junior nyahucho
Member
- Jun 17, 2022
- 17
- 12
uko vzr
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Gilbert yupo calm sana, anaishi na mwanamke asiye mvumilivu kabisa na asiyejali kuumiza hisia za mumewe.DYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA
★★★★★★★★★★★★★★★★
Grace akafumbua macho yake kwa kutotegemea jambo hilo, na hisia nyingi zikaanza kujengekea mwilini mwake; hisia ambazo kwa miaka mingi hakuwa amewahi kuwa nazo. Dylan akaibusu tena sehemu ya bega lake kwa wororo, naye Grace akashtuka kiasi baada ya kuhisi msisimko. Hakuwa amefikiria kwamba Dylan angeweza kufanya hivyo, na kwa sababu alikuwa mwanamke wa malengo tu, haingekuwa rahisi kwa yeyote kufanya kitu cha namna hiyo mwilini mwake na yeye amwachie tu; kwa sababu hakuwa hata na muda wa kuwazia jambo hili.
Lakini ni kama Dylan alimfanya ajihisi tofauti... udhaifu fulani hivi. Sikuzote Grace alikuwa mwanamke imara na thabiti, asiyependa michezo ya kitoto na yeyote kabisa. Lakini kwa huyu kijana ambaye alikuwa ametoka kumsimulia kuhusu maumivu yake, ilionekana kwamba alikuwa na aina fulani ya upendezi kumwelekea ambao ungempa ruhusa kijana huyu kufanya kitendo hicho.
Dylan naye hakujua kihalisi ikiwa jambo hili lingempendeza mwanamke huyo, lakini yeye sikuzote alifata moyo wake, na moyo wake wakati huu ulimwambia amwonyeshe Grace kwamba anapendwa. Akaanza kuubusu mgongo wa Grace hapa na pale kwa wororo sana, naye Grace akawa anasikilizia jinsi midomo ya Dylan ilivyompatia hisia zenye kusisimua. Kuna sehemu ya akili yake ilikuwa inataka kumwambia Dylan aache, lakini alilegea sana na kushindwa kujua kwa nini alikuwa tu hata amemwachia aifungue zipu; sembuse kuubusu mgongo wake!
Dylan akaanza kuishusha chini sehemu ya gauni iliyokuwa begani taratibu kuelekea chini kidogo kwenye mkono wake Grace. Grace alisisimka sana, naye akawa amekunja sura kwa hisia za kimahaba asijue la kufanya. Kusema kweli alikuwa akiogopa pia, kwa kuwa alifikiri wanaume wengi wangemtendea kwa njia ile ile kama yule aliyemnunua, hivyo hata kwa Dylan alihisi woga. Lakini njia ya Dylan ya kufanya mambo ilikuwa bila papara, na angalau jambo hili ni kama liliutuliza woga wake kwa kadiri fulani.
Dylan akaibusu sehemu ya bega lake Grace, kisha akaanza kupandisha taratibu kuelekea shingoni. Grace alifumba macho huku midomo yake ikitetemeka kwa mbali kutokana na hisia nyingi alizopata, naye Dylan akaendelea kuibusu shingo yake kwa upendo sana. Grace akageuka nyuma taratibu, na sasa midomo yao ikawa karibu sana huku wanatazamana kwa hisia. Hisia zilizokuwa zimempanda Grace zilimfanya awe na mzuka mwingi, naye akawa anapumua kwa kutetemeka sana.
"Its okay... its okay... I got you..." Dylan akamwambia kwa sauti yenye kubembeleza ili kumtuliza.
Grace akajitahidi kutuliza hisia zake za juu, naye Dylan akatabasamu kidogo na kuushika uso wake kwa kiganja chake. (.......).
(........).
(........).
(........).
(........).
Ijapokuwa kweli mgongo wa Grace uliwekewa makovu ya maisha, hii haikuwa sababu kwa Dylan kumwona hafai, na mpaka kufikia hatua hii alikuwa amemthibitishiahilo, na angeendelea kuthibitisha.
(........).
(........).
(........).
(........).
Dylan alijua alikuwa akishughulika na mwanamke ambaye alipitia maumivu ya kimwili zamani, na ambaye tokea wakati huo hakuwahi kujihusisha tena na mapenzi. Hivyo kwa njia fulani angepaswa kumtendea kama... bikra... ahakikishe anamrudishia hali ya kawaida ya kimahaba kwa uangalifu.
(........).
Grace alihisi maumivu, kama msichana kwa mara yake ya kwanza, na hii ilieleweka kwa kuwa hakuwahi kufanya tena mapenzi na mtu yeyote tokea alipotibiwa na Smith alipokuwa na miaka 16; hiyo ikimaanisha alikaa miaka 18 mpaka leo ndiyo akaweza kujiachia kwa Dylan kimapenzi. (.......).
(........).
(........).
(........).
Ilionekana wazi sasa kwamba Dylan alikuwa anamfurahisha mwanamke huyu. Dylan alifarijika sana kuona kwamba hatimaye Grace aliondoa hofu aliyohisi kwa miaka mingi kuelekea jambo hili, na sasa alichohisi kilikuwa ni raha badala yake. Dylan hakuvunja moyo hata kidogo kwenye kutoa mapenzi.
(.........).
(.........).
(.........).
Dylan pia alikuwa amezama kwenye raha nyingi aliyohisi kutoka kwa mwanamke huyu, hadi akawa amesahau mambo yenye kuvunja moyo aliyopitia siku hiyo. Hata alipohisi matambi yake yanakaribia kutoka, hakutaka kuacha kwa kuwa alihitaji raha hiyo iendelee tu. Kisha, baada ya kufikia mahala pazuri, Dylan alijiachia ndani kabisa kwa Grace.
Grace alipumua kwa uchovu sana, huku akiwa amelegea kitandani hapo. Dylan akamwangalia kwa sekunde kadhaa, akiona kuwa kweli mwanamke alikuwa ametua zigo zito la kipindi kirefu. Akambusu kwa wororo sana shavuni, na kuelekea mdomoni, huku Grace bado akiwa amefumba macho yake, kisha akambusu mdomoni na kuanza kuinyonya kwa upendo. Akaichomoa mashine yake taratibu kutoka kitoweoni mwa bibie na kumfanya agune kwa pumzi ya chini.
Ilikuwa ni kama wamechukua muda wa milele kumaliza safari ya mahaba yao, kwa sababu walipeana penzi kistaarabu na kihisia sana. Dylan aliona fahari kumsaidia Grace aondoe hofu yake, naye Grace hakuwa akiamini kama kweli aliweza kupita kwenye sehemu hiyo tena ambayo hakutaka kamwe kuipita. Alihisi usalama na imani kubwa kumwelekea Dylan.
Kutokana na mridhiko na uchovu aliohisi, Grace hakusema lolote ila kujilaza tu hapo kitandani akiwa amefumba macho. Dylan aliendelea kumbusu hapa na pale, huku akicheza na sehemu za mwili wake kwa kutumia vidole. Baada ya dakika chache, Dylan akatambua kuwa usingizi ulikuwa unamjia Grace, hivyo akasogeza shuka na kuufunika mwili wake. Grace akajigeuza kivivu upande mwingine ili aweze kusinzia vizuri, na kumwacha Dylan anautazama mgongo wake kwa huruma.
Kweli mwanaume huyo aliyemnunua kutoka kwa baba yake alikuwa amemfanyia mambo mengi mabaya sana ambayo hakuna msichana yeyote anastahili kufanyiwa. Alijua hata kama ingekuwa ni yeye, asingefikiria kuacha kulipiza kisasi, kama alivyotaka kumshauri Grace muda ule hajauona mgongo wake bado. Akajisogeza na kujiingiza ndani ya shuka, kisha akaukumbatia mwili wa Grace kwa nyuma na kulala miili yao ikiwa imegusana. Akaibusu shingo yake kwa nyuma, kisha naye akaanza kuutafuta usingizi pia.
★★★
Asubuhi ya saa mbili ilipofika siku iliyofuata, Grace akafumbua macho yake taratibu kutoka usingizini. Fikira za haraka zikaingia kwenye akili yake na kukumbuka jinsi alivyopeana mapenzi matamu na kijana Dylan usiku uliopita. Akaachia tabasamu la mbali na kugeukia upande wa pili wa kitanda, kukuta Dylan hayupo kitandani. Akajiuliza yuko wapi, na kwa haraka akakisia huenda Dylan alikuwa amekwishaamka na kuelekea kazini akimwacha yeye amelala.
Akajinyanyua kivivu na kuketi vizuri kitandani, akianza kujishika mwilini mwake huku akikumbukia kila mguso wa Dylan. Angetabasamu huku akiwa amefumba macho kwa kuvuta hisia nzuri alizopata jana kutoka kwa mwanaume huyo.
"Good morning sunshine."
Akatazama upande wa mlangoni baada ya kuisikia sauti hiyo. Ilikuwa ni Dylan, akiwa amesimama hapo huku ameshikilia sahani pana yenye vyakula mbalimbali na chai, huku anamwangalia Grace kwa tabasamu la furaha. Grace akatabasamu kwa mbali pia huku anamtazama Dylan kwa hisia. Kisha jamaa akaanza kuelekea hapo alipoketi bibie na kuiweka sahani hiyo kitandani katikati yao.
"Breakfast in bed... kama wazungu," Dylan akasema.
Grace akatabasamu na kusema, "Asante."
Hakufanya kitu chochote zaidi ya kuendelea kumwangalia tu Dylan, hivyo jamaa akachukua yai kidogo na kumwekea mdomoni ili ale. Grace alijihisi vizuri sana kwa kuwa Dylan alimtendea kwa njia yenye upendo. Akala, naye Dylan akaendelea kumlisha taratibu.
"Mbona wewe hauli?" Grace akamuuliza.
"Msosi wa jana usiku ulikuwa mtamu mno. Bado nimeshiba," Dylan akasema kichokozi.
Grace akatabasamu kwa haya kiasi na kutazama chini. Dylan akatabasamu pia, akifurahia jinsi ma-dimple yalivyochoreka kwenye mashavu ya Grace. Akaendelea kumlisha bibie mpaka aliposema kwamba inatosha, naye Dylan akamwambia ajitoe kitandani ili akajisafishe, kisha angemkuta kule chini. Grace akakubali, naye Dylan akabeba vitu alivyokuja navyo na kurudi navyo kule chini jikoni.
Grace akatoka kitandani na kuelekea bafuni ili ajisafishe. Baada ya kusafisha kinywa, akaingia 'shower' na kuanza kujimwagia maji. Wakati akiendelea kujiogesha, akahisi mikono ikimgusa kwenye mbavu zake na kumfanya ashtuke sana.
"Its okay... ni mimi."
Dylan akamtuliza kwa kumwambia hivyo. Grace akatulia kiasi, huku sasa akihisi jinsi mwili wa Dylan, ambao haukuwa na nguo, ukimgusa na kuubana wake kwa nyuma. Dylan akaanza (........).
(..........).
(..........).
(..........).
(..........).
Raha aliyopata Grace ilimfanya ajihisi ni kama hakuwa na matatizo kwa wakati huo, naye alitaka sana waendelee na mapenzi yao matamu licha ya mambo mengi waliyohitaji kushughulika nayo. Baada ya kutoka bafuni, walielekea kitandani na kuendeleza penzi lao murua; Grace akimwachia Dylan autawale mchezo wote na yeye aipate tu raha ambayo hakufikiria angewahi kuja kuifurahia namna hii.
Dakika kadhaa baadae wote walijiachia na kumwaga misisimko yao kwa pamoja, kisha wakajisafisha tena na kuanza kuvaa. Dylan aliwahi kutoka chumbani, akimwacha Grace anajiandaa, maana wanawake hutumia muda mrefu zaidi. Akashuka mpaka kule chini na kukaa kumsubiri Malkia wake mpya ashuke ili waweze kuondoka pamoja.
Grace alishuka kutoka juu ya ngazi taratibu baada ya dakika kadhaa, akiwa anaongea na Jafari kwenye simu. Alikuwa amevaa blauzi nyekundu ya kitambaa na suruali yake pana, na miguuni alivaa viatu vyeupe virefu, huku nywele zake akizitengeneza kwa mtindo wa kuzilaza mpaka kufikia mgongoni. Usoni alikuwa amependeza sana kwa kupaka lipstick nyekundu mdomoni na kuyaremba macho yake mazuri.
Baada ya kufika mwisho wa ngazi, akamalizia maongezi yake na Jafari, kisha akakata simu na kuangalia upande wa masofa sehemu ya sebule ile pana. Akamwona Dylan hapo akiwa ameketi huku anamwangalia kwa hisia. Jamaa akatabasamu kidogo kumwelekea, naye bibie akaachia tabasamu la upendo pia. Dylan akanyanyuka na kumfata Grace mpaka aliposimama.
"Umependeza mrembo," akamwambia.
"Asante," Grace akajibu huku anatabasamu.
"Ofisini?" Dylan akauliza.
"Yeah."
"Unajua... bado kuna mambo mengi tunahitaji kuzungumzia, siyo?"
"I know. Twende kazini, then we'll talk later. I'll tell you everything you wanna know (twende kazini kisha tutaongea baadae. Nitakueleza kila kitu unachotaka kujua)," Grace akamwambia.
Dylan akatikisa kichwa kukubali.
Kisha Grace akamwita Matilda ili kumwachia maelekezo fulani. Baada ya kumaliza, akakishika kiganja cha Dylan na kuvibana vidole vyao kwa pamoja, huku akimwangalia Dylan kwa upendo. Dylan akatabasamu, kisha wakatoka pamoja kuelekea nje ili wachukue gari na kuelekea kwenye kampuni.
★★★★★
"...bado tuko huku kwa nini? Kwa sababu tumekaa tu bila kufanya lolote!" Jaquelin akafoka kwa hasira.
"Jaquelin... kuna mambo mengine tunayoweza kukazia fikira na kujitahidi kuyakuza zaidi ili yatupe faida angalau kwa wakati huu," Gilbert akamwambia kwa upole.
"Mambo gani? Unataka tuendelee kutegemea restaurant hiyo ya kipumbavu wakati tuna kampuni kubwa ambayo WEWE umeipoteza? Huo haukuwa mpango wetu Gilbert... ulikuwa mpango wa Dylan. Kwa hiyo umeridhika kabisa sasa unajifanya kama maisha yako poa tu... wakati kila kitu umepoteza?!" Jaquelin akaendelea kulalamika.
Mambo hayakuwa yakienda shwari upande wa wazazi wake Dylan. Ilionekana kuwa sasa kampuni waliipoteza kabisa baada ya Mr. Bernard kutambuliwa kuwa raisi mpya wa kampuni hiyo miezi michache iliyopita. Hawakujua ni kwa nini mambo mengi waliyofanya ili kurudisha haki yao yalishindikana,lakini ni Mr. Bernard pamoja na MTU yule aliyeshirikiana naye ndiyo waliohusika kuhakikisha wanamkandamiza Gilbert ili apoteze kila kitu.
Mgahawa wa Dylan uliendeshwa vyema, lakini Jaquelin hakutosheka kabisa na mambo aliyoyaona kuwa madogo madogo sana waliyopata kutoka hapo. Alikuwa amepoteza uhusiano mzuri pamoja na marafiki zake wa zamani ambao walimtenga baada ya yeye kushuka kipesa; isipokuwa labda Beatrice, ambaye alimsaidia mara kwa mara vitu fulani na ushauri pia kama rafiki.
Gilbert alikuwa amewaza kuwa waendeleze biashara hiyo ya mgahawa, na kadiri ambavyo siku zingepita, wangetumia faida wanayopata kuukuza zaidi na hata kuifanya iwe hoteli kubwa. Alikuwa na matumaini sana kwamba jambo hili lingefanikiwa, lakini kwenye masikio ya Jaquelin ilikuwa ni kama kumpigia kelele zilizomuumiza. Ndiyo sababu iliyofanya mzozo huu kutokea wakati wako nyumbani.
"....kuna maisha mengine Jaquelin, usifikiri kwamba kuwa na pesa nyingi ndiyo kila kitu. Nilikwambia tupunguze gharama za matumizi ili tuishi maisha rahisi, lakini unang'ang'ania kuishi maisha kama hayo tuliyokuwa nayo. Hakukuwa hata na uhitaji wa kuwa na msaidizi wa kazi hapa, tungezifanya weny..."
"Unasema? Yaani nianze kujiumiza mimi mwenyewe kwa sababu tu wewe umefeli kurekebisha mambo? Hakuna kitu chochote kilichobaki tena, najua, lakini siwezi kuanza kuishi maisha ya kitumwa!"
"Hakuna kitu kingine kilichobaki? Jaquelin kwa nini unakosa shukrani?"
"Shukrani gani? Maisha gani haya umefanya tuanze kuishi? Miaka yote hiyo ya kazi ngumu kuijenga kampuni kuwa ilivyo leo eti imepotea ndani ya dakika mbili tu. Unafikiri Dylan angekuwepo angekuonaje?"
"Jaquelin funga mdomo wako."
"Ahah... ukweli unauma eeh? Umejitahidi sana kuweka mambo sawa hata aliporudi huku, lakini bado umeishia kuanguka..."
"Jaquelin nimesema funga mdomo wako! Usimwingize Dylan kwenye haya..."
"...bila shaka kama angekuwa hai angekuona kama baba yako tu... you are a failure! Umeshindwa kuongoza kampuni, baba yako kakugeuzia mgongo, familia ikavurugika kwa sababu ya..."
"Usiongelee masuala ya mimi kuku-cheat! Unajua wazi kwamba ni WEWE ndiye ulisababisha hilo! Usiigeuzie hatia yako mwenyewe kwangu, kwa sababu ijapokuwa unanidharau, bado sikukuacha... na hata kama nilifanya makosa, nilijitahidi kurekebisha hali lakini ni wewe ndiyo ukaendelea kuleta matatizo!"
Maneno hayo ya mwisho ya Gilbert aliyasema kwa hasira sana, naye Jaquelin akawa anamwangalia kwa hasira pia huku machozi yakimtoka. Walikuwa chumbani kwao wakiongea hivi kwa hisia zilizovurugika, naye Gilbert akatoka chumbani hapo kwa hasira na kushuka chini. Bado walikuwa wakiishi kwenye ile nyumba ya Dylan ambayo Gilbert alimrithisha, na mambo mengi hayakuwa yakienda vizuri tokea "kifo" cha mwanao.
Gilbert akaenda mpaka kwenye friji na kutoa maji kisha kunywa ili atulize hisia zake, huku msaidizi wao wa kazi akiwa hapo jikoni anaandaa chakula. Jaquelin akatoka chumbani ili amfate Gilbert waendelee kuongea, maana hakuwa amemalizana naye. Ni wakati alipofika sebuleni, pale mlango wa geti la nje uliposikika ukigongwa; kuonyesha kulikuwa na mtu nje aliyetaka kuja ndani.
Dada wa kazi akahakikisha kwamba mambo yako sawa ili aende kufungua, lakini Gilbert akamwambia angeenda kufungua yeye mwenyewe. Akampita Jaquelin bila kumwangalia wala kumsemesha na kwenda nje moja kwa moja. Jaquelin alimkata jicho la ukali sana, naye akaamua kutoka mlangoni aweze kuona ni nani alikuwa anagonga getini wakati huu kwa kuwa kulikuwa na giza nje na tayari ilikuwa imetimia saa 2 usiku. Gilbert alipoufungua mlango mdogo wa geti, aliachia tabasamu dogo kwa kuwa aliyesimama hapo alimfahamu.
"Fetty... hujambo?" akamwambia.
"Sijambo. Shikamoo?" Fetty akamsalimu.
"Marahaba. Karibu sana. Za huko kwenye harusi? Ndiyo umerudi leo?" Gilbert akasema.
Uso wa Fetty ulionyesha wasiwasi ambao ulimtaarifu Gilbert kwamba mambo hayakuwa sawa kwa binti huyo.
"Vipi Fetty? Kila kitu kiko sawa?" Gilbert akauliza.
"Yaani sijui nisemeje..." Fetty akajibu kwa kuonyesha wasiwasi.
Gilbert akaona amkaribishe ndani ili waweze kuongea vizuri. Fetty akamkuta Jaquelin akiwa amesimama mlangoni na kumsalimia, kisha wote wakaingia ndani. Walipofika usawa wa masofa, Gilbert akamwomba Fetty aketi, lakini binti akaendelea kusimama tu akionyesha hofu fulani usoni.
"Una tatizo gani? Mbona hukai?" Jaquelin akamuuliza.
"Kuna jambo fulani nahitaji kuwaambia... yaani sielewi imekuwaje..." Fetty akasema huku anafikicha viganja vyake kwa wasiwasi.
Gilbert na Jaquelin wakaangaliana, kisha wakamtazama tena Fetty.
"Ni jambo gani hilo?" Gilbert akauliza kwa upole.
Fetty akawa anataka kusema lakini anababaika tu.
"Ongea basi, una shida gani?" Jaquelin akamshurutisha.
"Nimemuona Dylan!" Fetty akasema.
Gilbert alibaki kumwangalia tu usoni asielewe anamaanisha nini. Jaquelin akakunja sura kimaswali huku pumzi zake zikianza kuongezeka kasi.
★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
★★★★★★★★★★★★★★★★
"Nimemuona Dylan jana." Fetty akarudia tena.
"Unamaanisha nini?" Jaquelin akauliza.
"Nimemuona sehemu fulani... alikuwa na mtu mwingine... yaani..."
"Wewe!" Jaquelin akamkatisha.
Fetty akamtazama kwa woga.
"Una kichaa eti?" Jaquelin akasema.
"Jacky..." Gilbert akataka kumzuia.
"Nini? Huyu binti ana matatizo gani? Umemuona Dylan wapi wakati unajua sehemu pekee aliyopo ni huko chini?" Jaquelin akasema kwa hisia.
"Hapana, nimemuona kweli! Nisingekuja hapa kuwaambia jambo kama hili... najua siyo utani huu. Lakini nina uhakika nimemuona... ninajua ilikuwa ni yeye..." Fetty akasema huku machozi yanamtoka.
Wazazi wote wa Dylan walishindwa kuelewa nini kilikuwa kinaendelea. Wakabaki kumtazama Fetty kwa kushangazwa na kile alichosema.
"F..Fetty una... una uhakika na unachokisema?" Gilbert akamuuliza.
Fetty akatikisa kichwa chake kukubali.
Jaquelin akaanza kutokwa na machozi huku anapumua kwa kasi. Hakuweza kuamini kama kweli jambo hili lilikuwa kweli.
"Umemwona wapi?" Gilbert akamuuliza.
"...nilikuwa na Patricia... rafiki yangu... tulienda kwenye bar fulani kubwa... tulipokuwa tumetoka kwenye sherehe... ni kama club... nikamuona hapo..." maneno ya Fetty yakatoka kwa kubabaika.
"Alikuwaje? Uliongea naye?"
"Si... sikuweza. Nilikuwa nashangaa kumwona... na yeye akaniangalia sana... lakini kuna mtu akamvuta mkono na wote wakaondoka. Nilipowafatilia nikaona... nikaona wanaingia kwenye gari halafu... wakaondoka... sijui walielekea wapi..."
Jaquelin akakaa kwenye sofa kwa kuishiwa nguvu. Gilbert akachuchumaa kumwelekea Jaquelin ili amwangalie kama yuko sawa. Alikuwa amechoka.
"Gilbert.... Dylan yuko hai! Yuko hai!" akasema Jaquelin kwa shauku yenye huzuni huku analia.
Gilbert akamkumbatia Jaquelin ili kumtuliza. Fetty alikuwa amesimama hapo pembeni akilia pia.
Baada ya Jaquelin kutulia kidogo, akamwomba Fetty awaeleze tena jinsi mambo yalivyokuwa, naye akafanya hivyo. Walitafakari sana ni nini ambacho kingekuwa kimetokea siku ile Dylan kapanda helicopter, lakini hawakuweza kupata jibu sahihi. Ndipo hapa Fetty akakumbuka kuhusu Mr. Bernard. Alimsikia akiongelea kuhusu mpango fulani wa kumwangusha Gilbert, na ungefanyika muda ule ule ambao Dylan alitakiwa kupanda helicopter. Gilbert na Jaquelin wote walishangaa kujua ukweli huu ambao Fetty hakuweza kuwaambia kutokana na majanga mengi yaliyotokea.
"Mshenzi mkubwa yule! Bila shaka ni yeye ndiye amesababisha mambo yote yale kutokea!" Jaquelin akasema kwa hasira.
"Kwa hiyo alisema mwisho wangu umekaribia... ndiyo maana akajaribu kumuua mwanangu!" Gilbert akasema kwa hisia za huzuni sana.
"Kwa nini hukutuambia mapema?" Jaquelin akamfokea Fetty.
"Sikuwa naelewa... nilitaka kumwambia Dylan lakini akawahi..."
"Usijali Fetty... Jaquelin... mtoto hana makosa... mambo mengi yalituvunja sisi sote..." Gilbert akasema.
"Ndiyo! Na ni kwa sababu ya huyo mpumbavu! Ngoja nimfate..."
Jaquelin akanyanyuka ili aondoke, lakini Gilbert akamwahi na kumzuia kwa kuushika mwili wake.
"Jacky.. Jacky... nisikilize..."
"Gilbert niachie... nimesema niache!"
"Tulia!" Gilbert akamfokea kwa sauti kubwa mno.
Jaquelin akatulia na kumwangalia usoni.
"Unataka kufanya nini? Uende ili na wewe akuue?" Gilbert akamuuliza.
"Ikiwa ataniua ni sawa tu... si ndo' mpango wake? Amuue Dylan... basi na mimi..."
"Hiyo siyo akili Jaquelin!" Gilbert akamkatisha.
Jaquelin akatulia.
"Tumetoka tu kujua mtoto wetu yuko hai... kitu cha kwanza kabisa cha kutanguliza inapaswa kuwa yeye," Gilbert akasema kwa hisia.
Jaquelin akaanza kulia kwa uchungu sana. Gilbert akaushika uso wake kwa upendo ili watazamane.
"Jaquelin... unahitaji kuwa strong kama jinsi navyokufahamu ili tuweze kumshinda adui yetu. Ni wazi kabisa kwamba kila kitu kilichotupata haikuwa coincidence... ilipangwa. Kwa hiyo tunahitaji kufanya kila jambo kwa akili sana... kwa sababu hawa watu ni wakatili, wanaweza kufanya lolote lile kutimiza haja zao. Hatupaswi kuhatarisha usalama wetu na... na usalama wa Dylan kwa mara nyingine tena..." Gilbert akamweleza kwa upole.
Jaquelin akaishika mikono ya Gilbert usoni mwake huku akimwangalia kwa hisia.
"...kwa hiyo tufanye nini?" akamuuliza mume wake.
Gilbert akamwangalia Fetty, ambaye alikuwa akiwatazama kwa simanzi wazazi hao wa Dylan, kisha akamwangalia Jaquelin tena.
"Tumtafute mwana wetu," Gilbert akamwambia kwa uhakika.
Jaquelin akatikisa kichwa kukubali, naye Gilbert akamkumbatia kwa ajili ya faraja.
Wenzi hawa hawakujua kilichofanya Dylan asirudi nyumbani au kuwatafuta mpaka wakati huu, lakini walikuwa na matumaini hakika moyoni kwamba wangeungana na mwanao tena ili waweze kujipanga kupambana na maadui zao.
★★★
Grace akawa ameketi pamoja na Dylan kitandani chumbani kwake, akimwambia kuhusu kila jambo alilohitaji kujua kuhusu mipango yake ya kisasi. Dylan alimsikiliza kwa makini na kupata kutambua ukweli muhimu ambao hakujua wala kukumbuka.
"Dylan ndiyo jina langu?" akauliza.
"Ndiyo. Jina lako halisi ni Dylan Gilbert," Grace akajibu.
"Kwa hiyo... muda wote huu ulikuwa unafahamu mimi ni nani... kwa nini hukuniambia?"
Grace akawa kimya tu akimwangalia Dylan kwa hisia.
"Grace nieleze. Nahitaji kujua ninahusika vipi kwenye mpango ulio nao mpaka ukaamua kunifichia jambo hili," Dylan akamsihi kwa upole.
"Well... ukweli ni kwamba... haukuwa sehemu ya mipango yangu mpaka miezi michache iliyopita. Kitu kilichosababisha upoteze kumbukumbu ni kwamba... ulipata ajali ya helicopter. Inaonekana ulianguka na kuumia mpaka kupoteza kumbukumbu yako, lakini watu waliokufahamu walifikiri umekufa. Ijapokuwa wengi waliiona kuwa accident, mimi nilifanya uchunguzi zaidi na kutambua kwamba haikuwa accident..." Grace akaeleza.
Dylan alikuwa ameshangazwa na ufunuo huu. Maswali yaliyopita kichwani kwake yalikuwa mengi mpaka akashindwa kujua aulize lipi aache lipi. Ni hapa ndipo Grace akachukua simu yake na kuanza kutafuta picha fulani. Dylan alikuwa anamwangalia kwa makini sana, naye Grace alipopata picha aliyoitaka, akampa Dylan simu aitazame.
Dylan alipoiangalia, aliona mwanaume fulani mwenye umri mkubwa akiwa amevaa suti na akitoa tabasamu kubwa. Lakini aliutazama sana uso wake, na hii ilikuwa ni kwa sababu alihisi kama anamfahamu.
"Looks familiar... doesn't he?" Grace akasema.
Dylan akauliza, "Ni nani huyu?"
"Huyo ndiyo yule mwanaume aliyenitendea kwa ukatili kipindi kile. Anaitwa Yakobo Bernard Sizwe. Wengi humfahamu kama Mr. Bernard," Grace akajibu.
"Mr....Bernard?" Dylan akauliza, akiwa kama analifahamu jina hilo.
"Yeah. Mnafahamiana. Amefanya kazi kama investor mkubwa kwenye kampuni ambayo ilikuwa ya baba yako, na sasa ameikwapua kutoka kwa baba yako na kuifanya iwe yake kwa sababu ya tamaa yake kutaka kuwa in control. Nimemfatilia kwa kitambo sasa, na ninajua hangeweza kufanya jambo hilo yeye mwenyewe; kuna mtu anamsaidia," Grace akaeleza.
Dylan alichanganyikiwa. Mambo ambayo Grace alikuwa akimtaarifu yalikuwa mengi mno kuweza kuyameza yote akilini kwa wakati mmoja.
"Anajihusisha na mambo mengi illegal: madawa ya kulevya, magendo, human trafficking, na ulaghai wa hali ya juu ambao umesababishia wengi matatizo. Kwa miezi michache iliyopita nilijitahidi kufichua maovu yake, kwa njia isiyo ya moja kwa moja, lakini kuna mtu fulani yuko nyuma yake ambaye anahakikisha Mr. Bernard hafikiwi na udhuru anaostahili. Nikiweza tu kujua mtu huyu ni nani, basi nita-attack haraka iwezekanavyo," akasema Grace.
Dylan akakaa kimya kwa sekunde chache, kisha akamuuliza, "Ulijuaje kwamba... kilichonipata hakikuwa accident?"
"Kama nilivyokwambia, nimekuwa nikimfatilia mwanaume huyo tokea Smith alipokufa. Mwanzoni, sikujua jinsi ya kutafuta vigezo vya kunisaidia ili nimwangushe, hivyo nikaamua ku-hire private investigator... jina lake ni Jafari. Alinisaidia kujua kuhusiana na operation za huyo mtu zilizofanywa kwa usiri wa hali ya juu, na mara kwa mara alikuwa anabadilisha njia zake za kufanya mambo yake mengi mabaya. Hivyo nikaamua kuweka focus kwenye kampuni yenu pia, na hasa kwa sababu ilikuwa inafanya kazi kama ya kwangu tu. Jafari alikuja kunipatia info baadae kuwa Mr. Bernard alikuwa anapanga kumwangusha Gilbert, baba yako, lakini hakujua ni jinsi gani angefanya hivyo."
Dylan akaendelea kumsikiliza.
"Nilikuja kutazama taarifa ya habari baada ya helicopter uliyopanda kuanguka, na hapo nikawa nimetambua huo ulikuwa ni sehemu ya mpango wake, kwa sababu inaonekana alihofia uwepo wako pale ulikuwa unairudisha nyuma mipango yake. Kwa hiyo nikamwamuru Jafari afatilie zaidi kuhusiana na kisa cha helicopter hiyo, na baadae akaja kuniambia kuwa inaonekana kuna tatizo lilitokea mkiwa huko huko juu. Jafari alipata taarifa baadae kuhusu parachute iliyoangukia maeneo fulani, kwa hiyo akaenda kuchunguza huko. Alikuja kupata wallet yako ambayo nafikiri ilidondokea sehemu fulani wakati unaanguka, na baada ya kuniletea, tukaanza kufatilia zaidi ikiwa uli-survive. Ndiyo miezi michache baadae Jafari akanitaarifu kuhusu habari zako za kujenga lile daraja, na alipokufatilia akatambua ilikuwa ni wewe, yaani Dylan."
Dylan akatulia kidogo, kisha akauliza, "Kwa hiyo kumbe ulipo...nitafuta, haukuwa na lengo la kunisaidia tu kimaisha... ila ulinifata kwa lengo la kunifanya niwe sehemu ya mipango yako?"
"I'm sorry Dylan... najua hii yote inakuumiza. Lakini kutoka ndani ya moyo wangu, nilitaka kukusaidia na kukulinda ili uwe salama; maana kama wale watu wangejua ulikuwa hai, wangekutafuta kukumaliza. Nilikuwa ninafahamu mambo kadhaa kukuhusu... na mengi yalikuwa kuhusu jinsi ulivyo mwerevu na jasiri. Kwa hiyo nilitaka kukufunulia kila jambo polepole ili uwe upande wangu... kwa pamoja tuweze kumwangusha huyo mpumbavu," Grace akajieleza.
Dylan akashusha pumzi na kusema, "Usijali, Grace. Kiukweli, haya yote yamenichanganya sana.... I feel so... lost. Lakini ijapokuwa bado sikumbuki mambo mengi, angalau sasa siko gizani. Kwa hiyo... mpaka sasa... wazazi wangu.... na kila mtu anayenifahamu huko... wanafikiri nimekufa, siyo?"
Grace akatikisa kichwa taratibu kukubali.
Dylan akatikisa kichwa kwa kusikitika sana, naye akanyanyuka na kuelekea upande wa dirishani na kutazama nje. Grace alikuwa anamwangalia kwa hisia za huruma, kwa kuwa alielewa mambo mengi yalimchanganya mpenzi wake huyo mpya. Yeye pia akanyanyuka na kumsogelea Dylan karibu akiwa nyuma yake, kisha akamshika begani kwa kujali.
"Mr. Bernard..." Dylan akasema kwa sauti yenye mkazo.
Grace akawa anamwangalia kwa kujali.
"Tamaa... tamaa ni kitu kibaya sana. Ni watu kama yeye ndiyo wanaosababisha maisha ya wengine yaharibike bila haki. Anaua... analaghai... anawatendea watu kama wanyama... halafu anafurahia maisha mazuri...."
Dylan aliyasema hayo yote kwa hisia nzito sana. Kisha akamgeukia Grace na kumwangalia machoni.
"I'm in!" akasema kwa hisia kali sana.
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
WhatsApp +255 787 604 893
wanawake wengi ndivyo alivyo wengi waoGilbert yupo calm sana, anaishi na mwanamke asiye mvumilivu kabisa na asiyejali kuumiza hisia za mumewe.
Hongera sana mtunzi kwa simulizi kali
Aisee, sio mchezo. Beatrice miyeyusho sana, sema nae Jaquline misifa inamponzaDYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI
★★★★★★★★★★★★★★
Moja kwa moja mpaka kwenye chumba kikuu cha mikutano cha kampuni ya Gilbert, ambayo sasa ilikuwa ndani ya mikono ya Grace, washiriki wote wakuu wa bodi ya kampuni, kutia ndani Mr. Bernard akiwa kama raisi, walikuwa humo wakijadili suala fulani ambalo liliwafanya wote washangae. Taarifa ilikuwa imeletwa na wawakilishi wa Grace (wenyewe walifikiri wawakilishi ni wa Smith Morgan), kwamba amebadilisha mfumo wa uongozi na kumpa mtu mwingine ndiyo awe raisi wa kampuni sasa.
Mr. Bernard alitaharuki sana kwa kuwa alishtushwa na habari hizi, naye akawa akiwaambia wawakilishi hao kuwa angehitaji kuonana ana kwa ana na "Smith" ili wazungumze kwa kuwa jambo hilo kwake halikukubalika hata kidogo. Wawakilishi wale walimwambia hakuna chochote angefanya ambacho kingebadili uamuzi wa mkubwa wao, hivyo angepaswa kutulia kwa sababu sasa kampuni ilikuwa ni yake (yaani Grace). Wote walikuwa humo wakisubiria raisi mpya afike, kwa hiyo Mr. Bernard akakaa kusubiri pia kwa shingo upande.
Baada ya dakika chache, Gilbert pamoja na Jaquelin waliingia kwenye chumba hicho cha mikutano wakionekana kuwa makini na tayari kikazi. Wengi walishangaa na kusimama kuwatazama, huku Mr. Bernard akiwa amekunja sura kwa mshangao asiamini kuwaona hapo. Baadhi ya washiriki waliokuwa na mioyo minyoofu kuwaelekea wawili hao walifurahi sana kuwaona na kuwakaribisha kwa shauku, huku wanafiki wakibaki kukunja sura tu. Mr. Bernard akatoa tabasamu bandia huku akiwa na wasiwasi, naye akasogea karibu na walipokuwa wamesimama.
"Jaquelin....Gilbert... karibuni sana...ni muda umepita," Mr. Bernard akajifaraghua.
Gilbert na Jaquelin wakamwangalia kwa mkazo sana.
"Aam...sikujua kama militakiwa kuwepo kwenye huu mkutano," Mr. Bernard akasema.
"Everyone, huyu ndiyo raisi mpya wa kampuni, Mr. Gilbert Mushi," mwakilishi mmoja akasema.
Mr. Bernard alitoa macho kwa kushangaa mno! Washiriki wengine walifurahi na kuanza kumpigia makofi ya hongera Gilbert pamoja na mke wake, ambao walionyesha shukrani pia. Wawakilishi wale wa Grace wakaongea kifupi na Gilbert, kisha wakawaaga wote na kuondoka. Gilbert akamwangalia Mr. Bernard kwa mkazo, kisha akampita na kwenda mpaka kwenye kiti cha mbele zaidi cha kiongozi na kuketi. Jaquelin pia akampita Mr. Bernard huku anamwangalia kwa dharau, na kufanya jamaa ahisi hapa kuna mchezo lazima umefanywa. Lakini yote kwa yote, akajirekebisha kwa kuliweka koti lake sawa na kwenda kuketi pia.
Gilbert aliongea na washiriki wa bodi ya kampuni kuhusiana na matatizo yaliyoipata kampuni, na kuwafanya watambue kwamba bila shaka Mr. Bernard hakuwa akifanya kazi kama alivyotakiwa. Jamaa alijitetea sana na kuwaomba wapambe wake wampe kichwa, lakini ni kama wengi wao walihofia kutoa support kwake tena kutokana na ukweli wa mambo ambayo Gilbert aliwaambia. Mwishowe, Gilbert akaanza kuwataarifu watu hao kuhusu mipango mingi ambayo "Smith" alikuwa amempa ili kusaidia kuirudisha kampuni juu tena. Mawazo hayo yangeanza kufanyiwa kazi haraka sana ili matokeo mazuri yaweze kuja mapema pia.
"Pia, kuna jambo la mwisho la muhimu nalotaka kusema," akasema Gilbert.
Wote wakakaa tayari kumsikiliza raisi wao alitaka kusema nini.
"Mr. Bernard..." Gilbert akaita.
"Ndiyo..." jamaa akaitika kwa shauku.
"Kaisafishe ofisi yako," Gilbert akamwambia.
Wengi walibaki kumtazama Mr. Bernard kimaswali, wakiwa wameelewa kuwa Gilbert alikuwa anamfuta kutoka kwenye kampuni yao. Mr. Bernard alichanganyikiwa na kuanza kuuliza sababu ni nini ya Gilbert kufanya hivyo, na kwa kejeli Gilbert akasema ni kwa sababu tu amependa. Akamwambia kama aliona shida kubeba vitu vyake na kuondoka, basi angeita walinzi ili waje kumtoa yeye pamoja na vitu vyake. Hakuwa na ujanja tena. Akanyanyuka na kuondoka akiwa anahisi aibu kubwa sana.
Wakati akitoka alikuwa anatazamwa mno na wafanyakazi wa hapo, ambao hawakupenda uongozi wake tokea alipowekwa kuwa raisi wa kampuni miezi michache iliyopita. Akaenda mpaka kwenye gari lake na kuingia akiwa na hasira, kisha akampigia yule mtu aliyesaidiana naye ili kumwangusha Gilbert. Akamweleza kuhusu kilichotokea na kusema alishindwa kuelewa iliwezekanaje mpaka wawili wale wakaweza kurudi namna hiyo, kwa kuwa aliwawekea vikwazo vingi sana ili wasifanikiwe.
Mtu huyo alikasirika sana na kusema haiwezekani, ni lazima angejua nini kinaendelea na kama kuna mtu amewasaidia basi yeye angeshughulika naye. Baada ya kukata simu, Mr. Bernard akaondoka akiwa ameudhika na kujiahidi kutoacha mpaka ahakikishe Gilbert anaanguka kwa mara nyingine tena.
★★★
Mambo yalikwenda vizuri kwa wazazi wa Dylan siku yao ya kwanza kurudi tena kwenye kampuni yao. Wafanyakazi wengi walifurahi kuona wamerejea, naye Gilbert aliwaahidi mambo yangekwenda vizuri zaidi wakati huu. Aliongea na wengi wao kuweza kujua kuhusu uzoefu, furaha, hofu na kero zao, ili ajipange kuwasaidia kwa njia nzuri na kuwafanya wafurahie kuendelea kufanya kazi hapo.
Jaquelin alikutana na rafiki yake Beatrice baadae. Kihalisi walitakiwa kuonana nyumbani kwake, lakini mambo yakabadilika hivyo wakaamua kukutana kwenye mgahawa mkubwa wa kisasa. Lilikuwa ni wazo la Jaquelin kwa sababu sasa alikuwa amerudi kwenye mahali alipoona alistahili kuwa...kwenye pesa. Akamsimulia rafiki yake kuhusu jinsi walivyorudi kwenye kampuni yao kwa kishindo na kumfukuza Mr. Bernard bila kukawia. Beatrice alikuwa anashangaa bado kuhusu mambo haya.
"Mmewezaje...yaani best mmenishangaza sana!" Beatrice akasema.
"Unashangaa nini nawe? Ndiyo sisi. Walisema ooh wamepotea, mara ooo hawatarudi...yako wapi? Alaah..." Jaquelin akajisifia.
"Ahahahah...ama kweli malipo hapa hapa duniani," Beatrice akasema.
"Ndiyo maana yake. Yaani tena huyo Bernard nilikuwa natamani kumpiga kofi la usoni kwa alichokifanya! Ana bahati tu kwamba..." Jaquelin akaishia hivyo.
"Ana bahati kwamba?" Beatrice akauliza.
"Aagh... achana naye," Jaquelin akasema.
"Unajua...huwa unasema tu jinsi unavyomchukia huyo...Mr. Bernard, lakini hujawahi kuniambia ni kwa nini. Na...wakati huu...kwa nini mmemfukuza namna hiyo?" Beatrice akauliza.
"We acha tu Tris. Mambo ni mengi sana."
"Mh...unanifanya nijali hata zaidi sasa. Niambie ni nini kinaendelea maana jamaa inaonekana aliwachokonoa pabaya."
"Siyo kutuchokonoa..yaani yule mshenzi ameyafanya maisha yetu yawe magumu...ni yeye ndiye aliyefanya mpaka hayo mambo yote yakatupata."
"Wewee...kumbe?" Beatrice akashangaa.
"Ndiyo. Tulipoteza kila kitu kwa sababu yake, na ni yeye ndiye alifanya mpango ili ile helicopter imwangushe Dylan!"
"Eh!" Beatrice akashangaa zaidi.
"Yaani wakati mwingine sipendi hata kulisikia jina lake huyo kinyago," Jaquelin akasema kwa hisia kali.
"Kwa nini sasa afanye vile huyo baba? Halafu kipindi kile nilipokutanaga naye pamoja na Alfred alionekana mstaarabuu...kumbe ndo'...."
"Mstaarabu? Heh...yaani yule ni nyoka. Na hapo bado...tutahakikisha anapoteza kila kitu kama alivyotaka kutufanyia mpuuzi yule," Jaquelin akasema.
"Aisee! Kwa hiyo sasa...mmewaambia polisi kuhusu alichofanya?"
"Hatujafanya hivyo."
"Kwa nini sasa? Mnatakiwa muwaambie mapolisi ili wamkamate kwa sababu alifanya kosa la mauaji!"
"Najua. Lakini mapolisi na wenyewe washamba tu. Sisi wenyewe tutadili naye...kwa sababu sasa hivi nguvu yangu imerudi," Jaquelin akasema kwa uhakika.
"Unamaanisha kuirudisha kampuni? Hicho tu ndiyo kitakufanya umlipizie kisasi? Je ukitoka hapa sasa hivi ukashtukia tu gari lako linalipuliwa?"
"Wewee hana ubavu huo. Na hata alipojaribu kumuua mwanangu hakufanikiwa."
"Nini?" Beatrice akashangaa.
Jaquelin akatazama pembeni kwa njia ya kuudhika.
"Best unamaanisha nini? Sote tunajua kwamba Dylan ame..."
"Hajafa!" Jaquelin akamkatisha.
Beatrice akabaki kumtazama kwa kuchanganyikiwa.
"Ahah...Jaquelin... samahani lakini...najua kifo cha Dylan kilikuumiza sana na ulipitia wakati mgumu ila...mimi ni rafiki yako...lazima nikwambie ukweli na uukubali. Dylan hatuko naye tena Jaquelin," Beatrice akamwambia kwa hisia.
"No. Dylan yuko hai. Unafikiri ni nani aliyetusaidia mpaka tukaipata kampuni tena?" Jaquelin akasema kwa uhakika.
"What...yaani...Dylan ndiyo amewasaidia mkaipata kampuni tena?"
"Ndiyo maana yake."
"Jaquelin...umeweka nini kwenye kinywaji chako?"
Jaquelin akazungusha macho yake. Ni wazi Beatrice alishindwa kuelewa nini kinaendelea.
"Rafiki yangu usi..."
"Tris nisikilize. Dylan hakufa. Sijui ilikuwaje lakini alisalimika kwenye ile ajali. Tumekuja kujua yuko hai wiki iliyopita, na sasa bila shaka ametusaidia ili mambo yakae sawa tena kwetu. Sijajua anapanga nini, lakini anaonekana kuwa makini kwa sababu hataki mtu ajue kwamba yuko hai...na ndiyo maana sisi pia hatusemi kwa yeyote kuhusu hilo," Jaquelin akaeleza.
Beatrice alimwangalia kimaswali sana, naye akatikisa kichwa chake taratibu kuonyesha kwamba jambo hilo lilimshangaza sana.
"Mh! Makubwa jamani. Kwa hiyo Dylan wangu yuko hai! Masikini..." Beatrice akasema kwa hisia.
"Mwanangu atarudi tu. Na akifika wote watamtambua. Hizi ni cheche tu najua anakuja na moto," Jaquelin akasema kwa ujasiri.
"Umeshamwona?" Beatrice akauliza.
"Hapana. Ametulia huko aliko bila shaka anaunda mipango yake kwa umakini zaidi."
"Lakini unawezaje kuwa na uhakika kwamba ni yeye? Je kama kuna mtu anawafanyia mchezo...halafu mnaingia mtegoni," Beatrice akasema kwa kujali.
"Beatrice usijali. Mambo mengi hayaeleweki kirahisi najua...lakini wewe tulia tu utaona. Dylan atawashusha WOTE wanaojaribu kumzingua...hawamjui mwanangu vizuri," Jaquelin akasema kwa uhakika sana.
Beatrice akabaki anamtazama rafiki yake kama vile ni mtu aliyerukwa na akili, lakini uhakika wa Jaquelin ulikuwa wa hali ya juu sana kupuuzia jambo hilo zito. Simu ya Beatrice ikaita, naye akapokea huku Jaquelin akiendelea kunywa juice yake. Beatrice akamaliza kuongea na simu na kurudisha umakini wake kwa Jaquelin tena.
"Boyfriend eeh?" Jaquelin akauliza.
"Mm hamna...hahahah...ni Harleen," akasema.
"Eee afu' kweli, Harleen ni muda sasa sijamwona. Anaendeleaje?"
"Mh...we acha tu. Walikorofishana na mchumba wake huko sijui wakaachana ghafla."
"Wewe! Kisa?"
"Aagh yaani me hata sikuwaelewa kwa kweli. Harleen anaingiaga kwenye mahusiano, lakini baada ya muda mfupi tu...wameachana. Nishamzoea."
"Lakini ni mtoto wako, unatakiwa kumwongoza mara nyingine hata kama amekua."
"Siyo mtoto huyo, anaweza kufanya maamuzi yake mwenyewe. Na kwanza huyo mwanaume hata sikumpenda ni basi tu Harleen anapenda kulazimisha mambo."
Jaquelin akacheka.
"Tena unajua nini...nafikiri Harleen atafurahi sana kama atajua Dylan ni mzima, maana..."
"No Beatrice, hapana. Usimwambie yeyote kuhusu Dylan. Ninakuamini wewe tu, usiseme kwa yeyote yule please," Jaquelin akamsihi.
"Okay sawa usijali, my lips are sealed. Ila maisha yenu yalivyo best kama movie vile..."
Jaquelin akacheka na kuendelea kupiga story na rafiki yake kipenzi. Baada ya muda fulani kupita, waliagana na wote kuelekea makwao baada ya kufurahia kiburudisho hicho cha urafiki pamoja.
★★★
Mr. Bernard alipigiwa simu usiku na yule jamaa aliyemtuma kumtafuta Pius, ambaye alimwambia alifanikiwa kumpata na kumfanya apoteze fahamu kwa kumnusisha madawa kwenye kitambaa. Kwa hiyo, alimweka kwenye gari lake na kumleta upande huu wa jiji; kwenye jumba la kutunzia nafaka ambalo halikuwa likitumiwa kwa muda mrefu. Hivyo, Mr. Bernard akamwambia amsubirie hapo na amchunge ili afike na kuzungumza naye. Mambo mengi yalikuwa yameanza kwenda vibaya kwa Mr. Bernard, kwa hiyo alitaka kujua kisa cha Pius kumkwepa kilikuwa ni kwa sababu gani.
Dakika chache baadae, Mr. Bernard akawa amefika sehemu ile na kuegesha gari lake nje. Akaingia ndani ya jumba hilo, lililokuwa tupu na lenye giza kiasi, huku kwa mbele chemli ikionekana kumulika sehemu ndogo ya humo ndani. Akasogea mpaka sehemu hiyo na kufika usawa wa ukingo wa ukuta na kukata kona. Ni hapo ndiyo akawa amefika kwenye chumba ambacho hakikuwa na mlango, na ndani palimulikwa na taa kutokea juu, hivyo aliweza kumwona Pius akiwa amelazwa chini akionekana kusinzia. Akaingia na kumkuta yule mwanaume na kumpongeza kwa kazi nzuri, kisha akamwambia amwamshe. Jamaa akaenda kujaribu kumwamsha Pius kwa kumpiga makofi, ambaye alianza kurejewa na fahamu polepole.
Pius alikurupuka baada ya kumwona Mr. Bernard akiwa hapo. Akasimama na kurudi nyuma kidogo, akishangaa alifikaje sehemu hii.
"Unaweza kunieleza ni nini maana ya wewe ku-dodge simu zangu?" Mr. Bernard akamuuliza kwa mkazo.
"Sija-dodge simu zako. Ni kwamba tu...nilikuwa nimejificha..."
"Kwa hiyo?"
"...nilifikiri ingekuwa busara kuwa makini..nisipokee maana...huwezi jua..mtu fulani angeweza ku-tap simu yangu," Pius akatoa kisingizio.
Mr. Bernard akatabasamu na kumsogelea karibu zaidi.
"Unaniona mimi kama mjinga mwenzako, si ndiyo?" akamuuliza.
"Hapana. Kwa nini useme hivyo? Mimi naku...nakuheshimu siwezi kukudanganya..." Pius akasema.
"Ahahahah... Kwa hiyo bado unaniona mimi mtoto mdogo sivyo?" Mr. Bernard akauliza.
Pius akabaki kumtazama tu.
"Pius...tusitaniane. Ninataka uniambie ukweli...nini kinaendelea?"
"Hakuna chochote..wala mimi sikutanii..siwezi..."
"Kimya! Niambie ukweli sasa hivi la sivyo..."
Mr. Bernard akafoka kwa hasira na kulishika shati la Pius kwenye kola huku akimvuta. Pius alijawa na hasira pia, naye akaitoa mikono ya Mr. Bernard kwa nguvu kutoka kwake. Mr. Bernard akashangaa.
"Unataka kujua ukweli? Sawa. Ukweli ni kwamba sitaki tena kujihusisha nawe kwa lolote. Ninajuta kukubali unitumie kwenye jambo lile la kikatili...sitaki tena!" Pius akasema kwa hisia kali.
"Hutaki nini? Una matatizo? Siyo wewe uliyenipigia simu ukasema unafatiliwa na unahitaji kujificha? Mnyoo gani amekuingia kichwani mpaka unanipandishia sauti namna hiyo? Umenisahau eeh?" Mr. Bernard akafoka.
"Sikuogopi. Wewe fanya mambo yako na mimi uniache kwa amani. Nimeshasema sitaki tena kujihusisha nawe...kama kufatiliwa sasa hivi sifatiliwi kwa hiyo sihitaji msaada wako," Pius akasema.
"Nini?" Mr. Bernard akauliza kimshangao.
Pius akampita Mr. Bernard akitaka kuondoka lakini yule mwanaume akamzuia kwa kusimama mbele yake. Mr. Bernard akamgeukia Pius na kumwangalia akiwa anahisi hasira sana.
"Mwacheni aende."
Wote walisikia sauti hii ikitokea sehemu ya kuingilia ndani ya chumba hicho. Wakageuka na kutazama ni nani aliyesema hivyo kwa utulivu mno, na hapo Mr. Bernard akatambua kwamba ilikuwa ni yule mtu muhimu aliyesaidiana naye kufanya mpango wa kumwangusha Gilbert. Alikunja uso kimaswali, akishangaa mtu huyo aliwezaje kujua walikuwa hapo. Akaingia ndani ya chumba hicho na kufika usawa wa mwanaume yule aliyemzibia njia Pius, na hapo mwanaume huyo akampisha na kusimama pembeni, kama kumwonyesha heshima. Pius hakujua mtu huyo alikuwa nani, lakini kufikia hapa akaweza kujiongeza kwamba alifahamiana na hawa watu.
"Pius Kimambo...habari yako?" mtu huyu akamsalimu.
Pius akawa anamwangalia tu kwa mashaka.
"Unafanya nini hapa? Umejuaje tuko hapa?" Mr. Bernard akauliza.
"Oh ninajua mambo mengi yanayonizunguka Bernard...nafikiri unajua hilo," mtu huyo akasema.
Pius akawatazama wote kwa makini, kisha akamkazia uangalifu zaidi mtu huyo.
"Kwa nini mnamzuia baba wa watu? Hii ni nchi huru...kama anataka kuondoka mwacheni aondoke," mtu huyo akasema.
"Nini? Aondoke kivipi...unaju..."
"Nimesema mwacheni aondoke!" mtu huyo akamkatisha Mr. Bernard kwa uthabiti.
Mr. Bernard pamoja na yule mwanaume mwingine walitazamana kimaswali sana, huku Pius akijipa ukakamavu wa kuonyesha bado ni jasiri.
"Pius...kama ulivyosema, hakuna lolote ulilobakiza hapa. Kwa hiyo waweza kwenda nyumbani...hawa wasikuzingue kabisa...nenda baba," akasema mtu huyo.
Pius akamwangalia kwa sekunde chache, kisha polepole akaanza kupiga hatua na kumpita ili aondoke zake. Mr. Bernard alikuwa amepigwa na butwaa, asielewe nini ilikuwa maana ya mtu huyu kumwachia Pius. Ni mpaka Pius alipokaribia sehemu ya wazi ya mlango pale wanaume wawili wenye miili mikubwa ya mazoezi walipomzibia njia ili asiweze kupita. Pius alishtushwa nao sana na kubaki kuwatazama kwa hofu, kwa sababu walikuwa na sura zilizoonyesha walitaka kumdhuru. Mtu yule, akiwa anamwangalia Mr. Bernard, akaachia tabasamu la hila, na hapo Mr. Bernard akawa ametambua kwamba alikuwa akimfanyia tu Pius mchezo; hatoki mtu hapo!
Mtu huyu akageuka taratibu na kumwangalia Pius, ambaye alikuwa anababaika asijue pa kwenda. Wanaume wale wakamkamata kwa nguvu na kumpiga tumboni, kisha usoni, na kumtupa chini mbele ya miguu ya mtu huyo. Akacheka kwa dharau, na wale wanaume wake wakacheka pia. Mr. Bernard alihisi ahueni kwamba hawakumwachia Pius aondoke, lakini hakujua kihalisi watu hawa wangeupeleka wapi mchezo huu. Pius akajitahidi kusimama huku analia na kutetemeka, akiomba wasimtendee kwa ukatili.
"...tafadhali...niachieni...mimi...mimi ni..."
"Wewe ni msaliti!" mtu huyo akamkatisha.
Mr. Bernard hakuelewa alimaanisha nini kumwita Pius msaliti.
"Na unajua dawa ya wasaliti huwa ni nini?" mtu huyo akauliza.
Kisha akarudisha mkono wake nyuma ya kiuno chake na kutoa bastola. Mr. Bernard akashtushwa kiasi, kwa sababu hakuwa na lengo la kumuua Pius, kwa hiyo hakujua atazamie nini kutoka kwa mtu huyo ambaye hakueleweka ikiwa alikuwa anatania au anamaanisha anachotaka kufanya.
"Dada tafadhali...usiniue...nina familia...wananihitaji...mwanangu ni mgonjwa...ana...ana...ananihitaji...tafa..." Pius akaendelea kuomba kwa huzuni.
"Dawa ya wasaliti huwa ni kifo. Hujasoma kuhusu Yuda Iskariote? Alimsaliti Yeshu Krishto kwa shilingi 50 tu! Akaweka mfano kwa kujiua yeye mwenyewe...na mfano huo mpaka leo unapaswa kufatwa; usaliti, kifo. Lakini...kwa kuwa hukujiongeza kujiua, naona bora nikusaidie...au unasemaje?" mtu huyo akasema kwa kejeli na kufanya wanaume wake wacheke.
"Please dada...usi...mimi ni binadamu mwenzako...usitende unyama huu..."
Mtu huyu, anbaye ni mwanamke, akawa anatabasamu kwa kejeli tu na kumwangalia Pius bila kujali hata kidogo. Akamnyooshea Pius bastola kama anataka kumfyatulia risasi, naye Pius akanyoosha mikono yake juu kidogo kumwonyesha kwamba anahitaji amwonee huruma. Mwanamke huyo akamwangalia Pius sana, kisha akashusha bastola yake.
"Agh! Kwa nini huwa mnatia huruma sana mkiomba tusiwaue? Umenifanya hadi nimeshindwa kukupiga," mwanamke huyu akasema.
"Tafadhali dada yangu...usiniue. Mimi ni baba...nina binti...nina watoto...ndugu wananitegemea...tafadhali..." Pius akaomba kwa huzuni zaidi.
Mwanamke huyo alimwangalia kwa hisia sana, kisha akawaambia wanaume wale wampishe ili aondoke. Wakatii, naye Mr. Bernard akazidi kupandwa na hofu kiasi.
"Ondoka haraka! Sitaki kukuona tena...harakisha!" mwanamke huyo akamwamuru Pius.
Pius akaanza kurudi nyuma huku anatetemeka, kisha akageuka na kuanza kuelekea mlangoni upesi. Alipofika tu mlangoni, mlio wa risasi ulisikika kwa nguvu na kumfanya ashindwe kuendelea kujongea baada ya risasi hiyo kuupiga mgongo wake. Watu fulani husema kwamba, bora risasi ikupige ukiwa unatazama sehemu ilipotokea, lakini ikikupiga bila kutarajia, huwa ni kama maumivu yake yanakuwa mara mbili zaidi.
Pius alihisi maumivu makali sana kwa kuwa risasi hiyo ilimtoboa mgongoni mpaka sehemu ya mbele ya upande wa ini lake. Hakuweza hata kufikiria lolote, na hapo hapo risasi nyingine ikampiga mgongoni tena na kutoboa mpaka sehemu ya tumbo lake. Baba wa watu akaishiwa nguvu na kudondokea magoti yake, kisha mwili wa juu ukaangukia tumbo, naye akawa anashtuka-shtuka huku damu nyingi zikimtoka mwilini mwake na kutapakaa chini, kisha mwili wake ukatulia kabisa.
Mr. Bernard alishindwa kuelewa kwa nini mtu wake huyu aliamua kufanya hivyo. Mwanamke huyo akawa anatabasamu kikatili, akiwa ameridhishwa kabisa na kile alichofanya.
"Nini maana yake Beatrice? Kwa nini umefanya hivi?" Mr. Bernard akauliza.
Ndiyo. Mwanamke huyu alikuwa ni Beatrice, rafiki kipenzi wa Jaquelin!
Tokea mwanzo, ni yeye ndiye aliyekuwa akimsaidia Mr. Bernard ili kuharibu maisha ya Gilbert na Jaquelin. Alikuwa na sababu iliyomwongoza atake kuyafanya maisha ya wawili hao kuwa mabaya sana........
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
WhatsApp +255 787 604 893
Asante kaka. Matumaini one day my talent will be realised and I'll go farKama hii simulizi haijakopiwa kutoka watunzi wakubwa wa nje bhasi hakika tumefikia viwango vya kimataifa. Kuiweka kwenye mfumo wa movies, budget yake ni kubwa na producers wengi wakibongo hawataweza. Yote juu ya yote hongera mtunzi
Mkuu tuombe uzima hapo mbele tunaweza kuwa angel investors wa entertainment industryAsante kaka. Matumaini one day my talent will be realised and I'll go far