaeleza.
"Story mbovu sana ku-cover jambo zito namna hiyo. Kweli... waseme tu eti fuel iliisha... ina maana wenye hiyo helicopter hawana mafunzo kujua mapema mambo yanayohitajika kabla chombo hakijapanda juu?" Grace akasema.
Dylan akazitazama picha tena, kisha akamwangalia Jafari na kuuliza, "Uliweza kuipata CVR?"
Jafari alishangazwa kidogo na swali la Dylan.
"CVR ndiyo nini?" Grace akauliza.
"Aam... ni ufupisho wa Cockpit Voice Recorder; kifaa fulani cha kurekodi sauti ndani ya helicopter. Umejuaje kuhusu hilo?" Jafari akaeleza na kumuuliza Dylan hivyo.
"Sijui... yaani sikumbuki lakini... najua tu kwamba najua," Dylan akasema.
Jafari akatabasamu na kusema, "Okay. Ninacho hapa."
Akakitoa kwenye boksi ambalo alikuja nalo lililokuwa na vifaa vingi vya upelelezi wake. Simu ya Dylan ikaanza kuita. Ilikuwa mezani, kwa hiyo yeye pamoja na Grace waliweza kuona jina la aliyepiga, naye alikuwa Leila. Dylan akamtazama Grace machoni, naye Grace akamwangalia pia. Kisha Dylan akakata na kuipotezea kabisa.
"Uliwaibia?" Dylan akauliza kiutani.
"Chochote kwa ajili ya boss," Jafari akajibu kiutani pia.
Dylan akatabasamu na kukichukua.
"Hiki kifaa huwa useful sana hasa kwa ma-investigatorwanaochunguza helicopter zilizoanguka. Nilihitaji kutumia resource nyingi ili nikichukue, lakini kila kitu alichosema rubani humo hakikunisaidia kujua nini hasa lilikuwa tatizo, ijapokuwa inaonekana tatizo hilo ni kitu ambacho hakuweza ku-solve," Jafari akamwelezea Grace.
Dylan akakiwasha, na wote wakaanza kusikiliza maneno ya mwisho ya rubani ya kuomba msaada wakati chombo kilipoanza kuleta shida mpaka kuanguka. Grace hakuona ulazima wala umuhimu wa kusikiliza mambo hayo, lakini akamwacha tu Dylan afanye utafiti wake ili aone kama angegundua kitu. Baada ya Dylan kuwa amesikiliza kwa makini, akaizima na kumtazama Jafari.
"Ni rotor," akasema kwa uhakika.
"Nini?" Grace akauliza.
"Yaani... kuna kifaa kinaitwa rotor ambacho huwa kinapokea nguvu kutoka kwenye engine ndani ya helicopter. Ndege za kawaida huwa zina redundancy kwenye vifaa muhimu ndani yake, na huwa zinasaidia flight control ili kama system moja ikifeli, basi nyingine inachukua nafasi ili kuisaidia ndege. Helicopter mara nyingi HAINA redundancy kwenye vifaa vyake muhimu. Ndege ya kawaida inaweza kupoteza engine moja na bado ikaendelea kwenda angani, lakini helicopter haingeweza. Nafikiri engineer aliyeishughulikia alifanya kui-crack kwa njia fulani ili baada ya muda ikiwa angani ipoteze mwelekeo," Dylan akaeleza kwa njia iliyomfanya Jafari astaajabu sana kuhusu ujuzi wake.
"Kimakusudi, si ndiyo?" Grace akamuuliza Dylan.
"Ndiyo," Dylan akajibu.
"Kwa hiyo tutumie vipi jambo hilo?" Jafari akauliza.
"Tutapaswa kujua helicopter ilitokea wapi na ni nani aliyeishughulikia tofauti na rubani aliyekufa. Mtu huyo ndiye aliyepewa maagizo ya kuifanya ifeli. Tukimpata na kuthibitisha kupitia yeye kuwa Mr. Bernard alihusika, huo utakuwa sehemu ya mwanzo mzuri wa kumwangusha mwanaume huyo," Dylan akasema.
Simu ya Dylan ikaanza kuita tena. Ilikuwa ni Leila kwa mara nyingine tena, naye Dylan akakata na kumwangalia Jafari.
"Nafikiri sehemu nzuri ya kuanzia ni kule helicopter ilikotokea asubuhi ile," Dylan akamwambia Jafari.
"Ndiyo... nitachunguza hilo. Boss, una jambo lingine la kuongeza?" Jafari akauliza.
"For now hapana. Just... give me updates on that if you get anything (utanipa taarifa za mapema ukipata chochote)," Grace akasema.
Jafari akakubali, kisha akakusanya vitu vyake na kuwaaga. Walikuwa wamemsihi akae ili apate chakula, lakini akawashukuru na kusema alikuwa anawahi sehemu nyingine. Hivyo akaondoka na kuwaacha wawili hao ofisini humo. Wakabaki wakiangaliana kwa sekunde kadhaa, kisha Grace akanyanyuka na kusogea mpaka usawa wa kiti alichokalia Dylan na kuanza kutembeza vidole vyake kwenye nywele zake.
"Twende tukapate chakula," akasema kwa sauti yenye kubembeleza.
Dylan akatabasamu na kusimama, kisha akamwangalia usoni kwa ukaribu sana na kutikisa kichwa kukubali. Grace akaondoka ofisini hapo, huku akimwacha Dylan anawaza bila shaka huenda Grace alihisi vibaya baada ya kuona Leila anampigia simu. Yeye pia akatoka ofisini humo na kuelekea sebuleni. Walikula pamoja mezani, kisha baadae Grace akarudi ndani ya ofisi yake ili apangilie mambo yake.
Dylan alielekea chumbani kwake, akitafakari mambo kadhaa kuhusu maisha yake. Alijiona kuwa kama mtu aliyepotea katikati ya msitu mkubwa, bila kujua aelekee wapi kwa sababu sehemu nyingi zilikuwa hatari. Lakini hakufa moyo; akaamua kuendelea kuwa imara kwa ajili ya yale ambayo yeye na Grace walidhamiria kufanya.
Baada ya masaa mawili hivi, Grace akawa chumbani kwake tayari, akiwa amesimama usawa wa dirisha pana la chumba hicho, akimtafakari Dylan. Hisia zake kumwelekea zilikuwa zenye nguvu kufikia wakati huu, lakini bado moyoni mwake alikosa amani kwa kufikiria uwezekano wa Dylan kuendelea kutoka kimapenzi na Leila. Dylan alikuwa amemfanya aijue raha ya kupenda, hivyo hangetaka kuwazia hata kidogo kumpoteza kijana huyo kwa mwanamke mwingine.
Ni wakati akiendelea kuwaza, pale Dylan alipoingia chumbani kwake na kusimama umbali mfupi kutokea aliposimama Grace. Grace alijua Dylan alikuwa nyuma yake, lakini hakugeuka. Dylan akawa anamwangalia kwa upendo, jinsi 'night dress' yenye kung'aa aliyovaa ilivyoupendezesha mwili wake ulionawiri vyema.
"Mbona bado hujalala?" Dylan akauliza kwa sauti ya chini.
"Usingizi haunitaki," Grace akajibu.
Dylan akatabasamu na kumsogelea karibu zaidi.
"Umeongea na Leila?" Grace akauliza.
"Ndiyo."
"And?"
"Alikuwa... anaomba samahani... anataka nimsamehe na tukutane ili tuongee vizuri," Dylan akasema.
Grace akakwazika kiasi. Dylan tayari alikuwa amekwishamwambia kuhusu usaliti wa Leila, kwa hiyo alijua vizuri mwanamke yule alihitaji msamaha wa nini.
"Kwa hiyo umeamuaje?" akauliza.
"Wewe unafikiri nimeamuaje?" Dylan akamuuliza pia.
"Nitajuaje sasa? Ni wewe ndiyo mwenye maamuzi. Najua... unampenda... kwa hiyo..." Grace akasema kwa njia ya kuvunjika moyo.
Dylan akawa ameelewa hilo. Akatabasamu na kusogea mpaka nyuma yake na kuizungushia mikono yake kiunoni mwa Grace. Grace akasisimka na kufumba macho yake, huku Dylan akiwa ameweka kichwa chake nyuma ya kichwa cha Grace.
"Kujua kwamba nimeongea na Leila kumekufanya uone wivu eti?" Dylan akauliza kiutani.
"Wivu? Unanitania?" Grace akakanusha.
"Aaah come on... usikatae, kubali tu nijue."
"Hakuna kitu kama hicho. Ukitaka m...mrudiane... ni wewe tu, me siwezi kuku..."
Kabla Grace hajamailiza kuongea, Dylan akamgeuza na kuanza kumpiga denda kwa wororo sana. Kama kawaida ya Grace, alilegea na kuanza kurudisha pigo za jamaa kwa upendo, akiunyonya ulimi wake kwa raha zote. Kisha Dylan akaiachia midomo yake taratibu na kumtazama machoni akiwa ameushika uso wake.
"Usiogope Grace.... mimi ni wako sasa," akamwambia kwa hisia.
Grace akatabasamu kwa hisia, akifurahia kujua kuwa Dylan alikuwa wa kwake peke yake. Akaifata midomo ya mwanaume wake sasa na kuendelea kudendeshana naye, akimwonyesha dhahiri kuwa alifurahia penzi lake. Dylan kama kawaida hakukwaza; aliendelea kuinyonya midomo ya bibie kimahaba huku mikono yake ikiishusha mikanda myepesi ya night dress aliyovaa Grace. (.......).
(........).
Haikuchukua muda mrefu hata kidogo, na wote wakawa mawinguni kihisia, wakionyeshana mapenzi ya dhati kwa vitendo vingi. Dylan alimpeleka Grace kitandani na hapo akahakikisha anapiga show ya kibabe mpaka Grace akatosheka. Wote walipitiwa na usingizi baada ya karibia masaa mawili ya kupeana malavidavi pamoja kitandani hapo.
★★★
Siku zilizofuata zilikuwa ni siku zenye ubize mwingi wa kimipango ya kazi na kisasi cha wawili wale ambao sasa walikuwa wapendanao; Grace na Dylan. Dylan alisoma kila kitu kuhusu kampuni ya baba yake na kupata kujua mambo mengi kuihusu. Kama Grace alivyomwambia, jambo kuu lilikuwa kupanga kila jambo vyema na kutambua anayemsaidia Mr. Bernard ni nani hasa, ili waweze kupiga hatua yao kwa usahihi. Dylan aliongeza mambo kadhaa kwenye mipango ya Grace kwa kutoa mawazo ya nyendo zitakazofaa zaidi ili kumwangusha Mr. Bernard na kumfichua msaidizi wake.
Upande wa wazazi wake Dylan, walikuwa wakiendelea kupambana kurudisha nafasi zao kwenye kampuni, huku wakitafuta mambo yatakayowasaidia kuweza kumpata Dylan kimya kimya. Gilbert alikazia mara kwa mara kwa Jaquelin kuwa hakupaswa kumwambia YEYOTE kuhusiana na jambo hilo, kwa sababu alifikiria bila shaka Dylan alikuwa na maana yake kutojitokeza kwao mapema.
Jaquelin alikuwa na hamu sana ya kumwona mwanae tena, hivyo wakati mwingine angehisi kukosa subira kwa kuwa bado hawakuweza kujua Dylan yuko wapi. Fetty alienda mara kwa mara kwenye club ile nje ya jiji lao ili kuona kama Dylan angefika tena, lakini aliambulia kuvunjika tu moyo. Ila hakukata tamaa. Aliamini kutoka moyoni mwake kuwa angemwona tena mwanaume huyo aliyekuwa ameanza kumpenda kwa dhati muda mfupi kabla ya taarifa za "kifo" chake.
Kwake Jafari, mambo yalipamba moto. Aliweza kumpata mwanaume yule ambaye alihusika pamoja na rubani wa helicopter katika udumishaji mzuri wa chombo hicho. Alimfatilia na kujua alikuwa mwanaume aliyeitwa Pius, mtu mzima mwenye miaka 54, ambaye alikuwa amesomea masuala ya vyombo vya angani na alifanya kazi kama mekanika wa vifaa vikubwa vya ndege.
Jafari alipopata nafasi ya kumbana na kumhoji kuhusu yeye kuihujumu helicopter ile (sabotage), mwanaume huyo alipinga vikali na kumwambia asimsumbue tena. Lakini Jafari alimhakikishia kuwa ushahidi anao kutoka kwenye kifaa cha kurekodi maneno ya rubani, ambayo yalionyesha kuwa kweli kuna 'sabotage' ilifanywa ambayo rubani huyo mzungu hakuitambua kwa sababu mwanaume huyu ndiye aliyeshughulikia eneo hilo la chombo.
Jafari akahusisha jina la Mr. Bernard pia, na hapo akaona jinsi mwanaume huyo alivyotangatanga kuonyesha dhahiri kwamba kuna jambo alificha. Ikabidi Jafari amwambie kuwa angempatia pesa nyingi zaidi ya pesa alizopatiwa na Mr. Bernard kwa ajili ya jambo lile ikiwa atasema ukweli, lakini Pius akakanusha na kusema haelewi lolote Jafari analosema. Pius akamkwepa Jafari na kuondoka eneo walilokuwepo ili asiendelee kumhoji tena, hivyo Jafari akawataarifu Grace na Dylan kuhusu yaliyojiri upande wake. Aliwaambia aliona bila shaka Pius kuna jambo alificha, na asingeishia hapo kumshawishi mpaka aseme ukweli.
Pius aliwasiliana na Mr. Bernard baada ya kumkimbia Jafari, kumjulisha kuwa kuna mtu alikuwa anafatilia jambo hilo ambalo alihusika kumsaidia. Ikawa wazi sasa kwamba, kweli Mr. Bernard alimlipa Pius aikwamishe rotor ya helicopter kitaalamu siku ile Dylan alipotumiwa helicopter hiyo. Kwa kuwa mpango wao ulifanikiwa, na wote walifikiri kwamba Dylan na wengine waliokuwemo mule walikufa, suala hili la mtu kumpeleleza Pius lilimshangaza Mr. Bernard. Alijiuliza ni nani ambaye angetaka kufufua jambo hilo kwa wakati huu; na kwa nini. Akamwambia Pius awe makini zaidi na akimwona tena mpelelezi huyo basi amjulishe haraka sana ili ashughulike naye.
Mr. Bernard akamjulisha jambo hili MTU yule ambaye amekuwa akimsaidia ili kuyaharibu maisha ya Gilbert na Jaquelin. Yeye pia hakuwa na wazo la ni nani ambaye alitaka kujua ukweli, lakini alitambua muda si mrefu jambo hili lingeweza kuzua tatizo kubwa. Hivyo akawa anaitengenezea akili yake mipango mingi zaidi ya kushughulika na hali hii, bila kumwambia Mr. Bernard lolote zaidi tu ya kumsihi awe mwangalifu zaidi. Hivyo, Mr. Bernard akamwambia Pius ahame eneo aliloishi haraka sana, na pale Jafari alipomtafuta kwa mara nyingine, akashangazwa kujua mwanaume huyo alitoroka na kuiacha familia yake. Kwa hiyo akafanya mpango wa kuendelea kumtafuta mpaka ampate tena; na zamu hii kingeeleweka.
Wakati hayo yakiendelea, Dylan alikuwa anafanya baadhi ya mipango yao yeye na Grace kuanza kazi. Kwa akili ya hali ya juu, alifichua siri nyingi za utendaji wa mambo haramu ya Mr. Bernard ambayo alijitahidi kuficha kwa siri kwa muda mrefu.
Mr. Bernard alifanya biashara nyingi haramu zilizohusisha uuzaji wa bidhaa ambazo zilikuwa zimeibiwa, kisha yeye angezibadili kwa njia ya kificho kupitia majengo yake ya biashara zisizo haramu ili kutovuta umakini wa vyombo vya usalama, na kuviingiza sokoni kwa bei nzuri tu. Kwa sababu Mr. Bernard alitenda kama mwasilishi wa kati baina ya wale waliomletea bidhaa zilizoibiwa na wateja ambao wangezinunua, aliwekeza pesa nyingi kwenye suala hili ambalo kwa muda mrefu lilimpatia faida. Zamani alihusika kwenye biashara ya watoto na wanawake kwa kuwaiba au kuwanunua na kuwauza kwa wenye pesa, lakini kwa wakati huu alikazia fikira zaidi magendo.
Kwa hiyo Dylan alipofanikisha kufichua kazi hizi haramu, ilikuwa ni jambo lililompiga Mr. Bernard kwa kishindo sana. Sehemu kadhaa zilizoendesha biashara hizo zilikamatwa na kukomeshwa. Lakini kwa sababu Mr. Bernard alikuwa amesafisha jina lake kupitia kazi rasmi kwenye kampuni ya Gilbert, hangeweza kutambuliwa kirahisi kwamba yeye ndiye aliongoza biashara hizo, kwa sababu pia hakutaka kujionyesha wazi kwa waliohusika nazo. Lakini mambo haya yalimpa hasara kubwa sana kwa sababu bidhaa nyingi za magendo zilipotaifishwa na kuteketezwa na mapolisi, ilimwacha bila pesa ya kuweza kugharamia potezo hilo.
Kwa kuharakisha mambo, akatumia pesa nyingi zilizowekezwa ndani ya kampuni ya Gilbert kujaribu kulipia makosa yake, na sasa kampuni ikaanza kutenda kwa njia mbovu sana baada ya hisa kushuka na kuporomoka kimapato. Ilikuwa ni kama ndoto kwake jinsi mambo yalivyobadilika upesi. Alipomwomba msaada MTU wake yule, alimwambia kwenye suala hilo angepaswa kushughulika nalo yeye mwenyewe kwa kuwa kwenye hilo hakuhusika; ilikuwa mzigo wa Mr. Bernard peke yake. Kampuni kuanza kuporomoka kidogo kidogo kuliwafanya washiriki wengi wa bodi ya kampuni wajiulize shida ilikuwa nini mpaka kusababisha hisa zao zilike, bila kutambua ni kiongozi waliyemchagua ndiye aliyechakachua.
Jambo hilo lilikuwa ndiyo lengo la Grace na Dylan. Walijua bila shaka Mr. Bernard angefanya kila awezalo kutafuta suluhisho, hivyo wao ndiyo wangekuwa suluhisho hilo. Mpango wa Grace ulikuwa kununua hisa ZOTE za kampuni ya Gilbert, ili iwe chini yake, kwa kuwa pesa ndefu alikuwa nayo. Hivyo wawili hawa walitumia mwakilishi aongee na kumshawishi Mr. Bernard kwa niaba yao kuwa kuna mwekezaji mkubwa aliyetaka kununua hisa hizo ili kuiinua kampuni zaidi kwa kuiwekezea pesa nyingi pia.
Mr. Bernard aliongea na washiriki wa bodi ili kuwashawishi, ambao nao pia waliona ni bora kukubali kwa kuwa mambo kweli yalikuwa yakienda vibaya. Alipoulizwa ikiwa alimjua mnunuzi, alisema ndiyo anamfahamu, na kwamba anajua ni mtu mwenye pesa na ana kampuni kubwa zilizoendelea hivyo angekuwa msaada mkubwa kwa kampuni yao pia.
Yote haya Mr. Bernard aliyafanya kwa papara kwa sababu alikuwa anahitaji suluhisho la haraka, hivyo hangeweza kutambua kwamba alijiingiza kwenye mtego ambao ungeyabadili kabisa maisha yake.
★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★
Jafari alifanikiwa kumpata Pius, yule mwanaume aliyemkimbia ili asiendelee kupelelezwa kuhusiana na ajali ile ya helicopter. Jafari aliweza kutambua kwamba Pius alifanya ionekane kama amekimbilia sehemu ya mbali, lakini akajua hiyo haikuwa kweli kupitia kusikiliza mawasiliano baina yake na watu wa familia yake. Pius alikuwa amekwenda kujificha nje ya wilaya aliyoishi, na mara kwa mara aliwasiliana na mke wake kuulizia hali nyumbani. Jafari alitumia utaalamu kuweza kuunganisha namba ya mke wake kwenye simu yake, ili atakapopokea au kupiga simu yoyote, aweze kuyasikiliza maongezi.
Baada ya Jafari kufanya utafiti na kugundua sehemu hususa Pius aliyokuwa, akawajulisha Dylan na Grace. Wakati huu, Grace alimwambia wanatakiwa kufanya mambo kwa umakini zaidi, ili kuweza kumnasa mwanaume huyo vizuri. Hivyo, Jafari akapiga hatua ya kwanza kwa kumfata eneo la sokoni, ambako Pius alikuwa na kawaida ya kwenda kununua chakula, kisha akaendelea kumfatilia polepole. Hakujionyesha kwake mpaka Pius aliporudi kwenye nyumba aliyokuwa amepanga chumba.
Pius alikuwa analipia chumba kidogo kwenye nyumba ya wapangaji, ambako aliweka godoro moja, neti na ndoo. Kutokana na kazi yake na hela nyingi alizolipwa kusababisha ajali ya Dylan, pesa ya kujikimu wakati amejificha alikuwa nayo. Ila bado aliogopa kwa kuwa hakujua ikiwa mambo haya yangeendelea au yangekwisha.
Wakati alipofika ndani kwake, akarudishia mlango na kuketi kwenye godoro chini; tayari kwa kuanza kula. Ila kabla hajaanza kula, mlango wake ukagongwa kuashiria kuna mtu nje alihitaji kuonana naye. Kwa haraka akafikiri ni mpangaji wa hapo, hivyo akaweka chakula pembeni na kwenda kufungua mlango. Macho yake yalitanuka kwa mshangao baada ya kumwona Dylan akiwa amesimama hapo. Alianza kurudi nyuma akiwa anatetemeka na kupumua haraka haraka kwa woga sana.
Dylan akapiga hatua na kuingia ndani mule, akifuatiwa na Jafari nyuma yake. Mwanaume huyo mwenye umri mkubwa aliogopa na kushindwa kuelewa nini kilikuwa kinaendelea. Jafari akapandisha T-shirt yake juu kidogo kumwonyesha Pius bastola kiunoni, kisha akaweka kidole chake kimoja mdomoni mwake kumwonyesha Pius kwamba asifanye fujo zozote.
Pius aliogopa sana. Alimwangalia Dylan kwa kutoamini kabisa kwamba ilikuwa ni yeye. Dylan akasogea karibu yake zaidi akiwa anamwangalia kwa njia ya kawaida.
"Habari yako Mr. Pius?" Dylan akasema kwa utulivu.
Pius akawa anamwangalia kwa wasiwasi.
"Najua me ni mdogo kwako lakini... shikamoo siyo kitu yangu kabisa," Dylan akatania, naye Jafari akatabasamu.
"Mnataka nini?" Pius akauliza.
"Wow! Tunataka nini? Yaani hauonyeshi hata woga kuona maiti inaongea?" Dylan akakejeli.
"Naombeni mniache... mimi sijui lolote mnalotaka..."
Kabla hajamaliza kuongea, Dylan alimpiga ngumi nzito usoni na kumfanya ajigonge ukutani. Ilimuumiza sana mpaka damu ikaanza kuvuja kutokea puani mwake. Jafari, akiwa nyuma ya Dylan, akatoa bastola yake na kumnyooshea Pius, kama anataka kumfyatulia risasi.
"Tafadhali... tafadhali... nina familia... jamani msiniue..." Pius akasema kwa woga.
"Kimya!" Jafari akamfokea.
Pius akaendelea kutetemeka kwa woga.
"Sema ukweli wote... kuanzia mwanzo hadi mwisho," Jafari akamwambia kwa mkazo.
*Mimi... mimi sijui..."
Hapo hapo Dylan akaishika shingo yake kwa nguvu na kumkaba huku amemkandamizia ukutani. Uso wa Dylan ukawa karibu na uso wa Pius, akimwangalia kwa hasira sana.
"Kuna vitu huwa nafanya wakati mwingine mpaka nakuwa sijielewi. Lakini naomba uelewe kuwa nimetokea kuzimu sasa hivi ambako wewe ndiyo ulikuwa njia ya kuhakikisha nafika, kwa hiyo nina hasira kidogo..." Dylan akasema kwa kejeli yenye ukali sana.
Pius akawa anahangaika kupumua na kutoa sauti za kukabwa.
"Una familia? Mimi pia nina familia. Lakini wakati wewe na mafala wenzako mnapanga kifo changu, haukujali hilo. Sikujui, hunijui, na sijali wewe ni nani. Ninakupa sekunde 10 uanze kuongea ukweli wote... zikipita sekunde kumi hujasema... Jafari mtandike risasi popote pale lakini asife... mpaka aseme," Dylan akasema kwa mkazo.
Jafari akaikoki bastola yake vizuri, naye Dylan akamwachia Pius na kusogea nyuma kidogo. Pius akawa anarudisha utaratibu kwenye kupumua, na sasa Jafari akawa anahesabu kama jinsi ambavyo sekunde hutembea.
"T...kkhohh.. tafadhali... tafadhali..usi..."
"...tano... sita... saba... nan...."
"Ni Bernard! Ni Yakobo Bernard! Ulikuwa mpango wake! Alinilipa pesa tu mimi nifanye vile... sikuwa na ubaya na mtu yeyote mimi..." Pius akaanza kuongea.
"Tutakuwaje na uhakika kwamba unachosema ni kweli? Je kama unamsingizia?" Jafari akauliza.
"Hapana... ni yeye ndiye aliyeniagizia bomu dogo na kunilipa ili nilipachike mule.... kwa njia ambayo halingeweza kuonekana..."
"Ili iweje?" Jafari akamuuliza.
"Ali... alitaka kumuua... kumuua huyu kijana... Mimi nilikubali tu kwa kuwa sikuwa na jinsi..."
"Hukuwa na jinsi? Angekuwepo mwanao kwenye hiyo helicopter ungekubali?" Dylan akamuuliza.
"Haiko hivyo... mwanzoni sikutaka lakini... Mr. Bernard alitishia usalama wa familia yangu..."
"Ulishindwa kwenda polisi?" Dylan akamuuliza kiukali.
"Mambo siyo rahisi kihivyo mwanangu..."
"Usiniite mwanao! Mambo siyo rahisi... kwa hiyo kuua mtoto wa mtu mwingine ni sawa eti kwa sababu wa kwako katishiwa? Hata kama jambo hilo lilikuwa gumu, hiyo hailifanyi liwe justified... aaaigh...." Dylan akashindwa hata kuendelea kutokana na hasira nyingi aliyohisi.
"Nisamehe kijana wangu... tafadhali nisamehe... nitafanya lolote lile..tafadhali..." Pius akaomba kwa huzuni.
Jafari akashusha bastola yake na kuirudisha kiunoni. Akatoa kifaa cha kurekodia sauti alichokuwa amekiweka mfukoni, ambacho kilikuwa kinarekodi kila kitu walichoongea muda huo wote.
"Mambo yote uliyosema yako hapa. Hiyo ni moja," Jafari akamwambia.
Pius akashangaa kwa kuwa hakujua alikuwa akichukuliwa sauti.
"Mbili, kwa kuwa umesema kwamba alikuagizia bomu, nahitaji uniambie aliliagiza kutokea wapi," Jafari akamwambia.
"...aam..." Pius akasita.
"Umesema utafanya lolote... ongea," Dylan akamwambia.
"Bla...black market," Pius akajibu.
"What?! Black market! Tanzania wana hizo?" Dylan akamuuliza Jafari kiutani.
"We acha tu," Jafari akajibu.
"Tafadhali nawaomba msinichukulie hatua mbaya..."
"Kaa kimya," Jafari akamkatisha.
Pius akatulia akiwa mwenye wasiwasi bado. Dylan alianza kumwonea huruma kwa kiasi fulani, lakini hakutaka hisia hizo zipite kiasi.
"Bila shaka ikiwa wewe ulihusika kwenye hili, basi najua kuna mkataba mfupi ulipewa, si ndiyo?" Jafari akamuuliza Pius.
"Ndiyo...unamaanisha wa kuafikiana na...kuagiziwa..."
"Ndiyo, namaanisha hivyo. Karatasi hizo unazo bado?"
"Aam...nilizificha kwenye..."
"Nitahitaji unipe," Jafari akamwambia.
"Lakini...haziko hapa...yaani..."
"Sijali ziko wapi. Unapaswa unipatie haraka sana...leo leo," Jafari akamwambia kwa uthabiti.
Pius akawa hana neno lingine la kipingamizi kabisa. Alijua kufikia hapa hakuwa na njia ya kutoroka tena kwa sababu mambo yalikuwa yamevurugika sana upande wake. Dylan akamgeukia Jafari.
"Contract ya nini unaongelea?" akamuuliza Jafari.
"Siyo kama mikataba ya kawaida inavyokuwa. Yaani kwa black market za huku, hasa kwa nature ya Bernard, najua atakuwa aliagiza kwa njia isiyo ya moja kwa moja...na ili imfikie huyu bila shaka kuna vitu vilifanywa vya kuthibitisha muamala huo. Ikiwa vilipita kwanza kwa Bernard, lazima tutapata disclosure ya physical description yake, au mfano wa mwandiko wake kwenye sahihi au kitu chochote alichoandika ambacho kitatusaidia kupata background info kuhusu uhusiano wake na ajali hiyo; ili ikihitajika kuthibitisha..."
"Uthibitisho tunakuwa nao," Dylan akamalizia.
"Yeah."
Dylan akamgeukia Pius na kusema, "Uko tayari kunisaidia?"
"Ndiyo. Nitafanya unachotaka," Pius akajibu.
"Kweli? Hata ijapokuwa nimekupiga ngumi usoni?" Dylan akatania.
Pius, akiwa kama mtu mzima, aliona aibu sana kutendewa namna hii na kijana ambaye kiumri alimwacha sana. Lakini kwa kuwa ilikuwa ni sehemu ya makosa yake, alijua malipo yangepaswa kuwa makubwa, hata kama angepelekwa jela. Hakuwa na njia ya kuepuka mkasa huu tena.
Dylan alimhimiza asiseme lolote kwa yeyote kwa kuwa angejiletea matatizo. Alimwahidi kwamba adhabu yake haingekuwa kubwa sana, hasa ikiwa angethibitisha kwa vyombo vya kisheria kuwa alilaghaiwa ili afanye mpango ule wa Mr. Bernard utimie. Jafari akamwambia kwa muda huu angepaswa kuacha kuwasiliana na Mr. Bernard mpaka wahakikishe wameweza kumdhibiti ipasavyo, kwa kuwa mipango yao ilikuwa imeanza kazi.
Pius alikubali, na alionyesha kweli anataka kurekebisha makosa yake kwa kumwambia Jafari angekwenda naye hiyo hiyo siku kufata kila kitu alichohitaji. Kwa hiyo Dylan akawaacha wawili hao waelekee huko, akiwa anajihisi vizuri kwamba mpango huo wa kumshawishi Pius ulifanikiwa, kisha yeye akaondoka na kuelekea kwa Grace.
★★★
Gilbert alipigiwa simu asubuhi moja na kuambiwa kwamba mwakilishi wa kampuni ambayo ilikuwa yake angekuja sehemu aliyoishi ili amletee ujumbe fulani muhimu. Aliuliza ilihusu nini, lakini akaambiwa asubiri tu mpaka mwakilishi huyo afike, naye angepata kujua ujumbe huo ulikuwa ni nini hasa. Akamwambia Jaquelin kuhusu hilo, ambaye pia hakuwa na wazo la ni nini ambacho watu hao walitaka kusema.
Walikaa nyumbani kusubiri mpaka ilipofika mida ya jioni saa 10, pale mwanaume fulani alipofika kwao, akiwa na mwonekano nadhifu wa suti. Gilbert wala Jaquelin hawakuwahi kumwona, kwa hiyo wakafikiri labda alikuwa mwajiriwa mpya kwenye kampuni. Lakini kihalisi, mtu huyu alikuwa mwakilishi wa kampuni ya Gilbert kwa niaba ya Grace, ambaye ndiye aliyekuwa amemtuma hapo. Wakamkaribisha ndani, lakini akasema hakuwa na muda mrefu sana wa kuweza kukaa, hivyo angewapatia taarifa aliyowaletea na kuondoka.
Mwanaume huyo akampa Gilbert faili fulani, kisha akamwambia, "Hongera Mr. Gilbert. Umekuwa raisi wa kampuni yako tena."
Gilbert na Jaquelin walibaki kushangaa sana. Wakatazamana kwa kuchanganywa na habari hizo za ghafla.
"Unamaanisha nini... imekuwaje... kivipi yaani?" Gilbert akauliza kwa kutoelewa.
"Nafasi yako kama raisi wa kampuni imerudishwa. Mambo utakayosoma humo yatakuelewesha kila kitu. Share zote za kampuni ziko chini yenu sasa; wewe na Mrs. Gilbert," mwanaume huyo akasema.
Jaquelin akatoa macho kwa kushangaa.
"Shares zote?!" akauliza.
"Ndiyo. Karibuni sana tena," mwanaume huyo akajibu.
Ilikuwa ni taarifa ambayo ingepaswa kuwafanya wafurahi sana, lakini ikawaacha wakiwa wamepigwa na butwaa. Mwakilishi huyo akawaambia watie sahihi karatasi fulani ya uthibitisho kuwa wameafiki jambo hili, nao wakasaini na kisha mwanaume huyo akawaaga na kuondoka zake. Wawili hao wakarudi ndani wakiwa wana maswali mengi vichwani mwao.
"Isije ikawa kwamba tunazungukwa tena Gilbert?" Jaquelin akasema.
"Sidhani Jacky. Tazama... kila kitu kiko in perfect order....yaani... we're in control of all shares... I can't believe this!" Gilbert akasema kwa hisia.
"Ni nani aliyefanya hivi? Una uhakika kweli..."
"Ndiyo, Jaquelin. Angalia...100% ya share zote ziko chini yetu sasa. Kampuni ilikuwa ikiperform vibaya... kuna mtu hapa anaitwa Smith Morgan amenunua zote, na corporate law imemsaidia kuhakikisha hakuna mtu yeyote anapinga jambo hilo. Kazihamishia kwetu... yaani ni kama..." Gilbert akaishia hivyo baada ya kuingiwa na wazo fulani.
Jaquelin akabaki kumwangalia kwa umakini, naye Gilbert akamgeukia na kumwangalia kwa njia iliyoonyesha alikuwa na jambo fulani kichwani kwake.
"Nini?" Jaquelin akamuuliza.
"Ni Dylan!" Gilbert akasema kwa uhakika.
Jaquelin akabaki kumtazama tu.
"Jaquelin, ni Dylan. Dylan ndiyo anafanya hivi... ahah..." Gilbert akaonyesha shauku.
"Unajuaje hilo?"
"Sijui lakini... think about it. Haiwezekani tu kampuni irudishwe kwetu kinagaubaga bila mtu anayeirudisha kwetu kuwa na nia fulani. Ni wazi kabisa kwamba Dylan amefanya hivi."
"Gilbert tutawezaje kuwa na uhakika kwamba ni yeye? Najua ingekuwa ni yeye angetuambia lakini hajajitokeza hata mara moja kwetu, unawezaje kuamini tu kwamba..."
"Sijaamini tu ovyo ovyo. Jaquelin, Dylan hajui kwamba sisi tunafahamu yuko hai. Ana... bila shaka amekuwa akifatilia maisha yetu... na sijui amewezaje kuzinunua hisa hizo zote lakini... anatusaidia bila kujulikana kwamba yuko hai. Jaquelin hiyo inamaanisha anafanya mpango fulani wa kumwondoa adui yake... na hii ndiyo njia ya kwanza..."
"Mr. Bernard," Jaquelin akasema kwa utambuzi.
"Ndiyo. Inaonekana anajua kuhusu Bernard ku-compromise helicopter, kwa hiyo Jaquelin, tunapaswa kumsaidia pia Dylan kwa kumhandle Bernard... kwa sababu sasa nguvu yetu imerudi," Gilbert akasema kwa uhakika.
"Ndiyo. Kwa hilo tuko pamoja. Mr. Bernard ni lazima aanguke," Jaquelin akasema kwa mkazo pia.
Wawili hawa wakaendelea kupitia masuala mbalimbali kwenye makaratasi ya faili waliloletewa, nao wakajiweka sawa kiakili ili waweze kurudi kwenye kampuni yao kwa kishindo.
Kutokana na furaha aliyokuwa nayo, Jaquelin akampigia rafiki yake, Beatrice, na kumwambia amerejea ngazi ya juu kwa mara nyingine tena. Beatrice alishangaa na kumuuliza alimaanisha nini, naye Jaquelin akamwambia angekuja kusikia tu matendo yake yeye mwenyewe wala asiwe na haraka. Ikabidi Beatrice amwambie angefika kwake kesho kumtembelea ndiyo angemsimulia vizuri, kwa kuwa alikuwa na muda hajamwona. Kwa mambo mengi, Jaquelin alipenda sana kujisifia, na sasa kurudishiwa kampuni yao lilikuwa ni jambo la kumfanya atambe; yaani wote waliomwonyesha dharau wangemtambua!
Gilbert alijipanga vyema kwa ajili ya kesho. Kwenye makaratasi aliyoletewa alipata kujua kuwa aliyenunua hisa za kampuni yao na kumrudishia nafasi yake alimtaka afanye kazi kwa njia yake anayojua ni bora ili kuirudisha kampuni kwenye mstari ulionyooka tena. Jina lilikuwa ni Smith Morgan, lakini Gilbert aliamini kabisa moyoni mwake kuwa ilikuwa ni Dylan. Alijua Dylan angetaka atoe jambo ambalo ni kikwazo kikubwa pale kwenye kampuni yao, kwa hiyo bila shaka angeanza na Mr. Bernard.
Kwa upande wa Mr. Bernard, ilikuwa ni wasiwasi tupu uliomjaa baada ya kuhangaika sana kumtafuta Pius bila mafanikio. Alijua mwanaume yule alikuwa akifatiliwa na mtu fulani na alikwenda kujificha kutokana na aliyemtafuta kumhoji kuhusu siri yao, lakini sasa kila alipomtafuta Pius kwa simu hakuweza kumpata. Ikambidi atume mtu wake mmoja (kama jambazi) ili aweze kumtafuta na akishampata amlete kwake; atake asitake.
Sasa Pius akaanza kusakwa na mtu huyo ambaye alikuwa ni mwanaume mwenye roho ya kikatili, aliyemfanyia Mr. Bernard mambo mengi mabaya kwa muda mrefu sana.
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
WhatsApp +255 787 604 893